Dk. Hamis Kigwangalla aikana kampuni ya Qnet

Dk. Hamis Kigwangalla aikana kampuni ya Qnet

Mere presence ya Waziri ni endorsement ya activity yoyote.

Waziri hakijui kitu chenyewe lakini anaenda kwenye uzinduzi!

Mambo kama haya ni Tanzania pekee. Hili linatosha kutumbuliwa bila ajizi.

Tusishangae mikataba mibovu kama mawaziri ni calibre hii.
 
Kigwangala na mwezie walikula mlungula, wakaenda kuzindua biashara na kusaidia kampuni ya kitapeli ku-win public confidence kwamba ni kampuni inayofanya biashara kihalali na serikali inajua kumbe ni wizi mtupu.

Niliwah kutoa mchango wangu hapa kwamba kwenye biashara mtandao kuna makundi mawili; wanaonufaika na watakaoliwa. Wanaonufaika ni wale wanaoingia mwanzo na watanufaika kwasababu kwa kushirikiana na kampuni wataendelea kula hela za walalahoi wanaoingia. Watakaoliwa ni wale ambao wataingia mwishoni kwasababu ili unufaike ni lazima watu waingie nyuma yako. Na ndio maana ukitaka ku identify biashara-tapeli ni lazima utengeneze scenario yenye idadi flan ya watu ndo utajua kwamba baadhi yao(wengi wao) hawatanufaika. Kwenye biashara halali KILA MSHIRIKI HUNUFAIKA (anayochance sawa ya kunufaika, ceteris peribus)

Ndio maana tool kubwa ya kampuni hizi ili kuata watu ni kwamba wanaficha information za watu wangapi wameshajiunga ili usijue kama ww ni wa mwanzo au ni wale wa mwishoni ambao wataliwa.
 
Kuna mijitu inaona raha kupata picha za kupost Instagram, Snapchat na Facebook ionekane ina connection kubwa kubwa kikinuka inakana!!..
Siku moja ataitwa kuzindua 'Danguro' na picha zitapostiwa!.
 
Hiyo Kampuni wana ka ' branch ' kao kamoja hivi kapo Sinza jirani na Hostels za UDSM ukienda hapo hata kama ni Saa Saba ( 7 ) mchana utasalimiwa kwa kuambiwa ' Good Morning ' na baada ya hapo utaanza ' Kuhubiriwa ' Kitapeli na Wanawake tofauti tofauti ambao huzungumza haraka haraka utadhani wamebanwa na Haja Kubwa na wanataka kuwahi Kujisaidia.
Goodmorni mkuu!hehehe
Hivi forex unaonaje nao ?najua wee una uelewaa sana na mbobezi wa hali ya juu ....hebu Sema Machache kidogo mkuu

Ova
 
Shinyanga Simba SC tumetoka sare ya magoli mawili kwa mawili na Mwadui FC na bado tunaongoza Ligi kwa tofauti ya alama tano na wale ' Wendawazimu ' wanaotufuatia ambao Kwao matokeo ya jana yalikuwa ni ' Sherehe ' Kwao kana kwamba vile wameshakuwa na alama sawa na Mnyama Mnyamani ( Simba SC ) wakati ukweli ni kwamba watajitahidi kuifukuzia Simba SC ila kuipita Simba SC wasahau.
Msimu huu tuko vizuri nyama yoyote ikitupitia mbele Yetu tunaila tu

Ova
 
Teuzi ya Kigwangala itenguliwe kwa utapeli huu
 
Husije shangaa kwa mtu kama Kigwangala kumkana hata baba yake mazizi,kwa ushahidi huu unakana vipi kuwa uifahamu kampuni ya QNET? Msomi wa kiwango chake,mbunge na waziri wa serikali anawezaje kuzindua/kushiriki kuzindua kampuni/bidhaa hasiyo ijua?
Alishakana mpaka jina lake halisi..Usimshangae
 
Teuzi ya Kigwangala itenguliwe kwa utapeli huu
Yaani dkt mzima unakwenda kwenye ufunguzi wa kitu fulani alafu Kumbe hujui Hata kampuni hiyo inafanyaje kazi...what a shame!
Ndomana viongozi wa nchi hii wanatuingizsga kwenye matatizo kwa ajili ya upumbv wao

Ova
 
Waliponifanyia presentation walitumia picha yak Mheshimiwa. Wakanambia ona hata waziri kaja kuzindua ofisi, ni real business. Ila asante Mungu sikununua high kippende chao...
 
Waliponifanyia presentation walitumia picha yak Mheshimiwa. Wakanambia ona hata waziri kaja kuzindua ofisi, ni real business. Ila asante Mungu sikununua high kippende chao...
Ungepigwa mkuu faster hawa Jamaa ni matapeli
 
Ni hatari kufanya jambo ambalo haulijui.

Hivi Waziri mzima anaalikwa bila kujua anaenda kwa ajili gani? Yaani bila kujiridhisha ni kampuni ya nini au ni matapeli Waziri anaenda tu, huyo Kigwangala kakosa umakini kabisa.. Hata katika matamko yake mengi he has no focus.. Ni kama anatafuta cheap publicity most of time
 
Goodmorni mkuu!hehehe
Hivi forex unaonaje nao ?najua wee una uelewaa sana na mbobezi wa hali ya juu ....hebu Sema Machache kidogo mkuu

Ova

Hapana nisiwe muongo Mkuu Kwaresma imeshaanza jana. Hao Forex wala siwajui japo nami nawasikia tu ' Utapeli ' wao kupitia Wadau humu na kwingineko. Hata hivyo kuna msemo wa ' Wahenga ' usema ' lisemwalo lipo na kama halipo laja ' hivyo yawezekana kuna tatizo hapo pia.
 
Hiyo Kampuni wana ka ' branch ' kao kamoja hivi kapo Sinza jirani na Hostels za UDSM ukienda hapo hata kama ni Saa Saba ( 7 ) mchana utasalimiwa kwa kuambiwa ' Good Morning ' na baada ya hapo utaanza ' Kuhubiriwa ' Kitapeli na Wanawake tofauti tofauti ambao huzungumza haraka haraka utadhani wamebanwa na Haja Kubwa na wanataka kuwahi Kujisaidia.
ila nimecheka
 
Hii Serikali kanyaboya imeshindwa kutekeleza ahadi walizowaadi watz ktk campaign zao kujenga viwanda ikiwemo, sasa wameamua kutuletea matapeli.
Huwa tunaikosoa serikali lakini kwa utapeli huu ni akili za watu wenyewe wanajitakia, mtu anashindwa kufanya uchunguzi juu ya hii biashara mwisho anaingia kichwa kichwa anapigwa hela mwisho anakuja kulalamika.
 
Back
Top Bottom