KERO DAWASA kuna rushwa kwenye ufungaji wa maji

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

maroon7

JF-Expert Member
Nov 3, 2010
11,144
15,144
Wanabodi (Kwa sauti ya Paskali Mayalla),

Nasikitika sana kuleta kero yangu kwa hawa DAWASA ambao wameamua kutufanyia uhuni sisi wateja wao wapya.

Binafsi nililipia kuunganishiwa maji tangu October 2023 ila tukaambiwa kuna upungufu wa vifaa tusubiri. Tukasubiri hadi mwaka ukaisha tunaambiwa bado vifaa havijafika.

January ikapita, February ikapita, na sasa ni March bado sijafungiwa maji (Tegeta A). Baada ya kuanza kufuatilia muungwana mmoja wa DAWASA akashangaa how comes muda wote sijafungiwa maji muda wote huo wakati vifaa vilishafika na kuna watu wamelipia mwezi February wamefungiwa.

Baadaye ikabidi afunguke kuwa wanafungiwa wateja wanaojiongeza kwa kutoa rushwa, na akanitajia baadhi ya waliolipia mwaka huu wamefungiwa tena ndani ya siku mbili tu wakati wengine tumesubirishwa miezi mitano.

Huu si uungwana kabisa kumbe mmeamua kutengeneza tatizo makusudi ili kutengeneza mianya ya rushwa.

Na mkibisha nitaweka ushahidi wote hapa, acheni ujinga fanyeni kazi kwa weredi kama wenzenu wa TANESCO hawakawii kukuletea huduma ya umeme ukilipia, njooni mtufungie maji wateja tuliotangulia kulipia. Miezi mitano mnatusubirisha na kumbe mna agenda yenu? Naomba waziri husika afuatilie hii hujuma.

Na ninaomba TAKUKURU mchunguze hata kwenye system mtagundua kuna wateja tuliolipia tangu October na November hatujafungiwa maji wakati kuna waliolipa mwaka huu na wamefungiwa, DAWASA wawaambie ni kwa nini.
 
Wanabodi (Kwa sauti ya Paskali Mayalla),

Nasikitika sana kuleta kero yangu kwa hawa DAWASA ambao wameamua kutufanyia uhuni sisi wateja wao wapya.
ujinga fanyeni kazi kwa weredi njooni mtufuungie maji wateja tuliotangulia kulipia. Miez mitano mnatusubirisha na kumbe mna agenda yenu? Naomba waziri husika afuatilie hii hujuma
DAWASA kuna nuka.
 
Wafanyakazi wanaitendea HAKI Ile kauli ya kula Kwa urefu wa Kamba.
 
Wanabodi (Kwa sauti ya Paskali Mayalla),

Nasikitika sana kuleta kero yangu kwa hawa DAWASA ambao wameamua kutufanyia uhuni sisi wateja wao wapya.

Binafsi nililipia kuunganishiwa maji tangu October 2023 ila tukaambiwa kuna upungufu wa vifaa tusubiri. Tukasubiri hadi mwaka ukaisha tunaambiwa bado vifaa havijafika.

January ikapita, February ikapita, na sasa ni March bado sijafungiwa maji (Tegeta A). Baada ya kuanza kufuatilia muungwana mmoja wa DAWASA akashangaa how comes muda wote sijafungiwa maji muda wote huo wakati vifaa vilishafika na kuna watu wamelipia mwezi February wamefungiwa.

Baadaye ikabidi afunguke kuwa wanafungiwa wateja wanaojiongeza kwa kutoa rushwa,na akanitajia baadhi ya waliolipia mwaka huu wamefungiwa tena ndani ya siku mbili tu wakati wengine tumesubirishwa miezi mitano.

Huu si uungwana kabisa kumbe mmeamua kutengeneza tatizo makusudi ili kutengeneza mianya ya rushwa.

Na mkibisha nitaweka ushahidi wote hapa,acheni ujinga fanyeni kazi kwa weredi kama wenzenu wa TANESCO hawakawii kukuletea huduma ya umeme ukilipia, njooni mtufungie maji wateja tuliotangulia kulipia. Miez mitano mnatusubirisha na kumbe mna agenda yenu? Naomba waziri husika afuatilie hii hujuma.
Na ninaomba TAKUKURU mchunguze hata kwenye system mtagundua kuna wateja tuliolipia tangu October na November hatujafungiwa maji wakati kuna waliolipa mwaka huu na wamefungiwa, DAWASA wawaambie ni kwa nini.
Wameruhusiwa kula Kwa urefu wa kamba yao
 
Dawa yao serikali ibinafsishe a8 iruhudu kampuni zingine za maji ili na wao kiwakute kilichowakuta TTCL .Walikuwa na nyodo hizo hizo unaomba kufungiwa simu zile za nyaya zao miaka mitatu ulishalipia miaka mitatu iliyopita kila siku porojo vifaa hamna kumbe uongo Zilivyokuja simu za nkononi watu wakaacha na kusema hatuhitaji tena hata kama tulilipia baking tu na hiyo pesa kwa heri.Wafanyakazi maelfu wakapoteza kazi TTCL wako mitaani wanalaani serikali kuleta wawekezaji na kubinafsisha sekta ya simu huku wananchi wanatabasamu kupata huduma nzuri kupitia sekta binafsi

Mtu kalipia me huduma Acha porojo

Waziri wa maji awe anaomba apelekewe ripoti ya watu wote kwa majina yao waliiomba kufungiwa maji kila wilaya na tarehe walizoomba na idadi ya watu waliowafungia maji kila mwezi kwa majina yao

Na maelezo kama kuna ambaye hawajamfungia ndani ya mwezi sababu ni nini?
 
Niliomba huduma ya maji safi, wakaja saveya, wakasema nyumba yako iko nje ya mita 50.
Andika barua kwenda kwa meneja, kwamba uko tayari kulipa gharama za mita zilizoongezeka. Nika andika huo mwezi wa August 2023.
Safari za nenda rudi zikaanze, mara hakuna mita, mara vile.

January 2024, jirani yangu ambaye yuko mbali zaidi yangu aliletewa maji ndani ya masaa 2.
Jirani wewe umefanya nini? akaniambia nimetoa rushwa ya laki tisa.

Nipe namba za wadau,
Kwangu waliomba 1.2milioni. Nikalipa laki tisa, na nikatumiwa control number saa moja jioni! siku iliyofuta nikaletewa maji safi.

Tunatumia ofisi ya dawasa salasala.

Kuna wadau hawa:

saveya mmasai
saveya mchaga (kaoa mwaka jana mwishoni)

Kuna wawekezaji wagiriki, wamewapiga pesa za kutosha.

Acha niishie hapa!
 
Mkuu...haya maelekezo unge waandikia kwa barua ukawatumia hao Dawasa...wangekuja kukufungia na wange kuheshimu sana.

Ila kwa kuandika humu ata kama wataona awatokuja kukuwekea. Watanzania tujifunze kuondoa uoga linapokuja kushinikiza huduma kwenye taasisi za UMMA.​
 
Mkuu...haya maelekezo unge waandikia kwa barua ukawatumia hao Dawasa...wangekuja kukufungia na wange kuheshimu sana.

Ila kwa kuandika humu ata kama wataona awatokuja kukuwekea. Watanzania tujifunze kuondoa uoga linapokuja kushinikiza huduma kwenye taasisi za UMMA.​
Mkuu hiyo barua kwanza hadi imfikie mhusika sio leo. Na ataisoma baada ya miezi. Tumeshafuatilia sana ofisi zao na tumekwama.Lengo la kuleta uzi humu ni kuwataka waache upuuzi na wawajibishwe sababu hata mawaziri wanasoma humu.
 
Back
Top Bottom