msani
JF-Expert Member
- Jun 13, 2011
- 1,801
- 1,191
Ndugu zanguni,nimekuwa kwenye facebook takribani miaka 2 sasa na imekuwa nzuri kwangu kwani imenifanya kukutana na baadhi marafiki zangu ambao tulipotezana kwa muda wa miaka mingi hasa wa shule ya msingi. Pia nimebahatika kufahamiana na watu wengi sana na kuwa nao karibu utadhani tulifahamiana hapo awali kabla ya facebook. Nilitokea kukutana na dada mmoja ambaye tulikuwa karibu sana naye,tulishirkiana katika mambo mengi na kiasi kwamba marafiki zangu walijua kila kitu baina yetu,ilifika hatua tukaamua kwamba tunaweza kufunga ndoa,lakini takribani mwezi haji kunitembelea kama ilivyokuwa awali na pia tulipenda sana kuchat kwenye facebook hasa usiku,baadaye alianza kubadilika hadi ikafikia tuko hewani lakini akatumia saa 1 kujibu meseji yangu,suala hilo likanichanganya nikaamua kufungua akaunti nyingine nikatuma friend request naye akakubali tukawa tunawasiliana naye vizuri sana,hapa nyumbani kuna compyuta 2,nikaonganisha zote na internet,tukawa tukiwasiliana kwa akaunti zote 2 ila hii yangu anayoijua yeye mawasiliano yakawa sio mazuri kama hii mpya,nikamuuliza kwenye akaunti mpya iwapo kama ana mtu akajibu hana,na hapo awali tuliamua kubadilisha status zetu wote na kuandika 'in relatioship' ingawa hakutaka tuandike tuko na nani kwenye hiyo relationship.
siku ya trh 2/08/2011 usiku alikuwa hewani ila hakuwasiliana na mimi kwenye akaunti yangu ya awali ila alikuwa ananijibu iwapo nitatumia akaunti mpya ambayo hajui anawasiliana na nani maana sikuweka picha! ila ilipofika asubuhi akanitumia meseji kwamba anashida na vocha kwamba anataka kuwasiliana na ndg yake aliyeko A town ambaye ni mimi bila ya yeye kujua
KAZI KWENU WANA JF KWA NASAHA ZENU
siku ya trh 2/08/2011 usiku alikuwa hewani ila hakuwasiliana na mimi kwenye akaunti yangu ya awali ila alikuwa ananijibu iwapo nitatumia akaunti mpya ambayo hajui anawasiliana na nani maana sikuweka picha! ila ilipofika asubuhi akanitumia meseji kwamba anashida na vocha kwamba anataka kuwasiliana na ndg yake aliyeko A town ambaye ni mimi bila ya yeye kujua
KAZI KWENU WANA JF KWA NASAHA ZENU