Mkuu
mharakati.
Nashukuru sana kwa ufafanuzi wako murua..Chadema wanatakiwa watufahamishe Wananchi mipango yao kwenye mikutano yao watawasaidiaje vijana, watawasaidiaje wakulima, watawasaidiaje wafanyabiashara, watawasaidiaje wawekezaji, watafanyaje kuhusu mikataba ya madini, na mbinu watakazotumia kuinua uchumi wetu.
Mwananchi wa kawaida utapomwambia people's power, hakuna kulala mpaka kieleweke, wao wana pesa sisi tuna mungu, tunataka kuwakomboa, sidhani kama hizi ndio sera za kuwavutia watu.
Itakumbukwa Chadema imekuwa ni chama cha matamko toka Bavicha wachaguane mpaka leo wameishatoa matamko yaidi ya 10 lakini hakuna hata tamko mmoja ambalo wamelezea mipango ya Chadema kimaendeleo kuwasadia vijana zaidi ya maandamano.