Ben
Ntarudi hila umekimbia sababu nyingi sana za msingi kama kwanini marekani kuna states ambazo wao wanavote upande mmoja siku zote bila ya kujali maslahi yao, kwanini kunatofauti kubwa ya kimawazo baina ya states na hii ni nchi inayoongoza kwa demokrasia na ufahamu wa mambo. Halafu kuna enough resources to deal with upheaval and leaders who understand their societies wewe unadhani kwanini John McCain aliposhindwa kitu cha kwanza kukisema 'America has spoken my friends we have lost the battle' na kuendelea na speech yake ambayo ilijaa kutuliza hasira zaidi kuliko normal conceding speeches.
Bado ujagusia majimbo yenye usumbufu huko India au huko Russia mpaka leo hii na wanasumbua serikali zao kwa kuwa bado democracy zao pia ni changa vilevile. Unakimbilia mfano wa uswisi na amerika ambapo huko ni strong liberal democratic societies na mambo yanafanyika tofauti sana. Mfano kuna watu wanaweza wa judge marekani kwa sasa kama wadini kutokana na interest zao za uchumi lakini uliza yule pastor aliechoma quran ndani ya america kama walimuacha au ukienda kwa waingereza uliza jamaa wanaojaribu kuleta ubaguzi wa dini kama maandano yanachukua hata nusu saa na aichukui muda wahusika wakuu kutungiwa kesi.
Point hapo ni kwamba usitoe mifano ya liberal democracies these people know how to control their societies scientifically to maintain peace, na nchi kama Tanzania kujiingiza kichwa kichwa katika vitu ambavyo vipo very complicated and can easily sway people allegiences towards division, leo unaona masheikh na mapadri wanavyo ichachafya serikali na hapa ndio mnasema uwanja wa wasomi na bado watu wanabishana kwa kuwatetea hata pasipo staili. Mtaweza kweli ku-control ukanda.
Bado narudi kwenye effective governance maana huko ndiko kwenye mjadala wenyewe ingawa ujaja na point zaidi ya mifano hewa tu ya kuelezea how governance would be like in your ideal federalism kwenye nchi kama yetu na si America or any other liberal democracy we are far from that sio tu kutokana na wananchi hata siasa zetu zenyewe bado hazija fahamiwa na wengi kuhusu namna gani maendeleo yao yanatakiwa kuja, sasa hivi wamechoka lakini the desperate methods are not encouraged by any developed society of any state formation.
Thank you Eric,thank You!
Kwamba ni kwa nini majmbo yana-vote tofauti na kuwepo kwa tofauti kubwa ya kimawazo ni kwamba kuna number of factors.Mojawapo amabyo ni relevant kwenye Discussion yetu ni kuwa kumekua na historia(historical) na urithi wa kiutamaduni(Cultural Heritage0 ambayo yapo influenced sana na historia ya utumwa,historia ya civil rights movement,Civil war e.t.c. Soma George C.Wallace-D's American Independent Party.
kwa mfano majimbo ya South yamekua aligned sana na Democrats kutokana na sera zao na ilani zao za uchaguzi kuegemea kwenye sentiuments na historia ya watu wa south hivyo kuendelea kuwa-shape katika reasoning in all aspects kwa kuwa politics is toxic and contagious.Majimbo ya kusini yalitegemea wafanyakazi watokanao na biashara ya utumwa kwa kuwa njia zao za kiuchumi zilikua ni Cash Crops.Dini pia imechangia hasa madhehebu ya Catholics na Protestants.
Vyama vya siasa vilipoingia Marekani katika muhula wa Kwanza George Washinton alipata sapoti ya North aliposimamia hoja ya Federalists wakati majimbo ya kusini yalisimama nyuma ya Thomas Jefferson na tafsiri yake ya 10th Amendment.Tofauti iliyokuwepo ya kimsimao katika masuala ya tax,tariffs,civil rights movement na slavery ilipelekea seccesion movement kama niliyoandika katika post zilizotangulia na kusababisha Civil war katika utawala wa Abraham Lincoln.Majimbo ya kusini yalifanya Jaribio hatari la kuunda confederate states of America na mji mkuu kuwa Richmond ingawa majeshi ya union yalishinda dhidi ya confederate Army lakini tunashuhudia walivyojifunza in hard way na mataifa mengine yalijifunza hata nigeria kwenye BIAFRA War.Ku Klax klan na falsafa zake zimeendelea kubaki kuwa learning curve kwenye theories of federation,decentralization and unitary systems.Hata hivyo tofauti ya voting bado imeendelea kuwa shaped kwani Republicans wameweza kuchukua baadhi ya majimbo ya South Kama New England na dems wamechukua Maine na Vermont.DIfferent opinions na deviation inatokana na history.Kwa mfano kuna yale majimbo amabyao ni swing states ambayo hayana uamuzi wa moja kwa moja.Hayo pia yameathiriwa na historia hasa hali ya kisiasa,kiuchumi na demographics.Kuna suala la uhamiaji ambalo huwa linategemea upoepo tofauti na baadhi ya factors ambazo partially ziko fixed kama spanish wanajulikana wako sympathetic na upande mmoja.Majimbo ya kusini yamekua na war veterans(McCain ni war veteran:Refer vietnam War).Katika marais 12 wa kwanza na wakuu wa majeshi Marekani walitokea south.Kwa hiyo kuna factors nyingi ambazo ni traditiona zinaleta influence
Huko india unataka nizungumzie jimbo lipi Eric? unataka nizungumzie jimbo la Jammu na Kashmir?Nagaland?Haya ni masuala ambayo yanaweza kujadiliwa kwenye mjadala mwingine hasa tutakapojadiliana kuhusu Insurgency,terrorism and counter-terrorism.Haya yote yapo kwenye subnationalism movement ambazo ni janga la kimataifa lakini kwa kuwa tunaiga demokrasia ya Magharibi basi hatuna budi kujifunza kutokana na historia ya makosa ya Mababa wa demokrasia tunaowaiga.India baada ya kupata uhuru wanasiasa walijiingiza kwenye mchezo wa power grabbing.uamuzi uliochukuliwa kuhusu Kashmiri na pia wanasiasa kufuata ntend ya lingustic ilikua kupalilia sub-nationalism.Kwa mfano kulikua na ant-hindi kule kwa watu wa Tamil Nadu.Hebu soma historia ya assasination of Indira Gandhi (Pamoja na kwamba kuna mwanasiasa kilaza aliandika hapa juzi kwenye makala na kuupotosha umma kwa maslahi yake) halafu historia ya kifo cha Rajiv Gandhi baada ya kupeleka Jeshi la India kupambana na waasi wa tamil Tigers kule Sri Lanka.Actuaally hapa kuna mambo mengi ambayo tunatakiwa kujifunza kutoka kwa wenzetu kabla hatujasubiria kujifunza kutokana na makosa yetu.Jenerali Ulimwengu juzi aliandika '
kujifunza kutokana na makosa yetu gharama yake ni kubwa mno'.Tusikubali sasa mfumo huu tulio nao utufundishe kulingana na makosa yetu
.Suala la Kashmir kuna religious hegemony ambalo ndilo lililosababisha Taifa la Pakistani kuundwa.Haya tunaweza kuyakwepa kwa kujifunza na kuna post yangu hapo juu niliongelea decentarlization na kujadili jinsi tunavyoweza kuwa na harmony kwa pande zote za bara na visiwani in regardless of muslims in Zanzibar and christians in mainland(Ingawa kote kuna dini zote)
Tafiti nyingi zinaonyesha Taifa kubwa kama la India lingeweza kuwa na kiwango kikubwa cha Rushwa bila kufuata mfumo huu.Ingawa bado India haifuati full federalism lakini mfumo huu umelisaidia Taifa hili la pili duniani kwa Idadi ya watu Bilioni 1 nyuma ya China.Kwa mfano ukitaka kuongelea tatizo la India kwenye Mfumo huu utaongelea upungufu wa nilichosema wa Rushwa kwenye Intelligence system ndiyo maana Maoist wanataka kujitenga na kuunda Taifa lao lenye mrengo wa China au Nepali.Wanasiasa wanatumia udhaifu wa mfumo huu kuchochea Movement kwa majimbo kama Jharkhand,Orissa,West bengal,Andhya Pradesh,Mandhya Pradesh,Utter Pradesh East na Bihar.majimbo haya mawili ya mwisho ndiyo maskini zaidi india.Na hata hivyo suala la umaskini wao lingeonekana kuwa mbaya zaidi kama kusingekua na mfumo huu.Pia ni jambo la hatari na linatakiwa kuwa adressed immediately kwa kuwa ni rare case kutokea kwa movement ambayo ina sapoti ya local people kuwa defeated.hili linaumiza vichwa magwiji wa subnationalisms.Hapa tunajifunza,CHADEMA ni chama cha utafiti na kinatumia wataalamu kufanya uamuzi.hayo yote hapo juu yanaeleweka na tumejipanga.Huu ndiyo msingi wa kuhimiza mafunzo na pia ku-encourage vijana,na wanasiasa wetu kuendelea kusoma vitabu kuufahamu mfumo huu ambao ni bora kulinganisha na mfumo tulionao.Tuna mfumo usiokua na kanuni na wala muongozo wa kushughulikia sub-nationalism.Hautoi taswira ya demokrasia zaidi ya taswira ya mabavu na ukoloni usiokua na chembe ya ustaarabu..mfumo tulio nao pamoja na mabavu na vitisho unapanda mbegu za sub-nationalism movement kwa kasi hasa pale ambapo raia wake wanapoelimika.UAMSHO ni mfano mmoja tu.
Switzerland nimetoa mfano kwa kuwa ni taifa lenye makabila,sura ya utaifa tofauti.ndani ya Taifa la Uswis kuna Ujerumani,Ufaransa,Italia,uingereza n.k. Cantonments zimekua na nguvu na kuhudumia raia wake kutokana na ubora wa katiba yao pamoja na kuwa na diversity kubwa.Ingependeza kama vyama vya siasa vingetoa elimu ya uraia kwa karibu kama CHADEMA kinavyofanya ili kutengeneza awareness.Tumeiga demokrasia huko,tutaiga yale mazuri na kujifunza kutokana na makosa.kuna uwezekano Tanzania chini ya CHADEMA ikawa The Giant nation in Africa in regardless kwamba wengine wameshindwa