Mentor elewa kwamba experience ndio mwalimu bora kuliko wote. Lara1 ameshikilia msimamo wa wadada wengi sana wa karne hii na msimamo huo sio kwamba walizaliwa nao ila wamejifunza kadiri wanavyokuwa. Wanaume wanaokutana nao, wanaofahamiana nao, wanaowaona na ndugu/marafiki au hata majirani ndio haswaa wamewafanya wajali kile ambacho wao wanaona kitawapunguzia maumivu pale itakapotokea mwanaume aliyempa nafasi ya kuwa nae amemuangusha kwa namna moja au nyingine.Yani badala ya kulia sana na kujutia yule aliyemtolea nje kwaajili jamaa na mwishowe jamaa kuoa mwanamke mwingine, atajifariji na kile ambacho alikipata akiwa na nae. Kama ni pesa, biashara, nyumba, usafiri n.k ataona angalau it wasn't all for nothing.
Kama mnataka mabadiliko, wewe na wakaka wengine anzeni kuwa watu ambao wanawake watataka kuwa na nyie bila kuwa na hofu ya nyie kuwaDISSAPOINT sana mpaka wafikirie kujiwekea insuarance kama sio assurance kuwa at the end of the day she won't be THE sour loser. Fanya wanaomzunguka yule ulonae wamuonee wivu, wamuonee raha na sio wamuonee huruma kwa kuwa naive, kujitoa kwa mtu asiye na shukrani au kugeuzwa tambara la deki. Fanya wale wanaomuangalia, hususani wadogo zake/marafiki zake waone kwamba kuna aina nyingine ya wanaume, wanaume walio reliable, wanaume walio faithful, wanaume wanaojali and so on. Mpe kile unachoweza (love, attention, support iwe financially au emotionally, msaada nyumbani) kadiri unavyoweza kwa roho moja bila malalamiko. Toa ili na wewe upokee. And ofcourse . . .acheni kutumia hiyo mishahara yenu yenye mipango mia kidogo kama chambo.
Lastly,kuingia kwenye ndoa takes more than ones mtazamo. Unaweza ukampata mwenye mtazamo unaotamani Lara1 angekuwa nao na bado ndoa yako ikawa kizungumkuti, na unaweza ukampata mwenye mtazamo sawa na wa Lara1 na ukajikuta unajiuliza ilikuwaje siku zote ulikuwa unapingana na kile kikufaacho.