Dawa ya Lowassa yapatikana

Dawa ya Lowassa yapatikana

Watanzania tunataka orodha ya mafisadi wapya wa escrow ambao wallchota mabilioni stanbic maana huko cag hakufichua siri nzito kutokana na wazito waliopo huko! Ccm mwaka huu kazi yenu ni kubwa sana, maana watanzania hatudanganyiki kwa hoja nyepesi nyepesi. Bora kumchagua lowasa kuluko ccm baba wa mafisadi!!!!
 
Lakini watafute na majibu ya swali la
1. " Kwa nini iwe sasa??!!"
2. "Je asingehama!!??"

Pia angeweza kufanya hayo bila baraka za crew nzima - baraza la mawaziri na mwenyekiti wake? Halafu maamuzi ya baraza la mawaziri ni siri sasa wao watatoaje siri. Pia Mwakyembe alishasema kuna sehemu ya taarifa yake ya bunge aliiondoa kwa sababu serikali nzima ingeanguka; hivyo serikali nzima haina tofauti na Lowassa au yale yote watakayomvisha Lowassa.
 
Ufisadi wa Richmond ungekuwa na nguvu kama ufisadi wa escrow usingekuwepo
 
Ccm ipo kwenye mstari wa kifo lazima mwaka huu iondoke hiyo team ya kuiondoa ccm madarakani.
 
Nimechunguza wote walioteuliwa kuwa kwenye timu ya kampeni ya ccm.nimegundua jambo moja hakuna hata mmoja anaeweza kumrushia jiwe Lowasa maana wote ni kama wale waliompeleka kwa Yesu yule mwanamke waliyemtuhumu kutenda dhambi ya uzinzi. Yesu aliwauliza neno moja tu kama yupo ambaye hana dhambi awe wa kwanza kurusha jiwe.kilichofuata badala ya kurusha jiwe wote waliondoka na kumwacha yule mwanamke na Yesu. Ninacho maanisha hapa ni kwamba hakuna msafi anayeweza kumrushia Lowasa jiwe katika wote.
Ccm bila vyombo vya dola ni walaini kama maini hiyo team ndo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuiondoa ccm madarakani mwaka huu.
 
Mkuu nakuaminia sana. List iliyotoka leo uliowataja wapo wote na ziada ila wanajisumbua sana kwani it's too late sasa. Kwanza 79% ya wapigakura wameshaamua watakayempigia kura na hawabadiliki.

Siku moja inatosha kumbadilisha mpiga kura.
 
Ccm ni kama 'Mfa Maji', haachi kutapatapa! Team ya watu 32!!!! Ili kumchafua tu mtu 1 tu. Upuuzi kabisa.
Badala kufikiria nini cha kuwaambia wananchi ili wawape ridhaa mnawaza ujinga tu. Ndio maana hata mgombea wenu hana vision yoyote, anasubiri tu maelekezo ya chama.
Kura yangu kuanzia ngazi ya chini hadi urais inaenda UKAWA, nimewachoka kabisa ninyi ccm. Kama ufisadi ninyi ndio wahed! Hamna jipya mwaka huu, mkubali tu yaishe.
 
Na wewe ututafutie majibu ya maswali haya:-
1. Kwa nini walimkata asigombee?
2. Kwa nini alisubiri akatwe ndio haondoke?
3. Kwa nini ukawa walikuwa wanasema kwa nguvu zote wana ushahidi wa yeye kuhusika na ufisadi lakini sasa wanaubishia?
4. Kwa nini wazee kama Slaa na Lipumba wanakaa pembeni?
Hayo maswali ni mepesi sana kuyajibu
1. Walimkata kwa sababu wanazojua wao! Hawakuwaeleza wanachama wao au hata wagombea! Kina Pinda, mwakyembe, sitta hata judge Augustino Ramadhani, Mwingulu walilakatwa bila kujitete! Mzee wangu Mwandosya naye alikatwa bila huruma. Hilo ukitaka walijibu litakula kwa ccm.
2. Alikuwa anakubalika miongoni mwa wagombea wote! Hilo latosha kusubiri hadi uone mwisho wake. Sio kuwa hakujua watamkata hapana! Hata JK alishasema mipango ya kuondoka ilishapangwa siku nyingi! Alisubiri ili litimie neno lililosemwa na manabii kuwa ccm ni mafia
3. CDM kama chama cha siasa kazi yake ni kushambulia na kukichafua chama pinzani ili kionekane hakifai mbele ya macho ya jamii! Kuna vitu vingi Dr Slaa alishasema na ushahidi kuwa anao lakini hajavitolea ushahidi! Unakumbuka wakati wa uchaguzi 2010 alisema anazo takwimu za kuwa alishinda lakini hadi leo hakuzitoa! Kuna vitu kweli babu alikuwa analishwa na anaropoka bila kuwa na ushahidi! List of shame inasemekana iliandaliwa na Lisu. Kuna possibility ushahidi wa moja kwa moja hawakuwa nao bali walilishwa sumu ya ripoti ya mwakyembe! Hilo sio tatizo kwenye politics!
4. Kuhusu Slaa na Lipumba, hiyo ni mitifuano ya kugombea uraisi! Slaa alishajiandaa sana kugombea na utakumbuka hata ziara zake za kwenda US zilikuwa moja ya mikakati ya maandalizi! Ujio wa Lowassa ulimpokonya nafasi hiyo! Siamini kama Slaa amezira kwa sababu Lowassa kaja Ukawa, ameziri kwa kuwa Lowassa kapewa nafasi ya kugombea uraisi. Lipumba alikuwa na mipango miovu dhidi ya chadema. Sidhani kama kukubali kwake kumuachia Slaa ilikuwa genuine, ukumbuke yeye na bwana mkubwa ni marafiki! Alikuwa atumiwe kuipasua Ukawa! Slaa angechukua form na lipumba naye angechukua! Maalimu Seif aliliona hilo na akacheza alivyocheza, lipumba akaangukia pua.
Ni vyema watu wakatambua muungano wa ukawa ni tishio kubwa kwa ccm! Linaunganisha vyma vikubwa viwili vyenye wafuasi wa dini kubwa mbili! Cuf inahusishwa na uislamu, cdm inahusishwa na ukristo! Hili ni kweli halina ubishi kwa kuwa hiyo mijadala ipo! Ukiwaunnganisha hivi vyama unapata matokeo mazito toka pande mbili na kuondoa dhana hafifu inayotumiwa na wanasiasa uchwara kuwa ni vyama vya dini fulani. Ccm haiko comfortable kuona huo muungano unadumu. So ni vita!!!
 
Hayo maswali ni mepesi sana kuyajibu
1. Walimkata kwa sababu wanazojua wao! Hawakuwaeleza wanachama wao au hata wagombea! Kina Pinda, mwakyembe, sitta hata judge Augustino Ramadhani, Mwingulu walilakatwa bila kujitete! Mzee wangu Mwandosya naye alikatwa bila huruma. Hilo ukitaka walijibu litakula kwa ccm.
2. Alikuwa anakubalika miongoni mwa wagombea wote! Hilo latosha kusubiri hadi uone mwisho wake. Sio kuwa hakujua watamkata hapana! Hata JK alishasema mipango ya kuondoka ilishapangwa siku nyingi! Alisubiri ili litimie neno lililosemwa na manabii kuwa ccm ni mafia
3. CDM kama chama cha siasa kazi yake ni kushambulia na kukichafua chama pinzani ili kionekane hakifai mbele ya macho ya jamii! Kuna vitu vingi Dr Slaa alishasema na ushahidi kuwa anao lakini hajavitolea ushahidi! Unakumbuka wakati wa uchaguzi 2010 alisema anazo takwimu za kuwa alishinda lakini hadi leo hakuzitoa! Kuna vitu kweli babu alikuwa analishwa na anaropoka bila kuwa na ushahidi! List of shame inasemekana iliandaliwa na Lisu. Kuna possibility ushahidi wa moja kwa moja hawakuwa nao bali walilishwa sumu ya ripoti ya mwakyembe! Hilo sio tatizo kwenye politics!
4. Kuhusu Slaa na Lipumba, hiyo ni mitifuano ya kugombea uraisi! Slaa alishajiandaa sana kugombea na utakumbuka hata ziara zake za kwenda US zilikuwa moja ya mikakati ya maandalizi! Ujio wa Lowassa ulimpokonya nafasi hiyo! Siamini kama Slaa amezira kwa sababu Lowassa kaja Ukawa, ameziri kwa kuwa Lowassa kapewa nafasi ya kugombea uraisi. Lipumba alikuwa na mipango miovu dhidi ya chadema. Sidhani kama kukubali kwake kumuachia Slaa ilikuwa genuine, ukumbuke yeye na bwana mkubwa ni marafiki! Alikuwa atumiwe kuipasua Ukawa! Slaa angechukua form na lipumba naye angechukua! Maalimu Seif aliliona hilo na akacheza alivyocheza, lipumba akaangukia pua.
Ni vyema watu wakatambua muungano wa ukawa ni tishio kubwa kwa ccm! Linaunganisha vyma vikubwa viwili vyenye wafuasi wa dini kubwa mbili! Cuf inahusishwa na uislamu, cdm inahusishwa na ukristo! Hili ni kweli halina ubishi kwa kuwa hiyo mijadala ipo! Ukiwaunnganisha hivi vyama unapata matokeo mazito toka pande mbili na kuondoa dhana hafifu inayotumiwa na wanasiasa uchwara kuwa ni vyama vya dini fulani. Ccm haiko comfortable kuona huo muungano unadumu. So ni vita!!!

Majibu yako yanaweza kuwa yana eleza uelewa wako. Kwa karne hii huwezi kutoa majibu ya kudhania tu ukadhani utaeleweka:-
1. Sababu za kumkata wamezisema sana ambayo kubwa ni kukosa uiadilifu. 1995 ilisemwa hivyo , chama kikataka kumvua gamba na uchaguzi huu pia wakamkata kwa ufisadi huo huo. Chama hakikusema wazi maana alikuwa mwanachama wao na sio siri kuwa kuna wajinga wengi wanaomshabikia
2.Kukubalika kwake umekupima wapi? Na umekupimaje? Kama kamati tu ya watu wachache hawakukubali hao wengi watakukubali vipi. Watu wengi wanajua jitihada ya kitumia pesa anayofanya ili watu wamshangilie na kuonekana anapendwa. Kibaya cha jitembeza ndugu yangu
3.Siasa sio uongo. Chama au mwana siasa anaetumia uongo kujipatia umaarufu ni wa kuogopa kama ukoma. Nchi nyingine ukigundulika umesema uongo unajiuzulu wadhifa wako. Tunataka Tanzania hiyo.
4. Lowassa analalamikia faulo kufanyiwa ccm; Iweje unataka slaa na lipumba wafurahia rafu hizo?

Fungua akili yako uangalie mambo kwa upana wake.
 
Tatizo Ccm sio magufuli akihamia Tlp tutampa kura..hapa tunaangalia nani aliyetuletea ufisadi wote huu...
 
Tunataka yoyote aliyekuwa kwenye baraza la mawaziri wakati wa sakata la Richmond asimame aseme lowasa ni muhusika!
 
Ccm ni kama 'Mfa Maji', haachi kutapatapa! Team ya watu 32!!!! Ili kumchafua tu mtu 1 tu. Upuuzi kabisa.
Badala kufikiria nini cha kuwaambia wananchi ili wawape ridhaa mnawaza ujinga tu. Ndio maana hata mgombea wenu hana vision yoyote, anasubiri tu maelekezo ya chama.
Kura yangu kuanzia ngazi ya chini hadi urais inaenda UKAWA, nimewachoka kabisa ninyi ccm. Kama ufisadi ninyi ndio wahed! Hamna jipya mwaka huu, mkubali tu yaishe.
Unaweweseka sana mfuasi wa ukawa
 
Back
Top Bottom