Dhana ya kuombewa

Dhana ya kuombewa

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
359,955
Reaction score
828,658
Ni neno la kawaida la kiimani kwa wale waamini na waaminio. Lakini awamu hii ya tano linaelekea kupata umaarufu
Nimejikuta napitia makabrasha mbalimbali ya kidini kuona ni nani wanaopaswa kuombewa na kwanini
.wagonjwa
.yatima
.Wajane
.wenye shida za kiroho
.wenye shida za kimwili
Hawa ndio tmefundishwa kuwaombea kwa imani ya kikristo
Lakini vile vile tuna maombi na sala maalum za kuombea Taifa na viongozi wake wote ...tuna maombi na sala rasmi kila siku ikianza na kila siku ikiisha
Napatwa na ukakasi mkubwa kuendelea kuombwa nimuombee mtu mwenye kila aina ya ulinzi kuanzia wa mitambo mpaka wa majeshi na usalama
Napatwa na mshangao kuendelea kuombwa nimuombee mtu ambaye hajui bajeti yake ya mahitaji ya kila siku kuanzia chakula usafiri ada za watoto shule , mahitaji ya ndugu na jamaa nk nk..vyote hivi anavipata bure na ziada
Hii ni aina fulani ya uchoyo na ubinafsi uliopitiliza...! Hivi yule mgonjwa pale Hospitali ataombewa na nani? Je yule mjane aliyedhulumiwa nyumba na mirathi yake yeye ataombewa na nani?
Nchi imezungukwa na matatizo na shida kila mahali ni vilio na maumivu...maisha magumu hela hakuna kazi hakuna....hawa ndio waombe? Wamuombee asiye na dhiki wala changamoto za maisha yetu haya???jamani mbona mnatuonea na kututia majaribu ni tumkufuru Muumba wetu
Yani kweli kabisa nitoke Muhimbili kumuangalia mgonjwa wangu ninayetakiwa kutafuta pesa ili aweze kutibiwa huku nadaiwa kodi ya nyumba na ada za watoto na mengine mengi...na uchovu wote na changamoto zote hizi halafu niombwe kumuombea mtu ambaye hata nilitaka kuonana naye siwezi? Kweli dunia ina mengi
Uongozi wa nchi ni uongozi wa kisiasa...michezo ya kisiasa inajulikana pote duniani ni michafu tena huku Africa ndio kabisa...kumhusisha Mungu kwenye mambo ya kisiasa ni kumdhihaki
Mtu Hapaswi kuwa na wasiwasi...kama una imani kwa Mungu wako na utendalo ni sahihi hata Mungu anajua , hupaswi kuwa na wasiwasi kwakuwa yeye hachagui wala habagui...na ukitenda kwa haki mkono wake utakuepusha na mabaya yote na malaika mlinzi atakuwa nawe bila hata maombi ya mzinifu, muongo, mtenda dhambi zote....
 
Uuuuwi, mkuu naona umeamua kuwachana... Wanataka kuombewa ili waendelee kupiga hela zetu na kufanya michezo michafu..
Hawa labda tuwarogee sio kuwaombea...
1469908389102.jpg
1469908397041.jpg
Kama taifa na kama binadamu tunapaswa kuombeana wote...tukiwaombea hao wenye maisha bora tayari na kila kitu tunawaombea ili iweje? Je hawa wenye mahitaji ya kweli ya maombi tunawaweka kwenye nafasi gani? Tupunguze ubinafsi na kujiona sisi ni bora kuliko wengine
1469908550948.jpg
1469908559551.jpg
 
Kumuombea asiyetenda haki ni sawa na kupaka upepo rangi, bora kuiombea familia yako ipate mkate wa kila cku, mtu hajui atakula nini kesho, akiugua hajui ka atapata huduma bora badala ajiombee mwenyewe anahangaika na mwenyewe ulinzi twenty four seven. Yesu aliwaambia wanawake wasimlilie yeye walilie shida zao na watoto wao. At the end kila MTU ataubeba msalaba wake.
 
Naam hakuna mtu ambaye yuko tayari kumuombea mtu katili, mwenye roho mbaya, mbaguzi, asiyejali maslahi ya nchi na wananchi wa nchi husika na ambaye kauli zake kila kukicha ni za vitisho tu dhidi ya wananchi wa nchi husika. Mtu anayejiona kama Mungu kwa kulewa madaraka.

Kumuombea asiyetenda haki ni sawa na kupaka upepo rangi, bora kuiombea familia yako ipate mkate wa kila cku, mtu hajui atakula nini kesho, akiugua hajui ka atapata huduma bora badala ajiombee mwenyewe anahangaika na mwenyewe ulinzi twenty four seven. Yesu aliwaambia wanawake wasimlilie yeye walilie shida zao na watoto wao. At the end kila MTU ataubeba msalaba wake.
 
Kuna sala huwa naona ni kufuru kwa Mungu.
Hivi fisadi anayekula hela za madawati ya masikini anaanzaje kuimba wimbo wa taifa? Tena kwa ujasiri anaanza Mungu Ibariki Tanzania?
 
Mkuu maombi hubadilisha mtu. Ukiona anaomba kuombewa ujue anajijua kuwa hayuko sawa hivyo anaomba aombewe roho chafu imtoke. Omba tu mkuu ili Mungu aone cha kumchanya .
Hana maana hii...huu ni ukweli mkavu
 
  • Thanks
Reactions: J C
Ni neno la kawaida la kiimani kwa wale waamini na waaminio. Lakini awamu hii ya tano linaelekea kupata umaarufu
Nimejikuta napitia makabrasha mbalimbali ya kidini kuona ni nani wanaopaswa kuombewa na kwanini
.wagonjwa
.yatima
.Wajane
.wenye shida za kiroho
.wenye shida za kimwili
Hawa ndio tmefundishwa kuwaombea kwa imani ya kikristo
Lakini vile vile tuna maombi na sala maalum za kuombea Taifa na viongozi wake wote ...tuna maombi na sala rasmi kila siku ikianza na kila siku ikiisha
Napatwa na ukakasi mkubwa kuendelea kuombwa nimuombee mtu mwenye kila aina ya ulinzi kuanzia wa mitambo mpaka wa majeshi na usalama
Napatwa na mshangao kuendelea kuombwa nimuombee mtu ambaye hajui bajeti yake ya mahitaji ya kila siku kuanzia chakula usafiri ada za watoto shule , mahitaji ya ndugu na jamaa nk nk..vyote hivi anavipata bure na ziada
Hii ni aina fulani ya uchoyo na ubinafsi uliopitiliza...! Hivi yule mgonjwa pale Hospitali ataombewa na nani? Je yule mjane aliyedhulumiwa nyumba na mirathi yake yeye ataombewa na nani?
Nchi imezungukwa na matatizo na shida kila mahali ni vilio na maumivu...maisha magumu hela hakuna kazi hakuna....hawa ndio waombe? Wamuombee asiye na dhiki wala changamoto za maisha yetu haya???jamani mbona mnatuonea na kututia majaribu ni tumkufuru Muumba wetu
Yani kweli kabisa nitoke Muhimbili kumuangalia mgonjwa wangu ninayetakiwa kutafuta pesa ili aweze kutibiwa huku nadaiwa kodi ya nyumba na ada za watoto na mengine mengi...na uchovu wote na changamoto zote hizi halafu niombwe kumuombea mtu ambaye hata nilitaka kuonana naye siwezi? Kweli dunia ina mengi
Uongozi wa nchi ni uongozi wa kisiasa...michezo ya kisiasa inajulikana pote duniani ni michafu tena huku Africa ndio kabisa...kumhusisha Mungu kwenye mambo ya kisiasa ni kumdhihaki
Mtu Hapaswi kuwa na wasiwasi...kama una imani kwa Mungu wako na utendalo ni sahihi hata Mungu anajua , hupaswi kuwa na wasiwasi kwakuwa yeye hachagui wala habagui...na ukitenda kwa haki mkono wake utakuepusha na mabaya yote na malaika mlinzi atakuwa nawe bila hata maombi ya mzinifu, muongo, mtenda dhambi zote....
Umeongea point moja ya maana sana ivi kweli unamuombea mfalme badala ya kumuombea maskini anayelala bara barani apate tahafifu ya mwenyezi mungu inashangaza
 
Naam hakuna mtu ambaye yuko tayari kumuombea mtu katili, mwenye roho mbaya, mbaguzi, asiyejali maslahi ya nchi na wananchi wa nchi husika na ambaye kauli zake kila kukicha ni za vitisho tu dhidi ya wananchi wa nchi husika. Mtu anayejiona kama Mungu kwa kulewa madaraka.
Mkuu Mungu afanya mambo principally, ukimwombea dikteta siyo kwamba unamwombea neema kimsingi ukiomba Mungu amlipe NEEMA kinachofanyika Mungu anamlipa kadri ya anachostahili usingae anapigwa na mabaraha, au Mungu akaamua kuumpa hekima iwapo ata shupaza shingo..

Rejea farao, na mhukumu wa Yesu pilato alipo shupaza shingo na kuwauwa mitume shingo lilivunjika.

Hivyo si mwanadamu mpaka umpe rushwa ukitenda uovu usizigeuza njia zako utaangamia tu.
 
hana tofauti na yule mchungaji wa south africa anayewalisha nyasi watumishi wake ngozi nyeusi tunatabu sana huu utindio wetu wa ubongo siye ng'ombe sijui tutapona lini Mungu atusamehe.
 
Halafu ni wachafu wazandiki waongo. ..mdomo mmoja unaomba kuombewa mdomo wa pili unatoa vitisho kuwa wewe hujaribiri
Mkuu ukiijua hekima ya Mungu ni raha sana, pilato alipshupaza shingo yake ilivunjika, ghadafi pia hivyo akawaita wana Mungu mende na mipanya akashupaza shingo Mungu akalivunja, farao na uzao wake kwasababu mioyo yao migumu Mungu aliwafanya ushuhuda kwa wanawaisraeli kwa kuwaangamiza, jamani Mungu wetu si mnafiki ata kidogo, anayo neema ya kumsamehe anaye kana moyo wake na kumridia ila atakaye shupaza shingo litavunjika.
 
Wenye Afya Hawahitaj Daktari Bali Wale Walio Wagonjwa.Yesu Hakuja Duniani Kwa Ajili Ya Walio Watakatifu.Bali Alikuja Duniani Kwa Ajili Ya Wote Wenye Dhambi i.e Wezi, Waongo, Wafiraji, Wasagaji, Wauaji, Wasengenyaji, Wenye Choyo, Wenye Wivu, Wala Rushwa, Nakadharika Ili Wapate Kutubu.Kwahiyo Ni Wajibu Wetu Kuzidi Kuwaombea Watu Hawa Ili Waziache Njia Zao Zilizo Mbaya.Kondoo Mmoja Aliepotea Ni Bora Kuliko Kondoo Tisini Na Tisa Walio Kundini.
 
Back
Top Bottom