BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,331
Nakubaliana nawe lakini Nyerere alikuwa ni kiongozi tofauti na hawa waliokuja nyuma yake. Nyerere hakuwa na tamaa ya kujilimbikizia mali kama waliokuja baada yake. Aliipenda Tanzania na Watanzania ukilinganisha na hawa wa awamu zilizofuata. Baba wa Taifa labda kwa makosa yaliyojiri wakati wa awamu yake akaona umuhimu wa kuwa na mfumo wa vyama vingi. Hivyo pamoja na tume iliyoundwa kupiga chini mfumo wa vyama vingi kwa kudai kwamba Watanzania waliotoa maoni wakati ule kusema ungeleta fujo na hata vita vya wenyewe kwa wenyewe yeye akaupigia debe na kusema kwamba nchi yetu imeshakomaa kisiasa na hivyo kuhitaji mfumo wa vyama vingi.
Fikiria haya madudu chungu nzima ya ufisadi wa kutisha katika awamu zilizofuata baada ya ile ya Baba wa Taifa ambayo yameugharimu sana uchumi na maendeleo ya nchi yetu. Mimi naamini kama si mfumo wa vyama vingi madudu haya yaliyojaa ufisadi wa kutisha KAMWE tusingeyafahamu hata chembe. MACCM yangeficha kuhusu rada, EPA, Richmond/Dowans, MV uozo, Nyumba za Serikali, mikataba ya madini, IPTL, SYMBION, Escrow, Kagoda, Meremeta, Uuzwaji wa NBC etc.
Fikiria haya madudu chungu nzima ya ufisadi wa kutisha katika awamu zilizofuata baada ya ile ya Baba wa Taifa ambayo yameugharimu sana uchumi na maendeleo ya nchi yetu. Mimi naamini kama si mfumo wa vyama vingi madudu haya yaliyojaa ufisadi wa kutisha KAMWE tusingeyafahamu hata chembe. MACCM yangeficha kuhusu rada, EPA, Richmond/Dowans, MV uozo, Nyumba za Serikali, mikataba ya madini, IPTL, SYMBION, Escrow, Kagoda, Meremeta, Uuzwaji wa NBC etc.
Ni kweli unachoongea maana yangu ni kwamba wakati wa utawala wa Mwalimu Nyerere hapa Tanzania ufisadi ulikuwa mdogo sana, akaja Rais Mwinyi akawa ni weakness ya kutokusanya kodi. Mambo yaliharibika wakati wa Rais Mkapa ubinafsisaji wa nyumba za serikali, NBC, mikataba mibovu ya serikali kwa migodi ya madini, shirika la posta na air tanzania kufa, alipokuja Rais Kikwete ndio mambo yakawa worse. Maana yangu ni kuwa wakati wa chama kimoja Tanzania haikuwa kama Zaire ya Mobutu ama Afrika ya kati ya Bokassa. Ukiangalia hata matumizi ya serikali wakati wa chama kimoja yalikuwa mazuri elimu na afya ilitolewa bure na nzuri.