David Kafulila kuikwaa tuzo ya Nobel

David Kafulila kuikwaa tuzo ya Nobel

Cc: kinana et al.
Kafulila ndiye yule uliyemwita sisimizi? Imekuwaje tena sauti ya sisimizi aliyekanyagwa na tembo isikike dunia nzima? Muwe mnatafakari na kufikiri kabla hujamtukana mwingine kwani matokeo yake inakuwa aibu yako. Hiki kiburi cha wizi na ufisadi hadi unajiona bora kuliko wengine kitawaumbua wengi kabla ya uchaguzi mkuu. Binafsi huwadharau kupita kiasi wale wote wenye kiburi cha pesa na madaraka kuwanyanyasa wengine.
Sikia wengine walivyoropoka, "nitamkata kafulila kichwa chake". AG anaongea live na mteuzi wake anamwacha tu bila kuchukua hatua! Kumbe aliujua usisimizi wa huyu shujaa, Kafulila. Kwa ufupi tu ni kuwa, ''Kafulila ni sisimizi anayewatesa tembo kwani sasa hawanywi maji'.
 
Sie yetu macho.....ngoja tuone mwisho wake itakuwaje.
 
usitake kuwachosha watu humu. Mpaka kufika kumtaja kama mshiriki tayari ana vigezo. Categorization watamfanyia wahusika kulingana na vigezo alivyo navyo. Mbona unahoji vigezo na kundi, kwani wewe ni jaji wa hiyo kitu? Mshangilie mwenzetu, ndugu yetu na shujaa wetu kwa kuiamsha dunia juu ya dhuluma na wizi tunaofanyiwa na hawa wahuni ccm na kukatalia kodi za wananchi wao kushibisha familia chache. Wahisani na marafiki, chondechonde, msitoe hata senti moja hadi warudishe walizoficha ughaibuni na kama inawezekana mzizuie na kukaa nazo hadi tutakapokuwa huru mtupatie.
Nani kamtaja? Au na wewe unakurupuka? Hebu lete source yako hata kama yupo kwenye hio orodha ya nominees
 
Afrika yote tangu inaumbwa wamepata watu 22 tu katika category ya Chemistry,Literature and peace. Hili la Kafulila sijua itakuwa category gani, ila kama atapewa Nobel basi itakuwa ya dinner set,kabati la nguo,vijiko na sahani na mgeni Rasmi atakuwa tamimusalim ndani ya ofisini ya IPTL
safiiii sana mkuu
 
Last edited by a moderator:
View attachment 200370

Kuna tetesi ambazo zinaenea ingawa bado hazijawekwa wazi kuwa mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila anaweza kuwa miongoni mwa watu watakaopata tuzo ya Nobel katikati mwakani,Kafulila ambae ameonekana na kujulikana hasa kulishikilia kidedea upotevu wa pesa katika sakata la wizi wa zaidi ya bilion200 katika sakata la ESCROW ameonesha ujasiri kupambana na jambo hilo hatari kwa manufaa ya watanzania masikini.

Mpaka sasa wahisani wamesitisha misaada ya thamani ya matrilion kwa Tanzania mpaka tahalifa ya CAG itakapo toka kwa mujibu wa mfadhili wa wahisani hao balozi wa finland nchini. Ongera Kafulila jitaidi uikwae tuzo hii kwani si mchezo
.

Dah, kweli wewe ni Tamimu Salimu. Unaujua mchakato wa Nobel Prize?
 
Ngoja tusubiru, atamtaja MAKONDA!

hahahahaha! Paul Makonda hebu pitia pande hizi. halafu makonda napenda kukujulisha kwamba mjadala wa katiba inayopendekezwa utarudiwa tarehe 16 kwenye venue ileile....unaombwa wewe na timu yako muwahi kufika eneo la tukio ili mvuruge tena...ila safar hii mje na bandage za kutosha maana hayo manundu mtakayopata hamtakuja kuyasahau!
 
Last edited by a moderator:
Dah, kweli wewe ni Tamimu Salimu. Unaujua mchakato wa Nobel Prize?
nadhani wewe unaona kitu cha ajabu sana ila ni vigezo tu hata wewe unaweza kushinda tuzo iyo, mbona malala yule mtoto toka pakistani alishinda sababu alijitolea maisha yake kutete wanawake waliozuiwa kusoma,sasa iyo si zaidi ya kafulila
 
Unadhani Nobel prize ni kama miss Tanzania? Nyerere mwenyewe hakupata
 
uko tanzania au uko wapi? Mkuu

Inaelekea hata hiyo NOBEL hujui ilianzishwa kwa madhumuni gani na vigezo gani hutumika mtu kuweza kutunukiwa!! Kafulila hakidhi hivyo vigezo na wala kelele juu ya ESCROW sio kitu cha kumfanya afikiriwe kupewa tunzo hiyo!!
 
Unadhani Nobel prize ni kama miss Tanzania? Nyerere mwenyewe hakupata
wakati wa nyerere tuzo ya nobel ilitolewa kwa wazungu tu,hata hivyo mataifa ya maghalibi walikuwa na wasiwasi na utawala wa nyerere kwamba ulikuwa wa kimabavu
 
Inaelekea hata hiyo NOBEL hujui ilianzishwa kwa madhumuni gani na vigezo gani hutumika mtu kuweza kutunukiwa!! Kafulila hakidhi hivyo vigezo na wala kelele juu ya ESCROW sio kitu cha kumfanya afikiriwe kupewa tunzo hiyo!!
huna lolote mpinzani wewe,au ndio wezi wenyewe
 
nadhani wewe unaona kitu cha ajabu sana ila ni vigezo tu hata wewe unaweza kushinda tuzo iyo, mbona malala yule mtoto toka pakistani alishinda sababu alijitolea maisha yake kutete wanawake waliozuiwa kusoma,sasa iyo si zaidi ya kafulila
Wewe kweli ni Tamimu Salum, hivi unaifahamu story ya huyo Binti Malala what happened to her? Kafulila hauwezi mfananisha na Wangari Mathae, au Whole Soyinka,hata chembe ya Nyerere ambaye alishakuwa nominee for several years
Na akakosa.
 
Afrika yote tangu inaumbwa wamepata watu 22 tu katika category ya Chemistry,Literature and peace. Hili la Kafulila sijua itakuwa category gani, ila kama atapewa Nobel basi itakuwa ya dinner set,kabati la nguo,vijiko na sahani na mgeni Rasmi atakuwa tamimusalim ndani ya ofisini ya IPTL

Ukipenda chongo utaita kengeza. Watanzania wengi wanasikiaga tu hizi tuzo. Nyerere mwenyewe alidesa.
 
Itakuwa ni tuzo ya kushangaza sana in history. Ila itakuwa poa tu kama itakuja tz.
 
Afrika yote tangu inaumbwa wamepata watu 22 tu katika category ya Chemistry,Literature and peace. Hili la Kafulila sijua itakuwa category gani, ila kama atapewa Nobel basi itakuwa ya dinner set,kabati la nguo,vijiko na sahani na mgeni Rasmi atakuwa tamimusalim ndani ya ofisini ya IPTL

Nimecheka vibaya sana dahh watu wabaya jamani!
 
Last edited by a moderator:
Nyerere hakupata hii tuzo pamoja na kuwa mpigania uhuru kwa nchi nyingi.
Hebu muweke Kafulila katika viatu vya Nyerere, je anaweza kuwemo hata kwenye orodha? Achilia mbali kufikiria kama atapata hio tuzo.
 
Back
Top Bottom