DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

DK. Bilali Chaguo la JK Kumrithi 2015?

Mkuu kupewa BAN si kazi ngumu muhusika akiamua. Ni kubonyeza kitufe cha Abuse au kuandikia admin na wao bila kusita watakupa BAN. Au unataka nijaribu kwa ile post yake uone ilivyo? Ili mradi umekuwa mstaarabu kutambua, wacha tuendelee.

Iko hivi Omari Juma hakuwa Mzururaji kama huyu Balali sorry Bilali.

Mohamed Shain hatukumuona.

Niaje huyu Babu anakata mbuga usiku na mchana tena kwa muda mrefu tu amekomaa na sasa kishaanza kukubalika?

Haahaa, huyu ana 'talent ileile' ya ki-zwangendaba. Mkimpa na.1 ataachana na uzwangendaba ataanza kumpiku vasco da gama! Nyie wa tz mmerogwa nn na ni nani aliyewaroga? Eti bilal ' presidential material' What a **** like ths?
 
Wanajamii;

Kwa wafuatiliaji wa habari bila ya shaka watakua wamegundua kuwa Makamu Wa Rais Mh. Dk Bilali kwa kipindi kirefu sasa amekuwa katika ziara za kikazi mikoani na wilayani na kupewa kipau mbele katika media za Tanzania. Ziara hizi kwa mtazamo wa haraka japokuwa ni za kikazi lakini zimekuwa ni nyingi sana zaidi ya kiongozi mwingine yoyote wa Kisiasa.

Ikumbukwe kuwa Dr. Bilali ni Makamu wa Rais na anafanya zile kazi ambazo Rais amemwagiza au yuko aware nazo.

Yawezekana kabisa kuwa Rais Kikwete ameamua kuchukua uamuzi huo wa kumuandaa na kumtangaza Bilali awe mgombea Urais wa CCM 2015 ili kukinusuru chama chake CCM kutokana na makundi ambayo itake isitake 2015 yatakimega CCM kabisa kwa asilia 100%. Huenda akawa na sababu nyingi lakini chache ni zifuatazo:


  • Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
​
  • Dk. Bilali hana Makundi na amekuwepo katika siasa za Bara na Visiwani na anakubalika (Of course ziara za sasa zimam-promote)
​
  • Dk. Bilali amekuwa Makamu wa Rais na anakubalika kama Presidential Material
​

  • Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
​

  • JK hataki aonekane kaivuruga Nchi ndo maana kwa mambo yote makubwa nchi hii kaamua bora tu akae kimya kuliko kusema. La kuhusu katiba ameona bora atofautiane na Chama chake ili kuacha Lergacy na kuleta utengamao katika Nchi.

Ni nini maoni yako binafsi kuhusu Dk. Bilali na harakati zake za kuzunguka mikoani na wilayani in connection na mbio za Urais 2015? Je yawezekana akawa ni Chaguo la JK?


Nawasilisha.

hapo kwenye red nakuunga mkono-hizi zunguka zake zote ni za kumuuandaa kuja kuwa rais-wanajaribu kufanya awe anafahamika kwa watu,
 
Dr Gharib Bilal kwa kisomo ni mtu anaye onekana anafaa, lakini ana dhambi ya kumuunga mkono Dr Salim Amour avunje katiba ili aendele kuwa rais wa mapinduzi zanzibar, wakati huo Gharib ni waziri kiongozi, kiasi cha kutaka kuvunja muungano kwa ushrikiano na majeshi ya nje, ndio Dr Salim akapigwa kata funua, Karume mtoto akaingia, na kuwaweka mbali saana Dr Salim na Dr Gharib, na chama kikamuona Gharib si mtu wa kuaminika kuulinda Muungano haswa haswa akipewa madaraka visiwani, sasa kuhusu hili la uruthi 2015 nafikiri ni harakati zake mwen, lolote la weza kutokeayewe, kwa kuona nafasi imetokea sasa akifanya hivyo , why not?, na kuhusu rahisi wa 2015 mpaka sasa hivi ni speculation tu, ingawa kuna watu wana nia na kuna viongozi wenye watu wao, lakini atakaye tokea ni bado saana
 
kama ni rais wa Uzini inakubalika hapa hana chake hakuna wa kumbeba kama alivyobebwa 2010
 
Mkuu kupewa BAN si kazi ngumu muhusika akiamua. Ni kubonyeza kitufe cha Abuse au kuandikia admin na wao bila kusita watakupa BAN. Au unataka nijaribu kwa ile post yake uone ilivyo? Ili mradi umekuwa mstaarabu kutambua, wacha tuendelee.

