Rapid maana yake kama kaambukizwa jana, juzi, wiki iliyopita, kipimo kitaonesha negative kwahiyo atakuambukiza. Hapo ni HIV peke yake,vipi kuhusu Gonorrhea mtapima rapid test? , Syphilis je? Trichomoniasis pia mtapima? Na kuna yale madude Kiswahili sijui ndo wanaita mafundofundo yanaletwa na Human Papilloma Virus kipimo chake unacho? Hapo sijaongelea Candida au kwa Kiswahili fangasi, una kipimo pia? Watu huwa hawajali halafu wakiumwa badala wakapate matibabu wanaenda kunywa Azuma, uzuri Azuma siku hizi wadudu wamekuwa sugu , ukinywa ni kazi bure tu, maumivu yanazidi basi unaenda kwa daktari kuvua nguo maana huna jinsi yamekufika shingoni.