Dalali akichukua pesa zaidi yako utakubali

Dalali akichukua pesa zaidi yako utakubali

mkuu dalali hawezi kukosa, mana akiondoka na mteja wake hakosi pengine pakumpeleka, utakaekosa ni wewe tu

Hivi inakuwaje mfano kama hivyo, mteja amependa nyumba, then anakuja mwenyewe peke yake ananunua. Dalali anagundua kuwa kumbe ulimuuzia yule mteja?
 
Hivi inakuwaje mfano kama hivyo, mteja amependa nyumba, then anakuja mwenyewe peke yake ananunua. Dalali anagundua kuwa kumbe ulimuuzia yule mteja?

hizo zinatokea ila ni very rear case, kiuhalisia mtaja imani yake ipo kwa dalali na ndio huwa mshauri wake mkuu kwenye hayo masuala. dalali akiamua kuipaka matope nyumba yako huwezi muona tena huyo mteja.
 
Kuna jamaa mmoja mtwara alimpa dalali kazi ya kumtafutia mteja wa eneo kwa bei ya milion 80 jambo la kushangaza mteja wa milion 120 akapatikana mwenye eneo akagoma kuuza
IKIKITOKEA KAMA HIVI WAKUUU FANYEN KAMA KAKA YANGU ALICHOFANYA ALIUZA KIWANJA MIL 140 MAKUBALIANO YALIKUWA MIL 90M....MNS DALALI KAMA MMEKUBAKIANA 10PERC ANA MIL 10 YAKE IKATOLEWA PEMBEN..

BAKI 40M
PASUPASU TENA WALIGAINA NYUMBAN NA MWANASHERIA ALETWA WALE WA KULA HELA ZA USHAHIDI ATUKUWA MBALI NAO
 
Mfano wewe unauza nyumba yako kwa milioni 10 umezunguka kutafta wateja mwaka mzima umekosa

Ukaamua kutafta dalali ukampa Kazi ya kuuza

Jioni ya siku hiyo anakuja na mteja na anainunua hiyo nyumba kwa milioni 100 dalali anatoa milioni 10 yako anakupa Kisha yeye anabaki na milioni 90

Je utakubali?
Tukae tuongee upya hataki akajenge nyumba yake auze kwa bei atayotaka..
 
Dalali anapaswa kuwa na ubinadamu. Ntakubali 65:35 au 60:40 si chini ya hapo, sasa kama atakubali kukosa 40m ili mm nibaki na nyumba na nikose 10m sawa.
Ilitokea hii kitaa...nyumba ni 20m inauzwa dalali kaleta mteja wa 50m
Mwenye nyumba akagoma kuuza nyumba yake ,ikawa bonge mija la utata,akamuambia tafuta yako ya kwnagu siuzi hyo bei au ukitaka kula 10m ,40m ya kwangu akagoma dalali
Baadae yule mteja akaja kunnua kwa 34 mbila dalali ile nyumba.
 
nature ya waswahili tuna roho mbaya sana, ila kiuhalisia hapo unatakiwa umuache ale zake na wewe uchukue 10 yako.
Mwenye mali ndio anayetamka bei kisheria ukishatamka millioni kumi dalali zake ni asilimia kumi basi hatakiwi kija na bei zake yeye huo ni utapeli ..
Maana alitakiwa akujulishe thamani ya nyumba yako kwa wakati huo ni kiasi kadhaa sio aje tu na bei mara tano zaidi yk then atake wewe uchukue kidogo huo ni utapeli.
 
Ilitokea hii kitaa...nyumba ni 20m inauzwa dalali kaleta mteja wa 50m
Mwenye nyumba akagoma kuuza nyumba yake ,ikawa bonge mija la utata,akamuambia tafuta yako ya kwnagu siuzi hyo bei au ukitaka kula 10m ,40m ya kwangu akagoma dalali
Baadae yule mteja akaja kunnua kwa 34 mbila dalali ile nyumba.
Dalali jinga.
 
Kuna jamaa mmoja mtwara alimpa dalali kazi ya kumtafutia mteja wa eneo kwa bei ya milion 80 jambo la kushangaza mteja wa milion 120 akapatikana mwenye eneo akagoma kuuza

moja ya tatizo kubwa la binaadamu ni ubinafsi, badala ya kuchukua 80 yake aliyoitaka alipanik kwa 40 atakazokula dalali
 
Mwenye mali ndio anayetamka bei kisheria ukishatamka millioni kumi dalali zake ni asilimia kumi basi hatakiwi kija na bei zake yeye huo ni utapeli ..
Maana alitakiwa akujulishe thamani ya nyumba yako kwa wakati huo ni kiasi kadhaa sio aje tu na bei mara tano zaidi yk then atake wewe uchukue kidogo huo ni utapeli.

Biashara ni makubaliano mkuu, hiyo ndio kanuni kuu kwenye suala zima la biashara.
 
Jihadhari sana na hawa madalali. Kuna mfanya biashara mmoja Mbeya alikutana na mtihani kama huo . Alitangaza nyumba inauzwa kwa sh. mil 20 akawakabidhi madalali kazi hiyo wakamleta mteja wa million 40. Hapo kumbuka anayeingiziwa hela ni mwenye mzigo sio dalali. Baada ya mwenye Nyumba kuingiziwa hela mil 40 aka kaza hataki kuwapa madalali chao. Kilichotokea jioni moja wakati anafunga duka mnamo saa 1 jioni walikuja jamaa fulani kama wateja dukani kwake wakatoa bunduki na kumpiga risasi akafa pale pale wakasepa kusikojulikana😔. Kwa hiyo muwe making nao. Ukihusisha madalali ongeza bei mara 2 au zaidi ili waje na mteja anayejitetea kupunguziwa bei uliyotaja.
 
Jihadhari sana na hawa madalali. Kuna mfanya biashara mmoja Mbeya alikutana na mtihani kama huo . Alitangaza nyumba inauzwa kwa sh. mil 20 akawakabidhi madalali kazi hiyo wakamleta mteja wa million 40. Hapo kumbuka anayeingiziwa hela ni mwenye mzigo sio dalali. Baada ya mwenye Nyumba kuingiziwa hela mil 40 aka kaza hataki kuwapa madalali chao. Kilichotokea jioni moja wakati anafunga duka mnamo saa 1 jioni walikuja jamaa fulani kama wateja dukani kwake wakatoa bunduki na kumpiga risasi akafa pale pale wakasepa kusikojulikana😔. Kwa hiyo muwe making nao. Ukihusisha madalali ongeza bei mara 2 au zaidi ili waje na mteja anayejitetea kupunguziwa bei uliyotaja.
Huyo mzee alikosea. Kama huwapi unasema kabisa sitatoa hivyo ueni biashara.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom