Madaktari (hasa wa tanzania)...wamejengwa na egocentrism ya kufa mtu.....na hii inaanzia mbali sana toka sekondari...dharau zinaanza kwa wanaosoma kombi nyingine...unaingia chuo labda tuseme Muhimbili...unajifunza kudharau waliosoma IMTU...unaingia kazini...unaanza kuona ma-AMO si kitu kabisa na inaendelea...ndio maana hakuna field yenye majungu kama medicine....hii ni kozi inachukua cream ya taifa ila kiukweli madaktari wengi "wamefulia" kwa ujinga kama unaounyesha hapo juu....nimekaa kota za muhimbili najua ninachoongea....tunajiona sisi ndio mwisho mpaka hatupendi kushirikiana na kusaidiana....sasa angalia hapo juu jamaa linamponda
ZeMarcopolo ati chinja chinja.....Majungu na Pombe tu....ndio maana waliopata division 3 na kwenda kozi nyingine wanapotupita kimaendeleo tuna-mind ila yote hii ni kutojitambua.......Wewe utakuwa na hasira na mtu fulani alisoma CBG sasa wakati mko sekondari ulifikiri ataenda kusoma "Chuo cha Nyuki" sasa kapata medicine kama wewe naona hata kulala umeshindwa....
Nishakueleza hapo awali...Physics muhimu ila sio kama unavyotaka kudanganya watu hapa ioenekane bonge la ishu...waliosoma Medicine wanalifahamu hilo.....Pole kama imekuuma ila endelea kubwabwaja ila watu wanasonga mjomba utashangaa giza limeingia ujafikisha hesabu....TAFAKARI