Demokrasia na Maendeleo ndani ya CHADEMA

umeandika maelezo mengi lakn pumba tupu.ninapata wasiwasi na uwezo wako wa kufikiri,SIO KAZI YA USALAMA WA TAIFA KAMA SIO WA CCM KUTUCHAGULIA VIONGOZI.VIONGOZI HUCHAGULIWA NA WATAWALIWA KUPITIA SANDUKU LA KURA.Na hao tiss na vyombo vyote vya usalama walikuwa wapi wakati pesa za EPA,KAGODA ZINAIBIWA? walikuwa wapi wakati mafisadi wanaiba twiga wetu na kuwapeleka uarabuni? biashara ya unga na majangili unataka kutuambia wahusika hawajulikani? wengi wa wanausalama hao unaowakingia kifua wanashirikiana na mafisadi wa ccm kuhujumu taifa huku wewe ukitaka wasisemwe hadharani? leo hii usalama wa taifa umegeuka kuwa uhujumu wa taifa.acha kujifedhehesha kwa vijipropaganda vya kipumbafu.


Siku moja nilimwuliza Dk. Slaa kwamba 'Ikiwa usalama wa taifa uliopo ni dhaifu kwa kiasi cha kugawanyika na sehemu yake kuripoti kwako kama unavyodai, je Chama chako kikiingia madarakani utafikiria kufumua na kuunda upya idara ya usalama wa taifa?' Slaa alikimbia na mods wakahamisha haraka ile thread!
Ndugu m4cjb, usalama wa taifa wanatuchagulia viongozi na wana jukumu la kuilinda serikali iliyopo madarakani, kulinda taifa dhidi ya maadui wa nje na ndani pia. Ni upotofu tu kuikejeli TISS, kama ilivyo kwa taasisi zote za usalama ulimwenguni sisi raia wa kawaida tunajua na kutambua pale failure inapotokea lakini hatujui mafanikio makubwa ya kiusalama yanayotokea daily!
Na kwa timu ya uongozi hapo chadema kwa sasa sifikirii kuwa kuna TISS inaweza kutoa go ahead through Vetting1
 
Last edited by a moderator:
Mimi sifikiri hivyo, Zito aliamua kutofautiana na muelekeo wa chama chake. Haikuwa sawa kuwafukuza akina J. Shonza na wenzake halafu ukamwacha Zito.Kwa wanaoiamini CHADEMA ilikuwa ni swali kubwa sana kumwacha ndani ya CHADEMA Zito. KILICHOFANYIKA MIMI NAONA NI SAWA. KUNA WAKATI KUNA HAJA YA KUCHUKUA MAAMUZI KAMA HAYA.

NI VEMA KUBAKI NA WATU WACHACHE WASAFI KWANI CHAMA KITAFIKA MBALI KULIKO KUBAKI NA WATU WENGI WATAKAOUA CHAMA KESHOKUTWA.

KWANI ZITO LAZIMA AWE CHADEMA ANAWEZA ANZISHA CHAMA AU KUJIUNGA CCM.
 
Rudi ukajifunze kuandika Bwana Le Mutuz.

Akili yako ni ya mtu asiye na mtazamo wa kichambuzi. Ni ya mtu hovyo tu.
 
Ukweli ambao chadema wanapaswa kuelezwa waelezwe tuh,hakuna tena haja ya kuwaficha,

Maji yamekwisha mwagika hayazoleki tena haya
 
It is advisable to settle down after any shock that has struck you.....then you can give what is very useful and fruitful....
Kijana analysis yako ni very poor....kwanza uchambuzi wako kwa kufuata "content analysis" kichwa cha habari hakikufaa kuwa Demokrasia....
Kitu kingine unasema suala la ushahidi wakati wewe mwenyewe hujatoa "evidence" ya kichwa cha habari hapo juu....
Suala la Zitto na Kitila ni suala la muda.....japo nawaunga mkono wasomi na wachambuzi hawa ila nakuomba relax kwanza....tafakari na kufikiri bila jazba....usiwe kama mfiwa,ambae hulaumu dereva wa ambulance,daktari,nesi na hata Muumba.
Thanks.
 
Inapofikia wakati wa kutulazimu kusimama na kuongea ukweli daima lazima tutasimama na kuzungumza ukweli huo pasi na hofu ya kuogopa kutukanwa,kubezwa,kudharauliwa na kupachikwa kila aina ya majina kutoka kwa hao wanaojidai wana hubiri demokrasia.


Siku zote nimekuwa naiduru durusu katiba ya chadema,kitu kikubwa hapo mwanzao kilichokanipelekea niweze kuipa nafasi chadema fikran mwangu hata kabla bado sijaamua kuifatilia kwa undan ni KATIBA YAO,nilipokawa naingalia katiba yao kwa kweli niligundua ina utofauti mkubwa sana na ile ya CCM kwa mambo mengi,ilijpambanua kweli kweli kuwa ni MKOMBOZI HASA WA WATANZAIA,hapo mimi nikaamua kuwatilia maanani na kufatilia siasa zao na kuunga maono yao,hasa lilipokuja suala la UTAWALA WA MAJIMBO NA KUSHUSHA MADARAKA HADI NGAZI YA CHINI KWA WANANCHI,

LAKINI NAONGEA KWA MASIKITIKO MAKUBWA KABISA NA WATANZANIA WENZANGU NAOMBA MNIZINGATIE,

NAJUA WAPO WATAKAOKUJA NA HOJA ZA KUNIITA LUMUMBA,MKANDA,MKABILA NA MCHOCHEZ LAKINI POTOLEA MBALI MIMI MISIMIMAMO YANGU IKO WAZI HUMU TOKEA NAINGIA KWENYE JUKWAA HILI NA KILA MWENYE FIKRA HURU ANALITAMBUA HILI,NILIAMUA KWA DHATI YANGU KUWA MSHABIKI WA SIASA ZA CHADEMA KWA KUWA NAJUA MIMI ADUI YANGU MKUBWA NI CCM,NA KATIKA CHAMA AMBACHO NIMEAPA KUJA KUTOKUKISAME MILELE DAIMA MAISHANI MWANGU NI CCM,SO NILIAMUA KABISA KUSHABIKIA CDM KWA KUJUA KWAMBA HAWA JAMAA NDIO MWARUBAIN WA KUIDONDOSHA CCM,KWNGU MIMI ILIKUWA LIWALO NA LIWE ILI MRADI CCM IANGUKE MADARAKANI TUANZE UPYA,NA BADO HADI KWA SASA HUONDIO MSIMAMO WANGU,LAKINI M'BADALA WA HAYO SIWEZ TENA KUAMINI KUWA NI CHADEMA,

KWANIN NASEMA TUSIAMINI NA KUWAPA NAFASI CHADEMA KAMA M'BADALA??

1.Chadema kinajimbanua kuwa hiki ni chama cha demokrasia,mimi niliamin hivyo na watanzania wote tuliamin hivyo,
lakin uhalisia ulivyo hakuna demokrasia ndan ya chama hiko,HUWEZ UKAHUBIRI DEMOKRASIA UKASHINDWA KUWEKA UKOMO WA UONGOZ NDAN YA TAASISI YA KIDEMOKRASIA,UKIULIZA NI KWANIN JIBU LINAKUJA KILA NAFASI NDAN YA UONGOZ WA CHAMA HAINA UKOMO,NA MTU ATAENDELEA KUONGOZA AS LONG AS ANAKUBALIKA NA WENGI NDAN YA CHAMA NA ILI MRADI UONGOZ WAKE NI IMARA NA HAUNA KASORO BASI AENDELEE KUONGOZA CHAMA...!!

HIYO NI DEMOKRASIA GANI??WANA TOFAUTI GANI NA MUSEVENI AU ROBERT MUGABE??KAMA NDAN YA CHAMA HUO NDIO MSIMAMO WAO WAKIPEWA NCHI ITAKUAJE??HILO LA KWANZA,

2.Chadema kimekuwa ni chama kinachopandikiza uhasama baina yake na TAASISI kuu za serikali ambazo ziko imara kulinda usalama wa taifa hili,wanadhan nani atawaamin na kuwapa dhamana ya kuongoza TAIFA ili hali wanapandikza chuki baina ya chama chao na vyombo vya TAIFA??

--- CHADEMA KILA SIKU INAITUKANA USALAMA WA TAIFA NA KUSEMA NI UMEKUWA KIBARAKA WA CCM,USALAMA WA TAIFA DHAIFU,USALAMA WA TAIFA WEZI,USALAMA WA TAIFA WANASHIRIKIANA NA MAFISADI KUHUMUJUMU TAIFA HILI NA KADHALIKA,
INAWEZEKANA IKAWA NI KWELI,SASA TUKIUWAULIZA USHAHID UKO WAPI JUU YA HAYO ILI TUAMIN HAWANA,SASA UNADHAN WATU HAWA TUKIWAPA NCHI ILI HALI TAASISI NYETIKAMA USALAMA WA TAIFA WAO WANAONA KUWA NI OPPONENT WAO KISIASA TUNAWEZA KUWA SALAMA??HATA KAMA WAO WANAONA HAWARIDHKI NA USALAMA WA TAIFA KWA NIN WASITUMIE NJIA STAHIKI KUZUNGUMZA NAO AU KUWASHITAKI KWA WATANZANIA KWA HOJA NA FACT NA USHAHID BILA KUWAKEJELI NA KUWATUKANA??UNADHAN NA HAO USALAMA WANAWEZA KUWA RADHI NA KUWAPA HAWA CHADEMA RIDHAA YA KUONGOZA TAIFA??


----CHADEMA KILA SIKU IKO KWENYE MALUMBANO NA JESHI LA POLISI.
Nakubali jeshi la polisi kuna wakati linaziingua na ni kero kubwa sana ndan ya taifa letu,
Kwa rushwa,kutowajibikia,kupemdelea CCM,kuchukua maamuz ya ukandamizaji na kadhalika,.hata SISI WATU WA KUSINI NI WAHANGA WA JESHI HILO,

Lakini kinachonishangaza ni kwa chadema kuwafanya jeshi hilo kuwa maadui zao wa wazi wazi kias cha kufikia hata kutaman kupigana nalo hasa pale wanapooona linakwena kinyume na matakwa yao,
Jeshi la polisi kama chombo cha serikali katika nch yyte daima wao hutii mamlaka ya serikali iliyoko madarakani,lakin tuseme ukweli kwamba kuna wakati wao kama wanadamu huwa wanachoka na mamlaka hizo na kuwa tayari kwa mabadiliko hasa kwa chama ambacho wanahisi kinaweza kuwa mtetezi wa haki na maslahi yao,sasa chadema kwanin kinajiingiza kwenye malumbano na jeshi hilo na kuacha kuonesha kuwa wao ni mkombozi wao??
Unadhan jeshi la polisi linaweza kuwa radhi kuiona chadema inachukua hatamu za uongozi??hilo haliwezekani hata kidogo...

----Na hapa karibun Chadema kilishajionesha kuingia kwenye utata hata na jeshi la wananchi wa tanzania na kusema ni jeshi bovu,jeshi lililoegemea CCM na kuacha kusimama kwenye utaifa na kadhalika,

Ni kweli kabisa,sisi wana kusini ni wahanga wa jeshi hili,na tumepewa vipigo vya kila aina hasa pale tulipoonesha tunasiama kupignia matumiz mazur ya RASIMALI GESI,lakin hatukuwahi kuthubutu kusimama na kulitukana jeshi hilo kwa kuwa tunajua wao pia hupewa AMRI na serikali iliyopo madarakani ambayo,ni ya CCM,
lakini kwa kuwa wao ni wanadamu kama sisi ukweli wanaujua,tunajua kwamba itafikia wakati hata wao wataichoka CCM na kuwa tayari kwa mabadiliko,kwahiyo kama wakiona chama chenye uelekeo ni chadema daima hawawez kuacha kukiunga mkono,lakini cha kushangaza chadema nao wamekuwa ni mahasimu wa jeshi hilo huku wakiamin siku moja wanaweza kuchukua uongozi wa taifa hili na kuilendesha jeshi hilo hilo wanalolitukana,hiyo inaingia vipi akilini??

Just to mention but a few of them hiyo ni katika kuonesha ni kwa namna gani chadema isivyopaswa kuamiminiwa na kupewa TRUST ya moja kwa moja kuongoza TAIFA HILI,
Yani ni watu flan ambao wapo na mission na vision zilizojificha na zisizoeleweka.

3.UKANDA,UDINI NA UKABILA

Mara nyingi ninaposoma katiba ya chadema hakuna sehemu naposoma kuwepo kwa vipengele vinavyohubiri ukanda,udini na ukabila ndan ya chama hiko,
Yan kwa ufupi sio itikadi za chadema kwa katiba yao kutukuza ukanda,udini na ukabila,

Hapo mwazo CUF ilivyokawa ipo juu miaka kadhaa iliyopita CCM ilikuja na propaganda ya udini kwa watanzani,na kusema kwamba chma hiko nii cha waislam na hivyo watanzania tusikiamin kwani kitakuja kuvuruga nchi,wengi tuliamin propaganda zile,na niseme wazi tuh hadi leo wapo wengi wanaziamin propanganda zile tena wengi wao ni wanachadema,

Sio mara moja wala mara mbili mimi nimeshawahi kukejeliwa humu ndan na wanachadema na kuniambia mimi sio chadema,niache kuyananga nanga mambo ya chadema na niende kwa waislam wenzangu CUF,sishangai hilo kwani tunatofautiana mawazo,

Nilirudishe hilo kwa Chadema,CCM wakaja tena na propaganda kama hiyo kwa CHADEMA,
CCM wakasema kwamba CHADEMA ni wakanda,wakabila na wadini,mimi nikawa nalifatilia hilo kwa umakin wa hali ya juu huku nikilinasibisha na propaganda zile za CUF,

Lakini kwa masikitko makubwa mimi naweza kusema kwamba nashawishika kuamin na propaganda zile kuwa ndan ya CHADEMA KUNA SIRI NZITO KUHUSU UKANDA,UDINI NA UKABILA,

KUJIUZULU KWA SAID ARFI NA KUSAKAMWA NA KWA ZITTO KABWE NA KITILA MKUMBO NAKUFANANISHA NA MADHILA YALIYOKAMPATA MAREHEMU CHACHA WANGWE NASHAWISHIKA KUAMINI KUWA KUNA HALI YA UTATA KUHUSU HILO NA AMBAYO INAPASWA KUMULIKIWA TOCHI YENYE MWANGA MKALI,

KATIBA YA CHADEMA HAIHUBIRI UDINI,UKANDA NA UKABILA,

LAKINI TUNAPIMA MAHUSIANO YA CHAMA HIKO NA PHILOSOPHIA HII YA UKANDA,UDINI NA UKABILA TUKIUNGANISHA DOTS TUNAPATA UKAKASI SANA KUAMIN KWAMBA WAO CHADEMA WANAWEZA KUKAA MBALI NA HILO,WENZAO CUF WAMEWEZA KUKAA MBALI NA PROPAGANDA HIYO,WAO NAONA WAMESHINDWA KUIPUNCH NA INAWATAFUNA,

ANGALIA TOP LAEADERSHIP YAO IKOJE,USHAWISH NA WENYE MAMLAKA YA KUATHIRI MAAMUZI NI WATU WA NAMNA GANI??UTAPATA PICHA HALISI,KAMA KWELI WANAHITAJIKA KUKUBAKIKA NA WATANZNIA NI LAZIMA WALIKUBALI HILO NA KUBADILISHA MFUMO WAO WA MAONO NDAN YA CHAMA,KWA SASA HAKUNA WA KUWEZA TENA KUWAAMIN..

Ni Muda tuh pekee ndio utakaowahukumu chadema,na kwa sasa kila mwenye akili timamu anafaham fika kwamba hakuna demokrasia ya dhati ndan ya chama hiko,

Kikubwa kilichopo ni kutumia mwamvuli wa demokrasia na kuwapumbaza wale wasiotambua aina ya siasa wanazozifanya wao chadema.

Watanzania tulio wengi tumeshoshwa moja kwa moja na UTAWALA WA CCM,na tuliamin moja kwa moja CHADEMA ingeweza kuwa M'BADALA SAHIHI WA CCM,lakin kwa masikitko makubwa tumeona ni jins gani chama hiki kilivyotupotezea muda wetu,klivyo vunja matumain yetu na ndoto zetu kwamba ipo siku moja wangekuja kuiangusha CCM na kuiondoa madarakani.,

Wamefeli kusimamia uongoz ndan ya chama,wameshindwa kusimamia demokrasia ndan ya chama,wameshindwa kuwaunganisha wananchi wa makabila mbali mbali,wananchi wa kanda mbali mbali,wananchi wa dini mbali mbali,

Pia Chadema wameshindwa kuziunganisha taasisi nyeti tunazozitegemea watanzania katika kuongoza nchi hii na kuwashawishi kuwa wao tukiwapa ridhaa wanaweza kuongoza taifa hili watawezaje kuchukua dola na kuongoza taifa??

SHUKRANI MUNGU KWA KUTUFUNULIA HILI,NA TUNASHUKURU TUMELIONA KWA WAKATI MUAFAKA...

TEAM ZITTO...
Toka uanze kula buk7 za Lumumba akili yako imevurugika sana... OOK vipi GESI inatoka haitoki?
 
Ukimaliza kusoma huo utumbo wako pia pitia na hii story....na useme ni lini ZZK alikanusha...

VIGOGO kadhaa wa Idara ya Usalama wa Taifa (TISS) wametajwa "kuingilia" Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), MwanaHALISI limegundua.

Taarifa zilizopatikana kutoka ndani ya idara hiyo zinaeleza kuwa vigogo hao wana mahusiano ya karibu na Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA, Zitto Kabwe.
Anayetajwa rasmi kuwa na mahusiano na Zitto ni Naibu Mkurugenzi wa TISS, Jack Zoka.
Kufichuka kwa taarifa za kuwapo "uswahiba" kati ya Zoka na Zitto kumekuja katika kipindi ambacho CHADEMA kimekuwa kikituhumu maofisa wa juu wa usalama wa taifa kuvuruga uchaguzi mkuu uliopita.
Aidha, kuibuka kwa tuhuma hizi kumekuja wiki moja baada ya gazeti hili kuchapisha taarifa mbalimbali za mawasiliano kati ya Zitto na Rais Jakaya Kikwete.
Baadhi ya mawasiliano hayo, ambayo Zitto ameyapeleka kwa rais, aliyapeleka pia kwa baadhi ya watuhumiwa ufisadi nchini.
Kwa mujibu wa mgombea urais wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa ambaye alitangazwa kushika nafasi ya pili nyuma ya Rais Kikwete; viongozi wa TISS walihusika, kwa kiasi kikubwa, katika kile alichoita, "Kuchakachua matokeo ya uchaguzi."
MwanaHALISI limefanikiwa kupata rekodi ya mshororo wa mawasiliano kati ya Zitto na Zoka.
Kuna mwingiliano wa simu za mdomo na maandishi (sms) kutoka kwa Zitto kwenda kwa baadhi ya vigogo wa ngazi ya juu serikalini na TISS, hasa Zoka.

Nyaraka za mawasiliano zinaonyesha kuwa Zitto amekuwa akiwasiliana na naibu mtendaji mkuu wa TISS huyo zaidi ya mara tatu kwa siku.
Kwa mfano, Zitto na Zoka walifanya mawasiliano ya simu mara tisa hapo tarehe 8 Agosti. Simu iliyotumika katika mawasilino hayo, ni Na. +255756809535 ambayo hutumiwa na Zitto na +255754787550 ambayo hutumiwa na Zoka.
Wakati mawasiliano hayo yanafanyika, Zitto alikuwa katika maeneo tofauti.
Mawasiliano ya kwanza kati ya Zitto na Zoka yalipokuwa yanafanyika, simu ya Zitto ilisomeka kuwa alikuwa katika maeneo mbalimbali.
Mathalani, wakati mwingine simu ilikuwa ikisomeka kuwa yuko Mtambani, Kinondoni Dar es Salaam, Kigoma Urban (Mjini), Kigoma Rural (Vijijini), Mtwara, Uwanja wa ndege-Ilala, Oyster Bay, Ukonga, Upanga na katikati ya mji.
Gazeti hili halikuweza kugundua mara moja undani wa mawasiliano ya Zitto na Zoka.
Kinachofanya baadhi ya wachunguzi wa mambo kujenga shaka ni kwamba mmoja ni mwanasiasa, tena kutoka chama kilichopo nje ya utawala; na mwingine ni mtumishi wa idara ya usalama inayolalamikiwa kukandamiza upinzani nchini.
Hata hivyo, taarifa zinaonyesha kuwa mawasiliano kati ya Zitto na Zoka yalianza kupamba moto kuanzia tarehe 6 Agosti 2010, siku moja baada ya CHADEMA kuzindua kampeni zake za urais.
Kulingana na uchunguzi, siku hiyo, tarehe 6 Agosti, simu ya Zitto ilisomeka kuwa yuko Kigoma Urban.
Katika mkutano wa ufunguzi wa kampeni, CHADEMA kupitia kada wake mashuhuri, Mabere Marando, iliibuka na lundo la tuhuma dhidi ya vigogo kadhaa wa serikali, CCM na idara ya usalama wa taifa.
Akizungumza na maelfu ya wananchi katika viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, Marando alisema wizi wa fedha katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), ndani ya Benki Kuu ya taifa (BoT), ulifanywa na serikali na washirika wake.
Miongoni mwa vigogo aliodai kuwa walihusika kufanikisha wizi huo, ni rais wa sasa, Jakaya Kikwete, rais mstaafu Benjamin Mkapa, mbunge wa Igunga, Rostam Aziz na Edward Lowassa.
Akiongea kwa kujiamini, Marando alisema, "fedha za EPA ni wizi uliotiwa baraka na serikali ya CCM na ndio uliomsaidia rais Kikwete kuingia madarakani mwaka 2005."
Kuanzia hapo hadi sasa, Zitto na Zoka wamekuwa na mawasilino ya mara kwa mara, na karibu kila siku huzungumza kwa simu.
Mawasiliano mengine ya mara kwa mara yalifanyika tarehe 7 Agosti 2010, siku mbili tangu hotuba kali ya Jangwani. Yalianza saa 10:17 na kuendelea tena saa 10:50, saa 10:51:31, saa 11:46:13, saa 12: 14:46, saa 12:26:48 na saa 13:50: 21.
Lakini Zitto alipoulizwa kuhusu sababu ya yeye kufanya mawasiliano ya mara kwa mara na vigogo wa TISS, alisema hajui na hakumbuki lolote kuhusu kuwapo mawasiliano hayo na Zoka au mkuu yeyote wa idara hiyo.

Zitto amesema yeye, akiwa mwanasiasa na kiongozi, anazungumza na watu wengi kutoka katika taasisi na mashirika mbalimbali ndani na nje ya nchi, lakini hajui kitu kuhusu usalama wa taifa.

Alipobanwa kuhusu mazungumzo yake na Zoka, hasa yale ya 3 Novemba 2010, saa nne na dakika 56 asubuhi, siku mbili baada ya uchaguzi kumalizika, Zitto alisema, "Siku hiyo nilizungumza na watu wengi sana. Siwakumbuki ni akina nani hasa."
Alisema, "Hicho ndicho kipindi ambacho matokeo ya uchaguzi nchini kote yalikuwa yakizuiwa ikiwamo kwetu Kigoma. Na ukumbuke mimi nilipigwa mabomu na polisi na usalama wa taifa. Nakumbuka viongozi wengi wa vyombo vya ulinzi na usalama walinipigia simu kunijulia hali na kupata taarifa ya kilichotokea," anaeleza.

"Sasa kama Zoka naye alinipigia siku hiyo sikumbuki; lakini nilipigiwa na wengi…Naomba uniambie kitu, hivi mnachokitafuta hasa ni nini?" aliuliza.
Katika njia ya kujitetea, Zitto aliuliza, "Mwanasiasa kuongea na wakuu wa vyombo vya usalama ni kosa? Maana, hata kama ningekuwa nimezungumza naye, kosa langu liko wapi?" alieleza mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini.

Alipoelezwa kuwa haoni hiyo ni hujuma dhidi ya chama chake kwa kuzungumza na viongozi wa TISS na kile ambacho amekuwa akikizungumza kikiwa hakifahamiki kwa viongozi wake, Zitto alisema, "Sijawahi kukihujumu chama changu mahali popote, siku yoyote."

Jitihada za gazeti hili kuzungumza na Zoka hazikufanikiwa katika kipindi chote
cha mwishoni mwa wiki, kwa vile kila alipopigiwa, simu yake ya mkononi ilikuwa haipokelewi.

Hata ujumbe mfupi wa maneno uliotumwa kwenye simu yake saa 2:53 asubuhi ya Jumapili; ukieleza sababu za gazeti kuzungumza naye, haukujibiwa.

Aidha, tarehe 2 Novemba, siku moja baada ya kuzungumza na Zitto, Zoka alinukuliwa akikana madai ya Dk. Slaa, kuwa TISS imesaidia kuvuruga uchaguzi.
Katika taarifa yake aliyoitoa mbele ya waandishi wa habari, ofisini kwake jijini Dar es Salaam, Zoka alisema, "Dk. Slaa amekuwa akidanganywa na watu wanaojiita maofisa wa usalama wa taifa."
Hata hivyo, kuna meseji mbalimbali kuhusu udini na uamuzi wa CHADEMA kususia hotuba ya rais Kikwete ambazo zilitumwa na Zitto kwa baadhi ya wabunge wa CHADEMA ambazo zinadaiwa kuandaliwa na idara ya usalama wataifa.
Ujumbe huo unadaiwa kuandaliwa kwa ustadi mkubwa katika kukuza suala la udini na kuleta mtafaruki katika chama.
 
Demokrasia bila mipaka ni uhuni.

Fahamu si kila sehemu demokrasia inafaa usaliti alioufanya Zitto ingekuwa jeshini saa hizi angekuwa hayati huko hakuna msamiati wa neno demokrasia.
 
It is advisable to settle down after any shock that has struck you.....then you can give what is very useful and fruitful....
Kijana analysis yako ni very poor....kwanza uchambuzi wako kwa kufuata "content analysis" kichwa cha habari hakikufaa kuwa Demokrasia....
Kitu kingine unasema suala la ushahidi wakati wewe mwenyewe hujatoa "evidence" ya kichwa cha habari hapo juu....
Suala la Zitto na Kitila ni suala la muda.....japo nawaunga mkono wasomi na wachambuzi hawa ila nakuomba relax kwanza....tafakari na kufikiri bila jazba....usiwe kama mfiwa,ambae hulaumu dereva wa ambulance,daktari,nesi na hata Muumba.
Thanks.


Thank you,

CHAGA DEVELOPMENT MANIFESTOPHSIM TUUNGANE NA KUIKOMESHA MOJA KWA MOJA,

TUSEME KWA PAMOJA SASA KUWA YATOSHA,TAIFA HILI NI LETU SOTE,TUWAKANE WAKANDA NA WAKABILA NA TULIJENGE TAIFA LETU...
 
TBS,
Ungetulia kwanza mmalize maombolezo na kuanua tanga kisha urudi kwenye jamvi.

Yaani umejichanganya na kujipinga mpaka basi. Rangi zenu, hisia zenu, malengo yenu, mipango yenu nk vyote viko wazi kama jua hivyo huwezi kuelewa maana ya neno "demokrasia". Pia kwa vile bosi wenu na washirika wenzake leo watakuwa na press conference, na kwa vile yeye ndiye mwenye kushikilia akili zenu basi msubiri halafu ufuate atakachosema 100% maana hiyo ndio aina ya demokrasia unayoijua na kuitaka.
 
Siku moja nilimwuliza Dk. Slaa kwamba 'Ikiwa usalama wa taifa uliopo ni dhaifu kwa kiasi cha kugawanyika na sehemu yake kuripoti kwako kama unavyodai, je Chama chako kikiingia madarakani utafikiria kufumua na kuunda upya idara ya usalama wa taifa?' Slaa alikimbia na mods wakahamisha haraka ile thread!
Ndugu m4cjb, usalama wa taifa wanatuchagulia viongozi na wana jukumu la kuilinda serikali iliyopo madarakani, kulinda taifa dhidi ya maadui wa nje na ndani pia. Ni upotofu tu kuikejeli TISS, kama ilivyo kwa taasisi zote za usalama ulimwenguni sisi raia wa kawaida tunajua na kutambua pale failure inapotokea lakini hatujui mafanikio makubwa ya kiusalama yanayotokea daily!
Na kwa timu ya uongozi hapo chadema kwa sasa sifikirii kuwa kuna TISS inaweza kutoa go ahead through Vetting1


Thank you,

Waeleze waelewee...
 
TBS,
Ungetulia kwanza mmalize maombolezo na kuanua tanga kisha urudi kwenye jamvi.

Yaani umejichanganya na kujipinga mpaka basi. Rangi zenu, hisia zenu, malengo yenu, mipango yenu nk vyote viko wazi kama jua hivyo huwezi kuelewa maana ya neno "demokrasia". Pia kwa vile bosi wenu na washirika wenzake leo watakuwa na press conference, na kwa vile yeye ndiye mwenye kushikilia akili zenu basi msubiri halafu ufuate atakachosema 100% maana hiyo ndio aina ya demokrasia unayoijua na kuitaka.


Sawa tuh,who cares??

KELELE NA MIZUKA MINGI NDIVO ZILIZO IBADA ZETU SISI WALOKOLE,SO WE USITUSHANGAE SANA,TUACHE NA MAMBO YETU.

NDAN YA CHAMA TUNA UHAKIKA KWA VILE WENYE MAKALI NI NYINYI BASI VITA HII MUMESHINDA,LAKIN NDAN YA TANZANIA NA KWA WANANCHI GAME BADO MBICHI HII,NA WEWE MWENYEW UNAJUA HADI SASA MSHINDI KESHAPATIKANA,CALM DOWN UKWELI UTAFAHAMIKA TUH NA HAKI ITATENDEKA
 
Tunawasomeni wanachadema mnavyogawana kuni, nipo zangu kijiweni nakunywa kahawa.
 
Sawa tuh,who cares??

KELELE NA MIZUKA MINGI NDIVO ZILIZO IBADA ZETU SISI WALOKOLE,SO WE USITUSHANGAE SANA,TUACHE NA MAMBO YETU.

NDAN YA CHAMA TUNA UHAKIKA KWA VILE WENYE MAKALI NI NYINYI BASI VITA HII MUMESHINDA,LAKIN NDAN YA TANZANIA NA KWA WANANCHI GAME BADO MBICHI HII,NA WEWE MWENYEW UNAJUA HADI SASA MSHINDI KESHAPATIKANA,CALM DOWN UKWELI UTAFAHAMIKA TUH NA HAKI ITATENDEKA

Kumbe ndio maana chadema inaungwa mkono na walokole wengi! Kumbuka chadema ni saccos ya wanaukoo wa mtei!
 
Tunawasomeni wanachadema mnavyogawana kuni, nipo zangu kijiweni nakunywa kahawa.

Mkuu Ritz,inakoelekea inaonekana haka ka saccos ka wanafamilia ya Mtei kanaelekea mwishoni! Hivi,ile nyumba waliopanga ya makao makuu ya saccos yao ni mali ya nani vile?
 
Back
Top Bottom