Masaa chache baada ya kuonja tena hewa ya uraiani, Wakili Peter Madeleka, ameavunja ukimya na kuwashukuru Watanzania waliopaza sauti kupinga kile alichokiita "ukandamizaji" dhidi yake.
Akitumia ukurasa wake rasmi wa mtandao wa X leo Agosti 18, 2026, Madeleka ametoa ujumbe huo mzito kufuatia kuachiwa kwa dhamana jana Agosti 17, baada ya kusugua benchi la mahabusu kwa siku tatu katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central) Dar es Salaam.
Katika maandishi yake yaliyowatag viongozi na wanaharakati nguli wakiwemo John Heche (CHADEMA), Boniface Mwabukusi (TLS), Maria Sarungi, na viongozi wa ACT Wazalendo, Madeleka ametupa kombora la shukrani:
"NAWASHUKURU watanzania wote WALIOPAZA SAUTI ZAO na KULAANI aina zote za UKANDAMIZAJI dhidi yangu. MUNGU awabariki sana. Ingawa siwezi KUWATAJA WOTE hapa, NATAMBUA na KUTHAMINI upendo wenu," ameandika Madeleka.
Mchakato wa kupewa dhamana hiyo uliratibiwa na kuthibishwa na Wakili Paul Kisabo kutoka Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC).
Kukamatwa kwa Madeleka kuliibua mjadala mzito tangu Agosti 14, 2026, aliponaswa na polisi katika viunga vya Mahakama ya Uhujumu Uchumi (Mikocheni B).
Jeshi la Polisi lilimshikilia kwa tuhuma za kudharau amri za Mahakama Kuutuhuma zilizojiri saa chache tu baada ya kutangaza mpango wa kupinga kisheria zuio la mawakili kuhojiwa na wanahabari maeneo ya mahakama.
#SasaLive #PeterMadeleka #PaulKisabo #THRDC #TLS CHADEMA ACTWazalendo HakiNaSheria .DarEsSalaam