Dawa ya Lowassa yapatikana

Dawa ya Lowassa yapatikana

Huwo msemo nimeanza kuusikia siku nyingi na haubadili sema matukio ndiyo yanabadilka, wenyewe uko pale pale!

Mtafanya familia ya fulani iumbuke kwa kujipatia fedha chafu wakati ule wa kubadilisha fedha na kuingiza fedha bandia na kuzihalalisha hadi leo tunazitumia na Lowasa hataacha kulizungumzia hilo na hapo ndio Balali atawekwa wazi na ni nani alimuondoa nchini na hata kama kafa ni nani aliyemuua kwani ikumbukwe Lowasa alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Usalama
 
Hakuna cha dawa,Lowassa haepukiki!
 
Mkuu heshima kwako kama ni dawa ya kutuliza maumivu, mwenye maumivu ni CCM kunyweni wenyewe.

Mmemkosa wakati wa kuchukua fomu NEC, fomu itarudishwa kwa tafadhali.

Halafu Lowasa kwa sasa hivi si mtu ni movement ya kuiondoa CCM inayosimamiwa na CCM yenyewe na kukubalika na wapiga kura.

Kuna habari ya sasa hivi toka Shinyanga ongezeni dawa ya kupunguza maumivu
 
Mkuu hiyo ndio siasa uchwara , jiuleze je Lowassa angebaki ndani ya ccm Chadema wangemsafisha.

Siri isingetoka na kusingekuwa na namna ya kumsafisha. Sasa ametoka na mambo aliyokaa nayo miaka 8 kayaweka wazi hivyo anasafishika.
 
Leo hii wakupiga kampeni watakuwa Olesendeka, Sitta na Mwigulu...???
Vuta-Nkuvute naona CCM wanajiandaa kupoteza muda wao kumtangaza Lowassa badala ya Dr. Magufuli...
Wananchi walishajua fisadi ni nani na yupi anasingiziwa...

Karibuni uwanjani...
 
Issue sio ufisadi tu...
Lowassa hana uwezo wa kuwa rais...hana utofauti na Membe..hapo bado hatujagusia suala la afya

Mkuu, nilikuwa ninajibu hoja ya ufisadi ya VUTA-NKUVUTE aliyoileta kuwa CCM wame_come up with.

Sasa kwa suala la kusema tu "hana uwezo" wakati ameshakuwa mtawala kwa miaka mingi katika "serikali ya CCM" na ndani ya chama hicho hicho sidhani kama una hoja hapa!

Suala la Afya yake, tafadhali tuthibitishie daktari wake alisemaje katika hili, au wewe kama 'daktari' ni kutushirikisha tu anaumwa nini ambacho unashauri awe exempted na kiti cha Urais.

Vinginevyo it is just background noise.
 
Last edited by a moderator:
JF huwa ni raha sana na story hazikomi...kwa mfano huyu nae kaja na story yake ya kina Nape wakati WENYEVITI wa CCM mkoa wanabwaga manyanga. Tusijisahau kupitiliza na kujifanya tunajua kuliko walio ndani ya CCM ambao hukaa kwenye vikao vinavyofanya maamuzi muhimu ya chama;hawa wanajua kinachoendelea na hiyo mikakati uliyoiita dawa ya EL hao wangekuwa kwenye position nzuri ya kuiona kuliko wewe usiyefika kwenye kikao hata cha mtaa.

Mbili sioni mtu kutoka zegambaz wakumshitaki EL kwa waTZ;hao uliowataja hawajai ktk sifa zao kwamba ni wazalendo wa kuwatetea watu. Jaribu kukaa chini uandike another vampire story ya kuwatisha waTz ila hii haijai ndugu yangu
 
Hatimaye chama tawala,CCM,kimepata dawa ya kumdhibiti mgombea wa Urais kupitia CHADEMA/UKAWA,Ndugu Edward Ngoyai Lowassa. Dawa husika inatengenezwa na wapambanaji wa ufisadi hapa nchini ambao wameapa kumuanika Lowassa ili watanzania wamjue. Tayari mikakati ya mtu-kati imesukwa.

Katika timu hiyo, itakayoshiriki bega kwa bega katika kampeni za kumnadi Magufuli,wanatajwa Sitta,Mwakyembe,Ole Sendeka,Mwigulu Nchemba,Lusinde aka Kibajaji na Nape Nnauye. Pia wapo wanaKitengo.

Upepo wa Lowassa umeonekana kuvuma kwa kasi ukisomba na kupeperusha watu na vitu. Tishio linakaribia mwisho zitakapoanza kampeni. CCM iko vizuri,itamdhibiti hadi awe mahututi kisiasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

"Apigwe tu..... tumechoka sasa!!"
-Kayanza Pinda
 
Hatimaye chama tawala,CCM,kimepata dawa ya kumdhibiti mgombea wa Urais kupitia CHADEMA/UKAWA,Ndugu Edward Ngoyai Lowassa. Dawa husika inatengenezwa na wapambanaji wa ufisadi hapa nchini ambao wameapa kumuanika Lowassa ili watanzania wamjue. Tayari mikakati ya mtu-kati imesukwa.

Katika timu hiyo, itakayoshiriki bega kwa bega katika kampeni za kumnadi Magufuli,wanatajwa Sitta,Mwakyembe,Ole Sendeka,Mwigulu Nchemba,Lusinde aka Kibajaji na Nape Nnauye. Pia wapo wanaKitengo.

Upepo wa Lowassa umeonekana kuvuma kwa kasi ukisomba na kupeperusha watu na vitu. Tishio linakaribia mwisho zitakapoanza kampeni. CCM iko vizuri,itamdhibiti hadi awe mahututi kisiasa!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Usiwe na hofu kijana CCM kushinda ni lazima.
Walifanya mbwembwe na maigizo ya kutuaminisha wana power kuliko yeyote ndani wakiwa ndani,tukawaamini na tukasema kama hali ndo hii kweli haya ni mafuriko na hakuna atakae yazuia ndani ya CCM.Chaajabu pamoja na mbwembwe walikatwa na kale kajamaa walikotuaminisha hakana jeuri na hapakuchimbika,wakaishia kufyata mkia na kuhamia kwa mchepuko.

Kama haka kajamaa kaliwakata huku,huko ndo wasahau kabisa na nakuhakikishia hapatachimbika wala kuandamana.Ni kelele na maigizo tu kiuhalisia Mamvi ni mwepesi sana.
Hivi kati ya watawala na wanainchi kundi lipi ndo huweka viongozi katika nchi zetu za kibepali?
 
Mfa maji haishi kutapatapa,hakuna asiejua kama El ni fisadi baada ya kuchafuliwa ndani ya miaka nane lkn bado watanzania wana imani nae kutokana na kazi nzuri aliyowafanyia wakati akiwa waziri mkuu,lazima alipwe fadhira zake,sioni magufuli anapomshinda El zaidi ya kuchukiwa na watu waliobomolewa nyumba zao walizojenga kwa nguvu zao,Sioni cha zaidi ccm watachomchafua El kwa sasa zaidi ya kutapatapa tu baada ya mafuriko
 
..Mwigulu, Nape, Lusinde "kibajaji." Halafu unachanganya na Mzee wa "aliselema."

..kweli ccm imebadilika. Yaani nawaonea raha mliozaliwa miaka ya 80 na 90 kwasababu hamna habari ccm ilikuwa chama cha aina gani.

Cc VUTA-NKUVUTE
 
Last edited by a moderator:
ukweli wa ccm leo utakuwa uwongo wenye kunuka mbele ya wa TANZANIA !!
LOWASSA NI MTU MTAKATIFU NDANI YA NAFSI ZA WATANZANIA 80% WATAKACHO ONGEA CCM MDA HUU NI SAWA NA MFA MAJI HAACHI KUTAPATAPA!!

unanuka ufisadi na unakosa uzalendo etiii msaf,mtu hafla zote huchangia mamilion ya hela,ameikamata serikali anageuka mungu mtu na watu wanamsujudia kwa lipi hasa alilolifanya kubwa katika taifa hili?hv kwel makada wa ccm wakubali kuhama kumfuata EL bure bure tu hebu kasome tena
 
Back
Top Bottom