Dege Hili la Kisovieti Balaa

Dege Hili la Kisovieti Balaa

Bingwaman

JF-Expert Member
Joined
Oct 22, 2010
Posts
548
Reaction score
288
Muungano wa Nchi za Kishoshalisti za Kisovieti (USSR) ulikuwa ni mahiri katika uundaji wa ndege. Moja ya aina nyingi za ndege nyingi zilizotengenezwa na USSR kabla ya kuvunjika kwake mwanzoni mwa miaka ya 1990 ni Tupolev Tu-114 iliyotumika kusafirisha abiria. Ndege hii iliyoruka mara ya kwanza 1955 na kustaafishwa 1976 bado inashikilia rekodi ya dunia ya kuwa ndege inayoendeshwa na mapangaboi (propellers) yenye kasi zaidi duniani. Muundo wake na injini za turboprop zenye nguvu kubwa ziliiwezesha Tu-114 kuruka kwa kasi ya kilomita 880 kwa saa, sawa na ndege za abiria za jet za wakati huu (modern jetliners). Iliporuka mara ya kwanza, Tu-114 ilikuwa ni ndege kubwa zaidi ya abiria duniani na yenye uwezo wa kusafiri umbali mrefu zaidi bila kutua (kilomita 10,000). Ndege hiyo iliweza kubeba hadi abiria 220 na ilikuwa na injini nne aina ya Kuznetsov NK-12 ambazo kila moja ina nguvu ya horsepower 14,000. Kuznetsov NK-12 ni injini za turboprop zenye nguvu zaidi kuwahi kutengenezwa duniani. Kila moja ya injini za Tu-114 iliendesha mapangaboi mawili yaliyozunguka pande tofauti (contra-rotating propellers). Mapangaboi hayo yalikuwa na kipenyo (diameter) cha zaidi ya mita tatu. Tu-114 ilitumika kumsafirisha kiongozi wa zamani wa USSR Nikita Khrushchev kutoka Moscow mpaka New York na kurudi bila kutua (non-stop) mwaka 1959 kabla ya kuanza kusafirisha abiria mwaka uliofuata. Wamarekani walikubali wamepigwa bao kabla ya kujibu mapigo na Boeing 707. Sehemu pekee unapoweza kuiona Tu-114 ni katika makumbusho kadhaa za usafiri wa anga nchini Russia.

Tu114%20CCCP-L5611%20d6.jpg


tu114_stevebrimley.jpg


Watoto wakiwa wamepozi pembeni ya mapangaboi ya Tu/114
TU-114_engines.jpg
 
Duh aisee hata nikilipiwa nauli hili dude sipandi....limekaa ki-kufa kufa.....

Mkuu, usiwe na wasiwasi. Ndege hizi kwenye picha zinaonekana chakavu kwa sababu zimekaa makumbusho zaidi ya miaka 30. Ikumbukwe kuwa ziliruka mara ya mwisho 1976. Tu-114 ni moja ya ndege za abiria zilizokuwa salama zaidi katika historia ya usafiri wa anga. Ndege hii ilipata ajali mara moja tu katika miaka 16 ya kusafirisha abiria na ajali hiyo ya mwaka 1966 ilitokana na uzembe wa rubani.
 
Mkuu Bingwaman nikushukuru kwa bandiko murua. Zaidi nafurahia kuona orodha inaongezeka ya wanajukwaa wanaobandika kwa kutumia Kiswahili (akina MziziMkavu, Millah, na wengineo). Inatia moyo kuona kuwa kumbe inawezekana kutumia Kiswahili kuelezea mambo ya kisayansi na teknolojia.

Asanteni sana!
 
Last edited by a moderator:
they are safer tha modern ndege tunazozipanda leo mimi nikipanda Jet huwa sina amani coz hata kunguru mmoja tu anatosha kuangusha ndege
 
Lilete huku mtaani kwetu tulipime chuma chakavu.
 
Warusi wako mbali sana ktk kuunda ndege.hivi sasa wana dege moja nimesahau jina linabeba kijiji kizima na mizigo na magari juu.ndani kuna mpaka hoteli na vyumba vya kulala
 
Warusi wako mbali sana ktk kuunda ndege.hivi sasa wana dege moja nimesahau jina linabeba kijiji kizima na mizigo na magari juu.ndani kuna mpaka hoteli na vyumba vya kulala

Hilo dge kiboko,huwezi kutuwekea picha zake mkuu,tupate kuliona......!!Yaani kama kijiji cha LUGOBA chooote ndani......:tape2:
 
Hiyo antonov inauwezo wa kubeba watu wangap mkuu?au uzito wa kias gan?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Wakuu hilo Antonov linaruhusiwa kutua bongo? Mbona hizo kama ingine ya train? Au macho yangu
 
Mkuu, usiwe na wasiwasi. Ndege hizi kwenye picha zinaonekana chakavu kwa sababu zimekaa makumbusho zaidi ya miaka 30. Ikumbukwe kuwa ziliruka mara ya mwisho 1976. Tu-114 ni moja ya ndege za abiria zilizokuwa salama zaidi katika historia ya usafiri wa anga. Ndege hii ilipata ajali mara moja tu katika miaka 16 ya kusafirisha abiria na ajali hiyo ya mwaka 1966 ilitokana na uzembe wa rubani.
...itazame hii post hapa chini...zile zinazoanguka congo ni vipi?
madege haya DRC bado yanatumika
kweli mkuu..ishadondoka kule
 
Hilo dge kiboko,huwezi kutuwekea picha zake mkuu,tupate kuliona......!!Yaani kama kijiji cha LUGOBA chooote ndani......:tape2:

Kinapatikana wapi hicho kijiji mkuu!
 
Back
Top Bottom