MUSSA ALLAN
JF-Expert Member
- Oct 13, 2013
- 18,925
- 13,279
Si mlisema hatuwezi kumng'oa kibaraka wenu, sasa ndo muisome namba, hatufanyi kazi kwa mazoea.. imekula kwenu..
Kwani Lengo la kumuondoa Zitto chadema limekamilika?
Si mlisema hatuwezi kumng'oa kibaraka wenu, sasa ndo muisome namba, hatufanyi kazi kwa mazoea.. imekula kwenu..
Hivi kwa akili yako unadhani game imeisha ndiyo kwanza kumekucha huu mchakamchaka mpaka 2015 kama Chadema haijabakia unga limited, peke yake kuna fita kubwa tunachochea kuni tu hapa.Si mlisema hatuwezi kumng'oa kibaraka wenu, sasa ndo muisome namba, hatufanyi kazi kwa mazoea.. imekula kwenu..
Bigshow unahangaika sana mkuu, wewe ni KAFU ambaye ni mke wa CCM.... inashangaza sana hasa kwetu tunaopenda utaifa zaidi ya siasa mnavyoacha siasa za maana na kukomalia kujadili yanayotokea kwenye chama kichanga na kisicho na serikali kwa sasa, chama pinzani
I think people like you wanachangia sana Tanzania kuwa maskini, hakuna sera, hakuna hoja bali ni kabila, dini, gesi haitoki mtwara wakati huohuo mkipewa vitender vidogovidogo mnabadilika kama vinyonga
it makes me sick kuona watanzania tunaacha kuangalia namna ya kusaidia wajukuu zetu kimaendeleo na kukomalia matatizo ya wanandoa wawili walio na shida zao.... TALAKA YA ADUI YAKO INAKUNYIMA NINI USINGIZI?? AU NDIO YALE KA KULA MKE WA MTU HALAFU AKIACHIKA UNALALAMA KAONEWA
SIASA ZA TANZANIA KIUJUMLA NI UTUMBO MTUPU, IWE CCM, CHADEMA, KAFU NA HATA KILE CHAMA CHA MCHUNGAJI MBWABWAJO AKA MTIKILA
IMEFIKA WAKATI TUANGALIE NAMNA YA KUPUNGUZA NGUVU ZA SIASA NA WANASIASA NA TUIPE SERIKALI MENO MAKALI YA KUNYOOSHA WAPUUZI
KUNA RUMOURS KWAMBA NUSU YA SERIKALI SASA IKO BIZE KUANDAA 2015 - WHICH IS WRONG
THE BIG SHOW heshima kwako. Nahisi kama hututendei haki wasomaji wa JF humu.
Unasema "uliamua kuingia CDM kwa dhati yako". Ina maana hukulaghaiwa wala kushawishiwa na mtu. Hukuweka tangazo hapa JF kuomba ushauri siku siku unaingia. Uliingia kimya kimya kwa misimamo yako...
Kwa nini leo unapotoka hutoki kimya kama ulivyoingia? Yes, umeona humo ndani hakuko kama ulivyodhani, kwa nini unataka kuwashawishi wengine ambao nao wameingia kwa dhati zao watoke na wewe? Tuna akili timamu zilizotufanya tuiunge mkono CDM kama ulivyofanya wewe... Akili zetu timamu tutakazozitumia ama kubaki ama kutoka kama tulivyoingia, bila kushawishiwa na maneno ya mtu yeyote...
Ukweli ni lazima tuuseme hata kama ni mchungu
Kuna watu wanatuma PM za matusi na vitisho kwaangu,
Na kuniambia nimetumwa na Usalama ili nikivuruge chadema,thats why nawaambia hivyo,
Nimeamua kwa dhati yangu,na nasema ili watu wengine wautambue ukweli,
CHADEMA NI WABAKAJI WA DEMOKRASIA'....
ushauri wa bure,kama chadema hakuna demokrasia huna sababu ya kulalamika nenda chama ambacho kinademokrasia kuna ccm,nccr,cuf,n.k sioni sababu ya kung'ang'nia demokrasia chadema labda kama una agenda yako ya siri.
Tunapokizungumzia Chadema tunazungumzia mambo mawili makuu; Demokrasia na Maendeleo. Ni imani yangu kuwa waasisi wa chama hawakukurupuka katika kutafuta hayo maneno mawili ili yawe mwongozo katika kile viongozi, wanachama na wananchi kwa ujumla wanaanimi. Ni vyema basi kujua kwa muhtasari nini maana ya maneno haya.
Demokrasia
Neno Demokrasia linatumika kijamii pamoja na kisiasa. Linatumika katika nyanja nyingi za maisha kama katika kazi, ndoa, dini, elimu, kiuchumi n.k. Ila neon hili linatumika zaidi katika siasa.
Demokrasia inaweza kutafsiriwa katika misingi yake toka lugha ya Kigiriki. Demos = the people, Kratos = power. Hivyo basi demokrasia ni mfumo wa kiutawala ambapo nguvu ya kisiasa inatoka kwa wananchi. Au ni mfumo wa kisiasa ambampo nguvu za kiutawala zinatoka kwa wananchi.
Kadhalika demokrasia inaweza kuwa ya moja kwa moja ama ya uwakilishi. Katika mazingira yetu hatuwezi wote wananchi mil 40 kufanya maamuzi kwa niaba na kwa ajili yetu. Hivyo umuhimu wa demokrasia ya uwakilishi ndipo inapohusika. Demokrasia ya uwakilishai ni pale ambapo watu wachache wamechaguliwa ama kuteuliwa kuwakilisha mawazo ya wengi, na kwa usawa na haki katika vyombo vya maamuzi kama serikali, bunge na mahakama.
Maendeleo
Umoja wa mataifa kitengo cha maendeleo kinafafanua maendeleo kuwa ni kuwa na maisha marefu nay a afya, kuwa na ufahamu, kuwa na uwezo wa kuzifikia rasilimali zinazohitajika kwa maisha bora na kuweza kushiriki katika maisha ya kijamii kwa ujumla. Kwa lugha nyingine maendeleo ni kuwajengea watu uwezo katika nyanja zote za kimaisha kama siasa, uchumi, kijamii, kiutamaduni ili watu waweze kudhibiti maisha yao, kuelezea mahitaji yao na kutafuta ufumbuzi kwa matatizo yao.
Demokrasia na Maendeleo ni dhana mbili zinazoelekea kufanana na wakati huo huo kutofautiana. Zinafanana kwa misingi kuwa dhana zote mbili ni hitimisho la maisha bora kwa wananchi husika. Zinatofautiana kwa misingi kuwa kipi kianze na kipi kifuate . wakati mwingine ili pawepo na maendeleo, nguvu ya ziada inabidi kutumika. Tuliona hili katika utekelezaji wa Azimio la Arusha. Tunaona hili kwa wenzetu kama ilivyokuwa kwa Ujerumani, USSR na mataifa mengine. Demokrasia kwa upande wake inataka maridhiano na maamuzi ya wengi ama uwakilishi wa hayo maamuzi, kitu ambacho kinaweza kuchelewesha utekelezaji kisa tu mawazo ya mtu/watu Fulani yaheshimiwe.
Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA
Tunapoangalia katika ngazi ya chama tunaona kuwa Chadema kikiwa na dhana zake mbili kinashindwa aidha kuwa na kauli moja ni dhana gani ifuatwe kwanza, ama mawazo ya nani yapewe kipaumbele. Inawezekana mambo kuwa shwari ndani ya Chadema ila ni media na Dola kutaka kuchafua tu hali ya hewa ya chama. Inawezekana pia kuwa ndani ya chama hali si shwari hivyo kusababisha mivutano ya utekelezaji wa dhana hizo mbili-kwamba nani anatekeleza demokrasia na nani anatekeleza maendeleo.
Labda tujadili kuanzia hapa. Ndani ya Chadema kuna wanaoamini katika demokrasia na kuna wanaoamini katika maendeleo ila mwisho wa siku wana kauli ya kikasuku ya People's Power! Kuna uwezekano wa kubeba dhana hizi mbili kwa wakati mmoja? Kuna haja ya kuchelewesha moja ili iliyobaki ifanye kazi ili mwisho wa siku lengo litimie? Tuyajadili haya kwa manufaa ya chama chenyewe, pamoja na imani na matumaini ambayo tumeyaweka juu ya chama kwa mustakabali wa maisha bora kwa kila mtanzania
Yajue pia ya CCM kwa ufupi hapa
Soma uchambuzi wa wengine hapa
Mkuu THE BIG SHOW , nakupongeza kwa kuonyesha nia ya dhati ya kuwa unapenda demokrasia itawale katika vyama vya siasa.
Ila Pia nikuase kuwa usipoteze muda mwingi saaana kuwafundisha hawa manunda wa CHADEMA somo la utawala bora, ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa! Hawasikii, hawaelewi, hawaoni, na hawataki kujifunza.
Duniani kote, CHADEMA ndio chama cha kwanza cha siasa ambacho muasisi na Mwenyekiti ni mtu na baba mkwe wake.
Hakika UDINI UTATUMALIZA mashabiki wengi wa ZITTO kwa sasa ni VIJANA wa CUF na MACCM walio kuwa wanashabikia CHADEMA kwa kuwa tu ZITTO ni MUISLAM, But hakika 2015 tutasaga meno na kulia, hapa LOWASAA vs MEMBE huku SLAA wote WAKRISTO, Sijuhi BAKWATA NA MUJAHDINA KAMA WEWE MTAJIFICHA WAPI.
TIMING, wewe kila siku unasema hauna chama vipi leo mbona umepanic.he is not chadema wala nini..... Anaganga njaa tu humu
Katika nukta hii nawataka wana Chadema wa Arusha Mjini, Mbeya Mjini, Ubungo na Singida Mashariki wayaangalie majimbo ya Hai, Moshi Vijijini na Kigoma Kaskazini..
Kwa kina Zitto Kabwe, Philemon Ndesamburo, na Freeman Mbowe watagundua tofauti na hila zilizoko ndani ya chama hicho..
Katu Mchagga hawezi kuitifua barabara ya Kilimanjaro, wala kuchoma jengo wala kuacha shughuli za kuzalisha mali akashiriki maandamano..
Ndio maana maeneo yao yametulia. Tukiangalia fujo za Mbeya tunaona wazi kwamba ziliandaliwa..
Na uharibifu mkubwa ulipangwa na kuratibiwa kwa umakini na Chadema
2015 ccm imepita kirahisi, hehehe
Kuna watu wanatuma PM za matusi na vitisho kwaangu,
Na kuniambia nimetumwa na Usalama ili nikivuruge chadema,thats why nawaambia hivyo,
Nimeamua kwa dhati yangu,na nasema ili watu wengine wautambue ukweli,
CHADEMA NI WABAKAJI WA DEMOKRASIA'....
CCM kweli mnachekesha.Wananchi watawahoji kama Mshahara wa 150,000/=unatosheleza mahitaji na si kwa kiwango gani mmefanikiwa kumnunua Zitto.Kwa ugumu huu wa Maisha CCM ijiandae kupoteza Wabunge wengi zaidi na ikiwezekana hata Urais.