Miss Halima
JF-Expert Member
- Aug 4, 2026
- 302
- 646
Takribani watu 30 wamefariki dunia na wengine 22 kujeruhiwa baada ya mlima wa taka kuporomoka na kuangukia nyumba zilizokuwa karibu katika mji mkuu wa Guinea, Conakry, kufuatia mvua kubwa kunyesha.
Tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku katika eneo la Dar es Salaam jijini Conakry. Serikali ya Guinea imesema dampo hilo liliporomoka ghafla baada ya mvua kubwa, huku ikihofiwa kuwa watu kadhaa wamekwama chini ya vifusi.
Serikali imetuma idadi kubwa ya vikosi vya usalama, ikiwemo jeshi, kushiriki katika shughuli za uokoaji.
Akizungumza na vyombo vya habari vya ndani, mwanamke mmoja amesema watoto wake watano wamefariki katika tukio hilo.
Mamlaka zinaendelea na shughuli za uokoaji, huku zikihofia kuwa watu zaidi huenda wamefunikwa na vifusi na hivyo idadi ya vifo ikaongezeka.
Waziri Mkuu wa Guinea, Amadou Ouari Ba, ametembelea eneo la tukio na kutathmini hali ilivyo.
Awali, kiongozi wa eneo hilo, Lansine Sila, aliliambia shirika la habari la AFP kuwa kulikuwa na hofu ya idadi kubwa ya waathiriwa. Amesema hadi wakati huo miili 18 ilikuwa imepatikana na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.
Tukio hilo limetokea majira ya saa nane usiku katika eneo la Dar es Salaam jijini Conakry. Serikali ya Guinea imesema dampo hilo liliporomoka ghafla baada ya mvua kubwa, huku ikihofiwa kuwa watu kadhaa wamekwama chini ya vifusi.
Serikali imetuma idadi kubwa ya vikosi vya usalama, ikiwemo jeshi, kushiriki katika shughuli za uokoaji.
Akizungumza na vyombo vya habari vya ndani, mwanamke mmoja amesema watoto wake watano wamefariki katika tukio hilo.
Mamlaka zinaendelea na shughuli za uokoaji, huku zikihofia kuwa watu zaidi huenda wamefunikwa na vifusi na hivyo idadi ya vifo ikaongezeka.
Waziri Mkuu wa Guinea, Amadou Ouari Ba, ametembelea eneo la tukio na kutathmini hali ilivyo.
Awali, kiongozi wa eneo hilo, Lansine Sila, aliliambia shirika la habari la AFP kuwa kulikuwa na hofu ya idadi kubwa ya waathiriwa. Amesema hadi wakati huo miili 18 ilikuwa imepatikana na kupelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti.