Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Mwalimu nimekuelewa sana ulipogusia kuhusu haya maneno matatu
Uwepo(existing)
Ishi(living)
Hai(being alive)
Kama nakumbuka vizuri maneno Haya yanategemeana sana kutoka kwenye hatua ya uwepo (existing) na ili uendelee kuwepo ni lazima uishi na kuishi ulikokuelezea wewe ni kupata mahitaji ya msingi yatakayokufanya uendelee kuwepo kitu ambacho wengi wetu tunaridhika tunapofikia katika hatua hii

Lakini pia mwalimu ukasema unaweza kwenda mbali zaidi na ukawaida kwamba kufanikiwa kimaisha si kwa kuwa unaweza kupata mahitaji yale unayoyaona kwako ni ya msingi peke yake hapana bali unapotazamia namna ambavyo unaweza kuikomboa jamii yako kiujumla pasipo ww kuathirika au kuteteleka kiuchumi

Swali langu lipo kwenye mtazamo wa kwamba endapo mtu huyu ana uwezo wa kuisaidia jamii inayomzunguka pasipo kuathiri mfumo mzima wa maisha yake na umesema kuwa jamii hyo inaanzia kwenye ukoo wangu
Kwa nn tusimuite mtu huyu amefanikiwa maisha kwa 100%
Yaan kwa lugha rahisi ameweza kufika katika kiwango cha yye kuweza kuitwa SUPERIOR

Asante
Vizy boy

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
Hahaha, swali zuri so far, umeenda mbio kidogo kuna somo baadae litazungumzia "kwanini binadamu hawezi kufikisha 100% za kuyafaulu maisha yake" kuna makosa ya kiubinadamu hamna aliyemkamilifu, na hapo uliposema utakuwa sawa na SUPERIOR ni kweli lakini utakuwa sawa na baadhi ya SUPERIOR kuna matabaka ya superior pia tutaenda kuwaangalia hao. Kuna Superior mwenye 80% lakini kuna mwingine mwenye 98%. Pia kwenye kusaidia jamii kuna namna nyingi za kusaidia, mwana ukoo anaweza kukuomba elfu tano ukampa na ikaonekana umesaidia na isiathiri maisha yako, hivyo kuna kusaidia kwa kutoa samaki na kutoa nyavu za kuvulia samaki, na pia kufikia asilimia kubwa za kuyafaulu maisha zinakamilishwa na vitu vingine zaidi ya hela tutakuja kuangalia somo lingine linaloitwa "peace of mind"

Kuna huyu mzee anaitwa Burren buffet anasema "if you get to my age in life and nobody thinks well of you, I don't care how your bank account is, your life is a disaster".

Endelea kufwatilia masomo haya na pia kujiunga WhatsApp kwa namba ya mwalimu hiyo kwa masomo mengine na tatizo lingine binafsi mengi utajifunza.

Sent from my GT-I9500 using JamiiForums mobile app
 
Somo la pili, sehemu ya tatu (Lesson 2, part three).

Karibu tena darasani mwanadarasa uzidi kuimarisha afya ya akili, ni imani ya mwalimu kuwa u buheri wa afya.
"Minds are like parachutes, they only function when opened"

Lakini kabla ya kwendelea nikukumbushe kuwa mwisho wa somo kuna namba ya simu ambayo utaweza kuwasiliana na mwalimu moja kwa moja kwa swala au tatizo lolote ambalo unaona mwalimu anaweza kukusaidia, lakini pia kwa ajili ya kuunganishwa kwa ajili ya masomo yatakayokuwa yanaendelea WhatsApp.

Sehemu yetu hii ya tatu itakuwa na kichwa;

LAWAMA, HUKUMU NA MAJUTO USIYOSTAHILI.

Kumbuka somo letu kuu linalosema;
Akili yako kufanya vitu isivyopaswa kuvifanya na kutovifanya vitu ipaswavyo kuvifanya.
Leo tutaenda kuangalia LAWAMA NA MAJUTO USIYOSTAHILI kama moja ya vitu isivyopaswa kuvifanya.

Lakini mwalimu anaona kwanza aeleze kidogo majuto na lawama unazostahili.

Katika sehemu ya kwanza ya somo hili la pili mwalimu anaimani kuwa utakuwa unakumbuka vyema yale makundi mawili kama umeyasahau rejea kusoma sehemu ya kwanza na ya pili katika somo hili la pili. Mwishoni mwa sehemu ya kwanza somo la pili nilisema lawama na hukumu zinakubaliwa katika kundi la pili ambalo mwalimu alisema linahusika na kuipuuza sauti ya ndani (inner voice) ambapo mwili hutawaliwa na nguvu ya milango ya fahamu, ni hapa ambapo tunapata neno tamaa na mwalimu alimalizia kuwa hapa huusika na maswala ya hisia kama mapenzi.

Mwalimu anasema katika kundi hilo la pili lawama, hukumu na majuto utakayoyapata baada ya matokeo kuja hasi hapo unastahili, kwa kukosa nidhamu juu ya ubinadamu wako na kuziheshimu tamaa, lakini hapa tutakuja kupaangalia zaidi katika masomo yatakayohusu HISIA (EMOTIONS) maana hatutaacha nyanja yoyote katika somo letu kuu la maisha, na pia kukubaliwa kwa lawama hukumu na majuto haitakuwa sababu ya kufeli maisha hivyo hali hii haitakubaliwa kudumu ili kuruhusu shughuli zingine ndani ya ubongo ziendelee na maisha yaendelee pia.

Na pia kama uliongozwa na sauti ya ndani kufanya kitendo chochote cha kihisia na ukapata matokeo hasi hutapaswa kujilaumu juu ya hilo ila utapaswa kutoka kwenye hilo, kwanini usijilaumu maelezo yake yataendana na mwalimu atakavyoeleza katika kundi la pili twende tukaliangalie.

Kundi la pili mwalimu alizungumzia kuwa ni kundi ambalo binadamu anajengwa katika msingi wa neno KAWAIDA ambapo hapa panahusisha shughuli zinazomuingizia kipato, hapa pia ataruhusiwa kujilaumu endapo amepta matokeo hasi ya shughuli yoyote kwasababu aliufwata msingi KAWAIDA na kuipuuza sauti ya ndani. Vivyo hivyo hali hiyo haitatakiwa kudumu ili shughuli zingine za ubongo ziendelee na maisha yaendelee.

Lakini vipi pale matokeo yatakuja hasi na wakati uliisikiliza sauti Mwalimu anakwambia usijilaumu wala kujutia wala kujihukumu kwanini twende tukajifunze na hapa ndipo msingi wa somo hili unaposimama.

Kuna vitu viwili vinavyotokea katika shughuli yoyote uwe makini hapa, vitu vyenyewe ni dhamira au nia NA matokeo hivi ni vitu viwili tofauti ambavyo ni lazima vitatokea katika shughuli yoyote ile, Dhamira siku zote huwa na upande mmoja yaanI huwa CHANYA lakini matokeao huwa na pande mbili HASI NA CHANYA hivyo lazima matokeo yataegemea upande mmoja, tutajikita zaidi kwenye upande HASI maana huku ndiko kwenye lawama, majuto na hukumu juu yako mwenyewe.

Hupaswi kujilaumu, kujihukumu wala kujijutia kwa matokeo hasi kwa sababu kwa binadamu yeyote mwenye akili timamu ni lazima atakuwa na DHAMIRA njema kabla ya kutekeleza shughuli yoyote hivyo usijilaumu kwasababu ya matokeo ndio maana kama wewe ni mkulima uliwahi kila siku saa kumi na moja kwenda shamba ukashinda huko mpaka jua lilipozama, pengine ukashinda hata na njaa kama wewe ni mfanyabiashara pengine ulitembea umbali mrefu kufuata bidhaa zako pengine ulitukanwa hata na wateja wako lakini bado ulifanya kwa moyo mmoja.

Ulifanya hayo yote kwasababu ya DHAMIRA iliyokuwa njema lakini mavuno yanapokosekana shambani au hasara yoyote inapotekea katika biashara siyo sababu ya kujilaumu wala kujihukumu kwasababu kwa kila shughuli unayopanga kuianza kabla ya kuifanya hauwezi ukapanga kuja kupata matokeo hasi.

Hivyo dhamira itabaki lengo kuu na matokeo yatabaki kama matokeo hivyo kwa matokeo hasi yanakuja ili kuboeresha ufahamu wako hivyo hatuna neno KUFELI pale matokeo yanapokuja hasi ila tuna maneno "Njia ambazo hazijaleta matokeo sahihi kulingana na dhamira" hivyo inakuhitaji ubadili njia na kubadili njia kunawezekana tu endapo akili yako haitakuwa na hatia juu yako hivyo kuupa ubongo wako nguvu ya kusukuma akili nyingi ili kuleta njia zingine bora.

Hivyo ndivyo ubize wa SUPERIOR unavyokuwa bize ni katika kutafuta njia bora wakati ubongo wa wewe mwingine unakuwa bize kwenye kujutia na kujihukumu, swali kwako mwanadarasa unafikiri ni nani ataendelea kusonga mbele kati ya hawa watu wawili anaetafuta njia na anaejihukumu?.

Kuna huyu jamaa anaitwa THOMAS EDSON mgunduzi wa bulbu anasema, katika jaribio lake la ugunduzi wa bulbu SIKUFELI MARA elfu kumi ila nilitumia NJIA elfu kumi ambazo hazikunipa majibu sahihi katika ugunduzi wa bulbu. Hivyo kataa neno kufeli itoe akili mahakamani songa mbele.
Screenshot_2017-07-13-12-21-33-1.png

Tuonane sehemu ya nne.

<H.FARADAY> (0625934471).
 
Darasa mbna limesimama tena mambo ndo kwanza bado alafu limesimama

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
Darasa mbna limesimama tena mambo ndo kwanza bado alafu limesimama

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
Usijali mwanadarasa leo tutaendelea na darasa letu.

Sent from my GT-I9500 using JamiiForums mobile app
 
Somo la pili, sehemu ya nne (Lesson two part four).

Karibu tena leo twendelee kuelimika, katika sehemu ya nne tutaenda kujifunza kitu kinachoitwa;

FANYA MAAMUZI SAHIHI NA SIYO MAAMUZI YA KUPENDEZA.

kuna misingi miwili msingi wa KUPENDA na msingi wa KUWEZA. Maamuzi yanayotokana na msingi wa KUWEZA huwa ni SAHIHI lakini maamuzi yanayochipukia kwenye msingi wa KUPENDA huwa 90% si sahihi na wanadarasa wengi wako hapa na huu ndo msingi unaokuwa wa kupendeza matokeo yake mwanadarasa anaenda kaskazini huku mafanikio yakienda kusini.


Moja ya kosa kubwa ambalo wanadarasa walio wengi hulifanya ni kushindwa kutofautisha maneno haya mawili KUPENDA na KUWEZA katika kuwaongoza kufanya maamuzi juu ya shughuli gani watakayoifanya itakayowaingizia kipato. Ni 10% tu ya watu ambao hufanikiwa kwa kuanza na msingi wa maamuzi wa KUPENDA kwa maana nyingine ni 10% tu ya wale wanaofanya shughuli fulani kwasababu wanaipenda na wakajikuta ndiyo shughuli haswa wanayoiweza lakini 90% ya watu hawafanikiwi kwasababu licha ya KUPENDA kwao huwa hawawezi.

Lakini watu wanaofanya shughuli fulani ya kuwaingizia kipato kwa kufuata msingi wa maamuzi wa KUWEZA ni 80% wanaofanikiwa pasipo kujalisha kama hicho kitu walikuwa wanakipenda au laah.

Kwanini 80% hii ni kwasababu KUPENDA na KUWEZA ni maneno ambayo yamezaliwa kutoka katika nyanja mbili tofauti, tukianza na KUWEZA hili limetokana na chimbuko la uumbaji au uweza aliopewa binadamu ndani yake na ni tofauti na aliopewa binadamu mwingine, lakini neno KUPENDA linatoka katika nyanja ya HISIA hivyo ni kitu kinachoweza kujengwa au kubomolewa wakati wowote.

Baada ya watu kuanza kufanya shughuli fulani kwa maamuzi ya KUWEZA huwa wanaanza na kutokuipenda hiyo shughuli lakini kwasababu KUPENDA ni kitu cha HISIA huanza kujijenga na kisha mtu huanza kuipenda hiyo shughuli, tofauti na aliyeanza KUPENDA hataweza kufanikiwa kwasababu kuweza hakuji njiani sio kitu cha hisia bali ni kitu cha uweza Hivyo huyo mtu hatafanikiwa kwasababu ataishia kuiga jinsi ya kukifanya kitu hicho kwa kuwa hana uwezo nacho.

20% zinaenda wapi kwa watu wanaoanza na msingi wa KUWEZA? hawa wanashindwa kufanikiwa kwasababu hushindwa kukuza hisia za KUPENDA wanachokiweza hivyo huwa ngumu kufanikiwa , kwasababu watafanya pasipo uhuru wa akili na nafsi na pia watafanya chini ya uwezo wao kwa kukosa ARI ya kukifanya hicho kitu. Hivyo tuna mifumo miwili ambayo ni
  1. KUWEZA-----> KUPENDA hapa ndipo mtu atakapofanya kitu kwanza kwasababu anakiweza kisha kupenda kutajijenga baadae kwasababu hisia hujengeka katika pande mbili furaha na huzuni hivyo hisia ya kupenda itakuja kutokana na furaha ya mafanikio.
  2. KUPENDA-----> KUWEZA huu mfumo wa pili 10% tu ndio watakao fanikiwa na hiyo itatokea endapo mtu pamoja na kuamua kukifanya kitu kwa kukipenda lakini ni kitu ambacho ndicho alicho na uwezo nacho, 90% hatafanikiwa kwasababu hawatakuwa na uwezo nacho hivyo wataishia kuiga.
Msingi wa KUWEZA mara nyingi hupuuzwa kwasababu mara nyingi kile mtu anachokiweza kinakuwa hakimpendezi machoni pake au hakipendezi machoni pa wanajamii, Hivyo hakitamfanya aheshimike au kitamfanya jamii imdharau hivyo atakikwepa na kwenda kung'ang'aniza kile anachokipenda, kwasababu 100% ni lazima atakipenda kitu chenye taswira nzuri mbele yake na jamii kiujumla. Mwanadarasa unaweza kuona wewe ni mtanashati ama mrembo hivyo kuuza juice au matunda kitakufanya usiheshimike mbele ya jamii na kikakushushia hadhi lakini ni kitu ambacho UNAKIWEZA kwa 100% yani ukiongea tu mteja kesho atakuja tena kwasababu uweza wako umejengeka katika kauli.

Inawezekana umejengwa uweza ndani yako ukamfundisha au kumwelekeza mtu mpaka akaelimika lakini kwasababu tu hutaki ualimu basi hautakuwa tayari kukifanya hicho kitu huku uking'ang'aniza kuwa mfanyakazi wa benki kwasababu hata jamii ikikuona kuwa upo sehemu ya kiyoyozi itasema ndiyo yule, ndo mtu fulani, lakini kuwa mwalimu kama FARADAY hapa jamii itakudharau.

Na hii misingi ndiyo ambayo hujengwa mpaka kwa watoto wetu na hivyo kuwaelekeza katika mwelekeo wa vitu vinavyoonekana na wanajamii vyenye kupendeza sana, Lakini tunasahau msingi wa kuwaelekeza watoto wetu katika mwelekeo wa vitu wanavyoviweza.

Mwanadarasa utakuwa shahidi hapa pale inapoinuka misemo kama

1."Napenda sana kufanya hiki lakini sifanikiwi nimetumia nguvu na akili yote lakini wapi" mwalimu anakwambia hapo akili haitumiki bali kivuli cha akili, ubongo hauwezi kusukuma akili ikafanye kitu ambacho hauna uwezo nacho, hapa utatumia akili inayotokana na nguvu ya macho kwa kuiga kile unachokiona.

2."Sipendi kufundisha" lakini matokeo kila yanapokuja somo lake ndilo ambalo la kwanza kufaulisha au wanafunzi wanajivunia kuwa nae kwasababu wanamwelewa" hapa ni pale unaposhindwa KUPENDA unachokiweza.

Msaada wa ASILIA (nature).

Asilia au nature kama wengi wanavyoelewa kwa urahisi husaidia sana kumlazimisha mtu arudi afanye kile anachokiweza hapa ni pale kauli hii hutokea
"Nilikuwa najaribu tu kufanya hivi lakini nimefanikiwa hata siamini nahisi nimebahatisha" hapo mwalimu anakuambia umeongozwa na nature kukusaidia kukuonesha kile unachokiweza ili uache kuhangaika na kile usichokuwa na uwezo nacho, lakini mtu hataendelea kukifanya kitu hicho kwa ufanisi zaidi akiamini ni bahati.

Hivyo mwalimu anakwambia mwanadarasa fanya kitu unachokiweza, KUKIPENDA kutakuja tu kwasababu kupenda ni HISIA, utakapofanya unachokiweza ndipo ambapo ubongo utasukuma akili nyingi zaidi na kukuonesha kile ambacho wengine hawakioni juu ya shughuli hiyo. Haijalishi hicho kitu unachokiweza hakina heshima sana mtaani au hakina heshima mbele ya macho yako lakini amini wewe ndiye utakaeenda kubadilisha taswira nzima ya hiyo shughuli na kuifanya iheshimike mbele ya jamii.

Usiende kuimba kwasababu Unapenda muziki nenda kwasababu unaweza muziki, Usifanye kitu kwasababu ya jina lake ambalo lilijengwa na watu waliokuwa wameumbwa na uwezo wa kukifanya hicho kitu, bali fanya kwasababu unaweza hatakama ni kidogo, kuna huyu jamaa anaitwa Napoleon Hill anakwambia "do small things in a great way"

Pia wewe umechelewa kukifanya unachokiweza mwanao hajachelewa tutakuja kuchambua vizuri tukifika katika nyanja ya Elimu lakini Usishangae Ronaldo pamoja na kuwa na hela nyingi za kuweza kumpeleka mtoto wake shule yoyote ile hata ikianzishwa sayari nyingine Lakini atampeleka Akademiki ya mpira kwasababu anampeleka kwenye kitu ambacho anaweza.

Tukutane sehemu ya tano na ya mwisho ya somo letu hili la pili ambapo tutakuwa na kichwa kinachosema "NJIA ZA KUSAFISHA UBONGO NA AKILI" muhimu sana hapa.

PIA USISAHAU KUMCHEKI MWALIMU KUPITIA NAMBA YAKE KWA AJILI YA KUUNGANISHWA WHATSAPP KWA MASOMO MENGINE YATAKAYOKUWA YAKIENDELEA HUKO.

<H. FARADAY> (0625934471).
 
Sasa mwalimu inakuaje mtu anafanya jambo ambalo ana uwezo nalo japokua alipendi lakini pia matokeo anayopata yanakua ayamridhishi kwa upande wake uoni kuwa itakuja imjengee majuto baadae kwa kufanya kitu ambacho akikumletea matunda mazuri
Lakini pia hakutakuwa na furaha ya mafanikio itakayompelekea yeye kupenda kulifanya zaidi jambo lile

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Sasa mwalimu inakuaje mtu anafanya jambo ambalo ana uwezo nalo japokua alipendi lakini pia matokeo anayopata yanakua ayamridhishi kwa upande wake uoni kuwa itakuja imjengee majuto baadae kwa kufanya kitu ambacho akikumletea matunda mazuri
Lakini pia hakutakuwa na furaha ya mafanikio itakayompelekea yeye kupenda kulifanya zaidi jambo lile

Post sent using JamiiForums mobile app
Okay katika kulijbu hilo swali kuna somo tutakuja kujifunza jinsi ya ku-proove unachokifanya je ndicho unachokiweza kwasababu unaweza kujiona unaweza kitu flani lakini kumbe siyo chenyewe lakini pia unaweza ukajiona sio kitu kimoja unachokiweza bali ni zaidi ya vitatu hivyo unashindwa kujua ni kipi haswa ambacho ndo chenyewe. Lakini siyo hivo tu inawezekana ukawa unafanya kitu ambacho unakiweza lakini unakifanya katika njia zipi je ni hizihizi za kawaida ambazo zimezoeleka? ni kitu gani cha tofauti ambacho wewe umeamua kujitofautisha na ufanyaji uliozoeleka? kwa mfano leo mtu anaweza kujiona anaweza kuimba na kweli sauti anayo lakini kuna zaidi ya wasanii zaidi ya elfu 50 hapa nchini hivyo utafanya nini ili tuweze kuisikiliza sauti yako tukaacha sauti za wengine elfu 49. Hivyo si kila unachokiweza unakiweza peke yako mnaweza mkawa hata elfu moja lakini NJIA za ufanyaji ndizo zitakazowatofautisha kuwa huyu sasa ni g vizy.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Mwalimu Leo vipi atuendelei

Post sent using JamiiForums mobile app
 
SOMO LA PILI sehemu ya tano (Lesson two Part five).

Karibu tena mwanadarasa katika mfululizo wa masomo haya, kama mwalimu alivyoahidi somo lililopita kuwa leo tutakuwa na somo muhimu kabisa lenye kichwa kinachoitwa;

NJIA ZA KUSAFISHA UBONGO NA AKILI.

Lakini kabla ya kuliangalia somo hili mwalimu anazidi kukumbusha kuwa tumia namba hiyo mwisho wa somo kuwasiliana na mwalimu kwa chochote, lakini pia ili aweze kukuweka kwenye list ya watu watakaounda group la WhatsApp kuna masomo mengine hususani katika nyanja ya Elimu yataendelea huko pengine mengine yasionekane hapa hii yote kwasababu ukweli ni mchungu, naimani watakuwepo ambao watakuwa wamemwelewa mwalimu hapa.

Tuendelee na somo letu kwa kuanza kuziangalia njia mbalimbali za kusafisha ubongo na akili.

●Njia ya kwanza

Samehe kizazi kilichopita.
Hapa tunazungumzia nini ni pale mtu anapata unyonge wa nafsi kutokana na familia iliyomleta duniani, kwa kushindwa kumuandalia mazingira thabiti ambayo yangemfanya asiwe hivyo alivyo. Anajiona alikuwa na uwezo mkubwa wa kuelewa masomo shuleni lakini kutokana na hali duni ya wale waliomleta akakosa kwenda shule nzuri ambayo leo ingemfanya aonekane mtu fulani katika jamii. Anajiona ana uwezo mkubwa wa kufanya biashara lakini kutokana na hali duni ya wale waliomleta anakosa msaada wa kuwezeshwa hata kupata mtaji. Kijimshahara anachokipata hakimtosherezi lakini ni lazima apate usumbufu wa kuombwa na hata kusaidia bila kuombwa kwasababu nayeye anaona hali ya uduni iliyopo.

Anaishia kulaumu nafsi yake, anaona HATIA iliyoambatana na huruma juu ya kizazi chake kilichopita kwa maana ni kweli lilikuwa jukumu la waliomleta duniani kumwandalia mazingira. Hasira ndani ya moyo wake inamjia akiona fursa zilizowazunguka waliomtangulia lakini walishindwa kuzifanyia kazi. Anapata WIVU ndani yake unaojawa na hofu ya kuogopa kukufuru, ukimwachia kauli ya kwamba "Mimi ndo ningezaliwa familia ile".

Mwalimu anakwambia kuja kwako wewe duniani siyo ili ufanane na waliokuleta bali ulete kitu kipya, muda mwingi unaotumia kuwaza na kunung'unika na kujiona si mwenye bahati NDIO kitu kitakachokufanya uje ufanane na waliokuleta kisha hali hii iendelee kwa kizazi utakachokijenga wewe. Mwalimu anakwambia jione mwenye bahati kwasababu wewe ndiye unayeenda kufanya NURU ndani ya kiza nene, ndiyo maana umeweza kuyaona haya.

Waliokutangulia hawakuyaona haya hivyo pamoja na fursa walizozikuta upofu wa kuziona uliwaandama, kumbuka msemo nilioutoa katika somo mojawapo lililopita kuwa "minds are like parachutes, they function only when open". Ona Fahari kwasababu wewe unaenda kuwafungua UBONGO wanaokuzunguka, ni Fahari kubwa pale unapokuwa MWANZILISHI wa mapinduzi yenye tija kuliko pale unapokuwa MWENDELEZAJI.

Epuka maneno yafutayo;
Epuka kutumia dini kama kigezo cha faraja ya hali duni uliyopo.
Kuna msemo wa huyu jamaa anaeitwa karl Marx anasema "Religion is the impotence of human mind to deal with occurrences it cannot understand" mwalimu anakwambia kama hali duni ingekuwa ndiyo njia ya kuitukuza dini yako basi ungelikuwa sahihi lakini hata yule aliyekuletea hicho unachokiamini hana hali kama uliyonayo, kulingana na imani yako dini ikusaidie kuja kukufikia kule unakoamini kuwa kuna maisha mengine baada ya kifo, kuliko ukishike hicho unachokiamini ili uweze kula, hahaha! Unaweza ukaishia kufanikisha kula na usifike unakoamini kuwa kupo. Umepewa akili na utashi maarifa na ufahamu vifanyie kazi.

Pia kumbuka bill gates anakwambia "kuzaliwa maskini siyo kosa lako bali kufa maskini" Hii ni njia ya kwanza ya kusafisha UBONGO na AKILI bado njia mbili twende taratibu ili tuweze kuzielewa baada ya hapo twende tukafanye mabadiliko.

Tuonane baadae tukiiangalia njia ya pili na ya tatu. Usikose

<H.FARADAY>(0625934471).
 
Yaan mm huwa naic mwalimu kama unanipunja manake manake nakuaga na shauku ya kujua vitu vingi siku ya pindi nahic kama tilio unalonipa linakua halinitoshi natamani niendelee kujifunza zaidi

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom