Ben Saanane
JF-Expert Member
- Jan 18, 2007
- 14,580
- 18,227
Nimefarijika sana na taarifa za chama changu CHADEMA kufuata muundo wenye sura ya majimbo. Kumbe ndani ya chama changu kulikuwa na watu wenye mawazo kama haya.
Hii ilikuwa kiu yangu ya muda mrefu na hoja hii iliwakuna vijana wengi wakati nagombea uenyekiti wa BAVICHA.
Wachambuzi na wasomi wengi wanakubaliana na hoja hii hata hapa JF tumeona baadhi ya wanachama na wapenzi wa CHADEMA wakihimiza na kushauri sana kuhusu muundo huu. Nimefarijika sana kwakuwa hii ilikuwa mojawapo wa ajenda zangu na niliipa kipaumbele namba 8 kama nilivyotangaza Tarehe 28/04/2011 pale Travertine Hotel nilipotangaza nia yangu ya kugombea nafasi ya kuongoza BAVICHA na nilidhamiria kuunda Baraza lenye muundo huu chini ya kauli Mbiu yangu katika uchaguzi ule ya MOVEMENT FOR RADICAL CHANGE.
Katika ajenda yangu namba 8 niliandika:-
Nimefurahi kuona jinsi chama changu kilivyo flexible na kufanya utafiti wa kina. Inawezekana kipindi kile ningeonekana nimekurupuka lakini CHADEMA siku zote wanatanguliza tafiti na kufanya siasa za kisayansi. Hii ni faraja kwangu kwamba hata sisi vijana tunaweza kuwa na mitizamo ambayo ikifanyiwa kazi kwa umakini inaweza kuleta mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ndiyo maana CHADEMA kimeendelea kuwa kinara kwa kupendwa na vijana wa kada zote.
Naendelea kuamini kuwa hakuna chama kinachoweza kwenda na kasi ya vijana katika mabadiliko tuyatakayo zaidi ya CHADEMA ambako mawazo huru na yenye muelekeo chanya yanafanyiwa Tafiti kwanza na kisha kuwekwa katika matendo.
Muundo huu utakisaidia sana chama chetu.
Robert Oberst aliandika kuhusu muundo huu wa majimbo changamoto na faida zake katika kitabu chake kiitwacho Administrative conflict and decentarlization : The case of Sri Lanka.
Pia Dr. Ugo Mattei aliandika kuhusu hili alipokua akijadili kwa undani utungaji katiba Afrika katika andiko lake ‘Patterns of African Constitution in the Making''.
Sasa kwa kuwa lengo la CHADEMA ni kuishi kulingana na tunayohubiri na kutoa taswira ya serikali yetu ya baadae naendelea kuhimiza wanasiasa vijana ndani ya chama changu kuendelea kusoma vitabu mbalimbali na kuuelewa mfumo huu kwa haraka wakati mafunzo yanaendelea kutolewa na kitengo husika.Diana Conyers wa Chuo kikuu cha Sussex anaendelea kufanya uchambuzi katika kitabu chake kwa kujiuliza '' Decentralization: The Latest Fashion in Development Administration?
CHADEMA, tuendelee kuweka katika matendo yale tunayohubiri ili kujitofautisha na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachohubiri kuwa ‘Chama cha Mapinduzi' lakini kinoogopa Mabadiliko makubwa ya kimfumo (Radical Reform) na wakati huo huo wakisindikizwa na unafiki wa kueneza itikadi ya Ujamaa huku Rushwa ikishamiri ndani ya chama chao kutokana na kutoka kaktika mfumo wa wa maadili yenye kiwango (deviation from moral standards). CHADEMA tunaendelea kujikita kwenye misingi yetu huku CCM wakiendelea kuondoka katika misingi waliyojiwekea. Ni dalili ya chama kinachoingia kaburini. Miaka miwili kabla ya Uchaguzi UNIP walionyesha dalili hizi kule Zambia, KANU walionyesha Dalili hizi miaka 4 kabla ya Uchaguzi kule Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1997, Chama cha Congress nchini India kilionyesha Dalili hizi kuanzia mwaka 1998 kabla ya kuwekwa Kando chama cha Bharhat Janarta Party (BJP) na hivyo kuwapa fursa ya kurudi kwenye misingi yao ndipo kikaweza kurudi madarakani.
Nampongeza Mhe. John Mnyika kwa kubeba ajenda ya Baraza Huru la Vijana na kutumia fursa yake ya kuwa mbunge kupeleka hoja binafsi bungeni. Huu ni mfano wa kuweka mahubiri katika matendo kwani alipokua akiongoza kurugenzi za vijana alipambana sana kuhusu BARAZA huru la vijana. Nilimuunga mkono katika mapambano hayo na ajenda hii niliendelea kuibeba katika kinyang'anyiro cha uchaguzi BAVICHA. Ilikuwa ajenda namba 5.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-wagombea-hawa-wa-bavicha-chadema-taifa.html
Siku za usoni nitaandika kwa kina kuhusu umuhimu wa muundo huu kulingana na itikadi na falsafa ya CHADEMA ya "Nguvu ya Umma" na pia nitalinganisha na vyama vya siasa na serikali zilizofanikiwa kwa kufuata Muundo huu.
Hii ilikuwa kiu yangu ya muda mrefu na hoja hii iliwakuna vijana wengi wakati nagombea uenyekiti wa BAVICHA.
Wachambuzi na wasomi wengi wanakubaliana na hoja hii hata hapa JF tumeona baadhi ya wanachama na wapenzi wa CHADEMA wakihimiza na kushauri sana kuhusu muundo huu. Nimefarijika sana kwakuwa hii ilikuwa mojawapo wa ajenda zangu na niliipa kipaumbele namba 8 kama nilivyotangaza Tarehe 28/04/2011 pale Travertine Hotel nilipotangaza nia yangu ya kugombea nafasi ya kuongoza BAVICHA na nilidhamiria kuunda Baraza lenye muundo huu chini ya kauli Mbiu yangu katika uchaguzi ule ya MOVEMENT FOR RADICAL CHANGE.
Katika ajenda yangu namba 8 niliandika:-
''8. Nitaliongoza baraza kuhakikisha chama kinafika katika kila kona ya nchi yetu kwa kuunda mtandao wenye sura ya mfumo wa majimbo ili kurahisisha ugawanyaji wa raslimali za kuliendesha baraza katika ngazi zote na kulisogeza karibu zaidi na wananchi (Decentralization).
Hili ni vuguvugu la nguvu (Aggressive Movement) lenye lengo la kukabiliana na chama dhalimu (Brutal party) kama CCM chenye fursa za ziada (Added advantages) za kumiliki raslimali za taifa kwa maslahi yake tangu enzi ya mfumo wa chama kimoja, katika kipindi ambacho Chama na Serikali vilikuwa haviwezi kutenganishwa.
Hii ni ajenda nyingine, inahitaji mjadala lakini nitaifanyia kazi.''
Nimefurahi kuona jinsi chama changu kilivyo flexible na kufanya utafiti wa kina. Inawezekana kipindi kile ningeonekana nimekurupuka lakini CHADEMA siku zote wanatanguliza tafiti na kufanya siasa za kisayansi. Hii ni faraja kwangu kwamba hata sisi vijana tunaweza kuwa na mitizamo ambayo ikifanyiwa kazi kwa umakini inaweza kuleta mabadiliko ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ndiyo maana CHADEMA kimeendelea kuwa kinara kwa kupendwa na vijana wa kada zote.
Naendelea kuamini kuwa hakuna chama kinachoweza kwenda na kasi ya vijana katika mabadiliko tuyatakayo zaidi ya CHADEMA ambako mawazo huru na yenye muelekeo chanya yanafanyiwa Tafiti kwanza na kisha kuwekwa katika matendo.
Muundo huu utakisaidia sana chama chetu.
Robert Oberst aliandika kuhusu muundo huu wa majimbo changamoto na faida zake katika kitabu chake kiitwacho Administrative conflict and decentarlization : The case of Sri Lanka.
Pia Dr. Ugo Mattei aliandika kuhusu hili alipokua akijadili kwa undani utungaji katiba Afrika katika andiko lake ‘Patterns of African Constitution in the Making''.
Sasa kwa kuwa lengo la CHADEMA ni kuishi kulingana na tunayohubiri na kutoa taswira ya serikali yetu ya baadae naendelea kuhimiza wanasiasa vijana ndani ya chama changu kuendelea kusoma vitabu mbalimbali na kuuelewa mfumo huu kwa haraka wakati mafunzo yanaendelea kutolewa na kitengo husika.Diana Conyers wa Chuo kikuu cha Sussex anaendelea kufanya uchambuzi katika kitabu chake kwa kujiuliza '' Decentralization: The Latest Fashion in Development Administration?
CHADEMA, tuendelee kuweka katika matendo yale tunayohubiri ili kujitofautisha na Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachohubiri kuwa ‘Chama cha Mapinduzi' lakini kinoogopa Mabadiliko makubwa ya kimfumo (Radical Reform) na wakati huo huo wakisindikizwa na unafiki wa kueneza itikadi ya Ujamaa huku Rushwa ikishamiri ndani ya chama chao kutokana na kutoka kaktika mfumo wa wa maadili yenye kiwango (deviation from moral standards). CHADEMA tunaendelea kujikita kwenye misingi yetu huku CCM wakiendelea kuondoka katika misingi waliyojiwekea. Ni dalili ya chama kinachoingia kaburini. Miaka miwili kabla ya Uchaguzi UNIP walionyesha dalili hizi kule Zambia, KANU walionyesha Dalili hizi miaka 4 kabla ya Uchaguzi kule Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1997, Chama cha Congress nchini India kilionyesha Dalili hizi kuanzia mwaka 1998 kabla ya kuwekwa Kando chama cha Bharhat Janarta Party (BJP) na hivyo kuwapa fursa ya kurudi kwenye misingi yao ndipo kikaweza kurudi madarakani.
Nampongeza Mhe. John Mnyika kwa kubeba ajenda ya Baraza Huru la Vijana na kutumia fursa yake ya kuwa mbunge kupeleka hoja binafsi bungeni. Huu ni mfano wa kuweka mahubiri katika matendo kwani alipokua akiongoza kurugenzi za vijana alipambana sana kuhusu BARAZA huru la vijana. Nilimuunga mkono katika mapambano hayo na ajenda hii niliendelea kuibeba katika kinyang'anyiro cha uchaguzi BAVICHA. Ilikuwa ajenda namba 5.
https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...a-wagombea-hawa-wa-bavicha-chadema-taifa.html
Siku za usoni nitaandika kwa kina kuhusu umuhimu wa muundo huu kulingana na itikadi na falsafa ya CHADEMA ya "Nguvu ya Umma" na pia nitalinganisha na vyama vya siasa na serikali zilizofanikiwa kwa kufuata Muundo huu.