Dar es Salaam: Sita wadakwa kwa kutozingatia bei elekezi ya sukari

Suley2019

JF-Expert Member
Oct 7, 2019
1,815
4,565

Bodi ya Sukari kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limewanasa watu sita ambao ni Wafanyabiashara kwa kushindwa kuzingatia Bei Elekezi ya Sukari kama ilivyotangazwa na Serikali.

Watuhumiwa hao Sita wamekamatwa kufuatia Msako mkali iliyofanyika Jijini Dar es Salaam kwenye maeneo tofauti kwa lengo la Kubaini Wafanyabiashara wanaouza Sukari kinyume na Bei iliyopendekezwa.

Bahati Hakimu ni Meneja wa Ufuatiliaji, Ukaguzi na Uthibitishaji kutoka Bodi ya Sukari ambapo amesema Oparesheni za kuwafichua Wafanyabiashara Wadanganyifu itaendelea kufanyika kwenye maeneo yote ya Mkoa wa Dar es Salaam.

"Tutaendelea kufanya msako mkali tukishirikiana na Jeshi la Polisi ili kuhakikisha kuwa Bidhaa hiyo muhimu 'Sukari' inawafikia wananchi kwa Bei Pendekezwa, kwa Sababu Serikali imeruhusi Sukari kuingia nchini na imeondoa kodi na kurahisisha uingiaji wake hapa nchini ili watanzania wanufaike" amesema Bahati.

Pia soma:
- Serikali yatangaza Amri ya Bei Elekezi za Sukari Tanzania Bara
 
Kinacho takiwa hatua kali zichukuliwe ili iwe fundisho kwa wengine, vinginevyo viongozi wenye dhamana waachie ngazi kwa kushindwa kusimamia vyema suala hili.
 
Hapo wanaona wamefanya kazi kubwa!!! Wakati sukari bado bei iko juu. Unawezaje kumdhibiti muuzaji wa rejareja ilhali msambazaji anajuamulia bei?

Ninunue sukari kilo moja tsh 3500 halafu unipangie kuuza 2500. Una akili?
Umesikiliza na kuelewa vizuri maelezo ya huyo meneja kutoka bodi ya sukari? Ukielewa alichoeleza pengine utalazimika kufuta hii comment yako.
 
Hapo wanaona wamefanya kazi kubwa!!! Wakati sukari bado bei iko juu. Unawezaje kumdhibiti muuzaji wa rejareja ilhali msambazaji anajuamulia bei?

Ninunue sukari kilo moja tsh 3500 halafu unipangie kuuza 2500. Una akili?
Unaacha hiyo biashara, kama hutaki ukikamatwa, ni kosa la jinai! It does not matter umenunua bei gani! Take note of that!
 
Huu ni ujinga mkubwa!! Pia imezalisha kundi kubwa la wala Rushwa wanaotishia wafanyabiashara na kudai Rushwa!! Pia imesababisha watu kuficha bidhaa husika!! Tangu lini nchi imekuwa na Baraza la kupanga bei kama sio uonevu Kwa wafanyabiashara!? Mbona chumvi, mafuta, unga, Michele, ngano, mkate, asali, na vinginevyo vingi hakuna bei elekezi!? Why sukari Kwa Sasa!?
 
Back
Top Bottom