Derick Gaspar Mkandala Lufufu afariki dunia

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Nimepokea habari hizi kutoka kwa msanii wa kuitwa Nash Mc, ameandika kwenye ukurasa wake wa FaceBook, sina shaka na habari yake kama na yeye hajasikia hewani hewani.

Kapteni Derick Mukandala Lufufu, Nimekuwa nikikuzingumzia mara nyingi sana kwa jinsi navyokubali umahiri wako pale unaposimulia na kutafsiri kwa Kiswahili picha za Ulaya na Marekani bila kusahau Wahindi,lakini muda si mrefu nimepokea taarifa za kifo chako na nimebaki sina la kufanya zaidi ya kusema,KAZI YAKE MOLA HAINA MAKOSA. Sina mengi ya kuongea kwani nimefanya watu waijue hata sura yako kupitia mitandao ya kijamii huo ni mchango wangu kwako.
M.A.P LUFUFU.

attachment.php


=========

Tumepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mkandala Rufufu aliyejipatia umaarufu mkubwa kwa kutafsiri filamu za lugha mbalimbali kiingereza, kihindi, kichina, na hata wakati mwingine kifilipino yote aliyafanya kwenda katika lugha mama ya kiswahili, tutamisi zile mbwembwe, fix, uwongo uwongo wenye maana, mikogo ya sauti al-muradi kunogesha sikio la mtazamaji.

Rufufu amefariki dunia jana usiku wakati akitoka nyumbani kwake kuelekea harusini ambapo kwa mujibu wa wasimuliaji wanasema kuwa presha ilimpanda ghafla akaanguka na watu waliokuwa karibu naye walimkimbiza hospitalini na kabla hajapata matibabu akawa tayari amefariki dunia.

Dah tulifaidi sana tafsiri za filamu ulizokuwa unafanya hasa tuwapo safarini Tz ndani ndani, (wilayani, vijijini, mkoa kwa mkoa).

Tunamwomba Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu Rufufu mahala pema peponi.

Amin!

Chanzo: MKALIMANI MAARUFU WA FILAMU NCHINI 'RUFUFU' AFARIKI DUNIA. ~ g sengo

 

Attachments

  • lufufu.png
    lufufu.png
    115.9 KB · Views: 8,147
Alikuwa anafanya shughuli gani? naona bila shaka sikuwa ktk ulimwengu wake!Simjui na ndo namsikia leo!
R.I.P.
 
Alikuwa anafanya shughuli gani? naona bila shaka sikuwa ktk ulimwengu wake!Simjui na ndo namsikia leo!
R.I.P.
Nyinyi watoto wa kishua amuwezi kumjua huyu mpk akupe KANYAMAZONGO wewe waulizeni watoto poli wa kitaa anod la jini km sio anod na mtoto jeni wapi dame na boloyanki kama hujaona picha mniga analiwa na mamba wewe siyo mjanja enzi hizo picha moja tsh 30 2 sh 50 adui na MZEE ASHANT araf limetafsliwa sasa na KAPTEN DERICK LUFUFU MKANDALA

LU
FU
FU
 
Alikuwa anafanya shughuli gani? naona bila shaka sikuwa ktk ulimwengu wake!Simjui na ndo namsikia leo!
R.I.P.

jamaa alikua amejiajiri mwenyewe,alikuwa akitafsiri movies na filamu za kizungu na kiarabu kwa lugha ya kiswahili na kufanya watu wengi waelewe main theme ya hiyo movie au filamu.Jamaa alikuwa na kawaida ya kuweka vionjo kadhaa vya maneno ili kunogesha hyo mambo.Kazi zake zilikua au zinapendwa sana uswahilini kwenye yale mabanda ya kuonyeshea video 'Vibanda Umiza'.Nimeanza kumfatilia Lufufu tangu nikiwa nasoma Sekondari miaka ya 1990
 
Nyinyi watoto wa kishua amuwezi kumjua huyu mpk akupe KANYAMAZONGO wewe waulizeni watoto poli wa kitaa anod la jini km sio anod na mtoto jeni wapi dame na boloyanki kama hujaona picha mniga analiwa na mamba wewe siyo mjanja enzi hizo picha moja tsh 30 2 sh 50 adui na MZEE ASHANT araf limetafsliwa sasa na KAPTEN DERICK LUFUFU MKANDALA

LU
FU
FU

hiyo movie ya mniga analiwa na mamba nilipoisoma mpaka mwili umenisisimka mdau Mzimu wa Kolelo umenikumbusha wakat nasoma primary school enzi hizo kulikua na programu ya sinema za bure ikiendeshwa na shirika la bima la taifa (NIC) KWENYE OPEN GROUNDS,kwanza mnawekewa sinema za faida ya shirika la bima,kisha mwisho mnawekewa hiyo ngoma ya 'MAKOMANDOO SITA'.
Daaaah zamani sana kwakweli
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom