Maendeleo hayaletwi na Demokrasia au Udikteta

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,260
Kama raia, tanapoyatamini na kuyatafuta maendeleo lazima kuna ukweli tunahitaji kuufahamu vizuri.

Mojawapo ni hili la kwamba demokrasia haileti maendeleo, pia udikteta hauleti maendeleo. Maendeleo ni huru(independent) ya aina zote hizo mbili za utawala. Ndio maana unaweza kuona kuna nchi za kidikteta kama China na Urusi zimeendelea na pia kuna nchi za kidemokrasia/kiliberali kama Marekani, Australia na Canada zimeendelea pia.

Maendeleo yanahitaji kufuata kanuni za msingi wake ikiwemo uwajibikaji wa viongozi, utabirikaji wa sera na maamuzi ya nchi, utulivu wa kisiasa, umoja ndani ya nchi, meritocracy, elimu bora, kuwa karibu na waliondelea, utamaduni n.k. Kimsingi haya ni mambo yanaweza kupatikana katika udikteta(benevolent dictatorship) au demokrasia.

Kitu cha ziada demokrasia inacholeta katika taifa ni kuyafanya maendeleo kuwa endelevu, jumuishi zaidi na kuhakisha utangamano katika taifa unadumishwa hasa kwa yale mataifa yenye jamii nyingi tofauti mfano za makabila, lugha, dini.
 
Chanzo kikuu cha maendeleo katika dunia ni matumizi sahihi ya akili katika kufanya fursa kwa kutumia natural resources zilizopo kujiletea kipato.
 
Mojawapo ni hili la kwamba demokrasia haileti maendeleo, pia udikteta hauleti maendeleo. Maendeleo ni huru(independent) ya aina zote hizo mbili za utawala. Ndio maana unaweza kuona kuna nchi za kidikteta kama China na Urusi zimeendelea na pia kuna nchi za kidemokrasia/kiliberali kama Marekani, Australia na Canada zimeendelea pia.
Not really, kitakwimu kabisa nchi zilizofuta mfumo wa chama kimoja na kicommunist yaani serikali kuhodhi kila kitu kuanzia siasa hadi uchumi zimeporomoka GDP as compared nchi zenye demokrasia ambazo uchumi na siasa ni huria.

China mathalani ina GDP kubwa ila maisha ya wananchi wake ni duni as compared to USA ndio maana bado ni nchi inayoendelea. Mfano malipo ya mfanyakazi wa China ni chini ya dollar 2 kwa siku sasa huyu utasemaje ameendelea!! Bado maisha sio nafuu as compared to malipo ya comparative role yake nchi za magharibi.

Na ndio maana hata US imewekeza huko maana kumlipa mchina kutengeneza simu ni bei nafuu kuliko kumlipa mmarekani.

Na hii pia ni shida Cuba, North Korea, Russia kuna uhusiano uliopo kati ya demokrasia/soko huria na Udikteta/usoshialisti na ukuaji wa uchumi.

Katika nchi top 100 kwenye GDP per capita (PPP) na Human development Index ukizi measure against Democracy Survey Index ya Transparency International utaona kuna correlation kati ya nchi zenye marks za juu kwenye demorkasia na position yao kwenye kupaa GDP/HDI

Cc The Boy Wonder Proved
 
Not really, kitakwimu kabisa nchi zilizofuta mfumo wa chama kimoja na kicommunist yaani serikali kuhodhi kila kitu kuanzia siasa hadi uchumi zimeporomoka GDP as compared nchi zenye demokrasia ambazo uchumi na siasa ni huria.

China mathalani ina GDP kubwa ila maisha ya wananchi wake ni duni as compared to USA ndio maana bado ni nchi inayoendelea. Mfano malipo ya mfanyakazi wa China ni chini ya dollar 2 kwa siku sasa huyu utasemaje ameendelea!! Bado maisha sio nafuu as compared to malipo ya comparative role yake nchi za magharibi.

Na ndio maana hata US imewekeza huko maana kumlipa mchina kutengeneza simu ni bei nafuu kuliko kumlipa mmarekani.

Na hii pia ni shida Cuba, North Korea, Russia kuna uhusiano uliopo kati ya demokrasia/soko huria na Udikteta/usoshialisti na ukuaji wa uchumi.

Katika nchi top 100 kwenye GDP per capita (PPP) na Human development Index ukizi measure against Democracy Survey Index ya Transparency International utaona kuna correlation kati ya nchi zenye marks za juu kwenye demorkasia na position yao kwenye kupaa GDP/HDI

Cc The Boy Wonder Proved
Correlation is not causation.
 
Kama raia, tanapoyatamini na kuyatafuta maendeleo lazima kuna ukweli tunahitaji kuufahamu vizuri.

Mojawapo ni hili la kwamba demokrasia haileti maendeleo, pia udikteta hauleti maendeleo. Maendeleo ni huru(independent) ya aina zote hizo mbili za utawala. Ndio maana unaweza kuona kuna nchi za kidikteta kama China na Urusi zimeendelea na pia kuna nchi za kidemokrasia/kiliberali kama Marekani, Australia na Canada zimeendelea pia.

Maendeleo yanahitaji kufuata kanuni za msingi wake ikiwemo uwajibikaji wa viongozi, utabirikaji wa sera na maamuzi ya nchi, utulivu wa kisiasa, umoja ndani ya nchi, meritocracy, elimu bora, kuwa karibu na waliondelea, utamaduni n.k. Kimsingi haya ni mambo yanaweza kupatikana katika udikteta(benevolent dictatorship) au demokrasia.

Kitu cha ziada demokrasia inacholeta katika taifa ni kuyafanya maendeleo kuwa endelevu, jumuishi zaidi na kuhakisha utangamano katika taifa unadumishwa hasa kwa yale mataifa yenye jamii nyingi tofauti mfano za makabila, lugha, dini.
Jibu ni hilo
 
Correlation is not causation.
Not really, causation huwa tunapima kwa regression au ARDL etc na hata majibu yake yanaitwa R squared ni hiyo hiyo correlation.

Kumbuka data hizo huwa zinakua normalised, zinafanyiwa stationary test, pia control variables kama Mortality rate, Political stability index, labor productivity etc zinakua factored in.

Under such conditions majibu unayopata yanaonyesha causation coz all other factors/control variables are held at constant.

Siku nitaweka uzi hapa ukiwa na full takwimu step by step na majibu yatakua interpreted hapa hapa.
 
Maendeleo Endelevu ni matokeo ya MSETO wa mambo mbalimbali ambayo yanamzunguka binadamu katika maisha yake yote ya kila siku, lakini Kiini na Chemchem ya Mseto huo wote unaosababisha Maendeleo ni Maarifa (Akili nzuri) na Demokrasia.
Akili nzuri (au Fikra Huru) daima huwa ndio Kiini na chimbuko kuu la suala zima kuhusu Ugunduzi, Uvumbuzi na Ubunifu mbalimbali.
Kukosekana kwa Uhuru wa Fikra mara nyingi huwa ndio kaburi la Maendeleo, ugunduzi, uvumbuzi na ubunifu.
 
Maendeleo Endelevu ni matokeo ya MSETO wa mambo mbalimbali ambayo yanamzunguka binadamu katika maisha yake yote ya kila siku, lakini Kiini na Chemchem ya Mseto huo wote unaosababisha Maendeleo ni Maarifa (Akili nzuri) na Demokrasia.
Akili nzuri (au Fikra Huru) daima huwa ndio Kiini na chimbuko kuu la suala zima kuhusu Ugunduzi, Uvumbuzi na Ubunifu mbalimbali.
Kukosekana kwa Uhuru wa Fikra mara nyingi huwa ndio kaburi la Maendeleo, ugunduzi, uvumbuzi na ubunifu.
Ujerumani ya Hitler iliweza kupiga hatua kubwa za maendeleo kila sekta bila uhuru wa fikra. Urusi, China, Malaysia,Thailand, Misri, Saudi Arabia, Qatar, UAE, Vietnam zinapiga hatua za maendeleo bila kuwa na demokrasia yoyote.
 
Udikteta uko wa aina tofauti, sio lazima wa serikali ya chama kuhodhi kila kitu. Udikteta wa Hitler ulikuwa ni chama kimoja na Ujerumani ilipiga hatua kubwa sana kimaendeleo bila serikali kuhodhi uchumi. China, Singapore, Malaysia na Korea Kusini zimeweza kuendelea zikiwa na chama kimoja au tawala za kijeshi. Msingi wa maendeleo ya Ghana ulijengwa na utawala wa kijeshi wa Jerry Rawlings.
Not really, kitakwimu kabisa nchi zilizofuta mfumo wa chama kimoja na kicommunist yaani serikali kuhodhi kila kitu kuanzia siasa hadi uchumi zimeporomoka GDP as compared nchi zenye demokrasia ambazo uchumi na siasa ni huria.

China mathalani ina GDP kubwa ila maisha ya wananchi wake ni duni as compared to USA ndio maana bado ni nchi inayoendelea. Mfano malipo ya mfanyakazi wa China ni chini ya dollar 2 kwa siku sasa huyu utasemaje ameendelea!! Bado maisha sio nafuu as compared to malipo ya comparative role yake nchi za magharibi.

Na ndio maana hata US imewekeza huko maana kumlipa mchina kutengeneza simu ni bei nafuu kuliko kumlipa mmarekani.

Na hii pia ni shida Cuba, North Korea, Russia kuna uhusiano uliopo kati ya demokrasia/soko huria na Udikteta/usoshialisti na ukuaji wa uchumi.

Katika nchi top 100 kwenye GDP per capita (PPP) na Human development Index ukizi measure against Democracy Survey Index ya Transparency International utaona kuna correlation kati ya nchi zenye marks za juu kwenye demorkasia na position yao kwenye kupaa GDP/HDI

Cc The Boy Wonder Proved
 
Ujerumani ya Hitler iliweza kupiga hatua kubwa za maendeleo kila sekta bila uhuru wa fikra. Urusi, China, Malaysia,Thailand, Misri, Saudi Arabia, Qatar, UAE, Vietnam zinapiga hatua za maendeleo bila kuwa na demokrasia yoyote.
Nadhani tunatofautiana definition ya demokrasia.... kumbuka demokrasia ina misingi 11 kuanzia uhuru wa mahakama, freedom of press na sio indicator ya model ya serikali pekee!! Having said that ukichukua nchi zenye demokrasia pekee say 50 na ambazo hazina demokrasia say 50 utagundua zenye demokrasia ndio zina uchumi mkubwa kuliko hao wengine.

Mifano hai ni nchi zote zilizofuata ujamaa ipi ilipiga hatua kiuchumi kulinganisha na zilizochagua uchumi wa soko huria?? Linganisha tu Kenya vs Tanzania n.k
 
Not really, kitakwimu kabisa nchi zilizofuta mfumo wa chama kimoja na kicommunist yaani serikali kuhodhi kila kitu kuanzia siasa hadi uchumi zimeporomoka GDP as compared nchi zenye demokrasia ambazo uchumi na siasa ni huria.

China mathalani ina GDP kubwa ila maisha ya wananchi wake ni duni as compared to USA ndio maana bado ni nchi inayoendelea. Mfano malipo ya mfanyakazi wa China ni chini ya dollar 2 kwa siku sasa huyu utasemaje ameendelea!! Bado maisha sio nafuu as compared to malipo ya comparative role yake nchi za magharibi.

Na ndio maana hata US imewekeza huko maana kumlipa mchina kutengeneza simu ni bei nafuu kuliko kumlipa mmarekani.

