Acha tamaa,zingatia makubaliano.
Na hapo kwenye hiyo 10 yako itabidi umpe na chake Cha udalali .
Mkuu umetoa jibu la mtu ambaye hajafanya biashara ya aina hiyo na asiyejua lolote kuhusu.
Dalali ni taaluma, ni ofisi na ni mshauri wa mwemye mali.
Kwa hiyo hawezi kuuza nyumba kimaghumashi nje ya utaratibu wa kiofisi na kisheria pamoja na makubaliano ya kazi.
Wewe unapouza nyumba unapanga bei yako, unapomtafuta dalali ataiangalia kisha atafanya tathimini kutokana na hali ya soko la kijiografia na kutoa ushauri kwa mwenye mali.
Mwenye mali kabla ya kutoa 'go ahead' watakubaliana na dalali malipo yake kutokana na % fulani ya malipo yatakayopatikana kutokana na mauzo ya mali.
Kwa hiyo let say kama nyumba ilikuwa inauzwa mil. 10, kisha yeye akaiuza kwa mil 100, hawezi kuchukua mil. 90 kisha akapewa tena malipo ya %yake kutoka mil. 10.
Kitachofanyika hapo ni yeye kunufaika na kupanda kwa % ya malipo ya kazi yake mliyokubaliana awali.
Hivyo kama ni 5% ya mauzo ya 10,000,000 ni 500,000 sasa kwa mil. 100,000,000 atalipwa 5,000,000.
Nakueleza hivyo kutokana na uzoefu, maana hatua ya mwisho huwa ni kati ya muuzaji mwenye mali na mnunuzi, kuna kujaza mikataba ya kisheria ya uuzianaji wa nyumba na kijwanja.
Hivyo hakuna longo longo itakayofanywa na dalali na mteja bila ya mwenye mali kujua.