Demokrasia na umaskini ni kama mafuta na maji, umaskini ni sumu ya demokrasia

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,597
46,230
Bila kuuondoa umaskini ni vigumu sana kusimika demokrasia.

Nchi zote zenye demokrasia iliyoshamiri zimefika hapo baada ya kupiga hatua kubwa kuuondoa umaskini.

Mambo matano ya yanayofanya umaskini kwa sumu kwa demokrasia ni;

1. Umaskini unadumuza kwa kiasi kikubwa uwezo wa raia kufikiri na kudadavua mambo. Mitazamo ya maskini na matajiri katika maisha ni tofauti sana. Maskini mara zote huwa anawaza mlo unaofuta utatoka wapi, matajiri huwa wanawaza miaka 2, 3, 5 wawekeze kwenye katika kitu gani kukuza zaidi utajiri wao. Kwa maana hiyo ata maamuzi ya kisiasa yanayofanywa na maskini ni kwa mtazamo wa muda mfupi wakati matajiri ni kwa muda mrefu.

2. Ukiwa maskini unakosa msimamo, mara nyingi inakubidi kukubaliana na misimamo ya wenye pesa au mamlaka ukifikiri maisha yako yatafanywa rahisi na wao lakini mara zote sio kweli kwamba maisha yanaboreka kwa kuwa

3. Maskini mara nyingi ni rahisi kupandikizwa chuki na kufanya mambo kwa hasira ambayo wakati mwingine hayana faida kwao. Hiyo ndio njia aliyoitumia Hitler kuingia madarakani. matajiri wao wanafanya mambo yao kwa kuangalia maslahi yao ya kibiashara, haijalishi mmetofautiana kiasi gani wao wanatanguliza biashara zao mbele zaidi kuliko hisia.

4. Maskini hawana umoja, ushirikiani na muunganiko wenye nguvu sana tofauti na wenzao matajiri. Masikini wanakosa "cooperation" kwa kiasi kikubwa tofauti na matajiri ambao mara nyingi ni rahisi sana kuungana dhidi ya mambo yanayotishia maslahi yao na ndio maana unaona wengi wanaokali viti vya mamlaka ni wenye hali nzuri kiuchumi.

5. Maskini hata akiwa "smart" sana sio rahisi kuchaguliwa kiongozi kupitia uchaguzi huru. Hii inasababishwa na ukweli kwamba matajiri wana connection, nyenzo na njia nyingi za kupenya na kuwa viongozi.

Umaskini ni mwiba mkali wa demokrasia, tupambane nao kwa nguvu zaidi.
 
Mbona Marekani walianza na demokrasia tangu mwanzo halafu wakatajirika baadae? Waliwezaje demokrasia kwenye nchi changa?
 
Nakubaliana nawe kwa kiasi kikubwa. Nakumbuka kwenye uchaguzi wa mwaka 2010 kuna kijana mmoja aliamua kumpa mgombea mgombea mmoja kura kwa sababu alinunuliwa pombe aina ya tembo wengine wanaita mmnazi hadi akalewa.

Kwa wakati huo bei yake ilikuwa sh. 50/= kwa chupa ya bia. Au hata akina mama wanaopigia wagombea kura kwa kupewa doti ya kanga. Baadhi ya vipengele hapa unaweza ukavipanua na kuvihusisha na umaskini wa nchi.
 
Marekani hawakuanza na demokrasia imara tangu mwanzo, baada ya kupata uhuru biashara ya utumwa ilikuwa ikiendelea hadi ikaja kusababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe 1861, wanawake walikuwa hawaruhusiwi kupiga kura mpaka 1920.

Pia Marekani wakati inapata uhuru haikiwa nchi maskini kama zetu na ilipata bahati ya kupata viongozi wa mwanzao ma"genius" na matajiri.
Mbona Marekani walianza na demokrasia tangu mwanzo halafu wakatajirika baadae? Waliwezaje demokrasia kwenye nchi changa?
 
Fact:
Democracy is said to survive only in places where there's a vibrant civil society and A LARGE AND PROSPEROUS MIDDLE CLASS.

Umasikini umekuwa mtaji wa watawala wetu miaka nenda rudi. CCM wao hawahangaiki ikifika wakati wa uchaguzi wanasambaza kofia na t-shirt vijijini kwa masikini nao kwa umasikini na ujinga wao wamekuwa wakiwachagua wala sio kwa sera zao bali kwa zawadi wanazopewa. Kununuliwa pombe na kupikiwa pilau kwa masikini hivyo ni ni vitu vikubwa mno.
 
Bila kuuondoa umaskini ni vigumu sana kusimika demokrasia .

Nchi zote zenye demokrasia iliyoshamiri zimefika hapo baada ya kupiga hatua kubwa kuuondoa umaskini.

Mambo matano ya yanayofanya umaskini kwa sumu kwa demokrasia ni;

1.Umaskini unadumuza kwa kiasi kikubwa uwezo wa raia kufikiri na kudadavua mambo. Mitazamo ya maskini na matajiri katika maisha ni tofauti sana. Maskini mara zote huwa anawaza mlo unaofuta utatoka wapi, matajiri huwa wanawaza miaka 2, 3, 5 wawekeze kwenye katika kitu gani kukuza zaidi utajiri wao. Kwa maana hiyo ata maamuzi ya kisiasa yanayofanywa na maskini ni kwa mtazamo wa muda mfupi wakati matajiri ni kwa muda mrefu.

2.Ukiwa maskini unakosa msimamo, mara nyingi inakubidi kukubaliana na misimamo ya wenye pesa au mamlaka ukifikiri maisha yako yatafanywa rahisi na wao lakini mara zote sio kweli kwamba maisha yanaboreka kwa kuwa

3.Maskini mara nyingi ni rahisi kupandikizwa chuki na kufanya mambo kwa hasira ambayo wakati mwingine hayana faida kwao. Hiyo ndio njia aliyoitumia Hitler kuingia madarakani. matajiri wao wanafanya mambo yao kwa kuangalia maslahi yao ya kibiashara, haijalishi mmetofautiana kiasi gani wao wanatanguliza biashara zao mbele zaidi kuliko hisia.

4.Maskini hawana umoja, ushirikiani na muunganiko wenye nguvu sana tofauti na wenzao matajiri. Masikini wanakosa "cooperation" kwa kiasi kikubwa tofauti na matajiri ambao mara nyingi ni rahisi sana kuungana dhidi ya mambo yanayotishia maslahi yao na ndio maana unaona wengi wanaokali viti vya mamlaka ni wenye hali nzuri kiuchumi.

5. Maskini hata akiwa "smart" sana sio rahisi kuchaguliwa kiongozi kupitia uchaguzi huru. Hii inasababishwa na ukweli kwamba matajiri wana connection, nyenzo na njia nyingi za kupenya na kuwa viongozi.

Umaskini ni mwiba mkali wa demokrasia, tupambane nao kwa nguvu zaidi.
Kuuondoa umasikini kwa watanzania ina maanisha watawala wamechoka .

Ukisha muwezesha masikini akawa na uwezo kimaisha basi jua ataidai haki yake.
 
Fact:
Democracy is said to survive only in places where there's a vibrant civil society and A LARGE AND PROSPEROUS MIDDLE CLASS.

Umasikini umekuwa mtaji wa watawala wetu miaka nenda rudi. CCM wao hawahangaiki ikifika wakati wa uchaguzi wanasambaza kofia na t-shirt vijijini kwa masikini nao kwa umasikini na ujinga wao wamekuwa wakiwachagua wala sio kwa sera zao bali kwa zawadi wanazopewa. Kununuliwa pombe na kupikiwa pilau kwa masikini hivyo ni ni vitu vikubwa mno.
Tena wali kwa maharagwe
 
True.Thus Mtu masikini Katu hawezi kuwa mwanasiasa mzuri,atanunuliwa tumeona waunga juhudi.
 
Umasikini ni sera kabisa kwenye nchi za kijamaa lengo kuu hasa ni kuwafanya watu wawe masikini ili waweze kuwatala.
Ccm na umasikini ni pacha.
 
Back
Top Bottom