Dar: Upelelezi kesi ya Watumishi 16 waliopiga Tsh. Bilioni 8.9 za Halmashauri ya Jiji Wakamilika

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,120
Upande wa mashtaka katika kesi inayowakabili watumishi 16 wakiwemo wahasibu wa Jiji la Dar es Salaam umedai upelelezi umekamilika wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 143 likiwemo la kuisababishia hasara jiji hilo zaidi ya Sh8.9 bilioni.

Wakili Serikali, Pendo Temu alidai mbele ya Hakimu Mkazi kisutu Pamela Mazengo wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika hivyo wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma mahakama kuu hivyo ameiomba mahakama hiyo ipange tarehe ya kutajwa.

"Upelelezi umekamilika wapo kwenye mchakato wa kuandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu," amedai Temu.

Washtakiwa hao ni Tulusubya Kamalamo, James Bangi ambao ni wahazini, Mohamed Khars, Abdallah Mlwale na Deogratias Lutatuza na Alinanuswe Mwakasumbe ni wahasibu pamoja na Judica Ngowo ambaye ni karani wa fedha.

Wengine ni Febronia Nagwa, Glory Eugen, Said Bakari, Josephine Sandewa, Dorica Gwihala, Jesca Lugonzibwa, Patrick Chibwana ambao ni wahasibu, Patrick Chubwana Ofisa Afya , Ally Baruan meneja na Khalid Nyakamande Afisa mtendaji wa mtaa.

Katika kesi ya msingi inadaiwa kuwa Julai Mosi, 2019 na Juni 30, 2021 jijini Dar es Salaam washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha na kujipatia kiasi cha Sh8.9 bilioni mali ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 11, 2023 kwa ajili ya kutajwa.

MWANANCHI
 
Sawa tumeona wanakamatwa dagaa tu wale Samaki wakubwa wakubwa hawashikwi popote

Mfano kuna yule mmoja alijitangaza kabisa kua yeye alikua anaiba Madini ya dhahabu alijitangaza hadharani kabisa sijawahi kusikia akiguswa
Hapo hakuna wakubwa wala wadogo
 
Upande wa mashtaka katika kesi inayowakabili watumishi 16 wakiwemo wahasibu wa Jiji la Dar es Salaam umedai upelelezi umekamilika wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 143 likiwemo la kuisababishia hasara jiji hilo zaidi ya Sh8.9 bilioni.

Wakili Serikali, Pendo Temu alidai mbele ya Hakimu Mkazi kisutu Pamela Mazengo wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika hivyo wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma mahakama kuu hivyo ameiomba mahakama hiyo ipange tarehe ya kutajwa.

"Upelelezi umekamilika wapo kwenye mchakato wa kuandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu," amedai Temu.

Washtakiwa hao ni Tulusubya Kamalamo, James Bangi ambao ni wahazini, Mohamed Khars, Abdallah Mlwale na Deogratias Lutatuza na Alinanuswe Mwakasumbe ni wahasibu pamoja na Judica Ngowo ambaye ni karani wa fedha.

Wengine ni Febronia Nagwa, Glory Eugen, Said Bakari, Josephine Sandewa, Dorica Gwihala, Jesca Lugonzibwa, Patrick Chibwana ambao ni wahasibu, Patrick Chubwana Ofisa Afya , Ally Baruan meneja na Khalid Nyakamande Afisa mtendaji wa mtaa.

Katika kesi ya msingi inadaiwa kuwa Julai Mosi, 2019 na Juni 30, 2021 jijini Dar es Salaam washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha na kujipatia kiasi cha Sh8.9 bilioni mali ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 11, 2023 kwa ajili ya kutajwa.

MWANANCHI
Kila msimu hakukosekaniki bangusilo
 
Upande wa mashtaka katika kesi inayowakabili watumishi 16 wakiwemo wahasibu wa Jiji la Dar es Salaam umedai upelelezi umekamilika wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 143 likiwemo la kuisababishia hasara jiji hilo zaidi ya Sh8.9 bilioni.

Wakili Serikali, Pendo Temu alidai mbele ya Hakimu Mkazi kisutu Pamela Mazengo wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika hivyo wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma mahakama kuu hivyo ameiomba mahakama hiyo ipange tarehe ya kutajwa.

"Upelelezi umekamilika wapo kwenye mchakato wa kuandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu," amedai Temu.

Washtakiwa hao ni Tulusubya Kamalamo, James Bangi ambao ni wahazini, Mohamed Khars, Abdallah Mlwale na Deogratias Lutatuza na Alinanuswe Mwakasumbe ni wahasibu pamoja na Judica Ngowo ambaye ni karani wa fedha.

Wengine ni Febronia Nagwa, Glory Eugen, Said Bakari, Josephine Sandewa, Dorica Gwihala, Jesca Lugonzibwa, Patrick Chibwana ambao ni wahasibu, Patrick Chubwana Ofisa Afya , Ally Baruan meneja na Khalid Nyakamande Afisa mtendaji wa mtaa.

Katika kesi ya msingi inadaiwa kuwa Julai Mosi, 2019 na Juni 30, 2021 jijini Dar es Salaam washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha na kujipatia kiasi cha Sh8.9 bilioni mali ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 11, 2023 kwa ajili ya kutajwa.

MWANANCHI
Tulikubaliana kwamba Chini ya Jiwe hakuna wizi Sasa hiyo 2019 nani alikuwa madarakani?
 
Siwalaumu, namimi yawezakua ningekua kwenye position hiyo ningezikung'uta vizuri tu
 
Bilioni8. 9+? Ni pesa ya mboga tu,
Poleni sana kwa kukamatwa, najua mlikuwa kwenye mchakato wa kujitoa kwenye "generational poverty curse" Japo muache ka ukwasi, kwa watoto,
Serikalini majizi yapo mengi Yale yanayopiga 100s of billions. Wale walioiba za escrow na kuzibeba kwenye viroba, hawatakamatwa kamwe mpaka yesu arudi.
 
Takukuru ndio levo yake watumishi wa halmashauri,poleni wadau hapo nao wanataka rushwa wapeni kesi iishe.
 
Pesa ya halmshauri ni pesa ya umma na hao watu ni sehemu ya umma, ndo shida inapoanzia hapo kujua hawa watu wamekula pesa ya nani hasa? ni muhimu kuweka mechanism za kuifanya pesa ya umma ifanye kazi kwa manufaa ya umma wa watu wengi na siyo wachache.
 
Upande wa mashtaka katika kesi inayowakabili watumishi 16 wakiwemo wahasibu wa Jiji la Dar es Salaam umedai upelelezi umekamilika wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu.

Washtakiwa hao wanakabiliwa na mashtaka 143 likiwemo la kuisababishia hasara jiji hilo zaidi ya Sh8.9 bilioni.

Wakili Serikali, Pendo Temu alidai mbele ya Hakimu Mkazi kisutu Pamela Mazengo wakati kesi hiyo ilipokuja kwa ajili ya kutajwa alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika hivyo wanaandaa taarifa kwa ajili ya kuituma mahakama kuu hivyo ameiomba mahakama hiyo ipange tarehe ya kutajwa.

"Upelelezi umekamilika wapo kwenye mchakato wa kuandaa taarifa kwa ajili ya kuituma Mahakama Kuu," amedai Temu.

Washtakiwa hao ni Tulusubya Kamalamo, James Bangi ambao ni wahazini, Mohamed Khars, Abdallah Mlwale na Deogratias Lutatuza na Alinanuswe Mwakasumbe ni wahasibu pamoja na Judica Ngowo ambaye ni karani wa fedha.

Wengine ni Febronia Nagwa, Glory Eugen, Said Bakari, Josephine Sandewa, Dorica Gwihala, Jesca Lugonzibwa, Patrick Chibwana ambao ni wahasibu, Patrick Chubwana Ofisa Afya , Ally Baruan meneja na Khalid Nyakamande Afisa mtendaji wa mtaa.

Katika kesi ya msingi inadaiwa kuwa Julai Mosi, 2019 na Juni 30, 2021 jijini Dar es Salaam washtakiwa wanakabiliwa na mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu, utakatishaji wa fedha na kujipatia kiasi cha Sh8.9 bilioni mali ya Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Septemba 11, 2023 kwa ajili ya kutajwa.

MWANANCHI
Panya wapo stoo!!!,,,,,naomba sumu!!!
 
Back
Top Bottom