Kama amejivua anadhihirisha kuwa alikuwa mnafiki na mzigo katika chama kwa hiyo wamemshtukia.
Mkuu Masanilo habari za Kyela....
Nadhani kama tuhuma hizi ni za kweli basi alifanya kosa la msingi kutenguliwa uongozi wake na sio kuvuliwa uanachama. angombamsamaha ndani ya chama yangeisha nadhani.Alisema kwenye Majira Nov 8 na Mwananchi Nov 9 kuwa Mbowe na Dr Slaa wamefanya kikao kisicho rasmi cha Gheto huko Dodoma na kufikia maamuzi ya kumvua uanachama. Akaitwa na sekretariati ya chama kuhojiwa akakiri kwamba kweli amesema maneno hayo. Akaambiwa athibitishe kuwa kikao cha Dodoma kilijadili kumfukuza uanachama akasema hana ushahidi wowote ila ameelezwa maneno hayo na waandishi wa habari. Akaambiwa akanushe maneno yake, akakataa. Akaambiwa aombe msamaha, akakataa. Uteuzi wake ukatenguliwa kutokana na kukiuka maadili ya chama kifungu cha 10 kinachokataza viongozi kutoa siri za chama, kuzingatia mipaka ya kimamlaka katika kutoa kauli za chama, kuepuka kuwatuhumu viongozi wengine hadharani bila kupitia vikao halali vya chama na kuacha kutoa tuhuma za uongo
serayamajimbo
Huyo kafulila aangalie asije akazunguka vyama vyote vya siasa kama Abas Mtemvu, inabidi aangalie dhamira yake katika siasa ni nini hasa, maslahi au ukombozi wa wengi!!....kwanza walikuwa CCM kabla, na pili wataenda CCM wataniacha mimi CHADEMA. CHADEMA kwangu mimi ni zaidi ya chama, ni Movement! Ni vuguvugu la harakati za kuhakikisha kuwa watanzania wanakuwa na demokrasia pana zaidi bila kuathiri uzalendo wa Taifa letu.
Wako wengi wa aina yake wakivuliwa uongozi hutimka..mfano...LWAKATARE ..never trust this kind of people..lolKama alifuata cheo Chadema na akavuliwa, basi malengo yake hayakutimia. Lakini kama alifuata mkumbo wa kujiunga na vyama ili kufanya ushushushu, bado ni mdogo na hatafika mbali. Na zaidi pia, atakuwa amepotea njia kama atakwenda CCM kwani hana mtaji wa kupendekezwa kwa nafasi ya uwakilishi. Ukishikwa, shikamana! Au hakumbuki ya Nturungeyi na Mrema TLP, Jidulama... na Cheyo UDP, CCM na Njelu?? Anaweza akawa amenyea kambi mapema mno!
Kafulila quits Chadema!
Kafulila kwa maelezo yake kilichomtoa CHADEMA ni mambo mawili (1) Matumizi mabaya ya fedha za chama (2) Hakuna demokrasia ndani ya chama-viongozi hawapendi mwanachama makini anayeuliza mambo yanayousu muelekeo wa chama ktk mambo mbali mbali.
Je wana chadema wakiwemo viongozi ili mnasemaje? je ni kweli ndani ya chama internal demokrasi ni zero na kuhusu ufujaji wa pesa ili likoje? naomba kuwasilisha.
Kafulila
Kwa mfano, Mh Chacha anazungumza hadharani kuwa ruzuku ya chama haiendi mikoani. Lakini anasahau kuwa Kamati Kuu ilisha agiza kuwa kila mkoa ufungue akaunti utumiwe sh 100,000/=(laki moja kwa mwezi). Je Chacha anaweza kutoa mfano wa mkoa uliokwisha fungua akaunti na haujatumiwa pesa hiyo?..Sio hayo, kila wilaya yenye diwani na zile za makao makuu ya mkoa ziilikwishaagizwa kufungua akaunti ili zitumiwe sh 200,000/= kwa mwezi tangu mwaka 2007.
Na ikumbukwe kuwa CHADEMA kinapata ruzuku ya kiasi cha takribani milioni60 kwa mwezi,dhidi ya CCM inayopata ruzuku ya bilioni1.2 kwa mwezi(takribani mara20 ya ile ya CHADEMA). Ruzuku ya CCM kwa mwezi ni takribani sawa na jumla ya ruzuku ya CHADEMA kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu.
Naamini nidhamu katika chama ni muhimu kuliko kitu kingine chochote. Kuhama chama si suluhisho la matatizo. Alihama Mrema CCM na bado CCM ikaendelea, sembuse David Kafulila Chadema!!
Slaa na Mbowe imarisheni nidhamu katika chama ili kuepuka migongano isiyo na tija kama hii inayotokea CCM sasa!!
Leila Abdul
From: Leila Abdul <hifa...@gmail.com>
Date: Wed, 18 Nov 2009 06:18:50 -0800 (PST)
Local: Wed, Nov 18 2009 9:18 am
Subject: Re: DAVID KAFULILA AJIVUA UANACHAMA WA CHADEMA
Naamini nidhamu katika chama ni muhimu kuliko kitu kingine chochote.
Kuhama chama si suluhisho la matatizo. Alihama Mrema CCM na bado CCM
ikaendelea, sembuse David Kafulila Chadema!!
Slaa na Mbowe imarisheni nidhamu katika chama ili kuepuka migongano
isiyo na tija kama hii inayotokea CCM sasa!!
Sijaingia mkenge, but anyway si ishu sana kwani ni wengi wamo kihivi humu. Tuendelee na Kafulila.Uko smart sana wewe ajabu umeingia mkenge mazee!
Mkuu Masanilo habari za Kyela.....