Wadau naomba mwenye details kuhusu diamites int. anambie please, ni nin na wanahusika na kazi gan, na malipo yao yakoje, maana nilitumiwa ujumbe niende kwenye majadiliano sinza mori na mim sipo karibu na dar. naomben mnieleweshe wadau mnaofahamu.
hilo tangazo la kazi uliliona kwnye gazeti la udaku au?manake sinza mori makampuni yaliyoko pale ni ya kutembeza mabakuli tu,dawa za mswaki,mabeseni,shtuka mkuu
Teh teh teh!!!! aksante kwa taarifa mkuu, hapo nimepata picha.Hiyo ni GNLD,kuuza dawa vitu kama hizo!jamaa wajanja kwel yaan hicho walichokwambia ni sehemu ya kilefu cha GNLD,so wameona wakikwambia kifupi utaijua na kupotezea!
hilo tangazo la kazi uliliona kwnye gazeti la udaku au?manake sinza mori makampuni yaliyoko pale ni ya kutembeza mabakuli tu,dawa za mswaki,mabeseni,shtuka mkuu
Hakuna kazi hapo,hii ilishawatokea wengi ndugu yangu kwa walioko hapa dar wanajua,yani wanataka utoke mkoani kuja kufanya kazi ya kutembeza vyombo,kama unataka njoo,ila utajutia nauli yako
Hawa jamaa wanachekesha umma...yaani wanafanya kaz ya kubahatisha tu namba za watu na kuwa tumia meseji! Ipo siku watamtumia hata mke wa waziri mkuu...!
hilo tangazo la kazi uliliona kwnye gazeti la udaku au?manake sinza mori makampuni yaliyoko pale ni ya kutembeza mabakuli tu,dawa za mswaki,mabeseni,shtuka mkuu
mimi nilipomaliza chuo niliona tangazo la kazi nadhani lilikua gazeti la udaku mahali pa interview hapo Sinza. kufika pale sikuwaelewa jamaa nikakuta vijana wengi wanafundishwa kama nyimbo na mazoezi mbalimbali ya kujenga team work baadae tukatolewa kwa magroup nikondoka na dada mmoja na wengine watatu wana mizigo ambayo sikujua ni vitu gani.on the way wakawa wananishauri maisha ni popote chamsingi ujipange na kuanza kwa namna yoyote. mara tukaingia get la wizara ya maji pale ubungo koote huko tumetembea kwa mguu. wkaniambia wewe baki hapa getini hujawa mwenyeji watakuzuia kuingia. wao wakachukua baadhi ya mizigo wakaniachia baadhi ya mizigo.walipoenda huko ndani nikaikagua kukuta ni dawa za miswaki, sabuni, na products kibao za alovera. yaani nilivyo kasirika mizigo yao niliacha hapo getini wala sikuaga mtu nikapotea zangu
ioMzee nikwambie kitu hii biashara inawapa wengine hela nyingi sana lakini si kwa kutembeza ila Kila mtu ana akili zake ndio maana utaona wengine wanatembeza mie sijawahi kufundishwa hivyo wala kufanya hivyo.Na mtu yeyote a natakiwa kujiuliza unaweza kutembeza budhaa ukajikimu kimaisha?
io
kitendo cha kutembeza sabuni kwenye mfuko wa rambo kwa kweli kilikua mbali sana na taaluma na uwezo niliojengewa kibiashara ila haya mambo ya ajabu saba yule mzee anayemiliki peacock hotel alikua anaelezea alivyoanza biashara hadi akafika hapo kweli hakuna njia ya mkato kwa matajiri wa ukweli amefanya biashara za ajabu na ndogo mno, hata yule mmiliki wa riverside nasikia kaanzia kushona viatu