Dhana ya kumwangalia mtu machoni

Dhana ya kumwangalia mtu machoni

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,888
Reaction score
831,218
Kuna jambo wana usalama wanafunzwa wanapokuwa mafunzoni ..uwezo wa kumwangalia mtu machoni...hii humfanya mtu anayeangaliwa kukosa ujasiri na kudondosha macho yake ama kuangalia pembeni.

Usifanye hilo kosa kabisa ukiruhusu kukwepesha macho yako umekwisha..hutapata ujasiri wa kimwangalia tena yule mnayeangaliana naye na hapo ndio atacheza na wewe atakavyo.

Macho huongea ukweli wa ndani..uhalisia wa vile ulivyo ama kile ulichokifanya...mara nyingi jambo jema hukupa ujasiri wa kuangalia bila kupepesa macho na jambo baya hukuondolea ujasiri wote na kuhisi unaonwa uovu wako wote.

Siku hizi kwenye makampuni makubwa kama ya simu nk kuna vyumba maalum vya mahojiano ya watuhumiwa wa makosa kazini...smart rooms..vyumba hivi ukituhumiwa unaingizwa hapo pekeyako na kufungiwa na kuanza kuhojiwa kupitia vipaza sauti na watu usiowaona lakini wao walikuona kupitia camera zilizofungwa kwenye hicho chumba. Daima watuhumiwa hufeli mahojiano kwakuwa chumba hurekodi movements na gesture zako zote kwa kila swali...

Kwenye mazingira ya kawaida kabisa mitaani mtu anapo win confidence yako umekwisha...atakuendesha atakavyo. Kuna swali watu wengi wanajiuliza juu ya ukimya mkuu vyombo vya usalama kwa wapinzani kipindi hiki...jamani hiki si ndio kilikuwa kilio chetu?
Sana sana ni ukimya wa CCM ..hawa wamepoteza ujasiri kabisa na kosa kubwaw la kwanza lilikuwa pale airport siku Lissu anatua akiwa na ujasiri wa ajabu mno.

Kwa miaka mitano nchi ilisimamiwa na sauti moja tu ..hakuna waziri wala mbunge aliyejaribu kusema kitu kuzidi sauti kuu ..mwisho wa siku wakawa kama wote wamepigwa ganzi.

Leo hii zinaposikika sauti za wapinzani wote wanaogopa kuzijibu kwa yale mazoea ya kusubiri ruhusa ama sauti kuu iseme..hata vile vitengo vya propaganda vipo kimya kabisa...wanashindwa kulianzisha...wanasubiri maagizo.

Kikubwa kwenye hili ni ile dhana ya ujasiri wa macho na kuhukumiwa na roho kwakuwa kila sauti ya wapinzani ikipaa inabeba ujumbe uliojaa ukweli na uhalisia..kitu kama hicho utaanzaje kukipinga kwa mfano.

Ganzi ya airport inazidi kushika kazi..tumetoka kwenye semi paralysis tunaelekea kwenye total paralysis..hata vyombo vya usalama vinauona uhalisia sasa...kwamba kumbe kile walichoaminishwa kuwa upinzani ni vurugu kumbe sio kweli kabisa.

Nina mashaka huko tuendako vyombo vinaweza kukengeuka maagizo na kufanya kinyume kama wajumbe walivyofanya. Macho huongea uhalisia wetu.

Macho husuta.

Macho hutuondolea ujasiri kama sisi ni watuhumiwa wa mambo mabaya...!!!

Na macho yakikuhukumu uso husawajika na sauti yako hupotea.

Ukimya wao umejaa maumivu mengi..!!!
 
Siku hizi kwenye makampuni makubwa kama ya simu nk kuna vyumba maalum vya mahojiano ya watuhumiwa wa makosa kazini...smart rooms..vyumba hivi ukituhumiwa unaingizwa hapo pekeyako na kufungiwa na kuanza kuhojiwa kupitia vipaza sauti na watu usiowaona lakini wao walikuona kupitia camera zilizofungwa kwenye hicho chumba
demeanour says it all!
asante sana Mshana Jr. Uko vizuri sana!

soma hii:
In assessing her demeanour, the trial court was impressed by PW1 as honest and truthful witness. In cross examination, the witness did not shake. She was consistent that she only recognised the second appellant as one among those who killed the deceased. She also identified him in the identification parade.

In the circumstances, we are satisfied that the second appellant was positively identified. For that reason, we are constrained to concur with the trial court and Mr. Kiria, learned Principal State Attorney that the quality of the identification was impeccable, and was not shaken by the second appellant's defence.
 
demeanour says it all!
asante sana Mshana Jr. Uko vizuri sana!

soma hii:
In assessing her demeanour, the trial court was impressed by PW1 as honest and truthful witness. In cross examination, the witness did not shake. She was consistent that she only recognised the second appellant as one among those who killed the deceased. She also identified him in the identification parade. In the circumstances, we are satisfied that the second appellant was positively identified. For that reason, we are constrained to concur with the trial court and Mr. Kiria, learned Principal State Attorney that the quality of the identification was impeccable, and was not shaken by the second appellant's defence.
nimeongeza maarifa kaka mkubwa
 
Philosophical mind yako ni below intellectuality ya kuelewa andiko la Mshana Jr!
Nijijibu tena, , kuhusisha kutazamana macho na siasa za uchaguzi Tz kipindi hiki cha kampeni ndio upuuzi wenyewe.
Mnajikutaga wereevu, kumbe mandezi tu, hamjifunzi mlundikano wa watu sio kura. Subiri iyo October
 
Hivi umekula maharage ya wapi wewe? Umeanza vizuri umemaliza pumba. Lis alishajimaliza mwenyewe, sisi ni akili kubwa tulishapiga hesabu zetu, si umeona anahamasisha uvunjifu wa amani?

Mwache aendelee tu then mwisho wa siku mwenyewe atajikaanga kwa wese lake mpaka aive, zisi is Tz nchi inayoongozwa na wenye akili kubwa mpaka mabeberu wanakosa pa kupitia ili kutuvuruga. Hata Znz tuko bomba Mwinyi ndiyo chaguo la wazenj
 
Nijijibu tena, , kuhusisha kutazamana macho na siasa za uchaguzi Tz kipindi hiki cha kampeni ndio upuuzi wenyewe.
Mnajikutaga wereevu, kumbe mandezi tu, hamjifunzi mlundikano wa watu sio kura. Subiri iyo October

Mshana Jr uelewa mdogo wa siasa za tz
 
He he! Mtu mmepewa nafasi lkn bado mnasema hivi mara vile!!.. tatizo mlizoea kufanya siasa za kujibiwajibiwa tu Sasa sahivi wameamua kukakaa kimya ati mnaona chichiemu inaenda kuzimu!!

Mmesahau maji yaliyotulia ndio huwa yanazamisha? Kuangalia usoni na kukwepesha macho si kigezo Cha kushindwa kwani kiletacho ushindi si macho bali mbinu.. something must kick your head.
 
Back
Top Bottom