Iko hivi Omari Juma hakuwa Mzururaji kama huyu Balali sorry Bilali.

Mohamed Shain hatukumuona.

Niaje huyu Babu anakata mbuga usiku na mchana tena kwa muda mrefu tu amekomaa na sasa kishaanza kukubalika?

Tatizo la huyu mzee kumbe hujalijua. Sio kama JK anampa promo, huyu anajipa promo mwenyewe kwa sababu ni mroho wa madaraka. Ni kweli anatamani sana kuwa rais pengine kuliko wote wanaotajwa humu. Hata hivyo hawezi, labda iwe kwa urais wa Zanzibar lakini sio wa Muungano.
 
Kune matope yanaandikwa hapa jf. Haya ya kwako ni zaidi ya uharo. Siku huyo mzee akiapishwa kuwa rais mi ntaenda kujinyonga kwenye paa la uwanja wa Taifa ili kila mtu aone.

Eeeeeh! Mkuu kiapo kibaya hicho! 2015 siyo mbali, Mungu akinipa uhai lazima niwe shuhuda wa utekelezaji wa ahadi yako!
 
Mkuu kwa hali ya siasa ya sasa hivi au tuseme kwamba kura ya urais inapigwa hivi sasa na chama chochote kikasimamisha mgombea wa Urais JMT toka upande wa pili, hakika nakuambia chama ambacho kitakuwa na mgombea toka upande wa bara kitaibuka mshindi! Siasa ya nchi hii kwa sasa imekaa tenge na hasa maneno ya akina Jussa toka upande huo yanatia shaka kuu!

Sasa hawa jamaa nao wametunisha misuri na kanzu zao wanataka zamu ya urais iwe kwao. Kwa upande wangu sioni sababu iweje rais atoke upande wa nchi wenye watu wachache kiasi kile. Tatizo liko kwa wana CCM, Aina ya sungusungu tuliowaona Mwanza wapo tayari kumpigia kura hata mbuzi mnyama ilimradi agombee kwa tiketi ya CCM tu.
 



  • Safari hii ni zamu ya Wazanzibar kutoa Rais. Kumbuka hii ni hoja rahisi kama walivyoamua kuwa safari hii Spika ni Mwanamke na hivyo kumweka Sita pembeni. K
​



  • ohoo!

    sasa akiibuka mtu mwingine akasema ni "zamu ya mkristo".... itakuwaje?
 
Eeeeeh! Mkuu kiapo kibaya hicho! 2015 siyo mbali, Mungu akinipa uhai lazima niwe shuhuda wa utekelezaji wa ahadi yako!

Sio kama ntajinyonga kwa sababu hali hiyo hali hiyo ni ngumu kutokea. Ntafanya hivyo kwa sababu sintaona faida ya kuishi chini ya utawala wa mtu huyo.
 
  • Ili kuzima chokochoko za Wazanzibari kuua Muungano dawa ni kumweka Mzanzibar. JK hawezi kuruhusu Zanzibar iwe Nchi au Dola (Historically na Kikatiba).
"Ili kuzima chokochoko za Wazanzibar kuvunja Muungano".... Kwa nini? Why?

Zanzibar ni koloni letu? Kwa nini tutake kuzima chokochoko za Wazanzibar za kuvunja Muungano?

Mengine yote umeyatolea reasoning na maelezo ila hilo tu. Kwa nini Kikwete hawezi kuruhusu Zanzibar iwe nchi, ana mashamba Zanzibar? Why not? What do you Tanzania Barans get out of Zanzibar? Kuna nini Zanzibar? Iweje muwabembeleze?

