DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

Mkuu utafute ule uzi hapa JF aliouleta Hutaki Unaacha.

Inasemekana Bilali yuko Kundi la EL, Shein pia aliwekwa na kundi hili na Karume pia analikubali.

If that being the case, is it Plan B ya EL kuwa Bilali achukue Nchi na EL awe Makamu wa Rais? Then baada ya Muda Bilali ajiuzulu kwa sababu yoyote ikiwemo Uzee ila EL achukue Nchi?

Watch out kipengele hicho kitakuwaje katika katiba mpya.


Great Thinker .....
 
mbona jamaa mwenyewe ameshakwisha hivyo.......nikijumlisha 3years naona atakuwa anakimbilia kwenye mkongojo...sidhani kama ataweza hata kufikiri kwa umakini vitu sensitive atakuwa kama shati lililopo sasa hivi, ni kukenua tuuuuuuuuuuu.

PingPong,

..actually Dr.Bilali seems to be getting better ukilinganisha na muonekano wake wakati wa kampeni za uchaguzi.

..nadhani LISHE ni kitu muhimu sana na hawa wakubwa wakishafika Ikulu lishe yao huwa ni ya uhakika.

..hivi umesahau Mkapa na Dr.Omar[r.i.p] jinsi walivyoota mashavu baada ya kushika madaraka?

..pia alikuwepo Sheikh Idris Abdul Wakil Nombe, Raisi wa 4 wa ZNZ. Mzee huyu alikuwa amechoka kweli kweli, lakini alipoingia Ikulu ya ZNZ akapatiwa lishe nzuri kiasi kwamba afya yake ilirudi kuwa imara akaweza kumuoa secretary wake na kupata mtoto!!!

..suala la umri na appearance lisikupe shida hata kidogo.
 

Jamani tuache utani huyu Mzee kachoka sana.


Ilulu.jpg

kachoka?? muulize huyu mama mwenye green hapo nyuma yake atakupa habari yake! lol....
 
Safari hii zamu ya Wakristu kutoa Rais. A Muslim need not apply. Yesu hawezi kukubal Rais ajaye awe Mwislamu.[You are entitled to your opinion]
 
Safari hii zamu ya Wakristu kutoa Rais. A Muslim need not apply. Yesu hawezi kukubal Rais ajaye awe Mwislamu.[You are entitled to your opinion]

Yesu tena, naye kakosa kazi za kufanya kaanza kugawa zamu za urais? Kama ndio hivyo, safari hii mama Rwakatare ndani ya ikulu 2015.
 
Wanajamii;

Kwa wafuatiliaji wa habari bila ya shaka watakua wamegundua kuwa Makamu Wa Rais Mh. Dk Bilali kwa kipindi kirefu sasa amekuwa katika ziara za kikazi mikoani na wilayani na kupewa kipau mbele katika media za Tanzania. Ziara hizi kwa mtazamo wa haraka japokuwa ni za kikazi lakini zimekuwa ni nyingi sana zaidi ya kiongozi mwingine yoyote wa Kisiasa.

Ikumbukwe kuwa Dr. Bilali ni Makamu wa Rais na anafanya zile kazi ambazo Rais amemwagiza au yuko aware nazo.

Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:


  • Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
​
  • Dk. Bilali hana Makundi na amekuwepo katika siasa za Bara na Visiwani na anakubalika (Of course ziara za sasa zimam-promote)
​
  • Dk. Bilali amekuwa Makamu wa Rais na anakubalika kama Presidential Material
​

  • Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
​

  • JK hataki aonekane kaivuruga Nchi ndo maana kwa mambo yote makubwa nchi hii kaamua bora tu akae kimya kuliko kusema. La kuhusu katiba ameona bora atofautiane na Chama chake ili kuacha Lergacy na kuleta utengamao katika Nchi.

Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?

Nawasilisha.



we ni mfu na mkatautepe mwenzako!
 
labda anafaa kwa uzinduzi wa majengo, shule , hospital na anafaa kwa zihara mbalimbali. mimi sijawahi sikia sikia sauti ya huyu jamaa yani hata nikiisika kwenye radio siijui mpaka mtu aniambie. na leo clouse fm wamemjadili mpaka jeradi hando kasema yeye anataka kuwa Makamu wa Rais mana hana kazi ngumu zaidi ya uzinduzi. wale mnaofwatilia power breakfast nadhani mnajua utani wa jeradi. he is too much simsikii kwenye mambo ya msingi na muhimu yanayoikabili nchi.
 
Safari hii zamu ya Wakristu kutoa Rais. A Muslim need not apply. Yesu hawezi kukubal Rais ajaye awe Mwislamu.[You are entitled to your opinion]
it might be true mana ukifwatilia trend kuanzia rais wa kwanza mpaka now ni kama wanapokezana hivi.
 
Dr. Bilal umri nao unaelekea machweo, sidhani kama hata yeye mwenyewe ana wazo la kugombea. Kwa jinsi watu walivyoichoka ccm, bila kupatikana mgombea kijana basi tutegemee uchakachuaji wa kura kwa mara nyingine.

Katiba mpya itakayoweka tume huru ya uchaguzi ndilo suluhisho la sivyo uchakachuaji huo utasababisha uvunjifu wa amani kwani watanzania watachoka kuvumulia dhuluma hii inayofanywa kwa kuchakachua kura na kulazimisha ushindi.
 
Wadau!
Kuna baadhi ya watu katika thread hii mmechangia na kusema kwamba, yawezekana Bilal akawa raisi na Lowassa akawa Makamu wake, halafu baada ya hapo Bilal akampisha Lowassa kwa njia yoyote ile labda BIlal anaweza kutoa sababu zozote ikiwemo Uzee, Uchovu au hata Ugonjwa ili Lowassa achukue nafasi ya uraisi..

Swali langu!
Hivi inawezekana au inakubalika kikatiba raisi anapoondoka/kufa/ achia ngazi makamu wa raisi anachukua kiti cha uraisi mpaka kipindi kingine cha uraisi au inakua kwa kipindi maalumu baada ya hapo unaitishwa uchaguzi mwingine?
maana ninavyojua mimi makamu wa raisi sio Chaguo la Wananchi bali ni pendekezo la raisi mwenyewe na Secretarieti ya Chama chake...
Naomba kujuzwa hapo wakuu ili tuende sambamba..
 
Inasemekana Bilali yuko Kundi la EL, Shein pia aliwekwa na kundi hili na Karume pia analikubali.

If that being the case, is it Plan B ya EL kuwa Bilali achukue Nchi na EL awe Makamu wa Rais? Then baada ya Muda Bilali ajiuzulu kwa sababu yoyote ikiwemo Uzee ila EL achukue Nchi?

Watch out kipengele hicho kitakuwaje katika katiba mpya
.

hapo nilipo Bold nahitaji kueleweshwa zaidi, hivi katiba mpya ikisema au kuanisha kua inapokuja ishu ya Makamu wa raisi kumrithi raisi madaraka, hatuoni kama itakua ni mchezo wa maigizo. Raisi anaachia ngazi kwa masilahi ya makamu wa raisi anachukua nchi, halafu tukumbuke makamu wa raisi sio chaguo la wananchi, na hii itapelekea hali fulani hata ya kufikia kuundia zengwe kama za kina Mwakyembe anapigwa mtu sumu halafu mtu mwingine anachukua position.... Sidhani kama nimeeleweka
 
labda anafaa kwa uzinduzi wa majengo, shule , hospital na anafaa kwa zihara mbalimbali. mimi sijawahi sikia sikia sauti ya huyu jamaa yani hata nikiisika kwenye radio siijui mpaka mtu aniambie. na leo clouse fm wamemjadili mpaka jeradi hando kasema yeye anataka kuwa Makamu wa Rais mana hana kazi ngumu zaidi ya uzinduzi. wale mnaofwatilia power breakfast nadhani mnajua utani wa jeradi. he is too much simsikii kwenye mambo ya msingi na muhimu yanayoikabili nchi.

Zihara ndio neno gani? Yaani humu jf kuna watu kiswahili kinawashinda sana hata sijui wamesoma shule gani. Mtu anatumia h sehemu ambayo haitakiwi kabisa, na hili tatizo limekuwa sugu sana humu jf. Inakera kiasi kwamba hata kama mtu ameandika points za maana lakini ukishaona tu hivyo hata hamu ya kuendelea huna? Kuzuhia, kuhaga, zihara, fulaa.....
 
HAHAAAAA!!!!!! TEHETEHE!!!!!!!!!!!!!DR BILAL si mwanasiasa hata kidogo ,kujieleza tu shida namafizikia yake sijui manyuklia ...hawezi ,,tatizo jingine hawezi kutoa ushindani ndani ya magamba atapigwa zengwe atachanganyikiwa ,,mtu safi hawezi kutoka kijani na njano.......
 
SHEIN is best of the best.....hana ****** wowote wa Makundi na jamaa ni intellectual wa ukweli hashoboki na mambo ya misifa km ni mgombea kutoka visiwani CCM wakitaka walete upizani wamchague Dr Shein....shule imekaa mahala pake na by the way is not muzungu worshipper
 
Hivi inakuwaje?? Rais yuko safarini majuu anatesa................. Makamu yuko mikoani anazurura. Sasa kazi za magogoni week nzima zinafanywa na nani??
 
SHEIN is best of the best.....hana ****** wowote wa Makundi na jamaa ni intellectual wa ukweli hashoboki na mambo ya misifa km ni mgombea kutoka visiwani CCM wakitaka walete upizani wamchague Dr Shein....shule imekaa mahala pake na by the way is not muzungu worshipper

Hapo nakuunga mkono, alipokuwa hapa wanawe walikuwa wanasoma shule ya kata. Anasema hawezi ku afford shule za akademi kwa mshahara wake. Maana huyo hana biashara wala kampuni nje ya kazi yake alioajiriwa Serikalini, kama anazo basi ni mtu wa siri na wa ajabu sana.

Sema nasikia alikuwa mkali kwa nanihii alipokuwa pale hospitali.
 
Futeni ndoto hizo, labda uwenyekiti wa CCM lakini siyo U Rais wa Tanzania. Hatukubali kutawaliwa na mtu anayetoka sehemu ambayo ina watu wachache kama wilaya ya Twmeke.

kwani Rais wa sasa katoka wapi? si katoka hapo msoga ..sasa kuna watu bilioni moja hapo msoga? jenga point yako vizuri ueleweke
 
Back
Top Bottom