Makonda hakubaliki hata kwa wana ccm wenzakeNimemuona DC Hapi katika maadhimisho ya asasi ya Patrice Lumumba.
Kuna maelezo aliyoyatoa kuhusu maisha ya watu wanaoishi maeneo ya uwanja wa fisi.
Amesisitiza kuwa yeye hataamuru polisi kupita nyumba kwa nyumba ili kuwakamata wanaoishi huko ambao wanajihusisha na uchangudoa kwenye madanguro.
Ameenda mbali na kusema kuwa anafikiria kulibadilisha eneo hili na kulifanya eneo la uwekezaji kwa kujenga shopping malls na vitu vya namna hiyo.
Ingawa hakugusia ni wapi wakazi hao watapelekwa lakini aliahidi kuwafidia.
Source ni channel ten jioni hii
My take:
Ana wazo zuri sana la kitaka kulibadili eneo hili la uwanja wa fisi lakini nina wasiwasi na kauli yake hii na dhamira yake kama sio ya kutaka kumnanga mkuu wa mkoa hasa hasa katika kipindi hiki tunachoshuhidia mvutano wa ndani ya mtandao.
Naamini haya aliyoyasema ni jibu kwa ile thread iliyoliliwa kumpa ban Lizaboni
Haya haya wana lumumba toaneni macho sasaNa wewe unaweza ukawa too positive to see what is behind the scene!
Jingalao nakuaminia ebu mpe za uso huyo ingizo jipya la lumumbaNa wewe unaweza ukawa too positive to see what is behind the scene!
Wacha watowane macho,sisi wenye jiji tumekaa pembeni tuna kula upepoHawa vijana wa CCM Magufuli awaangali sana, hawapo kwa maslai ya nchi zaidi ya matumbo yao.!
Ni utovu wa nidhamu DC kupinga agizo la RC hata kama linamakosa....ana namna nyingi za kuwasiliana Na boss wake....DC akumbuke alikula kiapo kwa RC.
Hapi anajiamini ndio maana anaongea mambo ya kimsingiFahari wawili hawakai zizi moja, hapa utakuwa ni mnyukano kila kukicha na kila mtu anajiona bora kuliko mwenzake.
Mimi naona Hapi anatumia sana nafasi yake kutaka kuhudumia jamii kuliko makonda anayetaka kujijenga kwa wateuzi wakeMwishowe wote watatimuliwa na hiyo itakuwa ni darasa tosha kwa wengine wanaopewa mamlaka na kuanza kufitiniana badala ya kuhudumia umma
Duh sorry,mwenye uzi kasema umekula ban!??Ban ipi Mkuu?
DC AMETUMIA AKILI SANA
Ni kweli lakini kwa hizi fitna zilizoanza lazima mmoja achomolewe hapa Dar.Hapi anajiamini ndio maana anaongea mambo ya kimsingi
Mbona nimepishana humu sasa hivi?Amekula ban ya maana
Itajirekebishaje wakati yenyewe ndiyo chanzo?Mkubwa naona unajilazimisha kusahau,huo ndiyo mfumo wa uendeshaji wa serikali ya awamu ya 5,katika awamu hii hakuna kiongozi hata mmoja anayejipa muda wa kutafakari kabla ya kuitoa kauli yake mbele ya Umma,wote ni wakurupukaji tu.Unajuwa kuwa hata wale waliotumbuliwa kwa mbwembwe mbele ya makamera wengi wao wamerudishwa katika utumishi wao kimya kimya?
Pamoja na nia njema ya serikali hii,lakini imejidhihirisha kuwa na nakisi kubwa sana ya hekima na busara,ikiirekebisha kasoro hiyo inaweza kuwa serikali nzuri sana,lakini ikiendelea na mwenendo huu wa "kutekwa na hadhira", inaweza kujikuta inalaumiwa kila kona.
Lizaboni yupo mbona ?Amekula ban ya maana
Mkuu usisahau ule usemi wa wahenga kuwa adui muombee njaa!Ni kweli lakini kwa hizi fitna zilizoanza lazima mmoja achomolewe hapa Dar.
Yupo,mwenye uzi kanilisha tangopori.Lizaboni yupo mbona ?