Dong Jin
JF-Expert Member
- Jun 4, 2018
- 754
- 1,442
Katika kusherehekea siku yake ya kuzaliwa msanii wa muziki wa Bongo Fleva nchini Tanzania, Diamond Platnumz amewaahidi mambo yafuatayo wakazi wa Tandale (mahali alipozaliwa na kukulia)...
1. Kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300,na wakazi wengine 700 (Jumla watu 1000) ndani ya mwaka mmoja....
2. Kutoa mitaji kwa akina mama 200, ya shilingi za kitanzania 100,000/= mpaka 200,000/=
3. Kutoa Boda boda 20 kwa vijana wasio na ajira na kuwatengenezea aina fulani ya menejimenti ambapo kila siku kila kijana itampasa akabidhi sh. 10,000/= ambayo itatumika kununua bodaboda nyingine kwa ajili ya vijana wengine....
4. Kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale ikiwa ni pamoja na kuweka matank kwa ajili ya kuhifadhia maji...
Diamond Platnumz
Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale pamoja na wasanii wenzake, wageni mbalimbali kutoka serikalini na mashirika binafsi waliojitolea kumuunga mkono.
1. Kulipia BIMA ya Afya kwa watoto 300,na wakazi wengine 700 (Jumla watu 1000) ndani ya mwaka mmoja....
2. Kutoa mitaji kwa akina mama 200, ya shilingi za kitanzania 100,000/= mpaka 200,000/=
3. Kutoa Boda boda 20 kwa vijana wasio na ajira na kuwatengenezea aina fulani ya menejimenti ambapo kila siku kila kijana itampasa akabidhi sh. 10,000/= ambayo itatumika kununua bodaboda nyingine kwa ajili ya vijana wengine....
4. Kukarabati Shule zote za msingi zilizopo ndani ya Kata aliyozaliwa ya Tandale ikiwa ni pamoja na kuweka matank kwa ajili ya kuhifadhia maji...
Diamond akiongea kwenye sherehe fupi iliyofanyika Live kupitia Wasafi TV, amesema kuwa siku ya Ijumaa Tarehe 5 Oktoba 2018 atatimiza ahadi hiyo ikiwa na pamoja kuchinja ng’ombe na kusherehekea na watu wake wa Tandale pamoja na wasanii wenzake, wageni mbalimbali kutoka serikalini na mashirika binafsi waliojitolea kumuunga mkono.