DC Jokate Mwegelo: Taa za kisasa kuwekwa eneo la nje mkabala na uwanja wa Benjamin Mkapa (Temeke)

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Jan 5, 2013
666
835
DC JOKATE MWEGELO: TAA ZA KISASA KUWEKWA ENEO LA NJE MKABALA NA UWANJA WA BENJAMIN MKAPA TEMEKE.

MKUU wa Wilaya ya Temeke, Mhe Jokate Mwegelo ametanabaisha dhamira yake ya kubadilisha taswira ya muonekano wa eneo la mbele ya Ofisi DC iliyopo maeneo ya uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wanahabari mara baada ya kukutana na Maafisa wa TARURA, wa Manispaa wakiongozwa na mkurugenzi wa Manispaa Mh. Jokate alisema eneo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya linatazamana na uwanja wa Benjamin Mkapa na kwamba hukutanisha maelfu ya Watanzania na watu wa mataifa mbalimbali, hivyo ni vyema taswira yake ikaendana na hadhi hiyo.

"Eneo hili lina taswira ya Kitaifa na Kimataifa kwa kuwa hutumika katika michezo na dhifa mbalimbali za kiinchi, hivyo ni lazima linafanane na hadhi hiyo", alisema.

Alisema ana taarifa za uhalifu nyakati za usiku ambapo eneo hilo kwa kukosa taa huwa na kiza kinene, kinachopelekea wepesi wa vitendo viovu kufanyika.

"Mimi ni mwenyekiti wa ulinzi na usalama wa wilaya ya Temeke haitaleta afya hata kidogo uhalifu kufanyika eneo la ofisi ya Mkuu wa Wilaya na kwa Temeke usalama ni moja ya kipaumbele chetu" Alisema Mhe. Mwegelo.

Meneja wa TARURA ambaye pia ni mratibu wa uendelezaji Jiji la Dar es Salaam, amesema kuwa zoezi la ukarabati na uwekaji wa taa 32 katika eneo hilo la barabara lenye urefu wa kilometa 1.3 litagharimu kiasi cha zaidi ya shilingi milioni 102 na litakamilika baada ya majuma mawili mara baada ya taratibu nyingine kukamilika.

Naye Diwani wa kata ya Miburani, Mhe.Juma Mkenga amemshukuru Mkuu wa wilaya Jokate kwa kutambua umuhimu wa eneo hilo na kwamba uwekaji wa taa hizo kwa kiasi kikubwa utapunguza matukio ya uhalifu na kulipa heshma eneo la uwanja wa Taifa.

Kwa kipindi kirefu wananchi wamekuwa wakilalamikia eneo hilo hasa kwa kukithiri kwa vitendo vya kiuhalifu kama uporaji hasa nyakati za usiku. Lakini mheshimiwa Jokate amedhamiria kukomesha uovu huo na kuwa historia.

IMG-20210630-WA0053.jpg
 
Yaani umewaza taa tu, hujafikiria hizo taa zinawekwa kwenye nini(Holder).Je installation yake itakuwa ni nini? Poles au posts?
Solar 300,000
Battery 250,000
Wiring 50,000
Post, nuts etc 250,000
Kokoto na Mchanga 50,000
Cement 2bags Sh. 40,000
Kuchimba shimo sh. 10,000
Ufundi kwa jumla sh. 100,000
Jumla Sh. 1,050,000

Tena hapo nimepiga hesabu za juu kabisa maana serikali sasa hivi inaendesha miradi kwa force account hivyo wananunua materials then wanamwajiri fundi.

Huyo meneja wa TARURA aache ujinga
 
Kwamba kila Taa gharama zote ni 3.1mil?

Sent using Jamii Forums mobile app
Aisee wee acha tu nilitaka kuandika nimeona na mwenzangu umepiga swali. Taa pamoja na labour fanya dola tena bei ya juu sana dola 400 Max kweli Million 102? hapana hii nchi tutafute aliyeturoga tena watu hata mishipa ya aibu hawaoni kutamka tu. Hii nchi ni shit
 
Kama DC jokate alikubali hiyo bei ya 3.1milioni kila taabbasi mamlaka iliyomteua imtengue. Wakuu wa idara wao ni kutegeshea tu .akizubaa hiyo bajeti itatumiwa na watanufaika kea uamuzi wake mzuri wa kuweka taa lakini nchi imeibiwa kea ignorance yake. Hivi kea nini bei ya kila mradi wa serikali ni mara 3 au zaidi ya bei halisi. Hivi ina maana hata kugogle bei ya taa za barabara I mkuu wa wilaya hawezi kupata ali baba wanazo na bei ni ya chini mno. Hapo ni kucreate mama Samia achukiwe kwa kigezo eti serikali imekuwa ya wapigaji.
 
Solar 300,000
Battery 250,000
Wiring 50,000
Post, nuts etc 250,000
Kokoto na Mchanga 50,000
Cement 2bags Sh. 40,000
Kuchimba shimo sh. 10,000
Ufundi kwa jumla sh. 100,000
Jumla Sh. 1,050,000

Tena hapo nimepiga hesabu za juu kabisa maana serikali sasa hivi inaendesha miradi kwa force account hivyo wananunua materials then wanamwajiri fundi.

Huyo meneja wa TARURA aache ujinga
Jamaa alijiona ana akili kutuzidi sisi sote kwamba kawaza mbali
 
Solar 300,000
Battery 250,000
Wiring 50,000
Post, nuts etc 250,000
Kokoto na Mchanga 50,000
Cement 2bags Sh. 40,000
Kuchimba shimo sh. 10,000
Ufundi kwa jumla sh. 100,000
Jumla Sh. 1,050,000

Tena hapo nimepiga hesabu za juu kabisa maana serikali sasa hivi inaendesha miradi kwa force account hivyo wananunua materials then wanamwajiri fundi.

Huyo meneja wa TARURA aache ujinga
Its Ok nakubaliana na wewe bado ni hela nyingi sana, more than an half.
 
Huyu mwanamke kumbe ni mwizi namna hii? Taa haiwezi kuwa 3.1 million aisee. Au anafunga taa za dhahabu?

Mama Samia asikubaliane na huu wizi please, Uboreshaji wa lile eneo ni muhimu sana Ila sio kwa hiyo gharama.

Huu ni wizi wa mchana kweupe.
 
Back
Top Bottom