Kwa Kikwete au Tanzania Bara, faida za kuwang'ang'ania Zanzibar ni nini, mbona hamsemi????
 
Katiba inasemaje akikosa kura kule?
Hili si suala la katiba. Ni suala la mahesabu. Anaweza kukosa kura zote za Unguja na Pemba lakini akapata kura nyingi za bara. Kadhalika mgombea anaweza kupata kura zote za Unguja na Pemba lakini akikosa kura za bara basi.
 

Jamani tuache utani huyu Mzee kachoka sana.


Ilulu.jpg
 
.....Inasemekana Bilali yuko Kundi la EL, Shein pia aliwekwa na kundi hili na Karume pia analikubali.If that being the case, is it Plan B ya EL kuwa Bilali achukue Nchi na EL awe Makamu wa Rais? Then baada ya Muda Bilali ajiuzulu kwa sababu yoyote ikiwemo Uzee ila EL achukue Nchi.....

Duh, hili bonge la scenario!! - EL anaweza kuchukua notes hapa.

Bilali hana ''mvuto'' wa kisiasa kwa Bara, labda huko kwao Zanzibar (mi si mbaguzi though...). Sidhani kama CCM wanaweza kucheza na mind za watu, of course labda kama wameshajiandaa kukwapua kura by hooks and crooks kwa mara nyingine tena.
 
Sasa hawa jamaa nao wametunisha misuri na kanzu zao wanataka zamu ya urais iwe kwao. Kwa upande wangu sioni sababu iweje rais atoke upande wa nchi wenye watu wachache kiasi kile. Tatizo liko kwa wana CCM, Aina ya sungusungu tuliowaona Mwanza wapo tayari kumpigia kura hata mbuzi mnyama ilimradi agombee kwa tiketi ya CCM tu.

Mkuu CCM wakijaribu hilo it will be suicidal decision. Hata hao sungusungu hawatakuwa tayari kuipigia kura. Hakuna haja ya zamu.
 
kama ni rais wa Uzini inakubalika hapa hana chake hakuna wa kumbeba kama alivyobebwa 2010

Kwa kweli! Sema mchakato wa kupata Rais nayo ni issue, lakini tungependa a visionary leader ambaye ataona Tanzania itakavyokuwa miaka ijayo.
 
Kune matope yanaandikwa hapa jf. Haya ya kwako ni zaidi ya uharo. Siku huyo mzee akiapishwa kuwa rais mi ntaenda kujinyonga kwenye paa la uwanja wa Taifa ili kila mtu aone.
Tazama Daily News ya leo Dr Bilali Front page, Jk Page three.
 
Dr. Bilal umri nao unaelekea machweo, sidhani kama hata yeye mwenyewe ana wazo la kugombea. Kwa jinsi watu walivyoichoka ccm, bila kupatikana mgombea kijana basi tutegemee uchakachuaji wa kura kwa mara nyingine.
Kwa hatua iliyofikiwa na CCM sasahivi issue ya umri katika presidential candidacy 2015 sio kigezo kinachoweza kuwa na nguvu. Tatizo ni kwamba CCM inamadoa ambayo hayawezi kufutika kirahisi ndani ya muda uliobakia kuelekea 2015. The only thing CCM wanachotakiwa kukifanya sasahivi ni kujiandaa na mipango ya uchakachuaji wa nguvu kwa ajili ya 2015.
 
Mkuu kwa hali ya siasa ya sasa hivi au tuseme kwamba kura ya urais inapigwa hivi sasa na chama chochote kikasimamisha mgombea wa Urais JMT toka upande wa pili, hakika nakuambia chama ambacho kitakuwa na mgombea toka upande wa bara kitaibuka mshindi! Siasa ya nchi hii kwa sasa imekaa tenge na hasa maneno ya akina Jussa toka upande huo yanatia shaka kuu!
Nitafurahi sana iwapo watanzania tutakuwa na mtazamo unaofanana na mawazo yako. Siasa ya visiwani imesha poteza mwelekeo. Nje ya vyama vingine kushika hatamu Zanzibar, CUF ikipata nafasi Zanzibar sio sehemu ya Tanzania tena.
 
Back
Top Bottom