Na hii pia ni shida Cuba, North Korea, Russia kuna uhusiano uliopo kati ya demokrasia/soko huria na Udikteta/usoshialisti na ukuaji wa uchumi.

Katika nchi top 100 kwenye GDP per capita (PPP) na Human development Index ukizi measure against Democracy Survey Index ya Transparency International utaona kuna correlation kati ya nchi zenye marks za juu kwenye demorkasia na position yao kwenye kupaa GDP/HDI

Cc The Boy Wonder Proved
Itoe China kwenye mfano wako weka India halafu naomba majibu yako.

Remember India inatambuliwa kama taifa kubwa la kidemokrasia duniani.
 
Nadhani tunatofautiana definition ya demokrasia.... kumbuka demokrasia ina misingi 11 kuanzia uhuru wa mahakama, freedom of press na sio indicator ya model ya serikali pekee!! Having said that ukichukua nchi zenye demokrasia pekee say 50 na ambazo hazina demokrasia say 50 utagundua zenye demokrasia ndio zina uchumi mkubwa kuliko hao wengine.

Mifano hai ni nchi zote zilizofuata ujamaa ipi ilipiga hatua kiuchumi kulinganisha na zilizochagua uchumi wa soko huria?? Linganisha tu Kenya vs Tanzania n.k
Kosa lako kubwa ni kuchanganya ujamaa na udikteta, soko huria na demokrasia.

Singapore haikuwahi kuwa nchi ya kijamaa wala kikomunisti ila ili fuata soko huria na ubepari na bado ilikuwa nchi ya kibabe kibabe.

Kuna nchi za Scandinavian zenye sera za kijamaa lakini sifikiri kama unaweza sema zinaongozwa kidikteta.
 
Nadhani tunatofautiana definition ya demokrasia.... kumbuka demokrasia ina misingi 11 kuanzia uhuru wa mahakama, freedom of press na sio indicator ya model ya serikali pekee!! Having said that ukichukua nchi zenye demokrasia pekee say 50 na ambazo hazina demokrasia say 50 utagundua zenye demokrasia ndio zina uchumi mkubwa kuliko hao wengine.

Mifano hai ni nchi zote zilizofuata ujamaa ipi ilipiga hatua kiuchumi kulinganisha na zilizochagua uchumi wa soko huria?? Linganisha tu Kenya vs Tanzania n.k
Correlation does not imply causation.
 
Kama raia, tanapoyatamini na kuyatafuta maendeleo lazima kuna ukweli tunahitaji kuufahamu vizuri.

Mojawapo ni hili la kwamba demokrasia haileti maendeleo, pia udikteta hauleti maendeleo. Maendeleo ni huru(independent) ya aina zote hizo mbili za utawala. Ndio maana unaweza kuona kuna nchi za kidikteta kama China na Urusi zimeendelea na pia kuna nchi za kidemokrasia/kiliberali kama Marekani, Australia na Canada zimeendelea pia.

Maendeleo yanahitaji kufuata kanuni za msingi wake ikiwemo uwajibikaji wa viongozi, utabirikaji wa sera na maamuzi ya nchi, utulivu wa kisiasa, umoja ndani ya nchi, meritocracy, elimu bora, kuwa karibu na waliondelea, utamaduni n.k. Kimsingi haya ni mambo yanaweza kupatikana katika udikteta(benevolent dictatorship) au demokrasia.

Kitu cha ziada demokrasia inacholeta katika taifa ni kuyafanya maendeleo kuwa endelevu, jumuishi zaidi na kuhakisha utangamano katika taifa unadumishwa hasa kwa yale mataifa yenye jamii nyingi tofauti mfano za makabila, lugha, dini.
Katika Nchi ambayo imeshaharibika kwa Ufisadi wa kila aina ni udikteta pekee ndio unaoweza kuwarudisha watu kwenye misingi ya Uzalendo na kuitumikia Nchi yao badala ya kutumikia matamanio na matumbo yao !!
Anatakiwa Dikteta muadilifu !!
 
Back
Top Bottom