Ilishawahi nitokea kabisa. Nilinunua shamba mwaka 2012 maeneo ya morogoro interior sasa ilipofika mwaka 2022 nikaamua kuliuza ila Kwa kugawa viwanja (ukubwa wa 30*20). Basi nikakata viwanja locally tu nikapata viwanja 20 nikatafuta dalali nikamwachia kazi. Bei 500,000 Kwa kiwanja kimoja .Baada ya wiki mbili dalali kanipia simu tayari anayo wateja wa viwanja vitano. Basi nikajongea Morogoro. Baada ya salamu dalali swali la kwanza akaniambia unakumbuka uliniambia niuze kiwanja shilingi ngapi? Nikamtajia then akaniambia sasa 2500000 ipo cash hayo mengine niachie ni ya kwangu, akaniambia hao wadau wakikwambia unauzaje waambie 1,200,000 Kwa kiwanja, yaan Mimi napokea laki Tano yeye laki Saba. Nilibadilisha gia angani nikamwambia mm nakula laki Tisa wewe utapokea laki tatu, hutaki napanda gari naondoka. Aisee ule mzozo ulikuwa sio wa kitoto lakini mwishowe anaikataaje laki tatu Kwa kiwanja kimoja? Mimi nikaambualia 4,500,000 na yeye 1,500,000