kahtaan
JF-Expert Member
- Jul 11, 2009
- 19,156
- 11,608
Kahtaan,
Salaam.
Nilichungulia hizi bayana zenu tangia majuzi,nami pia mumenipeleka mbali mno...Shukran nyingi zikufikeni juu yenu Maulamaa wangu!
Mimi binafsi nina hakika yakuwa sisi soote lazim itakua tunafahamiana uzuri tu,au itakua families zetu zajuana kitambo kingi!?...Wallahi,ni raha ilioje! Kwi! Kwi! Kwi!
Nakumbuka kitambo ilikua family yetu ikitembeleana mno na family ya Al Marhum Balozi Idd Mtingwa pale Mwanza. Yule Bwana alikua ni Sahib mkubwa mno wa Mzee Wangu.
Mara zoote tulipokua waduchu tukifikia kwake pale Mwanza,halikadhalika nao pia ilikua wakifikia nyumbani petu hapo D'salaam.
Kuna wakti nilikua nikizungumza na Shariff Ritz humu ,yeye ndo alonambia yakuwa kumbe yeye Balozi Mtingwa alikua ameoa kwa Al Marhum Sheikh Al-Amin pale Mwanza!?
Pia alinifahamisha yakuwa,yule Rukia Mtingwa ndo yupo pale Vodacom D'salaam. Mimi nilikua nikimkumbuka zaidi yule "Masele",dah! Yaani kitambo kingi sijakutana na hawa ndugu zetu maskini!
Lakini pia nakumbuka Shariff Abdallah Al Attas,pia kuna wakti alikwenda Mwanza na kumposea/kumuoza Alhaj Issa Mtambo. Najua Mzee Wangu alikuamo kwenye ule msafara wa Bwana harusi!
Nafikiri itakua basi wamfahamu yule Abass,aliekua akichezea Pazi Basketball Team,enzi ile pale Gymkhana Club!? Nafikiri huyu ni jamaa zao katika ile family ya Mwanza alokwenda kuoa Alhaj Issa Mtambo!?
Nakumbuka pale Mwanza pia palikua na family ya yule Al Marhum Jumbe Mkila,huyu Bwana nafikiri alikua na asili ya Bagamoyo!?
Lakini aliishi kitambi kingi pale Mwanza,wakti ule pia alikua ni mmojawapo ya Wafanyibiashara wazuri pale Mwanza khasa kwenye mambo ya stationeries. Baadae yule Nyerere na yule mpuuzi mwingine Moringe Sokoine walimtia ndani ati kwa yale makhanatha ya ule "uhujumu wa uchumi"!?
Maskini,kutokana na utu uzima wake na adhabu za kifungo kile cha kinafiki,alifariki nafikiri miaka michache baada ya kutoka kizuizini!
Dah! Yaani Nyerere kaadhibu mno Wazee Wetu,takriban katika kila pembe ya hiyo Tanganyika na katika awamu tafauti za utawala wake alituletea nakma/dhuluma za kiaina nyingine!
Mara ya mwisho binafsi kufika Mwanza ilikua kitambo kiduchu,nilifikia kwa family friend wetu/rafiki ya Mzee Wangu Mr Mwinjuma ndie aliekua GM wa ile MWATEX pale!
Pia nina hamu kubwa mno ya kurejea tena pale Tabora. Niliwahi kufika kitambo kingi mno.
Mara ya mwanzo ilikua kwenda kushuhudia wakti ule Mwenyekiti wa CCM Al Rais Bwana Ali Mwinyi,alipokwenda kuhutubia na kumpigia kampeni ndugu yetu Rostam Aziz,alipokua ndo anagombania ule ubunge wa Igunga kwa mara ya mwanzo!...lakini mie sina chama chochote cha kisiasa! Kwi! Kwi! Kwi!
Tabora pale pana personal memories nyingi mno za family yangu. Babu zangu woote wa pande zote mbili(kuumeni na kikeni),walisomea na kuhitimu pale Tabora tangia enzi ya Mjarumani.
Kuna wakti pia Mzee Wangu,alifuata foot steps naealisomea pale.
Napata khadith zilo njema mno za ndugu zetu/Wazee Wetu wa Tabora na Mwanza na kwingineko koote ndani ya Tanganyika kila mara nizungumzapo na Mzee Wangu. Hishma,mapenzi na tashrif nyingi mno alizopawa wakti mbali mbali wa shughuli zake kikazi na matembezi binafsi pia. Allah'amdulillahi...nafarijika mno nikiona/kusikia mshikamano mkubwa kama huu.
Mara ya mwisho kufika Tabora mimi binafsi,tulikwenda kumtembelea Lawrence Gama,wakti ule ndo alokua RC pale.
Huyu Mzee Gama,alikua ni mtu mstaarabu na mnyenyekevu mno. Nakumbuka ilikua ni Al Jumaa tupo pale Tabora.
Basi alitupeleka Masjid mimi na Mzee Wangu...na akatusubiria yeye na Driver wake mpaka Sala ilipokwishwa/ilipokamilika ndo tukarejea nae pamoja! Dah!
Yaani,kitambo palikua na watu waungwana mno...lakini amefariki maskini!
Nakumbuka siku ya pili yake bado tupo pale Tabora,akaja yule kichaa mwingine Augustine Mrema ati kukamata "mafisadi"!?
....hiyo story na vitimbi alivyofanza yule Mrema pale Tabora ni kichekesho na utacheka pita kiasi Akhiy! Kwi! Kwi!
Afrika bana... yaani mpaka leo nastaajabu mno,ilikuaje mpaka Rais Mwinyi kumpa kanjanja kama yule wadhifa/cheo cha Naibu-Waziri Mkuu!? Dah!
Yuwapi CHAMVIGA nae,nimpe khabar nilipopeleka "posa" yangu pale Soni!? kwi! Kwi! Kitambo enzi ya "ujahil" nalikua na mchumba kiduchu na kibarua chake alikua ni askari/Traffic pale Soni!? kwi! Kwi!
Hii story ni ndefu na ya kuchekesha mno Akhiy...mpaka siku tukikutana kwa furaha zetu Insha Allah.
Yaani pia napapenda mno poote pale Mazinde,Mombo,Lushoto,Soni,Kilindi,Vunjo na vijiji/maeneo mengi mno yazungukayo huko.
....miaka ya early 1950's,Babu yangu alifanza maskani/makao yake pale Mazinde na alikua na biashara kubwa mno,kilimo/ardhi kubwa/nzuri...na pia akijulikana na kuheshimikana koote takriban kwenye maeneo hayo.
Kila Vijiji alivyokua akipita nduguze/Wazee Wetu wa maeneo hayo walikua wakimtaka/wakimnasihi aongeze Mke kutoka kwao! Kwi! Kwi!
Lakini ilipofika ile nakma ya yule Nyerere,ule utumbo wa "Azimio la Arusha"-1967,"tulitaifishiwa"/tulidhulumiwa takriban nusu ya hiyo biashara/kilimo choote...wajua Babu yangu maskini haikuchukua muda mwingi alifariki maskini kwa joto la roho! Dah!
Khalaf,ati wanatokea brainwashed/mashangingi wa hoja humu JF,ati kutaka kunirubuni kwa hoja zao dhaifu ili nimpende yule khabith/maluuni Nyerere!? Thubutu thuma thubutu!!
Life is short...je nikuulize khabar za Mukaram,Sharjah,Seiyun au Sheibam mwenzetu!? kwi! kwi!
...nimefurahika Akhiy,hiyo offer ya kumuongeza Mke ndugu yetu Maulana Al Duktuur Kahtaan....lakini,naona keshajifanza kukwepa kiduchu,italazim tumfanzie hila zoote mpaka atimize wajibu huo wa kiungwana! Kwi! Kwi!
Wallahi,nimefurahika mno tumezungumza japo kiduchu.
Ahsantani sana.
al habeeb maulana gombesugu wallahi leo umenipeleka mbali mno! Yaani natamani leo hii nichikue likizo nije nikutembelee huko tukae tunywe kahwa huku tukikumbushana ya zamani!
akhiy umenitajia wazee wetu wote huko mwanza na tabora, ukoo wa mtigwa tulikuwa nao karibu mno! ajeeb
na yule mzee Lawrence Gama alikuwa yeye na kaka yangu kama ndugu pale Tabora,
Na wangine woote uliowataja HAKUNA MMOJA NISIE MJUA! subhannallah, amma kweli DUINI NDOGO HII!
Ama kuhusu kuongeza mke. teh teh teh teh teh ! alkhiy maulana life is Short amenipa ofa nzuri mno lkn kwa udhaifu wangu nimetafuta sababu alfu na moja kuikimbia. kwi kwi kwi kwi ! wallah madahifu tuko wengi mno!
manake jana namuonyesha wife huo ujumbe, anasema kama natafuta balaa basi nikaoe mke wa pili! namuuliza kwani wewe si mwislamu?? asema yeye hana neno lkn serikali ndio TATIZO! sasa minikamwambia 'kwani lazima WAJUE?' AKANIJIBU KUWA itabidi aifahamishe serikali kuwa nina wake wawili manake MUISLAMU HATAKIWI KUSEMA UONGO!!
teh teh teh teh, nikamwambia amma kweli wewe huna maana! yaani ktk ukweli umeona huo tu! nae kanijibu kuwa "NA WEWE KTK SUNNAH ZOTE UMEONA HIO YA KUONGEZA MKE TU? teh teh teh teh! amma ana bahati tuko kwa hawa wenye sharia za majahil tu lkn angelikuwa huko kwetu lzm mikwaju kidogo ingetembea hapa! kwi kwi kwi!
Akhiy l kareem nafurahi ndugu yangu leo kupita kiasi! umenikumbusha mbaali mno, Allah akupe furaha na we pia na ndugu zangu woote hapa jf na waislamu kila mahali.
iko siku panapo majaaliwa tutafanya reunion huko Tanzania Inshaa Allahu TAALAH
Ahsant
Last edited by a moderator: