Arusha ilikuwa inahesabika kuwa ni jiji linalokua kwa kasi sana baada ya Mwanza na DSM, kwa mwelekeo huu anguko la Arusha liko mbele yetu kwa sababu za siasa za kukamiana. Wanaofuatilia mambo watagundua kuwa mikutano yote ya kimataifa inayomhusisha Raisi wetu haifanyiki tena Arusha badala yake ni DSM au Dodoma (St. Gaspar); kwa kiasi fulani kwa wenye mahoteli jijini Arusha hili ni pigo kubwa sana. Zaidi sana tangu kuzinduliwa upya kwa East Africa Community mikutano yote ilikuwa inafanyika Arusha lakini mwaka huu Maraisi wa nchi za Africa ya Mashariki walikutana DSM badala ya sehemu iliyozoeleka ya jiji la Arusha.
Kwa wenye mahoteli hii ni changa moto kwa wao kuungana na ikiwezekana wagharamie vikao vya maridhiano ili amani iweze kurejea Arusha na biashara zao ziweze kushamiri. Kama wangekuwa wanaona mbali, wangetumia hata mbinu ya Jairo kupooza mambo kabla ya biashara zao hazijaingia kwenye misukosuko ya kushindwa kulipa mikopo