DID GIANTS EXIST? Historia ya Majitu ya Kale

DID GIANTS EXIST? Historia ya Majitu ya Kale

Hivi zinjasthropus nae si mtu wa mwanzoni mwanzoni kuishi?? Miaka milioni tatu wanasemaga..
Sasa kama watu wa zamani walikuwa na maumbo makubwa mbona zinja kifuvu chake ni kidogo sana???
 
Embu tuongeze info mkuu..... Hiyo video bado unayo au hata link tusafishe macho
ADAMU ANAKADIRIWA KUWA NA KIMO CHA FUTI TISINI

TWENDE SAWA HAPA

· Alikuwa mrefu kama Mnazi, Nywele nyingi kichwani
· Enzi za Nuhu kulikuwa na mtu mrefu, maji ya mafuriko yalimfika kiunoni
· Akina Ad walikuwa Majitu makubwa zaidi ulimwenguni
Na Maulamaa, Wanasayansi, Mfasiri Abu Kawthar
Makala hii itagawanyika katika sehemu kuu mbili; Mosi, itakuwa na nukuu ya Hadiyth za Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, kuhusiana na kuumbwa kwa nabii Adam na kimo cha umbo lake. Na pili, itakuwa na maelezo yaliyotokana na vumbuzi za kisayansi kuhusiana na kuumbwa kwa ulimwengu.
Hadiyth za Mtume, swallallahu alayhi wa sallam
Abu Hurairah kasimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema na amani zimshukie, amesema: Mwenyezi Mungu, subhaanahu wata’ala, alimuumba Adam kwa kimo cha dhiraa sitini, na Alipokwishamuumba, nenda kalisalimie kundi lile, hao walikuwa ni baadhi ya Malaika waliokuwa wamekaa hapo, na asikilize watakavyomjibu, na hiyo ndiyo itakuwa salamu yake na ya vizazi vyake. Adam akaenda na kusema: As-Salaam Alaikum (Amani iwe juu yenu)! Malaika wakasema: ‘As-salamu Alaika wa Rahmatu-l-lahi’ (Na wewe pia amani na rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yako). Wao (Malaika) waliongeza, “Wa Rahmatu-l-lahi”. Hivyo Yule atakayeingia Peponi ataingia kwa umbile la Adam, akiwa na kimo cha dhiraa sitini, kisha watu waliofuata baada ya Adam, wakaendelea kupungua kimo hadi kimo cha leo.” (Sahih Muslim, Kitabu 040, Namba 6809)
Ibn Abi Haatim kasimulia kwa isinadi sahihi kutoka kwa Ubayy ibn Ka’b kuwa Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, amesema: “Mwenyezi Mungu alimuumba Adam akiwa mtu mrefu mwenye nywele nyingi kichwani, alikuwa (mrefu) kama vile mnazi.”
Kasimulia Abu Hurairah: Mtume amesema: “Mwenyezi Mungu alimuumba Adam, akimrefusha kwa dhiraa 60. Alipomuumba, Akamwambia, “nenda ukalisalimu lile kundi la Malaika, na wasikilize watakavyokujibu, kwani hiyo ndiyo itakuwa salamu yako na salamu ya vizazi vyako.” Basi Adam akawasalimu (Malaika), As-Salamu Alaikum (yaani amani iwe juu yenu). Malaika wakasema, “As-salamu Alaika wa Rahmatu-l-lahi” (amani na rehema za Mwenyezi Mungu ziwe juu yako). Hapo Malaika walitia nyongeza katika salamu aliyoitoa Adam, ‘Wa Rahmatu-l-lahi’. Mtu yeyote atakayeingia Peponi, atafanana na Adam (kwa haiba na kiwiliwili). Watu wamekuwa wakipungua kimo tangu alipoumbwa Adama. (Bukhari, Juz. 4, Kitabu 55, Namba 543).”
Kasimulia Abu Huraira: Mtume wa Mwenyezi Mungu amesema: “Kundi la kwanza la watu watakaoingia Peponi litakuwa linang’ara kama mbalamwezi, na wale watakaowafuata watametameta kama nyota angavu zaidi angani. Hawatajisaidia haja ndogo, hawatajisaidia haja kubwa, hawatatema mate, wala hawatatoka makamasi. Vitana (Mashanuo) yao yatakuwa ya dhahabu, na jasho lao litakuwa na harufu ya miski. Mikunazi itatumika katikati yao. Wake zao watakuwa mahururaini. Watu wote watafanana, na watafanana na baba yao Adama (kwa kimo), urefu wa dhiraa sitini.” (Sahih Bukhari, Juz. 4, Kitabu 55, Namba 544)”
Abu Hurairah kasimulia kuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu, rehema za amani zimshukie, amesema: Kundi la kwanza la Umma wangu kuingia Peponi litakuwa kama Mbalamwezi usiku. Kisha wale watakaowafuatia watakuwa kama nyota zinazomeremeta zaidi kwa mwangaza, kisha baada yao, watafuata wengine kwa daraja zao. Hawatafanyiza haja kubwa wala ndogo, wala hawatakuwa na makamasi, wala hawatatema mate. Vitana vyao vitatengenezwa kwa dhahabu, na kuni za maziga yao zitakuwa mikunazi na jasho lao litakuwa miski na umbo lao litakuwa moja likilingana na kimo cha baba yao Adam, kimo cha dhiraa sitini..” Hadith hii pia imesambazwa kwa mapokeo ya Ibn Abi Shaiba kwa tofauti ndogo ya maneno. (Sahih Muslim, Kitabu 040, Namba 6796).
Hiyo ni kusema kuwa watu walikuwa na kimo kikubwa pale mtu wa kwanza alipoumbwa na wakaendelea kupungua kimo. Katika Kitabu Kitukufu, Qur’an, kuna utajo wa watu waliokuwa wakubwa mno ambao ni watu wa kabila la Ad ambao wanaelezewa kama ni watu wa “vimo hamsini.”
“Je! Hukuona jinsi Mola wako alivyowafanya (Adi) Iram (waliokuwa) wana majumba marefu marefu ambao hawakuumbwa mfano wao. “ (89:6-
cool.png

Mfasiri Shah Abdul-Aziz wa India yeye anasema, ilikuwa ni mijitu ya kimo kisichopungua yadi kumi na mbili. Kwa mujibu wa Hadiyth katika Kitabu Sh-Shafa cha Qazi Ayaz (uk.65), Adam alikuwa na urefu wa yadi sitini.
Katika Kitabu, Ghiyasu ‘l-Lughah, jitu moja kubwa (giant) linatajwa kwa jina la Uj ambaye alizaliwa katika zama za Nabii Adam na aliishi hadi zama za Nabii Musa, ni kipindi cha miaka 3500, na kwamba alikuwa mrefu mno kiasi kwamba hata maji ya mafuriko katika zama za Nabii Nuhu yalimfika kiunoni tu.
Zipo Hadith na kuna visa vya majitu makubwa ambayo makaburi yao yapo hadi leo, kila mahali kule Persia. Mkabala na nyuumba moja ya Kanisa la Misheni kule Peshawar (India), lipo kaburi lenye urefu wa yadi nane za mraba, ambalo linaheshimiwa na Waislamu na Wahindu.
Katika kitabu cha safari zake kule Persia, juz. 2, uk. 89, De le Belle anataja makaburi kadhaa makubwa ambayo yapo Persia. Makaburi makubwa mno yako mengi kule Hindustan.
 
KISAYANSI

Sayansi
Sayansi ya leo imethibitisha kuwa Mtu wa kwanza (Adam) alikuwa na kimo cha dhiraa 60. Soma nukuu zifuatazo katika Sehemu moja ya Toleo la Septemba 2001 la Jarida Mashuhuri la Sayansi la Israil, Ha-Mada Ha-Yisraeli B’ Angleet V’lvreet.” Kisha soma maoni chini yake.
Tel Aviv, Israil
Katika Kongamano la hivi karibuni nchini Israil lililozungumzia sayansi na dini, Dkt. Shlomi Lesser wa Chuo Kikuu cha Hebrew, na Mwenyekiti wa Taasisi ya Hofesh V’ Mada, akiwakilisha wanasayansi wenye shaka na dini, aliongoza mdahalo mkali baina ya wanabaiolojia na Wanazuoni wa ki-Orthodox wa Kiyahudi juu ya mada “Mwanzo wa Maisha”.
Wengi walioshuhudia mdahalo huo wakiwemo wale wenye msimamo mkali wa kidini, wakaibuka na hisia kuwa wanazuoni wa Kiyahudi hawakufanya vizuri dhidi ya wapinzani wao wa mrengo wa “Epicurean”.
Mwangaza wa mchana ulichomoza pale Dkt Lesser aliposhiriki katika kuulizana maswali; moja baada ya jingine na Rabbi Dovid Brown wa Chuo Kikuu cha Yeshiva.
Katika nukta moja, Dkt. Brown alimuuliza Rabbi Brown, je, mtu wa kwanza alikuwa na kimo gani? Mwanazuoni wa Kiyahudi akajibu, “aghalabu alikuwa na kimo cha mwanadamu wa wastani kwa mujibu wa Wahenga wa Kiyahudi (chazal)
Dkt. Lesser, akirejea utafiti ulioshirikisha taasisi yake na taasisi nyingine, akasema, “njia pekee ya mwanadamu kuweza kuja kutokana na jozi moja ya wazazi (wazazi wawili-Adam na Hawa) ni iwapo tu kama wazazi hao wa mwanzo walikuwa ni majitu makubwa katika zama za kabla ya elimu ya lishe.”
Hesabu zake zilionesha kuwa ili jamii ya mwanadamu kuweza kufikia hali ya maumbile waliyokuwa nayo katika karne ya 17, Kisa cha Adam na Hawa kingelikuwa na maana iwapo tu mtu wa kwanza angelikuwa na kimo cha futi 90. Hakuna njia nyingine ambayo mwanadamu angeliweza kuvuka kikwazo cha kijenetikia.”
Aidha, Dkt. Lesser anasema, kama Adam angelikuwa na kimo cha mtu mwingine yoyote yule kama wanavyosema wanazuoni wa dini ya Kiyahudi, basi hii ingekifanya kisa cha Adam na Hawa kuwa upuuzi ulio dhahiri.”
Ni jambo la kuvutia kwamba wakati wanabaiolojia hao wakidhani kuwa wanaipondaponda dini ya Kiyahudi kumbe wanauthibitisha Uislamu! Wanasayansi waliibuka na utafiti wa kijenetikia ambao uliwapelekea kufanya hesabu za kimo ambacho mtu wa kwanza angekuwa nacho kama Kisa (cha Adam na Hawa) kilikuwa cha kweli.
Wakaibuka na futi 90. Zingatia kuwa miaka 1400 iliyopita kabla ya wasomi hawa hawajafikia hitimisho hilo, Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, alishazungumzia kitu hicho. Kimahesabu, dhiraa sitini ni sawa na Futi 90.
Maisha yalianza Duniani Miaka Bilioni 3.8 iliyopita
Baada ya kupoa kwa gamba la ardhi, maji yalianza kuchukua sura yake, na mwezi ukaumbwa kutokana na ringi la majabali lililokuwa likiizunguuka dunia. Maisha kama haya tuliyonayo hivi leo yanakadiriwa kuwa yalianza takribani miaka bilioni 3.8 iliyopita. Umri wa dunia unakadiriwa kuwa ni miaka bilioni 4.6.
Dunia inakadiriwa kuwa ilikuwa na asilimia 10 tu ya ukubwa wake wa sasa. Ilikuwa ndogo zaidi, hivyo uzito wake ulikuwa mdogo zaidi. Na kadri ilivyokuwa ndogo ndivyo uzito wake ulivyokuwa mdogo, na ndivyo ilivyokuwa na viumbe vikubwa. Na hivyo, maumbile ya viumbe waliokuwa wakiishi wakati huo yalikuwa makubwa zaidi. Mathalani, dunia ilikuwa na mijusi mikubwa (dinosaurs).
Dahaha ni neno la Kiarabu lililotumika katika Qur’an. Maana yake ni kitu kutanuka, kuviringika, kuwekewa mizani (urari), na kuwekewa mwendo. Maana hii inashabihiana na jinsi ardhi ilivyotanuka, na inavyoendelea kutanuka.
Kwa uthibitisho wa maana hiyo, unaweza kusoma Kamusi ya Lisan Al-Arab pamoja na kamusi nyingine nyingi za Kiarabu ambazo zina maana na mifano ya mashairi, methali, Kauli na nukuu nyingine ambazo zinaonesha maainisho ya maneno fulani na namna yalivyotumiwa na Waarabu wa zamani.
Wanasayansi wanasema Sayari zenye uzito mdogo (low gravity) wa chini ya nukta 8 huwa na athari zifuatazo kwa watu wanaoishi kwa uzito huo:
* Maguvu ya viumbe huongezeka
* Kimo cha viumbe huongezeka
Ndiyo sababu dunia ilipokuwa ndogo ilikuwa na viumbe wakubwa, wenye nguvu nyingi na vimo virefu.
Kinyume chake, wanasayansi wanasema kuwa uzito wa sayari unapokuwa mkubwa, viumbe huwa na athari hizi:
* Nguvu za viumbe hupungua
* Kimo cha Viumbe hupungua
Ndiyo sababu kadri uzito wa sayari ya dunia ulivyoongezeka, maumbile ya viumbe yakapungua nguvu na vimo. Hii inashabihiana na Hadiyth za Mtume, swallallahu alayhi wa sallam, kwamba baada ya Adam, vizazi vikawa vinapungua kimo hadi kufika kimo cha leo.
Hivyo, Uislamu hauna mgongano na sayansi kuhusiana na kimo cha mtu wa kwanza duniani ambacho kilikuwa ni futi 90. Jamii ya kwanza ya wanadamu ilikuwa na kimo cha futi 90.
Vimo vikawa vinapungua miongoni mwa jamii za wanadamu hadi leo ambapo tuna watu wenye urefu wa futi 7, na tunao watu wenye ufupi wa futi 2. Sababu ni kwamba sayari ya dunia ilikuwa ndogo hapo mwanzo kuliko ilivyo sasa.

Asalaam Kudo
 
Kadri teknolojia inavyoongezeka wanadamu watazidi kudumaa kimaumbo, hata ukichukulia miaka ya zamani watu waliishi kwa kupambana na mazingira wakitumia nguvu nyingi sana hivyo kuwaimarisha miili yao kuwa imara zaidi.

Ndio maana hata umri wa kuishi unazidi kufifia kizazi kwa kizazi,

Lishe duni mfano chips yai, soda, ambapo watu/wa zamani walitumia vyakula vyao vya asili kama asali, nyama, vyakula jamii ya mizizi na matunda pori kwa wingi.

Modern mankind is a weakest creature ever existed!!
wangetumiaje soda chips na wakati hazikuwepo?
 
Khaaaaa😀😀😀
Lakini hawa watu wa aina hii bado wapo sema ni wachache sana mfano kuna movie moja ya Thailand kuna mtu yumo mwenye umbo kubwa sana sio edit ile movie hiyo inahusiana na wizi wa ngombe
Lakini pia kuna mcheza mieleka anaitwa GREAT KHAL nadhani ni mifano ya watu wa namna hiyo lakini hapa kwetu atakuw yule mfanyakazi wa global publishers jina simjui
 
Mkuu Kudo900 ahsante kwa darasa murua ila kuna vitu vimenishtua kidogo

1. Huyo UJ ambaye maji ya gharika yalimfikia kiunoni ndio yule UJ IBN ANAQ?? Ina maana alipona kwenye gharika??

2. Umegusia suala la dunia kuwa ndogo enzi hizo..... Je kuna ushahidi wa kisayansi kuwa dunia ya karne ya 21 ukilinganisha na karne za kwanza kabisa zinatofautiana size????

Embu tuwekane sawa hapo tuwe pamoja
 
Lakini hawa watu wa aina hii bado wapo sema ni wachache sana mfano kuna movie moja ya Thailand kuna mtu yumo mwenye umbo kubwa sana sio edit ile movie hiyo inahusiana na wizi wa ngombe
Lakini pia kuna mcheza mieleka anaitwa GREAT KHAL nadhani ni mifano ya watu wa namna hiyo lakini hapa kwetu atakuw yule mfanyakazi wa global publishers jina simjui
Ni kweli mkuu GREAT KHALI ule mwili duh sio wa kawaida kabisa..... Kuna mmoja pia nlimshuhudia kampala ni bodyguard wa kabaka muteebi mfalme wa baganda duh yule jamaa ni mrefu kma great khali na mwili wake kma the big show.... Anatisha kwa ufupi bado kidogo nikimbie nlihisi mnyama maana anavaa ngozi ya chui!!
 
Mkuu Kudo900 ahsante kwa darasa murua ila kuna vitu vimenishtua kidogo

1. Huyo UJ ambaye maji ya gharika yalimfikia kiunoni ndio yule UJ IBN ANAQ?? Ina maana alipona kwenye gharika??

2. Umegusia suala la dunia kuwa ndogo enzi hizo..... Je kuna ushahidi wa kisayansi kuwa dunia ya karne ya 21 ukilinganisha na karne za kwanza kabisa zinatofautiana size????

Embu tuwekane sawa hapo tuwe pamoja
Nadhani ukisoma vitabu kadhaa utaona dunia mwanzo ilikuwa ni moja bila kuwepo mabara hivyo ikarahisisha wakazi wake kuhama bila shida kwa kutumia ngamia na punda (vitabu vya dini vimeeleza baadhi ya misafara)ambayo leo ukiona jinsi dunia ilivyo utajiuliza walifikaje kwa usafiri wa punda na ngamia?

Tunasoma kwamba baadae kulitokea tetemeko lililoigwanya dunia vipande vipande ambavyo leo tunaita Mabara

Kifupi ni kuwa mkiwa eneo moja mtachangia hali ya hewa moja na mtazoea mabadiliko yake lakino ukihama kwenda eneo jingine lazima mwili wako utakabiliana na changamoto

Hivyo basi niseme kwamba wakati dunia inaumbwa ilikuwa moja kabla ya kugawanywa vipande na watu kujitenga kimabara baada ya kupata elimu so nadhani huko ndo kutanuka kwa dunia yaani ilisogea baada ya mpasuko ule tunaoambiwa na wanasayansi wetu

Nadhani umenielewa kama bado basi ngoja usingizi uniishe kesho tuelewashane

Asalaam kudo
 
Nadhani ukisoma vitabu kadhaa utaona dunia mwanzo ilikuwa ni moja bila kuwepo mabara hivyo ikarahisisha wakazi wake kuhama bila shida kwa kutumia ngamia na punda (vitabu vya dini vimeeleza baadhi ya misafara)ambayo leo ukiona jinsi dunia ilivyo utajiuliza walifikaje kwa usafiri wa punda na ngamia?

Tunasoma kwamba baadae kulitokea tetemeko lililoigwanya dunia vipande vipande ambavyo leo tunaita Mabara

Kifupi ni kuwa mkiwa eneo moja mtachangia hali ya hewa moja na mtazoea mabadiliko yake lakino ukihama kwenda eneo jingine lazima mwili wako utakabiliana na changamoto

Hivyo basi niseme kwamba wakati dunia inaumbwa ilikuwa moja kabla ya kugawanywa vipande na watu kujitenga kimabara baada ya kupata elimu so nadhani huko ndo kutanuka kwa dunia yaani ilisogea baada ya mpasuko ule tunaoambiwa na wanasayansi wetu

Nadhani umenielewa kama bado basi ngoja usingizi uniishe kesho tuelewashane

Asalaam kudo
Nmekusoma mkuu.... Ukiamka uje na nondo zaidi kuhusu huyo UJ BIN ANAQ ambaye maji ya gharika yaliishia kiunoni...... Imenishtua sana hyo story
 
Nmekusoma mkuu.... Ukiamka uje na nondo zaidi kuhusu huyo UJ BIN ANAQ ambaye maji ya gharika yaliishia kiunoni...... Imenishtua sana hyo story

Historia ya UJ ni pana sana tena sana na katika historia hiyo huwezi amini imeanzia Tanzania na ndipo ilipoanza kuonekana lakini kwa sababu tusizozijua historia hii imefichwa na hivyo wengi kuona Uj hakuna anaejua alikotokea.

Uj inaaminika kwamba fuvu lake lipo mexico kwa sababu ni fuvu la mtu mweusi na lilionekana sio la mtu wa kawaida (Giant)

Kwa kuwa ni historia pana juu ya mtu huyu basi kifupi naomba upitie hapa chini nawe waeza kuja nisaidia pale nilipokwama kuhusu mtu huyo ila ukweli ndio huu kwamba historia yake imeanzia hapa Tanzania

Unju bin Unuq (pia: Unju bin Unuku, Unzi Bin Ununuk) ni jina la jitu katika masimulizi ya wakazi wa pwani ya Tanzania. Hadithi zake zasimuliwa kuanzia Bagamoyo hadi Kilwa.

Historia yake inapatikana katika makumbusho ya Kaole huko Bagamoyo.

Moja ya mambo ya ajabu ya mtu huyu ni urefu wake yaani kimo, inasadikiwa alikuwa na urefu mkubwa ulioweza kumfanya atembee baharini na miguu yake kugusa chini.

Pia alikuwa akitembea kutoka nchi hadi nchi kutokana na urefu wake. Inasimuliwa kuwa moja kati ya nyayo zake inapatikana kwenye jiwe alilokanyaga huko Tabora, Tanzania, wayo wa mguu wa kushoto wakati wayo wa mguu wa kulia ulionekana kwenye jiwe alilokanyaga huko Kongo.

Inasimuliwa pia akitaka kula alikuwa akichukua samaki baharini kwa mkono na kuchoma katika jua kisha anakula.

Kuhusu maisha yake inasimuliwa kuwa Unju bin Unuk hakuoa wala kuolewa kutokana na umbo lake.

Sehemu nyingine ya hadithi yake ni alipokufa Unju bin Unuq, aligawanyika vipandevipande kutokana na urefu wake na inasemekana kidole chake chenye urefu wa kilometa moja kasoro ndicho kilichopatikana na kuzikwa pale Bagamoyo, lakini hakuna simulizi mwili wake uliobaki uliangukia wapi.

Unju bin Unuq alikuwa na ndugu yake aliyejulikana kama Geofrey bin Unuk, huyu alipatikana maeneo ya Dodoma. Au kwamba Unuq baada ya kupotea kwa muda wa miaka mingi ndugu zake wa mbali sana wameonekana katika mkoa wa Dodoma.




Asili ya jina la Unju bin Unuq katika Uarabuni na BibliaEdit

Jina lake linatokana na Kiarabu cUdj bin Unuq / ‘Anaq عوج بن عنق anayejulikana katika visa vya nchi nyingi za Uislamu kama jitu kubwa sana. Waislamu walipokea hadithi kutoka kwa Wayahudi anakojulikana kwa jina la Og עוֹג‬.

Asili kabisa ni taarifa za Biblia kuhusu mapigano kati ya Wanaisraeli waliotoka Misri na Ogu mfalme wa Bashani (Hesabu 21,33)[1]; Wanaisraeli walimshinda wakiongozwa na Musa.

Ogu alisemekana kuwa mtu mrefu; Kumbukumbu la Torati 3,11 kinamtaja hivi: "aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu".

Katika masimulizi ya Wayahudi tabia hii iliendelea kuongezeka; katika Kitabu cha Amosi 2,9 anatajwa (bila kusema jina) kama "Mwamori" "nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni".

Wataalamu Wayahudi wa baadaye waliona ya kwamba vipimo vya Kumb. 3 kuhusu kitanda chake chenye urefu wa mikono yaani dhiraa 10, sawa na mita 4-5, vilihusu mkono wa hilo jitu lenyewe, hivyo walimwona mkubwa zaidi tena.

Kwenye kitabu Berakhot cha Talmudi Ogu anasimuliwa ya kwamba aliweza kuinua mlima aliotaka kurusha dhidi ya Wanaisraeli, lakini Mungu alimzuia[2]. Katika kitabu cha Nidah katika Talmudi Ogu anasemekana ni mtu aliyeishi kabla ya gharika ya Nuhu akiwa ni mmoja wa hao ambao walitunzwa.[3]


Katika UislamuEdit

Masimulizi ya Kiyahudi yalipokewa na Waislamu na kupanuliwa tena. Ushahidi uko kwa Al Tabari aliyeandika ya kwamba maiti ya cUdj ilikuwa kama daraja juu ya mto Naili.

Al-Thaclabi aliandika ya kwamba cUdj alikuwa na urefu wa dhiraa 23,333 akiweza kunywa kwenye mawingu, kushika ngumi baharini na kuichoma kwenye Jua. Alitembea mbele ya Nuhu wakati wa gharika kuu lakini maji yalifikia magoti yake tu. Aliishi miaka 36,000. Alipoona kambi la Wanaisraeli na Musa alivunja mlima akashika kipande cha kuangamiza kambi lote kwa pigo moja, lakini Mungu alituma ndege waliokula shimo katikati ya mlima uliomuangukia na kumfunga katikati. Hivi Musa aliweza kumshinda kirahisi


Hii ni picha iliopigwa huko Mexico miongo kadhaa nyuma

Asalaam kudo
 
Historia ya UJ ni pana sana tena sana na katika historia hiyo huwezi amini imeanzia Tanzania na ndipo ilipoanza kuonekana lakini kwa sababu tusizozijua historia hii imefichwa na hivyo wengi kuona Uj hakuna anaejua alikotokea.

Uj inaaminika kwamba fuvu lake lipo mexico kwa sababu ni fuvu la mtu mweusi na lilionekana sio la mtu wa kawaida (Giant)

Kwa kuwa ni historia pana juu ya mtu huyu basi kifupi naomba upitie hapa chini nawe waeza kuja nisaidia pale nilipokwama kuhusu mtu huyo ila ukweli ndio huu kwamba historia yake imeanzia hapa Tanzania

Unju bin Unuq (pia: Unju bin Unuku, Unzi Bin Ununuk) ni jina la jitu katika masimulizi ya wakazi wa pwani ya Tanzania. Hadithi zake zasimuliwa kuanzia Bagamoyo hadi Kilwa.

Historia yake inapatikana katika makumbusho ya Kaole huko Bagamoyo.

Moja ya mambo ya ajabu ya mtu huyu ni urefu wake yaani kimo, inasadikiwa alikuwa na urefu mkubwa ulioweza kumfanya atembee baharini na miguu yake kugusa chini.

Pia alikuwa akitembea kutoka nchi hadi nchi kutokana na urefu wake. Inasimuliwa kuwa moja kati ya nyayo zake inapatikana kwenye jiwe alilokanyaga huko Tabora, Tanzania, wayo wa mguu wa kushoto wakati wayo wa mguu wa kulia ulionekana kwenye jiwe alilokanyaga huko Kongo.

Inasimuliwa pia akitaka kula alikuwa akichukua samaki baharini kwa mkono na kuchoma katika jua kisha anakula.

Kuhusu maisha yake inasimuliwa kuwa Unju bin Unuk hakuoa wala kuolewa kutokana na umbo lake.

Sehemu nyingine ya hadithi yake ni alipokufa Unju bin Unuq, aligawanyika vipandevipande kutokana na urefu wake na inasemekana kidole chake chenye urefu wa kilometa moja kasoro ndicho kilichopatikana na kuzikwa pale Bagamoyo, lakini hakuna simulizi mwili wake uliobaki uliangukia wapi.

Unju bin Unuq alikuwa na ndugu yake aliyejulikana kama Geofrey bin Unuk, huyu alipatikana maeneo ya Dodoma. Au kwamba Unuq baada ya kupotea kwa muda wa miaka mingi ndugu zake wa mbali sana wameonekana katika mkoa wa Dodoma.




Asili ya jina la Unju bin Unuq katika Uarabuni na BibliaEdit

Jina lake linatokana na Kiarabu cUdj bin Unuq / ‘Anaq عوج بن عنق anayejulikana katika visa vya nchi nyingi za Uislamu kama jitu kubwa sana. Waislamu walipokea hadithi kutoka kwa Wayahudi anakojulikana kwa jina la Og עוֹג‬.

Asili kabisa ni taarifa za Biblia kuhusu mapigano kati ya Wanaisraeli waliotoka Misri na Ogu mfalme wa Bashani (Hesabu 21,33)[1]; Wanaisraeli walimshinda wakiongozwa na Musa.

Ogu alisemekana kuwa mtu mrefu; Kumbukumbu la Torati 3,11 kinamtaja hivi: "aliyesalia katika mabaki ya Warefai ni Ogu pekee, mfalme wa Bashani; tazama, kitanda chake kilikuwa kitanda cha chuma; kitanda hicho je! Hakiko Raba kwa wana wa Amoni? Urefu wake ulikuwa ni mikono kenda, na upana wake mikono minne, kwa mfano wa mkono wa mtu".

Katika masimulizi ya Wayahudi tabia hii iliendelea kuongezeka; katika Kitabu cha Amosi 2,9 anatajwa (bila kusema jina) kama "Mwamori" "nalimwangamiza Mwamori mbele yao, ambaye urefu wake ulikuwa kama urefu wa mierezi, tena alikuwa na nguvu kama mialoni".

Wataalamu Wayahudi wa baadaye waliona ya kwamba vipimo vya Kumb. 3 kuhusu kitanda chake chenye urefu wa mikono yaani dhiraa 10, sawa na mita 4-5, vilihusu mkono wa hilo jitu lenyewe, hivyo walimwona mkubwa zaidi tena.

Kwenye kitabu Berakhot cha Talmudi Ogu anasimuliwa ya kwamba aliweza kuinua mlima aliotaka kurusha dhidi ya Wanaisraeli, lakini Mungu alimzuia[2]. Katika kitabu cha Nidah katika Talmudi Ogu anasemekana ni mtu aliyeishi kabla ya gharika ya Nuhu akiwa ni mmoja wa hao ambao walitunzwa.[3]


Katika UislamuEdit

Masimulizi ya Kiyahudi yalipokewa na Waislamu na kupanuliwa tena. Ushahidi uko kwa Al Tabari aliyeandika ya kwamba maiti ya cUdj ilikuwa kama daraja juu ya mto Naili.

Al-Thaclabi aliandika ya kwamba cUdj alikuwa na urefu wa dhiraa 23,333 akiweza kunywa kwenye mawingu, kushika ngumi baharini na kuichoma kwenye Jua. Alitembea mbele ya Nuhu wakati wa gharika kuu lakini maji yalifikia magoti yake tu. Aliishi miaka 36,000. Alipoona kambi la Wanaisraeli na Musa alivunja mlima akashika kipande cha kuangamiza kambi lote kwa pigo moja, lakini Mungu alituma ndege waliokula shimo katikati ya mlima uliomuangukia na kumfunga katikati. Hivi Musa aliweza kumshinda kirahisi


Hii ni picha iliopigwa huko Mexico miongo kadhaa nyuma

Asalaam kudo
Duh nashkuru kwa darasa ila kwa upande wangu story ya huyu Unju Bin Unuq nliwahi kusimuliwa kidogo na mtu wa pwani alidai huyu jamaa alikuwa anaishi pwani ya afrika mashariki na ndio aliyemsaidia Nuhu kujenga safina kwa kumletea mbao ngumu kutoka afrika ya kati (DRC ya sasa) maana mashariki ya kati ilikuwa na asili ya jangwa hivyo jamaa alichukua miti huku na kuifanya mbao na kuwapelekea nuhu wajengee safina

Pia wanadai kwakuwa wanadamu walimuona Nuhu kma "mzinguaji" sababu alikuwa anawaambia habari za waache madhambi n.k kila wakitaka kumvamia kumpiga au kumsonga songa basi huyu Unju bin unuq alikuwa anajitokeza kumkingia kifua wengine wote wanakuwa wapole

Simulizi hiyo inaishia pale wakati wa gharika wanadai kwamba kwakuwa yeye alikuwa sio uzao wa asili wa kibinadamu(huenda uzao wa malaika/majini) hivyo asingekuwa msafi kuwepo baada ya gharika hivyo baada ya KUFUNGA mlango wa Safina basi alijua wakati wake wa kufa umefika

Ila advantage aliyopewa ni kwamba hatokufa wakati wa gharika ila alikufa mwanzoni kabisa kabla ya gharika lile kushika kasi.....inadaiwa wakati mvua inaanza yeye aliteleza kwenye ardhi yenye matope tope ukanda huu wa afrika mashariki(wakazi wanadai mtwara) na mwili wake kupigizwa kwenye bahari hivyo mwili wake upo baharini kuendana na simulizi hii na wengine wanadai unyayo wake ambao ulitengeneza kma bonde upo huko mtwara

Naweza kubaliana na kisa hiki kuliko hicho cha wayahudi kinachosema alipona gharika sababu haiingii akilini gharika na maji kujaa siku zaidi ya 120 huyo mtu apone kumbuka kulikuwa na upepo.... Mawimbi.... Radi..... Mavolcano n.k sioni kivp angepona hayo mapito!!! Kingine angekosa chakula lazima sababu bahari ilichafuka angekula wapi?? Mizoga ya wanadamu??

Kuhusu mfalme ogu ni kweli alikuwepo ila sidhani kma ndie huyo huyo mmoja na Uj sababu mfalme ogu alikuwa ni muamori mtoto wa canaan mjukuu wa ham na kitukuu cha Nuhu ila hyu UJ alikuwepo kabla ya gharika hivyo sidhani kma angehusishwa na kabila moja tu

Wajuvi zaidi mtupe story ya LIJIMTU hili la ajabu kuwahi kutokea

Cc Mitha
 
Back
Top Bottom