DC Ally Hapi: Uwanja wa Fisi kubadilishwa na kujengwa shopping malls

Hapa nahisi kunaukosefu mzuri kati ya Hapi na Makonda vijana tunaita Beef kama hawakuwekana sawa huko mbele Mambo yataharibika.
 
Hawa vijana mambo wanayoongea ni sahihi kwa mtazamo wao na hata kwa mtazamo wa wengi, tatizo ni kuwa ukiwachunguza utadhani tangu mwaka 1961 nchi hii haijawahi kuwa na serikali na wao ndio wa kwanza kabisa kuanza kazi ya kuongoza/kutawala.
Kwa aliyeelewa maana ya mizuka basi hizi harakati za hawa vijana zinamhusu.
 
Nimemuona DC Hapi katika maadhimisho ya asasi ya Patrice Lumumba.

Kuna maelezo aliyoyatoa kuhusu maisha ya watu wanaoishi maeneo ya uwanja wa fisi.

Amesisitiza kuwa yeye hataamuru polisi kupita nyumba kwa nyumba ili kuwakamata wanaoishi huko ambao wanajihusisha na uchangudoa kwenye madanguro.

Ameenda mbali na kusema kuwa anafikiria kulibadilisha eneo hili na kulifanya eneo la uwekezaji kwa kujenga shopping malls na vitu vya namna hiyo.

Ingawa hakugusia ni wapi wakazi hao watapelekwa lakini aliahidi kuwafidia.

Source ni channel ten jioni hii

My take:

Ana wazo zuri sana la kitaka kulibadili eneo hili la uwanja wa fisi lakini nina wasiwasi na kauli yake hii na dhamira yake kama sio ya kutaka kumnanga mkuu wa mkoa hasa hasa katika kipindi hiki tunachoshuhidia mvutano wa ndani ya mtandao.

Naamini haya aliyoyasema ni jibu kwa ile thread iliyoliliwa kumpa ban Lizaboni
Amefeli 😂 na sasa Makala anajaribu nae kufeli kuhusu maeneo hayo
 
Back
Top Bottom