Darasa: Chakula cha akili (Mental food)

Yaan mm huwa naic mwalimu kama unanipunja manake manake nakuaga na shauku ya kujua vitu vingi siku ya pindi nahic kama tilio unalonipa linakua halinitoshi natamani niendelee kujifunza zaidi

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
Majukumu mengine ya kufanya wajukuu mkono uende kinywani yanamfanya mwalimu kutingwa sana, kesho mapema ataweka mwendelezo.

Sent from my GT-I9500 using JamiiForums mobile app
 
Somo la pili, sehemu ya tano (Lesson two part five) Mwendelezo.


Kengele imegongwa tayari baada ya mapumziko turejee tena katika kuiangalia sehemu yetu hii ya tano ya somo hili la pili ukiwa ni mwendelezo.

Tuliishia njia ya kwanza ya kusafisha ubongo na akili hivyo twendelee na njia ya pili.

NJIA YA PILI

JISAMEHE MWENYEWE.


Moja ya mzigo mzito ambao moyo, nafsi na ubongo wako unabeba ni HUKUMU ya ndani inayokupelekea ujione mwenye HATIA juu ya hali ya maisha uliyonayo na juu ya hali ya maisha uliyopitia. Na tena kabla ya kuzama ndani zaidi anza kwa kujisamehe kwa kutokuijua elimu hii, mwingine atajilaumu kwanini asingeyasoma yote haya kungali mapema. Mwalimu anakwambia huu ndio muda wako muafaka wa wewe kuyajua haya, kama haitakuwa juu ya faida yako basi itakuwa juu ya jamii yako inayokuzunguka.
Kuna huyu mzee mwenzangu anasema;
1499753819292-1.jpg



Hivyo usijihukumu kwa hili pia. Kujiona mwenye hatia juu ya hali ulizopitia katika maisha yako kunakuja baada ya mengi uliyoyafanya na matokeo yake yakawa ndivyo sivyo, Unawaza jinsi ulivyoianza biashara flani lakini mwisho wa siku ukaporomoka mpaka kuja kula mtaji na sasa umebaki hauna kitu, sura inaonesha tabasamu mchana lakini usiku ukizima taa basi unayawasha mawazo mpaka asubuhi huku swali kichwani likiwa kwanini sikufanya vile? Kwanini sikutumia njia ile?

Huku unasahau kuwa kabla ya kufanya ile biashara ulikuwa na dhamira njema, ukiomba kabisa na Mungu akusaidie uweze kuinuka katika maisha kupitia biashara ile, lakini ukasahau jambo moja kuwa DHAMIRA na MATOKEO ni vitu viwili tofauti, unatamani siku zirudi nyuma uanze upya, unaishia kujitupia lawama za kuona matokeo uliyoyapata ni UZEMBE.

Mwalimu anakuweka sawa juu ya neno uzembe, ni pale unapofanya jambo unalolielewa vyema bila ufasaha wake kwa mfano najua kabisa ili niweze kuvuna mazao yanipasa kuweka mbolea ya kukuzia lakini endapo sitaiweka, siku nikija kupata mazao hafifu kwasababu sikuweka hiyo mbolea ni UZEMBE haijalishi nilishindwa kuweka kwasababu gani.


Tofauti na hapa mwanadarasa anapojiona mzembe kwa kitu ambacho alitumia akili yake yote, maarifa ufahamu na nguvu zake zote katika kufanya kitu hicho, lakini kikaja kuleta majibu HASI huo sio uzembe bali ndipo UBONGO wako ulipoishia kusukuma kiwango cha akili iliyotumika katika kutekeleza kitu hicho. Hivyo hupaswi kujihukumu na kujiona mwenye hatia kwa kitu ambacho ulikifanya kwa DHAMIRA nzuri halafu kikaleta majibu hasi.
Nini ambacho ulitakiwa kukifanya ni hiki, kuna Dr mmoja anaitwa Dr.Seuss anasema “Don’t cry because it’s over, but smile because it happened” usilie kwasababu unaona ndo mwisho, mambo yote yameharibika laah bali tabasamu kwasababu tayari yamekwishatokea.

Kuna njia mbili za kujifunza.

Njia ya kwanza
kwa kuona, kwa kuuliza, kwa kuelekezwa, kwa kusikia na kwa kila aina ya kutumia milango yako ya fahamu ikiwa na maana yote ya kujifunza kitu kwa kupata usaidizi wa nje (external support).

Njia ya pili na ndo njia iliyobora na ndo njia inayokuja kuleta hukumu na hatia ndani yako ni njia ya JARIBIO, njia hii inahusisha “uhusika wa wewe mwenyewe katika kutekeleza kujifunza” na kupata msaada mdogo kutoka nje hapa ndo ambapo mtu anapoingia kwenye biashara kama ni ya nguo atakachohitaji msaada ni kuelekezwa kuwa sehemu gani atapata nguo za jumla lakini shughuli zingine zote zinazofuata zinakuwa juu yake, yeye ndo atajua nguo hii nilinunua elfu kumi hivyo mimi niuze elfu 15. kwanini tunaita jaribio ni kwasababu kitu chochote unapokifanya kwa mara ya kwanza linakuwa ni jaribio.


Kwamba una nadharia kichwani kwamba hiki kitu kinaenda hivi na hivi wana kemia wanaita (hypothesis formulation) lakini je ni kweli kiko hivo? Hivyo kukifanya ndo jaribio lenyewe ambapo utakuja kujua kama uko sahihi au hapana. Sasa basi kuwa makini hapa matokeo yoyote ya jaribio lako huwa ni njia ya kujifunza haijalishi matokeo ni mabaya ama mazuri, hapa ndipo unapokuja kujifunza kwa kitu tunachoita UZOEFU (experience).


Tatizo la mwanadarasa endapo matokeo yatakuja mabaya basi huwa ndo mwisho wa safari, mwalimu anakwambia hilo ndo kosa kubwa, yani unaacha kitu baada ya kukijua unapata hofu ya kukifanya tena baada ya kukijua na huku ulikifanya kwa ujasiri kabla ya kukijua inachekesha sana. Ndio maana katika kujutia kwako au kujilaumu kwako unazungukwa na mawazo ya kwanini nimefanya hivi na kwanini sikufanya vile lakini unasahau kuwa umezijua njia hizo kwasababu yametokea.


Unapishana na mavuno mwanadarasa, nini unatakiwa kufanya msikilize huyu jamaa anaeitwa Joseph Campbell anasema “we must let go of the life we have planned, so as to accept the one that was waiting for us” tuyaruhusu yale matokeo yetu yaliyotupata, tuyaache yaende maana yale ndiyo tuliyokuwa tumejipangia lakini kuna uhalisia wa jambo ambao ulikuwa unatusubiri lakini ulituhitaji tungali tumejifunza tayari. Sio huyo tu kuna huyu jamaa mwingine anaeitwa Thomas A. Edson mgunduzi wetu wa bulb anasema;
“Our greatest weakness lies in giving up, the most certain way to succeed is always just to try one more time” udhaifu wetu mkubwa ni kukubali kushindwa lakini njia ya mafanikio pasi na shaka ni kujaribu kwa mara nyingine tena.


Mwalimu anakwambia usijione mwenye hatia wala kujihukumu jisamehe jione uko huru akili ipate uhuru wa kuwaza njia bora ambazo ni zaidi ya zile ulizokwishazitumia. Kwendelea kujiona mwenye hatia ni kuzidi kupunguza muda wa akili nyingi kuelekezwa kwenye ufumbuzi kwasababu majuto sio tiba hata hivyo.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Africa.

Tuonane kwenye njia ya tatu na ya mwisho.



USISAHAU KUMCHEKI MWALIMU KWA NAMBA YAKE AKUWEKE KATIKA LIST.



<H.FARADAY> (0625934471).
 
"We must let go of the life we have planned,so as to accept the one that was waiting for us"

Hapa naomba mwalimu unifafanulie vizuri japo kwa mfano nipate kuelewa vizuri

Asante

Vizy boy

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
"We must let go of the life we have planned,so as to accept the one that was waiting for us"

Hapa naomba mwalimu unifafanulie vizuri japo kwa mfano nipate kuelewa vizuri

Asante

Vizy boy

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
Sawa mwanadarasa, ni nini huyu Campbell alikuwa anazungumzia ni hivi

Kwanza kumbuka tulikuwa katika kuongelea hali ambazo watu wamepitia ambazo hazikuwa nzuri mpaka kuwapelekea kujihukumu ama kujiona wenye hatia ndani mwao, kumbuka hali hizo zote ndo maisha yenyewe, na hizo hali zilitokea baada ya matokeo ya kitu/shughuli fulani kuwa hasi lakini kabla ya kufanyika hizo shughuli zote tulikaa chini tukaziandalia mkakati (Plans) lakini pale zilipoleta matokeo Hasi hatuna budi tukayacha maisha hayo yaende (maisha tunayoyazungumzia hapa ni mipango pamoja na njia tulizozitumia zilizotuletea majuto) ili tuyaanze maisha mapya (mipango, mikakati na njia mpya) ambayo yanatusubiri nje hatuyaoni kwasababu tupo ndani ya wingu la kujilaumu yaliyopita. Isikutishe ukaona sasa nayaacha vipi yale niliyo ya-plan hapana hatumaanishi kuacha shughuli uliyoi-plan bali hata kubadili njia kuachana na zile zilizokuletea matokeo hasi ni kuyaanza maisha mapya ambayo yalikuwa pembeni yakitusubiri tulipokuwa tunahangaika na zile njia ambazo hazikutuletea matokeo mazuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mwanadarasa, ni nini huyu Campbell alikuwa anazungumzia ni hivi

Kwanza kumbuka tulikuwa katika kuongelea hali ambazo watu wamepitia ambazo hazikuwa nzuri mpaka kuwapelekea kujihukumu ama kujiona wenye hatia ndani mwao, kumbuka hali hizo zote ndo maisha yenyewe, na hizo hali zilitokea baada ya matokeo ya kitu/shughuli fulani kuwa hasi lakini kabla ya kufanyika hizo shughuli zote tulikaa chini tukaziandalia mkakati (Plans) lakini pale zilipoleta matokeo Hasi hatuna budi tukayacha maisha hayo yaende (maisha tunayoyazungumzia hapa ni mipango pamoja na njia tulizozitumia zilizotuletea majuto) ili tuyaanze maisha mapya (mipango, mikakati na njia mpya) ambayo yanatusubiri nje hatuyaoni kwasababu tupo ndani ya wingu la kujilaumu yaliyopita. Isikutishe ukaona sasa nayaacha vipi yale niliyo ya-plan hapana hatumaanishi kuacha shughuli uliyoi-plan bali hata kubadili njia kuachana na zile zilizokuletea matokeo hasi ni kuyaanza maisha mapya ambayo yalikuwa pembeni yakitusubiri tulipokuwa tunahangaika na zile njia ambazo hazikutuletea matokeo mazuri.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwalimu hapo kwa lugha nyepesi naweza kusema kukata tamaa kwenye kutafuta mafanikio hakutokuongezea si tu majuto kutokana na njia ulizotumia kufeli Bali kukukatisha mwelekeo katika kutafuta mbinu mpya za kujaribu tena na tena

Kukata tamaa ni kitu kibaya sana katika maisha ya mwanadamu na kitu hiki hutokea tunapopanga plan na kushindwa kufanikiwa

Lakini pia mwalimu PLAN A ikishindwa kufanikiwa huwa tunaonelea tujalibu PLAN B na katika kufatilia kwangu sijawahi kusikia kuna PLAN C,D,na kuendelea hii inamaana kuwa matokeo ya kujaribu,kushindwa na kunyanyuka tena na kufanikiwa huwa yanategemea katika plan hizi mbili? Na kama ni hvyo vipi kuhusu kushindwa kwa plan hzo mbili hakuwezi kuzaa plan nyingine zenye matokeo makubwa zaidi ya zile plan kuu mbili za awali ?

Asante

Vizy boy

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
 
Mwalimu hapo kwa lugha nyepesi naweza kusema kukata tamaa kwenye kutafuta mafanikio hakutokuongezea si tu majuto kutokana na njia ulizotumia kufeli Bali kukukatisha mwelekeo katika kutafuta mbinu mpya za kujaribu tena na tena

Kukata tamaa ni kitu kibaya sana katika maisha ya mwanadamu na kitu hiki hutokea tunapopanga plan na kushindwa kufanikiwa

Lakini pia mwalimu PLAN A ikishindwa kufanikiwa huwa tunaonelea tujalibu PLAN B na katika kufatilia kwangu sijawahi kusikia kuna PLAN C,D,na kuendelea hii inamaana kuwa matokeo ya kujaribu,kushindwa na kunyanyuka tena na kufanikiwa huwa yanategemea katika plan hizi mbili? Na kama ni hvyo vipi kuhusu kushindwa kwa plan hzo mbili hakuwezi kuzaa plan nyingine zenye matokeo makubwa zaidi ya zile plan kuu mbili za awali ?

Asante

Vizy boy

Sent from my TECNO-W3 using JamiiForums mobile app
Swali zuri, Katika kufanya jambo/shughuli hatuna kitu kinachoitwa PLAN "B" wala F wala Z. Vuta subira kidogo kuna somo linaongelea vitu hivyo.

N:B haya masomo yanahitaji utulivu wa tofauti kidogo ili kuweza kuyaelewa. Kutoka kwenye misingi ya bandia tuliyojengwa nayo inahitajika nguvu ya ziada ni asilimia zisizozidi kumi ya vitu tulivyovigusa, kuna vingi sana mwalimu atatujuza twendelee kuwa nae.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Somo la pili sehemu ya tano (Lesson 2 part 5) hitimisho.


Ni siku nyingine tena karibu darasani mwanadarasa uendelee kujifunza. Sehemu iliyopita tuliongelea njia ya pili ya kusafisha UBONGO na AKILI hivyo leo twende tukaangalie njia ya tatu na ya mwisho.

NJIA YA TATU

WASAMEHE WANAOKUZUNGUKA.

Mwalimu anaposema wanaokuzunguka, hamaanishi majirani zako tu hapo nyumbani kwako/kwenu, bali watu wote ambao wanahusika moja kwa moja katika maisha yako. Kuanzia ndani ya familia yako, mahali unapoishi,kazini kwako, na Tanzania kwa ujumla mpaka hata dunia kwa ujumla kama una watu wanaokujua huko.
Ndani ya familia yako kunapokucha siku nyingine una majukumu fulani tayari ni sehemu ya maisha, ukitoka nje utasalimiana na majirani (degree of socialisation) tayari ni sehemu ya maisha, Utanyanyua simu kuwasiliana na mtu ambae yuko mkoa mwingine au nchi nyingine tayari nao ni sehemu ya maisha yako ni watu wanaokuzunguka.

Watu hawa wanaokuzunguka ni lazima wawe na uhusika wa moja kwa moja katika maisha yako, ni lazima ushirikiane na binadamu mwenzio ili kukamilisha maisha yako. Sasa katika kukamilisha huku maisha yako kwa uhusika wa binadamu mwenzio kutaambatana na matokeo mawili HASI na CHANYA.
Wapo ambao uhusika wao utakuletea matokeo CHANYA katika harakati za kuendesha maisha yako, hawa hatuna shida nao kwasababu hauwezi kuwa na kinyongo na mtu anaekuletea matokeo chanya. HAWA hatutawazungumzia kwasababu hawahitaji msamaha wowote.

Kwenye kundi hili lingine ambalo uhusika wao katika maisha yako unaleta matokeo HASI, hawa ndo walengwa haswa, hawa ndio ambao tunakinyongo nao kwa kuona pengine ugumu wa maisha tunaopitia umechangiwa/kusababishwa na wao. Hapa tunaongelea uhusika ulio ndani ya ubinadamu na si ZAIDI/NJE ya uwezo wa kibinadamu (beyond human capacity).
Tunapozungumzia uhusika wa zaidi/nje ya uwezo wa kibinadamu ni pale mtu anapoamini kukwama kwake au hali aliyonayo katika maisha ni kwasababu ya “KUROGWA” huku mwalimu hataongelea kwasababu huku kunasimamia katika msingi wa IMANI ya mtu.

Tukija kwenye uhusika wa ndani ya uwezo wa binadamu kumegawanyika katika makundi mawili, la kwanza;

Uhusika wa kiumbo.

Uhusika huu wa kiumbo ni pale mtu anapofanya jambo ambalo linaonekana na moja kwa moja linaathiri sehemu ya maisha yako au linakuletea matokeo hasi katika maisha yako.
Kwa mfano mtu uliekuwa unamtumia kwenye biashara zako kaingiza hasara kwa kutapeliwa, unafanya kazi fulani wafanyakazi wako wamefanya kazi fulani chini ya kiwango na kusababisha kutofikia lengo fulani, Umelima mifugo ya jirani yako imeingia shamba na kula mazao, wafanyakazi wenzako wanakuongelea vibaya kwa boss wako mpaka ikafikia boss kakusimamisha kazi, kuna hela uliziweka ndani mtoto wa mjomba wako ambae unaishi nae kakuibia, na mambo mengine mengi ambayo mwanadarasa umeyashuhudia au kufanyiwa na watu wanaokuzunguka yakakuletea matokeo hasi ya moja kwa moja ambayo yamepelekea kuwa na hali fulani katika maisha yako.

Mwalimu anaenda kukufundisha jinsi ya kupambana na uhusika huo, uwe makini hapa. Unaenda kupambana kwa njia ya saikolojia (psychology). Twende ukajifunze.

Moja ya kosa ambalo watu wanalifanya baada ya kutendewa jambo lililoleta matokeo hasi ni kutaka kulipa KISASI kwa mtenda. Mwalimu anakwambia Kisasi hakijawahi kuwa SULUHU na wala hakijawahi kuwa njia ya kukufanya mtendwa ukapata AMANI ndani ya moyo wako, mwanadarasa unabeba mizigo ndani ya moyo ambayo inakumaliza na kukuua na kukuwekea giza la kushindwa kuwaza nje ya zile 20%.
Kwanini kisasi hakijawahi kuleta AMANI ni kwasababu kabla ya kukitekeleza unakuwa na mzigo unaoitwa KINYONGO na kinyongo kinakuja kwasababu HAUJASAMEHE hivyo hata baada ya kutekeleza kisasi chako hautautua huo mzigo wa kinyongo kwasababu hakuna kisasi kinachokuwa kwenye mizani sawa na kinyongo, na hata yule unaemfanyia kisasi hautamfanya akuone wewe ni mwamba bali atatafuta njia ya kukufanyia kingine cha kukuumiza kwasababu asili ya binadamu imeumbwa kwa KUTOKUBALI kushindwa kwa jambo lolote lenye kuumiza.

Asili ya binadamu inamruhusu binadamu kukubali kushindwa kwa jambo la furaha hahaha hapa ndipo panapomchekesha mwalimu, binadamu anaweza kukubali kushindwa katika kufanya shughuli fulani ambayo ingemletea mafanikio ambayo yangemletea furaha, lakini hakuna binadamu anaekubali kushindwa kwenye jambo linalomuumiza kwa mfano mtu akipata ugonjwa atapambana na tiba zote hatokubali kushindwa mpaka dakika ya mwisho anapotokwa na roho, hivyo ndivyo asili yake (nature) ilivyo.

Hivyo hautafanya SULUHU kwa kisasi kwasababu ni kitu cha kuumiza hivyo mtenda hataishia kukubali kupokea kisasi chako bali atakuja tena kwa njia nyingine kama siyo leo basi kesho, kama siyo mwaka huu basi ni mwaka ujao na kama siyo yeye basi atakuja kufanya mwanae na kama siyo kwako basi hata kwa kizazi chako, na ndio sababu ya kauli hii kuja “Sio mara ya kwanza kwa yeye kunifanyia hivi mara ya kwanza alivyonifanyia nilimfanyia vile lakini bado hakomi sijui ananitafutia nini”.

Hivyo mwalimu anataka kukufundisha kitu cha tofauti cha kupambana na uhusika wa aina hiyo, ambao amesema unapambana kwa kutumia saikolojia (psychology). Unapambana na kitu kinachoonekana kwa njia isiyoonekana, Kwanini mwalimu anataka kukufundisha njia isiyoonekana kwasababu kila unachokiona kimefanyika kilianza kwanza kwa kutokuonekana, mtu kabla ya kukuibia aliwaza kwanza, mtu kabla ya kukuchongea kwa boss wako alikuwazia upande hasi kwanza, mfanyakazi wako alipofanya kosa fulani katika biashara kwa makusudi au laah bado aliwaza kwanza kwamba NGOJA nifanye hivi.

Hivyo tunaenda kupambana kwanza na mzizi wa tukio na sio matokeo ya tukio. Njia nyingi zilizozoeleka hazina ufumbuzi wa matatizo na ndio maana matukio yanajirudia katika jamii, nenda sambamba na mwalimu utajifunza mengi, siyo tu utofauti wa kufanya shughuli fulani ili ikuingizie kipato kizuri, bali pia utofauti wa kukabiliana na haya, unaweza ukafanya shughuli yoyote kwa utofauti na upekee mkubwa lakini usione mafanikio kwasababu ya kutoyajua haya.

Tutaanza kwa hatua kadhaa katika kutumia njia isiyoonekana.

Kwanza kabisa yanapotokea matukio hasi kabla ya kufanya chochote, kaa chini chukua dayari (diary) yako andika pembeni hilo tukio linakuletea funzo gani, umeibiwa na wanafamilia Nyumbani kwako kwasababu labda ni mgumu wa kutoa hela lakini unazo, labda kwasababu haujaweka usalama wa kutosha sehemu unapohifadhi vitu nyeti. Shamba lako mifugo imeingia na kula mazao labda sababu haujaweka mwangalizi wa shamba au labda haujazungushia wigo shamba lako na unajua sehemu uliyopo pana mchanganyiko wa wakulima na wafugaji kijana wako kafanya kazi chini ya kiwango labda ni kwasababu hautoi semina elekezi. Hivyo jambo lolote linapotokea ni funzo kwanza.

Baada ya hatua hiyo unaenda kufanya kitu cha kisaikolojia ambacho mtenda kitamsumbua sana na huku hamna kisasi patamu hapo, ni nini hicho nenda kale lunch kwanza upate nguvu ukirudi tuendelee.


N:B ilikuwa mwalimu ahitimishe muda huu lakini tofauti na vile alivyoyapimia mambo bado ataendelea na hii njia ya tatu, ina maelezo mengi hapo amegusia robo tu hivyo endelea kufwatilia nini kinachoendelea.
Unakumbushwa kutuma namba yako WhatsApp muda si mrefu masomo yataanza kutolewa huko bado haujachelewa.



<H.FARADAY>(0625934471).
 
Paulina ray ... hapa kuna mafunzo mazuri sana zaidi ya unavyohisi .. hili sio gazeti .. mi zaidi ya physics / chemistry / sijui biology na upuuzi mwingine wote usiokusaidia popote .... ni wapi uliwahi kutumia Pai kwenye maisha yako? lakini darasa hili litakusaidia wewe pamoja na vizazi vijavyo.
Afadhali umemuelimisha
Watu huwa tunapotea katika maisha kutokana na ukosefu wa taarifa na mafunzo kama haya

Hakika elimu hii imenifanya nitambue vitu vingi ambavyo hapo awali ckuwahi kuvitambua kabla

Ubarikiwe sana mwalimu bado ntaendelea kufuata mfulizo wa masomo haya kujua mengi zaidi

Your the best teacher

Vizy boy

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Afadhali umemuelimisha
Watu huwa tunapotea katika maisha kutokana na ukosefu wa taarifa na mafunzo kama haya

Hakika elimu hii imenifanya nitambue vitu vingi ambavyo hapo awali ckuwahi kuvitambua kabla

Ubarikiwe sana mwalimu bado ntaendelea kufuata mfulizo wa masomo haya kujua mengi zaidi

Your the best teacher

Vizy boy

Sent using Jamii Forums mobile app
Shukrani.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom