Daudi Mwakawago afariki Dunia

Status
Not open for further replies.
Julius,'
Ninayo kwenye cassette. Nikishatulia nitaiweka kwenye cd. Lakini si mkisikia sauti yangu identity yangu itajulikana? kwi!kwi!kwi!

Hebu acha kujidanganya bana.....hivi kweli unadhani watu hawakujui identity yako baada ya kufanya kazi ile sehemu miaka yote hiyo? Jasusi please.....

Hii ni kama Tido Mhando aseme anaogopa kujulikana id yake....lol
 
Hebu acha kujidanganya bana.....hivi kweli unadhani watu hawakujui identity yako baada ya kufanya kazi ile sehemu miaka yote hiyo? Jasusi please.....

Hii ni kama Tido Mhando aseme anaogopa kujulikana id yake....lol
kwi!kwi!
Bado kuna wasiojua id yangu. Anyway nitaitafuta cassette, nimtafute Steve D atusaidie kufanya vitu.
 

PM, naona unasingizia watu bana .........



Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiweka saini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa mwanasiasa mkongwe na mwanadiplomasia marehemu Balozi Daudi Mwakawago nyumbani kwake Msasani jijini Dar es salaam wakati alipokwenda kuifariji familia ya Marehemu.
 

Lakini kwa utamaduni wa Vasco lazima angeenda msibani...
 
Hapa ni wakati JK akiwasili makaburi ya Kisutu (picha zimepigwa toka mbali na kamera ya quality ndogo):

 
Hamtaki Rais aende kwenye msiba? Kwani anatatumia masaa mangapi. Mbona hii forum inakuwa kama genge la watu wajinga lakini?
 


Wakati wa mazishi: Pichani ni rahisi kujua nani huyo...


Na juu hapo ni kaburi baada ya mazishi
 
Hamtaki Rais aende kwenye msiba? Kwani anatatumia masaa mangapi. Mbona hii forum inakuwa kama genge la watu wajinga lakini?
Mkuu ukisema hivyo nawe utakuwa sehemu ya wajinga! Mbona 'mimi' nilikuwepo? Au unataka watu wote tuwe na mitizamo sawa?

Ndiyo maana ya jamii; lazima tutofautiane mitizamo, na hapo ndipo watu wataelezwa kwanini rais wao anaenda kwenye msiba kama huu, ndipo atajitokeza mwanachama wa kutoa ufafanuzi wa kina na kuwaelewesha Mzee wetu Mwakawago alikuwa nani na ametokea wapi na kwanini rais wetu awepo.

Think of it!
 
Mkuu, shukrani kwa kipande hiki... Kina mengi kwa wengi! Ubarikiwe sana
 

Hamtaki Rais aende kwenye msiba? Kwani anatatumia masaa mangapi. Mbona hii forum inakuwa kama genge la watu wajinga lakini?

Mkuu, soma maelezo hapo juu.......... na maelezo ya PM nimeyakariri ukurasa wa nyuma.
 
Touche, I withdraw my statement.. But I recently read a thread here claiming that the President attends too many funerals, nikaona ni jambo lakijinga kuzungumzia, ata akienda msiba wa kila mtanzania.. sio mbaya. Lakini considering the political paradigm in this matter, I stand corrected but still contest the preceding notion due to its ridiculous nature by and large, however as I said, I accept the specifics of this case.
 

Anyway maybe ur just kidding lakini kama ndiyo mawazo yako haya basi Mkuu utapata shida sana ukija kuamua kuwa Mwanasiasa. I mean hata muwe na ugomvi wa namna gani,hata muwe maadui vipi, mwenzako akipatwa na matatizo hasa ugonjwa au msiba ni lazima ujitokeze kumpa pole hata kuzika.

Ndiyo uungwana.

JK hawezi kuwa mjinga kiasi kwamba asiende kumzika Marehemu eti kwa vile Marehemu alimuwekea vikwazo fulani fulani au walikuwa hawawivi kisiasa au hata katika maisha ya kawaida. Katika siasa au hata maisha ya kawaida huna sababu ya kuonyesha physically eti una chuki na mtu fulani au kikundi fulani. Unakwenda kwenye uchaguzi, kuna kitongoji fulani kinakunyima kura,au Mwenyekiti fulani wa Kata alikuwa mpiga debe wa mpinzani wako halafu ukashindwa uchaguzi, eti unaanza kuwanunia!! No no hawa inabidi hata usiwaonyeshe wala kuwashutumu kwanini hawakukuchagua, huwezi jua next time wanaweza kuwa upande wako!!

Ability to hide emotions and feelings ni muhimu sana na hata professions nyingi wana insist. Ukiweza hii basi utafanikiwa sana na ndiyo maana hata ukifanya diplomasia lazima ukutane na hii kitu. Muonyeshe mpinzani wako kuwa huna chuki nae lakini chini kwa chini unamlima tena kiroho mbaya!!

RIP Balozi Mwakawago.
 
Sijui kama ulinielewa. Anyway, mimi sikutaka kuweka maneno yangu mwenyewe ila maneno ya FMes na PM.

Siku kadhaa kabla Marehemu Kolimba hawajamkolimba, watu kama Mangula (katibu mkuu wa CCM wakati ule) walisimama wima na kumsiliba bin kumchamba ch00 Kolimba. Ghafla wakashtuka jamaa ameshakolimbiwa. Duuu sasa itakuwaje? Siku tatu nne baadaye, hawa hawa WANAFIKRI wamesimama kwenye mazishi wanaanza kumwaga sifa za Marehemu Kolimba.

Nilibahatika kuongea na dada yake Kolimba na akasema wazi kuwa wakati anaongea Mangula, walianza kucheka.......... Ifike wakati Watanzania tuanze kuita Koleo ni koleo.

By the way dada Anamaria hujambo wewe? Umepotea siku nyingi kidogo. Nilifikiri umejifungua ati. Au ulizuiliwa na bwana nyumbani?
 
Tell that to Lowassa. Nasikia ni mtu wa kisasi kweli kweli!
 


Call a spade a spade ni kwenye utendaji siyo katika situation hizi za maafa.Kwa mfano katika issue ya Richmond,pale unaita koleo koleo ili watu wawajibike.Msiwe mnakariri tu misemo kama kasuku.
Tafadhali acha kwenda personal mkuu.Kata issues,achana na kashfa manake hazinisaidii,hazitakusaidia wala kusaidia wengine hapa wanaofuatilia hii thread.Lakini ukitaka kwenda huko pia hamna noma,u just bring it on!
 
Tell that to Lowassa. Nasikia ni mtu wa kisasi kweli kweli!

Hata JK naye nasikia ni wa visasi.Uzuri wake hakuonyeshi,mtaongea,mtacheka,hata miaka inaweza kupita.Lakini siku ukaingia kona zake,basi unaweza juta kwanini hata ulijuana nae!And i like the character especially in playing politics!
 
Nawapenda Wazungu kwa hilo. Atakuja kukuambia moja kwa moja "siwapendi Mipingo".

Mipingo atajifanya anakuchekea, hakuna lolote. Tumejaa unafiki kishenzi. Kama humpendi mtu si useme wazi na hata kwa mazishi yake unazua safari na dharura?

Kwa mfano mie nasema openly 'SIKUPENDI ANNAMARIA'.

Huo ndiyo ukweli. I HATE YOU............. Hata tukikutana lazima ufahamu nafasi yako iko wapi na hata mazishi yako siji na yangu usije. Hivi ndivyo inatakiwa iwe. When you say you love somebody, you just let him know about it (Kool & the Gang) na kama humpendi mtu, si itangazie tu dunia nzima? Tuache unafiki.

Kama Kikwete alikuwa akimpenda Mzee Mwakawago, ni VIZURI sana kaenda kumuaga huyu mzee. Ila kama kaenda tu kuuza sura na ukweli alikuwa hampendi..... Mungu anajua.

Yes, i Sikonge, I HATE YOU ANNAMARIA............

Ngoja nikose sasa kura za ubunge wa Sikonge.
 

Siyo wazungu wote wako hivyo Mkuu.Wengine ni mabingwa wa ku pretend.Atacheka nawe,atakwambia anakupenda kumbe si lolote na bado anaweza akakufananisha na nyani vilevile.
Mkuu hunilishi,hunivishi,huna undugu na mimi na wala huna effect yoyote katika maisha yangu.Hiyo chuki yako haitanitisha kamwe na wala kunikatisha tamaa kufanya au kusema au kusimamia lile ninaloamini ni sahihi katika maisha yangu.Ni bora mtu akikuzidi akili na maarifa ukamuheshimu Mkuu,manake najua hapa ndipo chuki yako ilipo..damn!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…