Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

Dhana dhanifu juu ya kutekwa Mo Dewji

Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi.

Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa

Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.

Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake

Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake.

Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia.

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je, watekaji wanataka nini kwake?

Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea.

Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina.

Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karibu kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!

Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka sasa kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa
Umesema vzr
 
Kama watekaji wangetaka kumteka mo, wangemteka akiwa anatoka nyumbani, na sio huku gym ambapo watu wengi wanaona.

Pili, watekaju huwa hawateki matajiri, kwani tajiri hana pesa mkononi, na pia inakuwa ngumu kumshinikiza atoe pesa kutokana uchunguzi wake huwa mkubwa mno. Wangemteka mwanaae hapo sawaa.

Mo kaingia kwenye muvi ya kishamba sana, kajiharibia credibility. Urafiki na bashite utampunguzia heshima.
Kwahyo mkuu hapa tumechezewa masinema ya nguvu wana nchi. Ila Tundu lissu alishutiwa hadharani, ujue watekaji huwa na agenda
 
Katika serikali zilizotangulia maskini alikuwa anaweza kufanywa chochote na tajiri mfano kumpiga, kumfunga au kumdhalilisha kwa namna yoyote.

Lakini katika serikali yangu ni tofauti, Tajiri anaweza KUFANYWA CHOCHOTE, akileta za kuleta.
 
Naunga mkono uchambuzi
Kwa kuongezea tu najiuliza Suppose I was the perpetrator na ni mzungu au mzungu in disguise!?!?
1-Abduction imetokea saa kumi na moja, police response yao ni kama ya masaa matatu late.
Hivyo ni rahisi ku execute exit plan yangu bila usumbufu.
2-Wameweka road barriers kwa ajili ya ukaguzi na wamesema hawato ruhusu gari ipite bila kukaguliwa.
Me thinking like a criminal kiukweli kwa kua ni mzungu na eneo ni karibu na fukwe it's obvious jamaa nimemuweka kwenye container na yupo kwenye shipping line yeyote ile kwa sasa in the deep sea far from land.
3-Kama perpetrator nategemea nini?
Kiukweli sitegemei matamko ya RPC au Bashite na Mikwara mingine.
Nategemea jamaa waseme okay mmemteka MO what's your demand.
Simple.
4-Kwakua polisi wamekua fooled na ID inawezekana kabisa mimi mtekaji ni mbongo na as we speak tupo Kenya.
Kwa V8 ni mwendo wa saa nne kutoka eneo la tukio mpaka boda.
It's obvious na weza kua nje ya nchi by now.
Je ukiacha Mikwara kuna effort yeyote ile ya kimawasiliano na wenzao Kenya?
5- Mnaweza mkawa mnahangaika kutafuta mbali kumbe nipo less than kilometer kutoka eneo la tukio.
Somewhere kwenye basement nobody knows about.

Sifundishi mtu kazi lakini sometimes police lazima wajiulize wao ndio wangekua watekaji wangefanya nini ili polisi wapate ugumu kuwa trace.

If you want to catch a criminal, you have to think like a criminal.
Nashauri hao wanasiasa wapigwe stop, police wafanye kazi yao.

Sometimes perpetrators wanaweza kua na demand zao, lakini wakati huo huo hawana cha kupoteza wakimzuru hostage.

So ni vizuri hii operation ifanyike kwa uangalifu mkubwa hao wapenda kamera watoswe, hii kitu itaambatana na consequences nyingi.
Natumaini yupo okay mpaka sasa,na jeshi letu litampata yeye na hao jamaa wasiojulikana.
 
na hawezi kutoa izo videos maana itaathiri uhusiano wa ki diplomasia
by the way walijuaje ni wazungu wakati mashuuda wadai watekaji walvalia kininja?
avatar yako tu hiyo,dah!this is my rifle and this is my gun!... movie nzuri sana...back to the topic...kinachoendelea hapa kwenye sakata la kuteka ni kama sinema...inabidi wasakwe Na wapelekewe moto
 
Shikamoo Kaka Mshana Jr,sina la kuchangia ila nilikua nauliza kama una jero hapo nikanunue ugoro Tandale.
"Wazungu wasiojulikana wametoka wapi tena jamani!!!"
 
Naunga mkono uchambuzi
Kwa kuongezea tu najiuliza Suppose I was the perpetrator na ni mzungu au mzungu in disguise!?!?
1-Abduction imetokea saa kumi na moja, police response yao ni kama ya masaa matatu late.
Hivyo ni rahisi ku execute exit plan yangu bila usumbufu.
2-Wameweka road barriers kwa ajili ya ukaguzi na wamesema hawato ruhusu gari ipite bila kukaguliwa.
Me thinking like a criminal kiukweli kwa kua ni mzungu na eneo ni karibu na fukwe it's obvious jamaa nimemuweka kwenye container na yupo kwenye shipping line yeyote ile kwa sasa in the deep sea far from land.
3-Kama perpetrator nategemea nini?
Kiukweli sitegemei matamko ya RPC au Bashite na Mikwara mingine.
Nategemea jamaa waseme okay mmemteka MO what's your demand.
Simple.
4-Kwakua polisi wamekua fooled na ID inawezekana kabisa mimi mtekaji ni mbongo na as we speak tupo Kenya.
Kwa V8 ni mwendo wa saa nne kutoka eneo la tukio mpaka boda.
It's obvious na weza kua nje ya nchi by now.
Je ukiacha Mikwara kuna effort yeyote ile ya kimawasiliano na wenzao Kenya?
5- Mnaweza mkawa mnahangaika kutafuta mbali kumbe nipo less than kilometer kutoka eneo la tukio.
Somewhere kwenye basement nobody knows about.

Sifundishi mtu kazi lakini sometimes police lazima wajiulize wao ndio wangekua watekaji wangefanya nini ili polisi wapate ugumu kuwa trace.

If you want to catch a criminal, you have to think like a criminal.
Nashauri hao wanasiasa wapigwe stop, police wafanye kazi yao.

Sometimes perpetrators wanaweza kua na demand zao, lakini wakati huo huo hawana cha kupoteza wakimzuru hostage.

So ni vizuri hii operation ifanyike kwa uangalifu mkubwa hao wapenda kamera watoswe, hii kitu itaambatana na consequences nyingi.
Natumaini yupo okay mpaka sasa,na jeshi letu litampata yeye na hao jamaa wasiojulikana.
#5 kwa kua ni wazungu ( km walivyosema /,kuripotiwa na media ) inawezekana point yako hii #5 ,jamaa wako huko huko masaki /oysterbay ambako hao so called wazungu wanaishi sana na ni wengi
 
Moderator huu ni uchambuzi wa viashiria mbalimbali na uhalisia wa tukio baada ya Mo kutekwa hivyo naomba msiunganishe huu uzi na zile nyingine zinazoripoti

Habari huanza kama tetesi ama uvumi hilo limekwisha fanyika
Baada ya tetesi ama uvumi kuthibitika ni kweli habari husika hukoma kuwa tetesi ama uvumi.

Kinachofuata baada ya hapo ni breaking news hapa kila mtu huongea lake la masikitiko la majonzi la huruma nknk....tuko kwenye hatua hii kwa sasa

Vumbi likishatulia ndio uchambuzi huanza..na sasa ni muda wa uchambuzi na sio tetesi wala breaking news tena!

MO KATEKWA! ndio habari kubwa kwa asubuhi hii ya tarehe 11.October.2018
Kila tuko linalotokea huwa na mlolongo huu
Wazo
Sababu
Mchoro/mpango
Muda
Wahusika
Vitendea kazi
Bajeti
Uchaguzi wa eneo la tukio
Nani afanye nini nknk

Matukio ya utekaji huambatana na
Visasi
Fidia
Vita ya kibiashara
Mambo ya kisiasa
Mapenzi na mahusiano...nknk

Kutekwa si jambo geni masikioni mwetu ,wengi walishatekwa ....wachache wkapatikana wakiwa hai na wengine wafu....wengine hawakupatikana tena.

Kwanini MO?
Huyu si mtu mdogo ni mfanyabiashara mkubwa mwenye mafanikio mengi...amewahi kuingia kwenye kumi bora na ishirini bora za matajiri vijana duniani, Afrika na hata katika mgawanyo wa kikanda... Kumteka huyu maandalizi yake si ya kitoto
Wiki moja Kabla nilimuona akifanya mahojiano na mwandishi mmoja ..sikumbuki ni kituo gani cha luninga ...lakini katika mahojiano yale alitaja mafanikio yake mengi na pia kuelezea ratiba yake ya siku nzima na wiki pia
Kwa maneno yake mwenyewe hii ndio ratiba yake

Anafika ofisini saa 12 asubuhi na kuanza kusoma na kujibu emails mpaka saa mbili asubuhi
Baada ya hapo hujipanga kuingia kwenye vikao vya bodi mbalimbali kuhusiana na makampuni yake.

Akimaliza kwenye saa sita nadhani hupata wasaa wa kupitia magazeti mbalimbi,kupumzika na ikifika saa nane HUENDA GYM kupata lunch na baadae kurudi ofsini mpaka usiku...weekend hukutana na marafiki na hupata muda wa kuwa na familia pia.

Leo alfajiri katekwa akienda/akitoka gym! Ni wazi kwenye yale mahojiano alidanganya kuwa anaendaga gym mchana...hii haina shida ni mbinu shirikishi ya kujilinda

Je, watekaji wanataka nini kwake?

Ni wazi hawana nia ya kumdhuru la sivyo wangeshamaliza mchezo pale pale walipomtekea.

Kwa jicho la haraka hawa wanataka fidia (ransom )na kama hili likithibitika basi tutakuwa tumeingia kwenye zama mpya mbaya sana kiuchumi na swala zima la uwekezaji....

Je kwasasa yuko wapi?
Its a million dollar question...lakini watekaji ni watu waliojiandaa hasa...eneo walilomtekea lina ulinzi wa kampuni binafsi ya ulinzi yenye vifaa vya uhakika lakini pia kuna CCTV CAMERAS...hivyo basi walijua wanachokifanya na hata kuruhusu waonekane kama ni wazungu ni cover up nyingine...siku hizi kuna vinyago vya kila aina.

Kiinteligensia Dar ni padogo sana na eneo letu la bahari liko huru mno...ni rahisi mno kutega speed boat ufukweni maeneo ya Coco na kuondoka na mtu salama salimini...

Neno la Makonda
Kwa kawaida baada ya mtu kutekwa watu husubiri masaa24 kusikia watekaji watasema nini...kipindi hiki cha mpito mamlaka husika hukaa kimya kabisa zikifuatilia kwa Karibu kila taarifa...sanasana zitatoa tu taarifa kuthibitisha tetesi...huwa hazikurupuki kupayuka!

Ndugu yetu huyu kwa nafasi yake ya mkuu wa mkoa kasema WALE WAZUNGU NI WAGENI!
Kajuaje kama ni wazungu kweli
Kajuaje kama ni wageni!?
Ana taarifa zao?
Wamekamatwa?
Kwa kupayuka huku mtu anaweza kuharibu kila kitu ama kugeuka na kuwa chanzo cha habari na kuacha mashaka mengi.....

Mpaka sasa kinachosemwa ni Mo katekwa na majambazi...lakini bado hatuna hakika kwa asilimia zote ninini hasa kimetokea....wakati tukiendelea na huu mjadala tuwe makini na kauli zetu,tusije tukajikuta ni sehemu ya ushahidi..

Tumuombee...tuiombee familia yake ndugu jamaa na marafiki katika kipindi hiki kigumu cha sintofahamu kubwa

Alihojiwa na Spora katika kipindi cha Spora show kinachorusha na Star tv .
 
Back
Top Bottom