Dawa ya fungus za miguuni

Dawa ya fungus za miguuni

chumvi ina saidia lakini haiui vimelea ndani ya mwili kitunguu swaumu ndio penyewe tumia hakika utatupa matokeo hapa
 
Naomba msaada wa dawa kama itakuwepo nime2mia dawa nyingi sana na hospital nyingi sana kupata sululisho la mguu wangu umepata fungus tangu mwaka 2010 ila kila nikitibiwa cpati nafuu plz nisaidie doctor

jaribu kutumia dawa inaitwa Mycoter, itumie kwa muda mlefu kwa kadri utakavokuwa unaona unafuu
 
Fangasi za miguu zinataka kukata vidole vyangu. Je, dawa ya asili ni ipi?

Jamani nimenyeshewa mvua nikiwa nafungua geti si mnajua tena kazi yangu ya ukolokoloni na haya masika kila anayekuja na gari hata kwenda kununua vocha wanatoka na gari basi nimelowa mfululizo kwa wiki sana na mbaya zaidi nimevaa viatu na soksi hivyo vimenisababishia fangasi za miguu na sijapata muda wa hospitali kabisa si ujua tena nikikosa siku moja tu kibarua kinaota nyasi.

Anayejua dawa ya asili ya fangasi naomba anisaidie.
 
Uluza aliesoma Pugh sec akusaidie alivyopona
 
Nenda hospitalini,uwe unafua hizo soksi siyo ukivua ukisimamisha inasimama yenyewe.

Btw acha kutukana wazee kama kina Slaa na Mbowe who knows may be ni laana
 
Tafuta hela uende hospitali ya Apolo India ndo kuna tiba nzuri sana.
Kule ndo kuna madaktali, hapa kwetu kuna wajukuu wa madaktari tu-hawana uwezo wa kutibu kabisa.
 
Wazee naumwa inakuaje mnaleta utani?.kama hujui bora ukae kimya tu nauliza anayejua dawa hasa zile za asili
 
ponda kitunguu saumu paka eneo liliothirika.
 
Fangasi za miguu zinataka kukata vidole vyangu je dawa ya asili ni ipi. Jamani nimenyeshewa mvua nikiwa nafungua geti si mnajua tena kazi yangu ya ukolokoloni na haya masika kila anayekuja na gari hata kwenda kununua vocha wanatoka na gari basi nimelowa mfululizo kwa wiki sana na mbaya zaidi nimevaa viatu na soksi hivyo vimenisababishia fangasi za miguu na sijapata muda wa hospitali kabisa si ujua tena nikikosa siku moja tu kibarua kinaota nyasi.anayejua dawa ya fangasi nisaidie
Fungus katika ya vidole ni fungus ya

kawaida inawezekana wewe mtumiaji sana wa maji, kwani maji huchimbua mwili!! kwahivo

vijidudu kama hivo huingia na kupambana na white blood cells lakini kwa kuzidiwa nguvu ndio

fungus hujitokeza, kama fungus uliyoisema wewe ni ya kawaida ila ina kero kwakweli. Kwanza

kabisa kama mtumiaji wa maji sana upunguze yaani sio kutumia maji kwa kunywa laa!

kutumia maji yaani kuchezea maji inawezekana ukikoga unatumia maji zaidi au kila wakati

unakosha miguu yako na mambo kama hayo. Hata hivo ipo dawa moja na nafikiri inajulikana

sana nayo ni ndimu na jivu. Unachukua jivu unaweka katika sehemu hiyo katikati ya kidole na

halafu unanyunyizia ndimu! Dawa nzuri lakini inawasha sana na ndio dawa tu.

 
Fangasi za miguu zinataka kukata vidole vyangu je dawa ya asili ni ipi. Jamani nimenyeshewa mvua nikiwa nafungua geti si mnajua tena kazi yangu ya ukolokoloni na haya masika kila anayekuja na gari hata kwenda kununua vocha wanatoka na gari basi nimelowa mfululizo kwa wiki sana na mbaya zaidi nimevaa viatu na soksi hivyo vimenisababishia fangasi za miguu na sijapata muda wa hospitali kabisa si ujua tena nikikosa siku moja tu kibarua kinaota nyasi.anayejua dawa ya fangasi nisaidie

Dawa ya asili ni usafi tu! Wa soksi, viatu na miguu yako! Hakuna mazingaombwe hapo
 
Twanga kitunguu swaumu kizima thn pasha maji moto kidogo kiasi cha nusu glass baada ya hpo changanya na hicho kitunguu alafu unywe.ni chungu sana ila jikaze.
Ukishamaliza kaa bila kula au kunywa chochote kwa nusu saa.ni dawa sana kwa fungus sugu na minyoo ndugu.ukimaliza naomba urudi kwa ushuhuda.
 
Wapenzi wana jamiii, nimeona kwenye thread zilizopita watu wengi wakionesha kusumbuliwa na tatizo la fungus sehemu za Siri pamoja na mba wa kwenye ngozi (sio kwenye nywele). Nimeona ni bora kushea some ideas zitakazo weza kuwafaa wengi.
Dawa nyingi za dukani za kutibu gonjwa la fungus zimechemsha hasa wanapokuja fungus sehemu za siri na hata mba wa kwenye ngozi. Matunda ya dawa nyingi huanza kuonekana baada ya takrabini wiki mbili lakini ugonjwa wenyewe huchelewa kupona hata mtu akizingatia kanuni za usafi.

Basi napenda kuwashauri kutumia dawa aina ya IODINE ambayo inauzwa kwenye maduka ya kawaida. Niligundua nguvu ya dawa hii baada ya kusumbuliwa na mba wa ngozi kwa kipindi kirefu nikaamua kuchukua iodine niliyokuwa nayo ndani nijipake ili kuficha makovu ya mba maana nilikuwa na mtoko by then. Nilishangaa jinsi wale mba walivyokauka kwa upesi. Ndipo nikaaanza kutafuta kujua kwa nini dawa hii ina uwezo mkubwa namna hii.

Jinsi ya kutumia dawa hii, nunua iodine tincture kwenye duka la dawa lolote. nunua na gloves pamoja na pamba. Paka iodine sehemu iliyoathirika na mba au fungus. Vaa gloves ili kuzuia idoine ising'ang'anie kwenye ngozi ya mikono. Fanya hivi hasa nyakati za usiku ambazo uko nyumbani mda mwingi. Asubuhi oga au nawa sehemu uliyopaka dawa ya iodine.
Tahadhari. Kwa kuwa dawa hii imechanganywa na Spirit inaweza kupelekea muwasho mkali hasa ikipakwa sehemu za siri. Ni vema kuwa na chombo chenye maji, au taulo lililochovywa kwenye maji ili kupoozea sehemu iliyopakwa dawa.
Ni matumaini dawa hii itawasidia wengi walioteseka na ugonjwa huu mbaya kabisa.

For ref please soma hapa chini.

Iodine exhibits activity against bacteria, molds, yeasts, protozoa, and many viruses; indeed, of all antiseptic preparations suitable for direct use on humans and animals and upon tissues, only iodine is capable of killing all classes of pathogens: gram-positive and gram-negative bacteria, mycobacteria, fungi, yeasts, viruses and protozoa. Most bacteria are killed within 15 to 30 seconds of contact.Iodine is by far the best antibiotic,antiviral and antiseptic of all time.- Dr. David DerryDr. Derry says that iodine is effective "for standard pathogens such as Staphylococcus, but also iodine has the broadest range of action, fewest side effects and no development of bacterial resistance." There is a world of difference between using an antibiotic – anti-life substance – and a antibiotic, antiviral and antifungal substance like iodine, which is life serving because it is a basic and most necessary nutritional substance.Iodine kills single celled organisms by combining with the amino acids tyrosine or histidine when they are exposed to the extra-cellular environment. All single cells showing tyrosine on their outer cell membranes are killed instantly by a simple chemical reaction with iodine that denatures proteins. Nature and evolution have given us an important mechanism to control pathogenic life forms and we should use it and trust it to protect us in ways that antibiotics can't.

Iodine and Antibiotics | Dr. Sircus
 
Jf mimi ninasumbuliwa na tatizo la kutokwa na harufu mbaya kwenye miguu.najitahidi kuosha miguu na kuvaa viatu ambavyo sivyakufunika ila bado inaendele, kama kuna mwenye kujua dawa naomba msaada Wako/wenu.
 
Habari doctor
Vijana wangu wawili hucheza sana kwenye maji, sasa wamepata fangasi za vidole vya miguu, zinawasha sana huyu mdogo anabaki kulia, naombeni msaada wenu, kwa dawa yeyote ile inayoweza tuliza maumivu na muwasho, Asanteni.
 
Back
Top Bottom