Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Daraja la Kigamboni ni White Elephant Project, Hatulihitaji!

Unazungumzia DART nyingine. Lakini Kumbuka kuwa itawasaidia wakazi wa huko. DART ya Kigamboni ndiyo hilo daraja.
Kila sehemu ina mahitaji yake tofauti na sehemu nyingine. Kigamboni wakaa binadamu pia. Ni mawazo yangu tu lakini si mkazi wa Kigamboni!
Mkuu hatahivyo mawazo yako yanaweza kua sehemu ya utekelezaji wa kauli mbiu ya "pigeni mbizi"
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Mkuu mwarobaini wa haya yote ni flying over, tutaruka sarakasi zote huku tukiwa kwenye vazi la kanzu na msuli pasipo kufanikiwa. Huko kenya mpaka leo bado wanazidi kuongeza flying over huku sisi huku sisi tiking'aa sharubu na upanuzi wa barabara wakati junction ni ileile moja ya mnara wa askari..!!
 
Mabilioni yaliyowekezwa kwenye Ujenzi wa hili Daraja ni kama yamepotea bure kwa maana halihitajiki, halina umuhimu mkubwa kiasi hicho kwa maana ya kwamba halitasaidia kuboresha maisha ya wakazi wa Dar kwa walio wengi ukilinganisha na gharama ya Ujenzi wake hii ni prestige project ambayo kwa nchi masikini na yenye kila aina ya shida inayojulikana na binadamu hapa Duniani hatukupaswa kulijenga badala yake hizi fedha zingewekezwa kwenye miradi mikubwa kama DART kwa mfano hii fedha ingetosha kujenga DART nyingine kutoka Mwenge mpaka Kivukoni hivyo kuwa na DART mbili ambazo zingesadia sana wakazi wa Dar, kuliko hili Daraja!

Itatuchukuwa muda sana sisi Watanzania kuja kuendelea, mpaka tuje tuweke vipaumbele vyetu sawa tuna safari ndefu sana, mradi mwingine ambao nasikia uko mbioni na namwomba Rais Magufuli auzuie huu mradi kama ule wa bandari ya Bagamoyo ni wa kujenga daraja baharini ktk daraja la Salenda kuunganisa na Coco Beach, hili daraja hatulihitaji badala yake hizi fedha ziende kujenga DART nyingine labda ya Br. ya Mandela- Buguruni -Kariakoo!
Hoja hii ni ngumu kupata mashiko kwani ni yakufikrika zaidi. Haina chembe za takwimu kuipa mwelekeo wa kutatua tatizo la usafiri kijiji Dar. Kujenga DART Mwenge-kivukoni ni kuongeza msongamano kwenye Kivuko cha Magogoni ambako abiria wote huduma kwenda Kigamboni. Kuwa na daraja la Kigamhoni itakunguza msongamano kwenye Kigula. Ujenzi wa daraja la Salender-Coco Beach ni kupunguza msongamano kwenye daraja la Salender ambalo ndio kiungo kikuu kwa watu kutoka kaskazini ya jiji kuingia City Centre ambako shughuli nyingi za kiserikali na kibiashara hufanyika. Kwa hiyo miradi hii miwili ni muhimu kuboresha usafiri na kupunguza muda unaopotea barabarani. Matokeo chanya ni kuboresha shughuli za kijamii na kiuchumi katika jiji la Dar es Salaam. Kwa hiyo ujenzi wa DART: Mandela-Buguruni-Kariakoo na Mwenge-Kivukoni ufanyike bila kuadhiri miradi ya yale madaraja mawili. Bahati Darajani la Kigamboni litafunguliwa mwezi Machi 2016.
 
Kupinga Daraja la Kigamboni kunatokana na mtu kutofahamu tabu na adha ya foleni wakati wa kusubiri kivuko, muda unaotumika ni mrefu na hiyo huwa kwa mtu anaetoka mjini kwenda Kigamboni na vice versa. Kigamboni kuna mahoteli, airstrips na recreation sites ambazo zinavutia wageni na wenyeji lakini ambao wanakatishwa tamaa kuzifikia kutokana na usumbufu wakati wa kuvuka.
Wakazi wengi wa Dar es salaam wanamiliki maeneo wanayoshindwa kuyaendeleza kutokana na ugumu wa kuyafikia na wengine wanashindwa kuanzisha makazi katika maeneo wanayomiliki kwa kuwa shughuli zao ziko center na kufika huko kwa wakati kunakwamishwa na foleni ya kupanda kivuko.
Kigamboni ni wilaya mpya ambayo inatarajiwa kuwa jiji jipya la kisasa, shughuli zote za kuliendeleza na kulikuza jiji na kufikia viwango vinavyotarajiwa, itahitaji mfumo mwanana wa usafirishaji wa vifaa na watu watakaoshiriki katika mchakato mzima wa kulijenga jiji hilo na daraja ni suluhisho muafaka wa kuyafanya yote hayo yawe rahisi.
Ukiachana na mradi wa mji mpya, tayari Kigamboni kuna miradi mingi mikubwa ya makazi mapya ya kisasa ambayo yanatarajiwa kuaccommodate maelfu ya wazalendo na wageni. Mifano mizuri ni: Dege eco Village, Avic Town, Mradi wa Nssf Mwongozo, Mradi wa Nssf Kibada, Mradi wa Nssf Tuangoma na midogo ya makazi Mwasonga ambayo iko katika maeneo matatu katika kijiji hicho.
Hivi kweli bado Daraja lisiwe na maana? Inaingia akilini kweli? Tafiti kabla ya kuzungumza.
 
Haujanielewa sijasema kwamba daraja siyo muhimu kwa wakazi wa Kigamboni La Hasha! Bali nimesema siyo muhimu kwa Mji wa DSM kwa ujumla wake kwa maana watumiaji wa hilo daraja hawafiki hata asilimi 10% ya wakazi wote wa DSM na hawo ambao unasema wanatumia Pantoni hata baada ya kukamilika kwa hili daraja bado asilimia 90 % yao watakuwa bado wanatumia hizo pantoni na msongamano utakuwa pale pale na ndiyo maana nasema kama lengo lilikuwa ni kuboresha usafiri jijini DSM ili kuchangia uchumi wetu basi tumepoteza fedha tu kwani kuna maeneo mengi ambayo hizi fedha zingeweza kupelekwa na kutoa mchango mkubwa zaidi, kama vile mradi mpya wa DART!
Hujui ulisemalo hata kidogo, hujui shida waliyonayo watu wnaoishi huko, hujui makazi yalivyoendelezwa na yanavyoendelezwa huko. hufahamu miradi ya nssf, nhc za makazi na idadi ya watu walioko huko na wanaotarajiwa kuishi huko. Nenda kafanye utafiti halafu uje hapa useme kama msimamo wako ni ule ule au umebadilika
 
Dawa ni kujenga railways Toka kibaha hata ikiishia ubungo then ubungo waweke monorail za juu, waige mfano malaysia tu
 
Kupinga Daraja la Kigamboni kunatokana na mtu kutofahamu tabu na adha ya foleni wakati wa kusubiri kivuko, muda unaotumika ni mrefu na hiyo huwa kwa mtu anaetoka mjini kwenda Kigamboni na vice versa. Kigamboni kuna mahoteli, airstrips na recreation sites ambazo zinavutia wageni na wenyeji lakini ambao wanakatishwa tamaa kuzifikia kutokana na usumbufu wakati wa kuvuka.
Wakazi wengi wa Dar es salaam wanamiliki maeneo wanayoshindwa kuyaendeleza kutokana na ugumu wa kuyafikia na wengine wanashindwa kuanzisha makazi katika maeneo wanayomiliki kwa kuwa shughuli zao ziko center na kufika huko kwa wakati kunakwamishwa na foleni ya kupanda kivuko.
Kigamboni ni wilaya mpya ambayo inatarajiwa kuwa jiji jipya la kisasa, shughuli zote za kuliendeleza na kulikuza jiji na kufikia viwango vinavyotarajiwa, itahitaji mfumo mwanana wa usafirishaji wa vifaa na watu watakaoshiriki katika mchakato mzima wa kulijenga jiji hilo na daraja ni suluhisho muafaka wa kuyafanya yote hayo yawe rahisi.
Ukiachana na mradi wa mji mpya, tayari Kigamboni kuna miradi mingi mikubwa ya makazi mapya ya kisasa ambayo yanatarajiwa kuaccommodate maelfu ya wazalendo na wageni. Mifano mizuri ni: Dege eco Village, Avic Town, Mradi wa Nssf Mwongozo, Mradi wa Nssf Kibada, Mradi wa Nssf Tuangoma na midogo ya makazi Mwasonga ambayo iko katika maeneo matatu katika kijiji hicho.
Hivi kweli bado Daraja lisiwe na maana? Inaingia akilini kweli? Tafiti kabla ya kuzungumza.

Kwa kuongezea tu kigamboni hata makazi yake asilimia kubwa yamepimwa na manispaa enzi hizo temeke, maeneo kama kibada, gezaulole, mwongozo, mikwambe, toangoma etc yote yamepimwa na watu wanaajenga majumba ya kisasa kwenye sehemu zenye miundombinu ya kisasa. huko kimara sijui gondolamboto kupo ovyo ovyo alafu anataka kuendelezwe....hatari sana
 
Daraja la Kigamboni linatarajiwa kusaidia kutatua changamoto ya ongezeko kubwa la watu wasiokuwa na makazi bora, upungufu wa miundombinu, ukosefu wa ajira, kuongezeka kwa ujenzi holela, ukosefu wa nyumba bora za kuishi, msongamano wa magari na upungufu wa maeneo ya biashara na shughuli za uzalishaji mali.

Kihistoria kuwapo kwa mji wa Kigamboni ni wazo la miaka mingi tangu Serikali ya Awamu ya Kwanza chini ya Mwalimu Julius Nyerere, Ilikubalika kuwa Kigamboni iwe eneo la kitovu cha huduma katika mpango kabambe wa Jiji la Dar es Salaam wa mwaka 1979 na baadaye katika mpango mkakati wa mwaka 1992.

Eneo la Kigamboni lilichaguliwa kwa kuwa liko umbali mdogo kutoka eneo la kati (Ccentral Business District) la Jiji la Dar es Salaam, lina bahari na visiwa ambavyo ni vivutio vya uwekezaji na pia lina ardhi kubwa ya kutosha kupangwa upya kwa matumizi ya sasa na ya baadaye.

Sijui kama umeishwahi kufika Kigamboni naona unapinga tu ili muradi unapinga.

Huyu amekurupuka, tumuelimishe
 
Kwa daraja la Kigamboni nitoe pongeze kwa NSSF kwa kuona mbali. Hizo ndo project ambazo tunazihitaji katika nchi yetu. Hii ni long term project.
 
Oh My God! Siwezi hata kufikiri kwamba kuna kiumbe anaye weza kuja na hoja kama hii. It's a total embassment. I thought hii forum ni ya Great Thinkers. What a waste of time!
Think about congestion ya traffic in the inner city. Think about mafuta yanayo potea bure kwenye hizo foleni, think about kuboresha sehemu zingine za jiji, think about maendeleo ya satellite cities, etc. Halafu eti unasemaje???



Mimi siyo Great thinker na wala sijawahi na sitowahi kujitambulisha hivyo ila kama wewe unaona unastahili kuitwa hivyo hiyo ni juu yako!

Haya niambie hili daraja litapunguza msongamano wa kiasi gani kwenye huu Mji? Ni asilimia ngapi ya wakazi wa Dar watalitumia kila siku kwenda na kurudi kazini ikilinganishwa na gharama iliyotumiwa kulijenga?
[/QUOTE]

rafiki,
kwanza hili daraja linajengwa kwa hela za NSSF kwa asilimia kubwa na kias Serikali
pili kigamboni ina serve watu wa Kigamboni, Gazaulole,Kimbiji,Mwasonga,Kibada,Tua ngoma,Kongowe mpk Mkuranga
Tatu. Kigamboni ni Wilaya Kamili
nne. Hili daraja litahudumia zaid ya watu 100k kwa siku
tano: usilinganishe gharama as lumpsum na marejesho yakifanyika kidogo kidogo
 
Back
Top Bottom