Song of Solomon
JF-Expert Member
- Aug 5, 2021
- 2,733
- 5,490
BIASHARA ya ukahaba, licha ya kushamiri katika maeneo makubwa ikiwemo Dar es Salaam, madhila wanayokutana nayo makahaba ni makubwa ikiwemo kushiriki ngono na kutolipwa, kubakwa, kupigwa na pia ni kazi ambayo inahatarisha maisha yao na pengine kupoteza maisha.
Uchunguzi uliofanywa na Habarileo Online katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, umebaini kuwepo kwa madanguro ambapo wanawake na wasichana walio na umri kati ya miaka 15 - 40 hujihusisha na biashara hiyo.
Biashara hiyo kongwe katika historia ya maisha ya binadamu, imekithiri zaidi katika majiji makubwa duniani ambapo wanawake huuza miili yao ili kujipatia fedha za kuendesha maisha.
Maeneo maarufu ambayo biashara hiyo ya dada poa ufanyika ni Sinza, Magomeni, Friends Corner, Kinondoni Masaki, Oysterbay, Ubungo, Urafiki, Riverside, External, Manzese, Maeneo mengine ni Kimboka (Buguruni), Tabata Magengeni, Segerea, Kinyerezi, Temeke Mwisho, Sudan, maarufu kwa Wahaya, Mbagala Kizuiani, Zakhem na maeneo yanayotazamana na Mlimani City Barabara ya Sam Nujoma.
Mtandao huu pia imebaini baadhi ya wanandoa wanashiriki katika vitendo ama kwa wanaume kununua au wanawake kuwa sehemu ya dadapoa wanaosaka wateja kwa makubaliano ya malipo ya fedha.
Aidha mtandao huu pia umebaini kuwa wengi wanajitumbukiza kwenye biashara hiyo ya ukahaba ili waweze kujikimu kimaisha, lakini je yapo matumaini?
Hatari wanayopitia:
Sarahabiba binti anyejihusisha na ukaaba maeneo ya Manzese anasema “Tunaonekana ni watu tusio na maadili kwenye jamii, tunaepukwa na wengi kwenye jamii inayotuzunguka, wanatunyanyapaa.
“Tunapitia hatari nyingi, tunajiweka rehani maisha yetu ili tu tuhakikishe familia zetu zinapata kula,” anasema Rahel, binti mwingine anayefanya biashara ya ukhaba eneo la Ubungo External jijini Dar es Salaam.
Kuna wakati tunapitia misukosuko mingi, kukamatwa na askari, kupigwa na wateja wetu, wakati mwingine kuuliwa.
“Mtu anakuchukua mnaelewana vizuri, akishapata huduma hataki kutoa hela ukihoji wakati mwingine unaishi kushambuliwa kwa kipigo, wapo waliopoteza maisha kutokana na kazi hii.
“Kuna mwenzetu alichukuliwa vizuri lakini hakuonekana na baada ya siku mbili tukapata taarifa za mwili wake kuonekana ukiwa umetelekezwa kwenye majani maeneo ya ustawi wa jamii.”anasema Rachel
Amina, mwenye miaka 22 sasa , mkazi wa Kinondoni, anasema alianza biashara ya ngono akiwa na umri wa miaka 15 alipopata mimba ya mtoto wake Subira, mpenzi wake alimuacha,
“Napitia haya yote kwa ajili ya binti yangu, nimepitia uchungu mwingi sana eneo hili, nataka mwanangu aje kuwa wakili ili anipiganie mimi na wengine wanaodhulumiwa
Binti mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Rose mkazi wa Sinza, akielezea alivyojitumbukiza kwenye biashara ya ngono anasema “Wazazi wangu baba na mama walifariki nikiwa mdogo (kilio).”Ninaambiwa walifariki kwa ajali, nililelewa na bibi, lakini nikiwa na miaka 10 bibi yangu alifariki, pale ndipo nilianza kuishi maisha ya uchungu, sitaki kuyaongelea haya (kilio).
Mikasa kwenye maisha ya Rose iliendelea baada ya kulazimika kukatisha masomo na kuingia mitaani kufanya kazi za ndani ambako alijikuta akiishia kubakwa na baba mwenye nyumba.
“Kutokana na maisha niliyoyapitia, nikajikuta naingia kwenye biashara ya ngono, yale niliyoyapitia sitaki wapitie wengine, ndio maana nimekuwa nikisimama imara napigania maisha yangu kwa nguvu hadi tone la mwisho la damu yangu.
Happy mkazi wa Magomeni, akielezea madhila ambayo amewahi kukumbana nayo katika kazi yake hiyo ya biashara ya ngono anasema “Nilikutana na jamaa klabu, akanichania nguo, akachukua na hela yangu sh 60,000 kutoka kwenye sidiria yangu, nilikuwa nang’ang’ana kutoka ila alinipiga kwa nyuma ya shingo, angeniua maana alinishtukiza ila mabaunsa wa klabu walinisaidia na alichukuliwa na Polisi.
Kuna wakati pia tunakamatwa na Polisi kwa uzururaji unalazwa lokapu hujui nyumbani watoto inakuaje?
Umaskini:
Chonge mkazi wa Mwananyamala, anayefanya biashara ya ngono maeneo ya pembezoni mwa Leaders Club anasema “wengi tunalea watoto wenyewe bila ya usaidizi wa baba, maisha ni magumu, pesa inavyoadimika ndio na hatari zaidi kwetu inavyoongezeka, maana ili tujikimu inabidi tuendelee tu kufanya biashara hii.
Tumekuwa tukikutana na madhila mengi, ni biashara ngumu wengine wamekuwa wakiishi wengi kwenye chumba kimoja maarufu ya ghetto, lakini wengine wamepangisha vyumba na kuishi maisha mazuri.
Corona yachagiza ugumu wa maisha:
Ugonjwa wa Corona umefanya maisha yao kuwa magumu zaidi, kuanzia mwaka jana mwezi wa tatu serikali ilipotangaza kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Corona nchini, biashara imekuwa ngumu zaidi kwa madada poa.
“Kidogo sasa hivi hali inaanza kuwa nzuri, lakini kipindi Corona imeshamiri biashara ilikuwa ngumu, ilifika kipindi unapigwa na baridi hupati mteja hata wa buku yaani,” anasema dada Poa aliyefahamika kwa jina la Pili mkazi wa Magomeni Usalama na kuongeza “Lakini kwa sasa hesabu ya wateja angalau inaanza kuongezeka.
Kabla ya Corona mtu unauhakika wa kupata kuanzia sh 50,000 hadi 100,000 kwa usiku mmoja, na wakati mwingine siku inakuwa nzuri zaidi unaweza pata zaidi ya kiasi hicho.
Lakini tangu kuingia kwa ugonjwa huu, mambo ni magumu, ukipata sh 30,000 unashukuru, wateja walipungua sana
Wanenavyo wanaume:
James Lweno (sio jina halisi) anasema, huwa tunawafuata mitaani kwa kuwa kuna kahaba zaidi ya 1,000 mjini Dar es Salaam wanaohangaika kusaka maisha.
Gerald mkazi wa Kigamboni anasema “Kwangu mimi naona biashara hii ya ukahaba imeota mizizi nchini kwa kuwa wanaume wengi wana msongo wa mawazo, hakuna sheria kali, umaskini na malezi, ushawishi toka kwa makundi rika.
Akifafanua anasema “Wanaume wanakuwa na msongo wa mawazo hawana mahusiano mazuri na wenza wao hivyo wanaona chaguo sahihi ni kwenda kununua ngono. Pia hakuna sheria kali inayozuia biashara ya ukahaba nchini, kungekuwa na sheria kali ya biashara hiyo, ukimkamata kahaba, mkamate na anayemnunua, biashara hii ingepungua nchini.
Aidha amesema “Watoto wamezaliwa katika familia duni wanajikuta wanaingia mitaani kujitafutia kipato na kujikuta wanakuwa katika malezi yasiyo sahihi, hivyo wanajitumbukiza kwenye ukahaba ili wapate mkate wa kila siku.
Pia Makundi rika mabinti wanashindwa kujizuia tamaa za mwili, kwa kuona wenzake wana maisha mazuri hivyo nae anafuata mkumbo.
Takwimu za Corona:
Kwa mujibu wa takwimu za Tanzania zilizorekodiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) hadi Novemba 9, 2021 zinaonyesha watu 26, 196 wameambukizwa Corona huku kati yao watu 725 wakipoteza maisha.
POLISI
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, anasema elimu itolewe kwa wanaume kwani ndio chanzo cha madada poa, wakiacha kuwanunua wataacha kujiuza.
“Wanaume wakiacha kuwafuata huko mtaani, mara moja watakosa soko na wataachana na vitendo hivyo. Mimi kwa sasa sitatoa SMG kwenda mitaani kukamata dadapoa, ninapambana na majambazi na wahalifu," anasema.
WANASHERIA
Wakili wa Kujitegemea, Daniel Kalasha anasema hakuna sheria inayowabana wanawake wanaojiuza (dadapoa), bali iliyopo inawabana wamiliki wa madanguro na baa zinazotumika kufanya biashara hiyo.
"Mmiliki wa danguro anashtakiwa kwa kosa la kuendesha danguro na akipatikana na hatia anahukumiwa kwa mujibu wa sheria," anasema.
Wakili Kalasha anasema dadapoa akikamatwa, hushtakiwa kwa makosa ya uzururaji katika Mahakama ya Jiji na wakipatikana na hatia wanalipa faini ambayo ni kuanzia Sh. 50,000 hadi 200,000.
Anasema wanaoshindwa kulipa faini, wanakwenda jela miezi sita lakini uzoefu wake unaonyesha kesi hizo mara nyingi haziendelei mpaka mwisho.
Naye Mwanasheria Reuben Semwaza ‘Kinara’ anasema kuthibitisha makosa ya kujiuza ni vigumu kutokana na uhitaji wa uthibitisho kwamba aliposimama au eneo ulipomkuta alikuwa akijiuza.
Semwanza, anasema wamiliki wa madanguro hushtakiwa hata kwa makosa ya kufanya biashara haramu ya binadamu ambayo adhabu yake iko kisheria.
"Ukimiliki danguro kisheria unashtakiwa kwa kuzuia uhuru wa mtu, ukikamatwa una watu umewahifadhi, ukashindwa kujieleza wako kwa ajili ya nini, hakuna taarifa za uwapo wa watu hao, hawana kazi yoyote, unaweza kushtakiwa kwa makosa mawili.
"Kwanza; unashtakiwa kwa kuwa na nia ovu, kumiliki danguro na kosa la pili unaweza kushtakiwa kwa kufanya biashara haramu ya binadamu," anafafanua.
Wakili huyo anarejea kifungu cha namba 4(5) cha Sheria ya Biashara Haramu ya Binadamu inatoa adhabu ya kulipa faini Sh. milioni tano na isiyozidi Sh. milioni 10 au kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka miwili hadi 10.
"Kifungu namba 4(1a) cha Sheria ya Biashara Haramu ya Binadamu kinazungumzia madanguro, uzinzi, umalaya na makosa yote hayo adhabu yake ni faini Sh. milioni tano na isiyozidi Sh. milioni 10 ama jela miaka miwili na isiyozidi miaka 10," amefafanua
Habari leo Nov 18,2021
Uchunguzi uliofanywa na Habarileo Online katika maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam, umebaini kuwepo kwa madanguro ambapo wanawake na wasichana walio na umri kati ya miaka 15 - 40 hujihusisha na biashara hiyo.
Biashara hiyo kongwe katika historia ya maisha ya binadamu, imekithiri zaidi katika majiji makubwa duniani ambapo wanawake huuza miili yao ili kujipatia fedha za kuendesha maisha.
Maeneo maarufu ambayo biashara hiyo ya dada poa ufanyika ni Sinza, Magomeni, Friends Corner, Kinondoni Masaki, Oysterbay, Ubungo, Urafiki, Riverside, External, Manzese, Maeneo mengine ni Kimboka (Buguruni), Tabata Magengeni, Segerea, Kinyerezi, Temeke Mwisho, Sudan, maarufu kwa Wahaya, Mbagala Kizuiani, Zakhem na maeneo yanayotazamana na Mlimani City Barabara ya Sam Nujoma.
Mtandao huu pia imebaini baadhi ya wanandoa wanashiriki katika vitendo ama kwa wanaume kununua au wanawake kuwa sehemu ya dadapoa wanaosaka wateja kwa makubaliano ya malipo ya fedha.
Aidha mtandao huu pia umebaini kuwa wengi wanajitumbukiza kwenye biashara hiyo ya ukahaba ili waweze kujikimu kimaisha, lakini je yapo matumaini?
Hatari wanayopitia:
Sarahabiba binti anyejihusisha na ukaaba maeneo ya Manzese anasema “Tunaonekana ni watu tusio na maadili kwenye jamii, tunaepukwa na wengi kwenye jamii inayotuzunguka, wanatunyanyapaa.
“Tunapitia hatari nyingi, tunajiweka rehani maisha yetu ili tu tuhakikishe familia zetu zinapata kula,” anasema Rahel, binti mwingine anayefanya biashara ya ukhaba eneo la Ubungo External jijini Dar es Salaam.
Kuna wakati tunapitia misukosuko mingi, kukamatwa na askari, kupigwa na wateja wetu, wakati mwingine kuuliwa.
“Mtu anakuchukua mnaelewana vizuri, akishapata huduma hataki kutoa hela ukihoji wakati mwingine unaishi kushambuliwa kwa kipigo, wapo waliopoteza maisha kutokana na kazi hii.
“Kuna mwenzetu alichukuliwa vizuri lakini hakuonekana na baada ya siku mbili tukapata taarifa za mwili wake kuonekana ukiwa umetelekezwa kwenye majani maeneo ya ustawi wa jamii.”anasema Rachel
Amina, mwenye miaka 22 sasa , mkazi wa Kinondoni, anasema alianza biashara ya ngono akiwa na umri wa miaka 15 alipopata mimba ya mtoto wake Subira, mpenzi wake alimuacha,
“Napitia haya yote kwa ajili ya binti yangu, nimepitia uchungu mwingi sana eneo hili, nataka mwanangu aje kuwa wakili ili anipiganie mimi na wengine wanaodhulumiwa
Binti mwingine aliyejitambulisha kwa jina la Rose mkazi wa Sinza, akielezea alivyojitumbukiza kwenye biashara ya ngono anasema “Wazazi wangu baba na mama walifariki nikiwa mdogo (kilio).”Ninaambiwa walifariki kwa ajali, nililelewa na bibi, lakini nikiwa na miaka 10 bibi yangu alifariki, pale ndipo nilianza kuishi maisha ya uchungu, sitaki kuyaongelea haya (kilio).
Mikasa kwenye maisha ya Rose iliendelea baada ya kulazimika kukatisha masomo na kuingia mitaani kufanya kazi za ndani ambako alijikuta akiishia kubakwa na baba mwenye nyumba.
“Kutokana na maisha niliyoyapitia, nikajikuta naingia kwenye biashara ya ngono, yale niliyoyapitia sitaki wapitie wengine, ndio maana nimekuwa nikisimama imara napigania maisha yangu kwa nguvu hadi tone la mwisho la damu yangu.
Happy mkazi wa Magomeni, akielezea madhila ambayo amewahi kukumbana nayo katika kazi yake hiyo ya biashara ya ngono anasema “Nilikutana na jamaa klabu, akanichania nguo, akachukua na hela yangu sh 60,000 kutoka kwenye sidiria yangu, nilikuwa nang’ang’ana kutoka ila alinipiga kwa nyuma ya shingo, angeniua maana alinishtukiza ila mabaunsa wa klabu walinisaidia na alichukuliwa na Polisi.
Kuna wakati pia tunakamatwa na Polisi kwa uzururaji unalazwa lokapu hujui nyumbani watoto inakuaje?
Umaskini:
Chonge mkazi wa Mwananyamala, anayefanya biashara ya ngono maeneo ya pembezoni mwa Leaders Club anasema “wengi tunalea watoto wenyewe bila ya usaidizi wa baba, maisha ni magumu, pesa inavyoadimika ndio na hatari zaidi kwetu inavyoongezeka, maana ili tujikimu inabidi tuendelee tu kufanya biashara hii.
Tumekuwa tukikutana na madhila mengi, ni biashara ngumu wengine wamekuwa wakiishi wengi kwenye chumba kimoja maarufu ya ghetto, lakini wengine wamepangisha vyumba na kuishi maisha mazuri.
Corona yachagiza ugumu wa maisha:
Ugonjwa wa Corona umefanya maisha yao kuwa magumu zaidi, kuanzia mwaka jana mwezi wa tatu serikali ilipotangaza kuwa na mlipuko wa ugonjwa wa Corona nchini, biashara imekuwa ngumu zaidi kwa madada poa.
“Kidogo sasa hivi hali inaanza kuwa nzuri, lakini kipindi Corona imeshamiri biashara ilikuwa ngumu, ilifika kipindi unapigwa na baridi hupati mteja hata wa buku yaani,” anasema dada Poa aliyefahamika kwa jina la Pili mkazi wa Magomeni Usalama na kuongeza “Lakini kwa sasa hesabu ya wateja angalau inaanza kuongezeka.
Kabla ya Corona mtu unauhakika wa kupata kuanzia sh 50,000 hadi 100,000 kwa usiku mmoja, na wakati mwingine siku inakuwa nzuri zaidi unaweza pata zaidi ya kiasi hicho.
Lakini tangu kuingia kwa ugonjwa huu, mambo ni magumu, ukipata sh 30,000 unashukuru, wateja walipungua sana
Wanenavyo wanaume:
James Lweno (sio jina halisi) anasema, huwa tunawafuata mitaani kwa kuwa kuna kahaba zaidi ya 1,000 mjini Dar es Salaam wanaohangaika kusaka maisha.
Gerald mkazi wa Kigamboni anasema “Kwangu mimi naona biashara hii ya ukahaba imeota mizizi nchini kwa kuwa wanaume wengi wana msongo wa mawazo, hakuna sheria kali, umaskini na malezi, ushawishi toka kwa makundi rika.
Akifafanua anasema “Wanaume wanakuwa na msongo wa mawazo hawana mahusiano mazuri na wenza wao hivyo wanaona chaguo sahihi ni kwenda kununua ngono. Pia hakuna sheria kali inayozuia biashara ya ukahaba nchini, kungekuwa na sheria kali ya biashara hiyo, ukimkamata kahaba, mkamate na anayemnunua, biashara hii ingepungua nchini.
Aidha amesema “Watoto wamezaliwa katika familia duni wanajikuta wanaingia mitaani kujitafutia kipato na kujikuta wanakuwa katika malezi yasiyo sahihi, hivyo wanajitumbukiza kwenye ukahaba ili wapate mkate wa kila siku.
Pia Makundi rika mabinti wanashindwa kujizuia tamaa za mwili, kwa kuona wenzake wana maisha mazuri hivyo nae anafuata mkumbo.
Takwimu za Corona:
Kwa mujibu wa takwimu za Tanzania zilizorekodiwa na Shirika la Afya Duniani (WHO) hadi Novemba 9, 2021 zinaonyesha watu 26, 196 wameambukizwa Corona huku kati yao watu 725 wakipoteza maisha.
POLISI
Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, anasema elimu itolewe kwa wanaume kwani ndio chanzo cha madada poa, wakiacha kuwanunua wataacha kujiuza.
“Wanaume wakiacha kuwafuata huko mtaani, mara moja watakosa soko na wataachana na vitendo hivyo. Mimi kwa sasa sitatoa SMG kwenda mitaani kukamata dadapoa, ninapambana na majambazi na wahalifu," anasema.
WANASHERIA
Wakili wa Kujitegemea, Daniel Kalasha anasema hakuna sheria inayowabana wanawake wanaojiuza (dadapoa), bali iliyopo inawabana wamiliki wa madanguro na baa zinazotumika kufanya biashara hiyo.
"Mmiliki wa danguro anashtakiwa kwa kosa la kuendesha danguro na akipatikana na hatia anahukumiwa kwa mujibu wa sheria," anasema.
Wakili Kalasha anasema dadapoa akikamatwa, hushtakiwa kwa makosa ya uzururaji katika Mahakama ya Jiji na wakipatikana na hatia wanalipa faini ambayo ni kuanzia Sh. 50,000 hadi 200,000.
Anasema wanaoshindwa kulipa faini, wanakwenda jela miezi sita lakini uzoefu wake unaonyesha kesi hizo mara nyingi haziendelei mpaka mwisho.
Naye Mwanasheria Reuben Semwaza ‘Kinara’ anasema kuthibitisha makosa ya kujiuza ni vigumu kutokana na uhitaji wa uthibitisho kwamba aliposimama au eneo ulipomkuta alikuwa akijiuza.
Semwanza, anasema wamiliki wa madanguro hushtakiwa hata kwa makosa ya kufanya biashara haramu ya binadamu ambayo adhabu yake iko kisheria.
"Ukimiliki danguro kisheria unashtakiwa kwa kuzuia uhuru wa mtu, ukikamatwa una watu umewahifadhi, ukashindwa kujieleza wako kwa ajili ya nini, hakuna taarifa za uwapo wa watu hao, hawana kazi yoyote, unaweza kushtakiwa kwa makosa mawili.
"Kwanza; unashtakiwa kwa kuwa na nia ovu, kumiliki danguro na kosa la pili unaweza kushtakiwa kwa kufanya biashara haramu ya binadamu," anafafanua.
Wakili huyo anarejea kifungu cha namba 4(5) cha Sheria ya Biashara Haramu ya Binadamu inatoa adhabu ya kulipa faini Sh. milioni tano na isiyozidi Sh. milioni 10 au kwenda jela kutumikia kifungo cha miaka miwili hadi 10.
"Kifungu namba 4(1a) cha Sheria ya Biashara Haramu ya Binadamu kinazungumzia madanguro, uzinzi, umalaya na makosa yote hayo adhabu yake ni faini Sh. milioni tano na isiyozidi Sh. milioni 10 ama jela miaka miwili na isiyozidi miaka 10," amefafanua
Habari leo Nov 18,2021