Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Mradi wa Bil 200 kwa wakazi wasiozidi laki tano (5)...

Ni usanii wa hali ya juu.
Watanzania bana kwa hiyo kama wapo laki 5 hawatakiwi kuwa na daraja?

Ukifika dubai nadhani utashangaa sana wana nchi yao wapo milioni 2 lakini wana madaraja mengi kuzidi sisi tupo milioni 45.

Hilo daraja siyo kwa wakazi tu wa Kigamboni itasaidia kukuza uchumi wa hotel, viwanda, na ofisi za watu binafsi pamoja na serikali.
 
Watanzania bana kwa hiyo kama wapo laki 5 hawatakiwi kuwa na daraja?

Ukifika dubai nadhani utashangaa sana wana nchi yao wapo milioni 2 lakini wana madaraja mengi kuzidi sisi tupo milioni 45.

Hilo daraja siyo kwa wakazi tu wa Kigamboni itasaidia kukuza uchumi wa hotel, viwanda, na ofisi za watu binafsi pamoja na serikali.
Jumlisha hotel, migahawa, vioski na uchafu wote kigamboni hawazidi 1mil... Huo ni usanii tu... Unaenda kupita kurasini alafu unakutana name foleni ya masaa nane ya kuja Posta na maeneo mengine hiyo ni akili au matope?!
 
Lakini TanZania siyo nchi iliyoendelea usisahau hilo kwanza!

Mradi wa DART siyo mbaya ila tatizo ni kwamba tu haueleweki, watu wengi hawauelewi, lkn ni mradi mzuri sana na ungesaidia kwa kiasi kikubwa sana kupunguza adha ya usafiri, hata nchi zilizoendela pia zina miradi kama hii, miji mingi tu Duniani inatumia mradi kama Dart, kwa kifupi ni kwamba Dart ni kama vile kuweka trams sema kwa gharama nafuu trams ni ghali zaidi na mazingira ya nchi yetu bado hayaruhusu kuwa na trams na mfano ni mdogo tu Umeme, trams zote au nyingi zinatumia umeme sasa umeme wenyewe wa kukati kakatika unawezaje kuendesha treni kwa ufasaha? na isitoshe nchi yenye watu zaidi ya milioni 40 na inatumia MW 1500 tu huwezi kutumia huwo kuendesha treni za Umeme na haya yote waliyaafikiria wakati wanabuni huu mradi!

Lakini kwa ngazi ya maendeleo ya nchi yetu DART ni mradi mzuri sana na ungesaidia kwa kiasi kikubwa kama tungeuelewa vizuri!
Daraja la Kigamboni linatarajiwa kusaidia kutatua changamoto ya ongezeko kubwa la watu wasiokuwa na makazi bora, upungufu wa miundombinu, ukosefu wa ajira, kuongezeka kwa ujenzi holela, ukosefu wa nyumba bora za kuishi, msongamano wa magari na upungufu wa maeneo ya biashara na shughuli za uzalishaji mali.

Kihistoria kuwapo kwa mji wa Kigamboni ni wazo la miaka mingi tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Julius Nyerere, Ilikubalika kuwa Kigamboni iwe eneo la kitovu cha huduma katika mpango kabambe wa Jiji la Dar es Salaam wa mwaka 1979 na baadaye katika mpango mkakati wa mwaka 1992.

Eneo la Kigamboni lilichaguliwa kwa kuwa liko umbali mdogo kutoka eneo la kati (Ccentral Business District) la Jiji la Dar es Salaam, lina bahari na visiwa ambavyo ni vivutio vya uwekezaji na pia lina ardhi kubwa ya kutosha kupangwa upya kwa matumizi ya sasa na ya baadaye.

Sijui kama umeishwahi kufika Kigamboni naona unapinga tu ili muradi unapinga.
 
Yeye kaona dart ndo yenye manufaa zaidi kwa sbb anaishi maeneo uliko mradi
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!

Yaani sehemu zote ulizo bold ndio ulizoandika pumba..naona umedhamiria kutuonyesha ulivyp na akili nzito
 
Jumlisha hotel, migahawa, vioski na uchafu wote kigamboni hawazidi 1mil... Huo ni usanii tu... Unaenda kupita kurasini alafu unakutana name foleni ya masaa nane ya kuja Posta na maeneo mengine hiyo ni akili au matope?!
Wewe unatoka Moshi uwezi kujua Kigamboni ilivyo mkuu.

Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) na wawekezaji wakubwa kwa lengo la kuleta ufanisi zipo kampuni mbili zilizosaini mkataba wa maridhiano (MoU) moja ni Miworld kutoka Dubai inayowekeza katika ujenzi wa nyumba 5,000.Nyingine ni Kampuni ya China Hope, inayowekeza nyumba 15,900 na serikali itatoa ardhi na kupata angalau asilimia 15 ya dhamana ya thamani ya nyumba. Wananchi watafidiwa kwa bei za soko kwa mujibu wa sheria, hekari moja ya ardhi itafidiwa milioni 141 na zitakazomuwezesha mwananchi kulipia gharama ya nyumba mpya mbadala.Anayefidiwa atahimizwa kutumia angalau asilimia 10 ya fidia yake kununua hisa zitakazouzwa katika soko la hisa la Kigamboni Development Agency Trust na kutokana na utaratibu huo mwenye ardhi atabaki katika ardhi hiyo kupitia hisa.

Wanakigamboni kama walivyo Watanzania wengi ni waelewa na wanatambua mtu anapopinga tu kukwamisha juhudi za kuleta maendeleo kwa maslahi yake binafsi na chuki kama zako, Kusema kweli hiyo ni tabia mbaya ambayo tunatakiwa kuikemea kama taifa. Mtu unamkuta anapinga kwa kuwa hakupata kitu fulani au anafikiri mtu mwingine atapata sifa akikamilisha kazi au mradi mkubwa kama huu wa daraja.
 
Kwani kigamboni sio Dar??
Dar inawakazi laki tano tu?!
Teh teh teh!!

Hilo daraja inaonekana kabla ya kupanda unaulizwa wewe mkazi wa Kigamboni au maaneo mengine kama siyo mkazi wa Kigamboni unashushwa.
 
Na labda kibaya zaidi pia NSSF ambao ndiyo wametoa hizo fedha wako hoi kifedha na hata kulipa Mishahara ya Wafanyakazi inasumbua, ni nani aliweza kufikiria kwamba NSSF watakuja kupata shida kulipa Mishahara? Lkn ndiyo hivyo na wanaonitukana hapa wanategemea siku wakistaafu waende NSSF kuchukuwa malipo yao wakati hakuna hata shilingi sasa sijui watakula hilo daraja ngoja, tusubiri!
Siyo kweli kuwa NSSF wapo hoi kifedha hizi ni porojo za kwenye vijiwe vya mapuya tu NSSF watu wanachukuwa mishahara yao tarehe 25.

Teh teh teh!
 
Tulishaandika sana sana huku kuhusu miradi ISIYO NA TIJA NA HASARA YA MILELE KTK TAIFA HILI...

1: IPTL..

2: Mradi wa Mabasi ya Dar.. DART..

3: Bandari ya Bagamoyo

4: Mradi wa mji mwema wa Kigamboni

5: Vitambulisho vya TAIFA..

6: DARAJA LA KUUNGANISHA COCO NA SARENDAR la juu baharini...

7: Mradi wa UJENZI WA GAS YA KINYEREZI PHASE 3... eti 60% Kampuni ya Kichina ndio imepewa...? How on Earth..? While phase 3 ndio kubwa it has 850 MW... ila JK Mungu atakuadhibu tu... Hizi fedha za Mradi wa Kinyerezi serikali ilizikopa zote toka China... iweje kuna 60% YA MCHINA NDANI KTK PHASE 3... AMBAYO NDIO KUBWA KABISA... Serikali ya Magufuli itupie macho haraka hapa... ni Uwizi wa mstaafu wake... just like Bangamoyo port.. ni HASARA YA MILELE KWA TAIFA HILI..


ila mradi wa Daraja la Kigamboni UNA FAIDI KWA TAIFA... sioni hasara yake... all calculus are clear, and very beneficial... watu wataenda Kigamboni kwa mabasi na gari private kwa haraka sana...
 
Hii habari hapa chini ya Bavicha wewe unaileta JF serikali imeishakanusha hizi porojo.

"namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo"
 
Daraja la kigamboni lina umuhimu sana kwa wakazi wa dsm sio kigamboni tu

Kwanza litarahisisha usafiri na pia kusaidia kukua kwa mji wa kigamboni ambao unakua kwa kasi sana

Uchache wa watu sio kugezo cha kuchagugua gharama za uwekezaji. Mawazo kama hayo ndo yaliyotuletea msongamano kwrnye miji yetu hasa dam.

Barabara zetu zilijengwa as if watu hawaongezeki sasa zimekua hazitoshi hata kidogo. Tujenge miundombinu sahihi kwa gharama uoyote ili tusije kucompromize future generation

Marekani hawajajenga barabara wala metro mwaka jana au juzi wana miundombinu ya mwaka 1850, dubai wana watu hawazidi 4m ila ubora na kutosheleza kwa miundombinu yao kila ntu shahidi

Serikali na taasisi washirika wajenge tu
 
Mimi siyo Great thinker na wala sijawahi na sitowahi kujitambulisha hivyo ila kama wewe unaona unastahili kuitwa hivyo hiyo ni juu yako!

Haya niambie hili daraja litapunguza msongamano wa kiasi gani kwenye huu Mji? Ni asilimia ngapi ya wakazi wa Dar watalitumia kila siku kwenda na kurudi kazini ikilinganishwa na gharama iliyotumiwa kulijenga?

We've failed to priotize our contemporary needs.
 
Ethiopia metro train imegharim usd475mil kujenga 34km
Kigambpni bridge usd136mil kujenga 0.678km hii pesa kama ingejenga hiyo metro train kwa Dar ingeje km kama 10km yani kutoka posta/k.koo mpaka ubungo au sehemu nyingine lkn kwa urefu huo wa 10km. Hakika manufaa ya kua na hiyo metro hapa dar ingekua kubwa kulik daraja la kigamboni, kweli tunahitaji sana hilo daraja lkn tukipima kisawa sawa halikua kipaumbele kwa nchi ambayo inavitu vingi na Muhimu sana vinavyptakiwa kufanywa.
Mi nadhan tukubali tu tuna viongoz ambao sio creative na hawawez ku-prioritize issues.
 
writings with empty contents.

andika vitu kisomi kama hujui ukafanye tour uelezewe cost benefit analysis ya huo mradi ndio uje hapa
 
F
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Fikiria miaka 50 mbele
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Wewe ni mwana chama wa ccm,ulishindwa nini kwenda kutoa mawazo yako haya ambayo kimsingi ni mazuri kabla ya huo mradi kuanza kutekelezwa?
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Naona unapingana na lumumba mwenzio mkulima wa kiteto
Cc mkulima wa kiteto
 
Back
Top Bottom