Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

"The training of children is a professional, where we must know to waste time in order to save it" (by -jean-jacques-Rousseau `philosopher).
put a link here where we copied so that we can give an appreciation by siting him/her in our lesson. Thank you.
Lete vitu achana na wavimba macho wenye wivu kama huyo, nayeye akopi alete humu kama kukopi rahisi
 
Sehemu ya nne

Mwalimu hana shaka juu ya Afya yako mwana darasa hivyo anakukaribisha tena kwa mara nyingine upate kuelimika.

Katika somo letu hili la kwanza linaloitwa

JITAMBUE na KUTAMBUA ni nini umebeba na una NGUVU na UWEZO kiasi gani (self esteem).

Maneno yenye herufi kubwa ndiyo msingi wa somo letu hili, Tayari mpaka sasa tumeweza kuyaangalia yote, tulianza na sehemu ya kwanza na ya pili ambazo zilikuwa chini ya neno KUJITAMBUA tukajiuliza kuwa sisi ni akina nani na kwanini tuko hivi tulivyo. Lakini siyo hivo tu pia tukaweza KUTAMBUA neno MAISHA ambalo ndo msingi na somo kuu. Hatukuishia hapo tukaendelea kuangalia UWEZO na NGUVU tulizonazo zilizo ndani ya ubongo wetu lakini tumeshindwa kuzitumia kwa kushindwa KUONA (taking in the sights), KUNUSA (taking in the smell) na KUONJA (taste).

Leo katika sehemu hii ya nne tutaenda kuangalia kitu kinachoitwa;

KUPUMBAZWA kwa mwanadarasa.

Kabla ya kupaangalia hapo mwalimu angependa kukuambia wewe mwanadarasa kuwa kuna philosopher mmoja anaitwa AYN RAND anasema "The truth is not for all men, but only for those who seek it" <kuujua ukweli si kwa watu wote isipokuwa wale watafutao kuujua> hivyo mwanadarasa usijihisi mpweke ukiwa peke yako darasani endelea kuhudhuria mwalimu hatoacha kukufundisha wewe maana jamii haianzi kubadilishwa na kijiji isipokuwa mtu mmoja (a single person).

Mwalimu anaanza kutufundisha sehemu hii ya nne kuwa hapa duniani kuna jela za aina kuu mbili ya kwanza jela inayoonekana kwa macho ya nje (visible prison) na ile isiyoonekana (Indivisible prison) hapa tutaenda kuangalia hii isiyoonekana, kabla ya kwenda kuiangalia hiyo jela mwalimu anakwambia kuwa hii ndo sehemu inayoenda kuhitimisha somo letu hili la kwanza. Kwamba pamoja na kujitambua wewe ni nani na pia kujua kuwa kwanini uko hivyo ulivyo na kuelewa neno maisha MZIZI wa kwanini haukuyajua hayo yote ni kwasababu upo JELA na hii jela ndo jela isiyoonekana ni ipi hiyo twende tukaiangalie.

Jela isiyoonekana ni jela ya akili, ufahamu na maarifa, jela hii na ile inayoonekana mtumwa wake ni lazima apate adhabu au kutumikishwa kwa mwanadarasa ambae amewahi kwenda jela hizi zinazoonekana atakuwa ni shahidI kuwa jela siyo sehemu ya starehe, vivyo hivyo jela hii isiyoonekana inatoa adhabu kali adhabu hii ni HALI ya maisha ya mwanadarasa.

Mwalimu hakulaumu wewe mwanadarasa kwa kushindwa kujitambua na kutambua kuwa kwanini uko hivyo ulivyo siyo hivyo tu bali pia kushindwa kuelewa dhana ya neno maisha ni nini
Kwasababu siyo wewe tu ambae ni mtumwa wa hiyo JELA bali JAMII nzima, jela hii isiyoonekana imewekwa na yule anaeonekana yuko juu yako (superior) wewe mwanajamii, yuko juu yako wewe mtanzania na pia yuko juu yako wewe mwafrika, utasaidia kumwambia mwalimu kuwa ni nani. Jela hii imeifunga akili, ufahamu na maarifa kwa kuipumbaza hivyo kukulazimisha mwanadarasa kuishi kwa kumuiga SUPERIOR. Mwalimu anakuomba mwanadarasa utulize akili ili uweze kupaelewa hapa ambapo panaenda kutuonesha ni nini kilichopo kati yako wewe na SUPERIOR na kama hautaelewa usisite kuja kuuliza tena na tena

Maisha ya binadamu ni SAFARI, mwalimu pamoja na wewe mwanadarasa tunasafiri katika safari tunakutana na mabadiliko ya hali hivyo inatulazimu kubadili vitu mbalimbali ili tuweze kwendana na mabadiliko ya hali, kinachotokea hapa ni kwamba SUPERIOR anabadilika lakini huku akiwa ameipumbaza akili yako isibadilike sawa na yeye bali isubiri yeye abadilike kwanza ndipo wewe uje uige mabadiliko. Mwalimu anatoa mfano kuwa zamani kulikuwa na wanasayansi na wagunduzi wa vitu mbalimbali kama Isaac Newton, Michael Faraday,Albert Einstein baada ya hawa viumbe muhimu kabisa kuwahi kutokea katika uso wa dunia wengine waliofwata baadae walikuja kuthibitisha michango ya waliowatangulia na kuweza kuongezea au kukosoa palipobidi hivyo pia waliofwata walikuja kuanzia walipoishia wengine.

Hii inakuja kuonesha kuwa maisha ni hatua na kila hatua inayokuja lazima iendelee kwenye ile iliyoisha (final stage is the beginning of the next stage) hivyo ndivyo wafanyavyo SUPERIOR mwalimu anakwambia mwanadarasa kuwa KOSA halikuwa kujua SUPERIOR anafanya nini, anaishi vipi na ameishia kwenye nini, KOSA ni kwamba kama yeye na wewe wote mna ubongo tofauti kwanini kila mmoja asitumie akili, ufahamu na maarifa yake kuweza kujua ni nini kinachofuata? Mpaka mwanadarasa unaamua kuwa MUIGAJI? na yeye amekwisha kuiunda mizizi ili ujione wewe bila yeye hauwezi kuishi, na anajua kuwa mwanadarasa hutaki kushughulisha ubongo na unapenda vitu rahisi na hakuna kitu RAHISI duniani kama kuiga.

Hivyo falsafa ya kupumbazwa inatokana na kitu kinachoitwa kuiga. Mbali na kuanzia ambapo Afrika inamuiga superior, Tanzania inapomuiga superior, bali pia ndani ya jamii inayokuzunguka mwanadarasa kuna mwanajamii mwenzako ambae unamuiga, naye anaonekana ni superior na mwanadarasa anatamani kabisa kuwa kama huyo mwanajamii-superior hivyo ndivyo mwanadarasa unapozidi kupumbazwa na SUPERIOR mkubwa asiwe na wasiwasi wowote wa kwamba ipo siku utaamka.

Kupumbazwa huku hutambuliwa na nafsi na huku nafsi ikikutaka utoke katika kifungo hicho lakini wingu zito lililokutanda linaipinga hapa ndipo kinazaliwa kitu kinachoitwa KUJIAMINI na KUAMINI mwalimu anaeleza kuwa binadamu yeyote hukumbwa na majibizano ndani ya nafsi yake majibizano haya hutokea baada ya nafsi kuona kile kilichopo ndani ya ubongo na hivyo kukuambia mwanadarasa KIFANYIE KAZI lakini ghafla inainuka nafsi iliyojaa kutokujiamini na kutokuamini (inferiority complex) ambayo inakuwa imetengenezwa na SUPERIOR.

Hiyo inferiority complex inakuwa na majibu yafuatayo <Mbona sijawahi kuona mtu yeyote akifanya kitu kama hiki?>, <watu wote dunia hii wasingeweza kukiona na kukifanya hadi niwe wa kwanza mimi?>, <jamii itanielewa kweli? Na itanichukuliaje?> na majibu mengine Mengi HIVYO hitimisho litakuja kuwa NISIJISUMBUE kisha mwanadarasa huenda kufanya kitu ambacho kinafanywa na wanajamii wengine kwasababu anajitengenezea ulinzi kuwa < hata nikishindwa sitakuwa wa kwanza mimi maana wapo waliotangulia kufanya hivo na wakashindwa>.

Mwalimu anaenda mbele zaidi kuwa kuna msemo wa kifilosofi unasema "THE MEANING OF PEACE MEANS THERE'S NO OPPOSITION" <maana ya amani ni kukosekana kwa kipingamizi/upinzani> hivyo wanadarasa wengi mmejaa AMANI nafsini mwenu huku mkikosa furaha ya maisha. Kuna kitu hiki ambacho ni muhimu kabisa kukijua.

Nacho ni wanadarasa hawataki kusikia kitu kinachoitwa sayansi kwa kuona ni kigumu ni kweli ni kigumu na ndio maana hakifwatwi, SAYANSI msingI wake mkubwa umejengeka kwenye neno Majaribio Hivyo ugunduzi wa chochote unachokiona ulianza kwa jaribio hivyo kile nafsi yako inakwambia kwa kukiona ndani yako mara tu kitakapokuja nje ya mwili kitaanza kufanyika kwa njia ya jaribio hapa ndipo tunapata kitu kimoja kinachoitwa UJASIRI (SELF CONFIDENCE). Ukiwa nacho hiki na kukisimamia ndipo utakapoweza kuingia kwenye kundi la HUYU mtu anaeitwa SUPERIOR.

Tumepumbazwa katika nyanja mbalimbali katika uchumi, biashara, kilimo, kisiasa na kielimu. Mwalimu atagusia kidogo kwenye elimu maana ndiyo kitako cha hizo nyanja zingine.

Tukiangalia katika Elimu kuna huyu aliyekuwa mtu mashuhuri anaeitwa WASHINGTON CARVER anakwambia <Education is the key to unlock the golden door of freedom> Elimu ni ufunguo wa kufungua mlango wa dhahabu uliofunga UHURU. Kuwa huru ina maana ufanye kile unachoona wewe mwanadarasa ni sahihi kwa kutumia Elimu yako na si Elimu itumike kufanya kitu kwa kutumia uhuru wako. TUTAKUJA KUCHAMBUA ZAIDI TUKIFIKA KWENYE NYANJA YA ELIMU ambapo tutaweza kuangalia kitu kinachoitwa elimu unayoifuata na kuitumia wewe mwanadarasa na kujiona una kiwango fulani cha elimu ni ELIMU INAYOKUPUMBAZA NA SI KUKUZINDUA utanielewa zaidi utakapo jifunza UTOFAUTI KATI YA ELIMU YA "KUFAHAMU" NA ELIMU YA "KUTUMIKA"




Tuonane katika somo lijalo LESSON TWO (2)


By <H.Faraday> (0625934471).
 
mh.nakurudisha nyuma kidogo sehemu ya pili ulituahidi sehemu ya tatu utaletaa tofauti ya majukumu ya mwafrica hususani mtanxania na wazungu nimefutilia sijaona
 
Mwalimu ulisema sisi tunatumia asilimia20% ya ubongo wetu kipi nikikifanya ntajua kweli nimetumia zaidi ya hizo asilimia
 
Mwalimu ulisema utatufundisha kutumia 80% ya brain iliyobaki nmesoma mpaka mwisho sijaona au umefumba?
 
Mwalimu ulisema sisi tunatumia asilimia20% ya ubongo wetu kipi nikikifanya ntajua kweli nimetumia zaidi ya hizo asilimia
Katika sehemu ya tatu kuna Aya nimeandika "mwalimu anakutaka uchukue daftari uandike kiporo kuwa tutakuwa na somo linaloitwa set of mind na pia tutaenda kuangalia asilimia 80% kuwa ni za nini na zinatumikeje" Hilo ni somo la tatu hivyo endelea kufwatilia mwanadarasa utazijua tu.
 
Mwalimu ulisema utatufundisha kutumia 80% ya brain iliyobaki nmesoma mpaka mwisho sijaona au umefumba?
Kama umesoma na umeelewa unaweza kugundua kitu kuhusu hizo 80% maana kama umejua 20% unazitumia kwenye nini na ni nini ambacho hujakiona wala kukinusa wala kukionja ambacho kinakuhitaji utumie asilimia zilizo kwenye hazina <80%>.

Lakini isiumize kichwa endelea kuhudhuria ni Somo la Tatu ambalo litaongelea kitu kinachoitwa set of mind na hizo 80% ni za nini na zinatumikeje, kama nilivyoahidi kwenye aya moja katika Somo la kwanza sehemu ya tatu. Siwezi kufumba kwasababu mwanadarasa amefumbwa hivyo itakuwa fumbo juu ya fumbo hivyo vitu ambavyo najua vinahitaji maelezo ya kina ili mtu aweze kuelewa vimeandaliwa somo lake kabisa.
 
SOMO LA PILI (LESSON TWO).

AKILI YAKO KUFANYA VITU ISIVYOPASWA KUVIFANYA NA KUTOKUFANYA VITU IPASWAVYO KUVIFANYA.

Ni imani ya mwalimu kuwa mwanadarasa u mzma na unaendelea kufwatilia mfululizo wa masomo yetu. Endelea kufwatilia yameandaliwa masomo mengi kwa ajili yako, usisite kuuliza sehemu yoyote ambayo utakuwa haujaielewa.

Somo letu la pili sehemu ya kwanza lina kichwa kinachoitwa;

MAHAKAMA NDANI YA NAFSI YAKO (HUMAN SPIRITUAL INNER COURT).

Mwalimu anaanza kwa kuelezea kwa maana rahisi kitu kinachoitwa mahakama, kuwa ni sehemu ambapo tunapata HUKUMU ya tatizo lilitokea kwa kufuata haki chini ya sheria fulani iliyowekwa ili kuleta usawa, suluhu na amani katika jamii husika. Tutajikita zaidi kwenye neno hukumu kama ambavyo nimeliandika hapo juu.

Ndani ya mwili wa binadamu kuna kitu ambacho wanafilosofia tunakiita CONSCIENS tunasema ni sauti ya ndani kabisa inayomuongoza mtu kwenye kipi sahihi afanye na kipi si sahihi asifanye (an inner voice or feeling viewed as an acting as guide to the rightness or wrongness of one's behaviour), hii sauti mara nyingi hupuuzwa (ignored) baada ya matokeo ya kile ulichoenda kukifanya kuwa siyo hii sauti inakupeleka kwenye mahakama ambayo ni nafsi kisha unaanza kuhukumiwa ndani, baada ya tukio lote hilo kufanyika kinakuja kitu kinachoitwa majuto (regression). Kumbuka vitu vyote hivi vinafanyika ndani yako hapa mwanadarasa utakuwa shahidi pale muda mwingine unatembea uko peke yako lakini unajiona kama uko na mwenzako kama mnapiga stori kabisa mwisho mtu anaweza hata kucheka peke yake hivyo kipindi hayo yote yanafanyika ni ngumu binadamu mwingine kujua kwasababu kipindi vinafanyika vyote hivo mwili wa nyama huendelea na majukumu yake kama kawaida.

Majuto haya huja kujionesha kwa hali ya nje ya kimwili ambapo mtu huyo anakuwa na msongo wa mawazo (stress) na pia huwa mwenye hasira au mnyonge kitu ambacho kinaleta madhara pia kwa binadamu ya kiafya kama Magonjwa ya moyo na mengineyo. Mwalimu anatoa mfano kidogo.

Mfano huu nitautoa kwenye mlengo wa mapenzi, inawezekana mwanaume ambae yupo ndani ya mahusiano lakini akapita sehemu na kumuona mwanamke flanI akavutiwa nae akaamua kwenda kumtongoza hiki kitendo cha kwanza lazima kitaambatana na sauti nyingine nyuma ndani yake inayomwambia MBONA UNAE LAKINI WA KWAKO ataamua kuipuuza, baada ya kumtongoza huyo binti akiulizwa swali labda kweli hauna mwanamke mwingine? Mwanaume atakachojibu kuwa SINA, lakini kutakuja sauti nyingine ndani yake inamwambia ACHA UONGO MBONA UNAE kumbuka huyu mtu anafanya majibizano bila mwanamke kugundua, hivyo huyu mwanaume anaweza kukubaliwa na mwanamke sasa ikijatokea labda mwanamke ni mwathirika na huyo mwanaume amekuja kuambukizwa ugonjwa. Hapo ndipo maneno yafutayo yanapojitokeaza na maneno hayo huenda nawewe mwanadarasa umewahi kumbana nayo katika tukio lolote flanI lilikutokea maneno hayo ni kama
  1. Lakini Moyo ulisita sana kufanya
  2. Nilihisi haya yangetokea
  3. Nilijua tu.
Na maneno mengine mengi hivyo hufanya kwenye nafsi yako kutawaliwe na migogoro kumbuka siyo tukio moja unalopata matokeo hasi, hivyo moyoni mwako kunakuwa na mlundikano wa Lawama na majuto ndani yako. Sauti hii hupuuzwa katika nyanja nyingi zinazohusu maisha ya binadamu, sauti hii hupuuzwa pale binadamu anapofanya shughuli ya kumuingizia kipato. Nini sabubu ya sauti hii kupuuzwa twende tukaiangalie.

Sababu ya sauti hii ya ndani (inner voice) kupuuzwa ni kutokana na msingi wa maisha uliojengwa kwa huo, msingi ambao unasimamia kwenye neno kawaida yaani kila utakachokifanya ni kitu ambacho kimeshafanywa tayari kitu ambacho kinakutaka upitie hatua moja mbili tatu zilizowekwa tayari ili uweze kufika, HUKU ukisahau hizo hatua hazikuwepo kabla isipokuwa ni mtu aliziona ndani ya ubongo wake na kuziweka hadharani leo hii inakuwa ndiyo njia (PATHWAY) ya wewe kupita.

KAWAIDA tunayozungumzia hapa ni kawaida ambayo jamii nzima imejengwa kwa hiyo, ambapo ndani ya jamii tunakutana na kauli hii "ili uweze kufanya hiki kitu kwa kawaida tunafanya hivi" lakini tunasahau huyo mwasisi wa hiyo inayoitwa kawaida ni mtu mmoja. Mfano wa kawaida mojawapo "mtoto anaefaulu darasa la saba, akafaulu na form four kisha form six na kwenda chuo moja kwa moja huyo ndo mwenye akili" lakini huyu ambae ataenda kukisomea kitu ambacho ndicho amejaaliwa nacho na kukibobea kabisa na kisha kuwa mtaalamu wa hicho basi mtu huyo hataheshimiwa kama msomi wala hataheshimiwa ama kuonekana ni mwenye akili kwasababu hajapita kwenye hiyo njia ya chuo kikuu, ila tu ataonekana anajua kitu fulani, hiyo ndo kawaida ambayo jamii imejengwa kwa hiyo, na kawaida zingine unazozifahamu wewe mwanadarasa.

Sababu nyingine inayofanywa sauti hiyo ipuuzwe ni kuusikiliza mwili wa nje ambao umejengwa ndani ya dhana ya kuamini kile tu ambacho kimekwisha kutokea hivyo kuamini kile ambacho hakijatokea bado huwa ni ngumu kwasababu mwili huu huona kama unaenda kinyume na uhalisia lakini pia huu mwili wa nje unaoongozwa na milango mitano ya fahamu ambapo hujitokeza neno tamaa kwa kuona au kusikia, pia hii nayo ni moja ya sababu inayopelekea kuipuuza hii sauti.

Mpaka hapo tunaweza tukatenganisha haya makundi mawili makubwa, la kwanza;

Kundi la kwanza Sauti hii inapuuzwa na msingi ambao umemjenga mwanajamii ambao uko juu ya neno kawaida hapa uhusika zaidi na kupuuza sauti inayohusika na shughuli za kuyajenga maisha zinamuingizia mtu kipato.

Kundi la pili sauti hii inapuuzwa na mwili wa nje unaoongozwa na milango ya fahamu ambapo tunapata neno TAMAA hapa panahusika na shughuli zinazohusu hisia kama mapenzi (love affairs).

Athari ya jumla ni kwamba unaupa ubongo ubize wa kushughulika na kazi ambayo haikupaswa kushughulika nayo, ubongo wako na wa SUPERIOR unakuwa uko bize ila tofauti ni aina ya ubize sehemu ya pili tutaangalia ubize wa superior ni upi wakati wewe mwanadarasa ubize wako ni kusuluhisha hiyo migogoro.

Hivyo baada ya Sauti hii kupuuzwa kinachokuja kufwata ni LAWAMA na HUKUMU ndani yako ambayo huendeshwa na mahakama ambayo ni NAFSI yako. Lakini Lawama na Hukumu hii huwa inakubaliwa katika kundi la pili kwa maana nyingine kujutia kunakubaliwa katika kundi la shughuli za kihisia KWANINI na pia vipi kuhusu kundi la kwanza ambalo linahusika na shughuli za utafutaji je majuto yanakubaliwa?? Na vipi kama niliisikiliza sauti na bado nikapata majibu hasi???

Tuungane sehemu ya pili ya hili somo la pili.

<H.Faraday> (0625934471).
 
Kwenye soma la mahakama ya ndani ningeomba pia ungetuwekea njia zakukwepa iyo kawaida na tamaa zinazo tokana na mwili wa nje
 
Somo la pili Sehemu ya pili (lesson two, part two).

Leo mwalimu ameamua kukuletea huu mwendelezo bila kuchelewa akiamini kuwa mwanadarasa una kiu na njaa ya kujifunza mengi.

Katika sehemu hii ya pili ya somo la pili tutaenda kuendelea kuangalia baadhi ya vitu tulivyovianza katika sehemu ya kwanza leo tutaenda kuanza na kundi la kwanza kwenye sababu za kupuuza sauti ya ndani (inner voice).

Sehemu ya kwanza kuna AYA ililitaja kundi hilo la kwanza nayo ilikuwa hivi;

"Kundi hili la kwanza sauti hii inapuuzwa na msingi ambao umemjenga mwanajamii ambao uko juu ya neno KAWAIDA hapa uhusika zaidi na sauti inayohusika na shughuli za kuyajenga maisha zinazomuingizia kipato"

Ni imani ya mwalimu kuwa Aya hiyo unaikumbuka vyema na kama haukumbuki rejea kusoma sehemu ya kwanza ili uweze kwenda sawa na mwalimu.

Hapa tuliongelea kwamba mwanadarasa amejengwa katika msingi ambao shughuli zake azifanyazo kila siku ili aweze kuwa hai (alive) basi shughuli hizo ni zile za KAWAIDA ambazo tayari zipo na zinafanywa katika jamii, au kwa lugha rahisi zinafanywa kwa mazoea au zimezoeleka kufanyika katika jamii, hebu tazama kulia na kushoto mwanadarasa hicho unachokifanya kikoje au nawewe unakifanya kwasababu umekuta kipo kinafanyika? Basi hapo utakubaliana na mwalimu kuwa unalitukuza neno KUIGA kama mwalimu alivyolizungumzia katika masomo yaliyopita, na kwa njia hiyo unazidi kumpa raha SUPERIOR.

Jinsi ya kutoka kwenye huu msingi uliojengeka kwenye neno KAWAIDA au mazoea ni kuiruhusu akili yako iende mbali zaidi kufanya REASONING nje ya zile 20%, kwasababu kuendelea kudumu katika msingi wa neno KAWAIDA au mazoea REASONING inayofanyika hapo ni chini ya 20% kwasababu akili inaenda kwa KUIGA ambapo hapo kutajitokeza neno lingine linaloitwa "ULIZA"

Neno ULIZA ni kijimsingi kidogo ndani ya msingi KAWAIDA kijimsingi hiki kinaenda kinyume na REASONING, wakati kitendo cha reasoning kimesimamia neno KUJIULIZA huu msingi unaenda kijimsingi kinachosimamia neno ULIZA haya ni meneno mawili tofauti ambayo moja linakutaka wewe utumie uwezo wako huku lingine likikutaka utumie uwezo wa mwingine na nirahisi kutumia uwezo wa mwingine kwasababu kitu ni KAWAIDA kimezoeleka hapa ndipo mwanadarasa anapokuwa na utegemezi wa kifikra na utumwa wa kifikra.

Mwalimu anakukumbusha mwanadarasa kuwa mtu tunaemzungumzia hapa ni yule ambae anataka kufaulu maisha kwa njia halali (legal ways) hivyo mwalimu hahusiki na wale ambao kuyamudu maisha ni kwa njia ambazo ziko zaidi ya UBINADAMU.

Kutokana na kuwepo ndani ya msingi KAWAIDA mwanadarasa lazima ufeli maisha, wote unaowaona ambao wako ndani ya msingi huu hawapo hata kwenye 10% ya kufaulu maisha yao mwanadarasa anaweza kuona kuwa mbona wapo ambao wapo kwenye huu msingi ambao wanajishughulisha na ualimu kwasababu walikuta kuna kitu kinachoitwa ualimu au ni polisi kwasababu walikuta kitu kinachoitwa polisi na wana nyumba na usafiri wa kutembelea mwanadarasa ukaona hawa watu wamefaulu,

Mwalimu anakwambia mwanadarasa kuwa hawajafaulu hivyo kipimo cha kufaulu maisha ni nini???..................

Itaendelea

<H.FARADAY> (0625934471)
 
Back
Top Bottom