Derby ya Azam vs Young African ndio mechi yenye burudani zaidi kwa Tanzania

Smt016

JF-Expert Member
Jan 11, 2016
2,286
3,018
Habari wanamichezo, ikiwa siku kadhaa zimesalia kuelekea ufunguzi wa pazia jipya la ligi kuu Tanzania bara. Ikiwa ni mechi ya vigogo wanne waliobora kwa Tanzania hapa nazungumzia Yanga, Simba, Singida na Azam. Hawa ndio waliong'ara katika ligi na katika Azam Federation cup kwa wao kuwa top 4 kote kote.

Kwasasa kwa Tanzania, kwa maoni yangu hakuna mechi tamu yenye burudani kama Azam wakikutana na Yanga, ni wazi ukiachana na matokeo ya uwanjani watazamaji kwanzia uwanjani hadi kwenye luninga huwa wanarifhika ela zao walizotoa kwa kushuhudia kandanda safi, ufundi na mbinu safi inayopelekea kuwe na soka tamu kabisa uwanjani.

Wiki ijao bila shaka tunaenda kuonana radha zaidi ya tuliyoiona hapo kabla, kwasababu kila upande una watu haswa na benchi ni jipya kwa kila upande. Hivyo kama kawaida tutashuhudia mpira usiokuwa wa papatu papatu wala kukamiana bali tunaenda kuona mpira wa kitabuni, mpira wa kasi na ufundi na ni mechi inayoongeza hisia zaidi hasa baada ya Feisal na Bangala kuongeza kitu kwa upande wa Azam wakitokea Yanga.

Weka utabiri wako hapa kutokana na vikosi vya timu zote mbili je ni timu ipi itavuka kucheza fainali ya ngao ya jamii?
 
Kwasasa kwa Tanzania, kwa maoni yangu hakuna mechi tamu yenye burudani kama Azam wakikutana na Yanga, ni wazi ukiachana na matokeo ya uwanjani watazamaji kwanzia uwanjani hadi kwenye luninga huwa wanarifhika ela zao walizotoa kwa kushuhudia kandanda safi, ufundi na mbinu safi inayopelekea kuwe na soka tamu kabisa uwanjani.

 
Ratiba ya kwanza ilikuwa ni Simba na Azzam, Mara tuna kuja kuambiwa ni Yanga na Azzam.

Halafu sijui nchi gani nyingine ngao ya Jamii inagombewa na timu 4?
Naamini akichaguliwa rais mpya wa TFF, ataufuta huu upuuzi wa Karia mara moja.

Na ukimuuliza sababu za hatua zote za hayo mashindano kufanyikia kwenye uwanja mbovu wa Mkwakwani, sidhani kama atakuwa na majibu sahihi.
 
Naamini akichaguliwa rais mpya wa TFF, ataufuta huu upuuzi wa Karia mara moja.

Na ukimuuliza sababu za hatua zote za hayo mashindano kufanyikia kwenye uwanja mbovu wa Mkwakwani, sidhani kama atakuwa na majibu sahihi.
Kuna sababu zipi za kutochezwa Mwanza ambako hawana timu ya ligi kuu?

Tanga imechezwa fainali ya FA juzi, na sasa ngao ya jamii Tanga tena, imekuwa kama Magufuli na Chato yake.
 
Sema waTz bana,
Jamaa kaweka mada safi, bila mihemuko wala kuegemea upande wowote, ila sasa wachangiaji 😂😂
Unagundua watu wengi hawana akili,

Btw, .hio match na mimi naiona ni match bora zaidi Bongo,
Match mbovu ni Simba na Yanga, ni full kukamiana bila ufundi wowote ule
 
Sema waTz bana,
Jamaa kaweka mada safi, bila mihemuko wala kuegemea upande wowote, ila sasa wachangiaji 😂😂
Unagundua watu wengi hawana akili,

Btw, .hio match na mimi naiona ni match bora zaidi Bongo,
Match mbovu ni Simba na Yanga, ni full kukamiana bila ufundi wowote ule
Uzi uliwalenga wapenzi wa mpira wa miguu, ila kwa bahati mbaya wachangiaji waliokuja kuchangia ni lile kundi la wapenzi wa timu.
 
Azamu ni mdebwedo kwa Yanga, Fanya kuangalia mechi za 2022/23. Azamu ikicheza na Simba & Azamu vs Yanga utaona tofauti. Ili azamu iwe na mafanikio iachane na usimba na uyanga.
 
Back
Top Bottom