Dada zetu wengi wanapambana kuolewa na wazungu tu

Kwa muda Sasa toka nihamie kufanya kazi katika bank Moja hapa Kariakoo. Katika pitapita zangu nikakutana na Dada mmoja akanialika kwenye party ya vikoba ili niwashauri namna ya kuweka pesa na kupata mikopo.

Sasa nilifika kwenye party Ile nikakuta waume wanne na wasichana umri wa Kati kama 50 hivi. Kwa haraka niliona wote wazuri sana na wengi wanafunguo za Magari.

Kadri muda wa party unavyoenda nikajitosa kupata mrembo mmoja wa kunipa company. Nikachambua wote Hatimaye nikakutana na mrembo mmoja hana kasoro.

Nikamwita akaja kwa shauku sana. Nikaropoka nimekuchagua akanijibu na Mimi nimekuchagua.
Tukacheeka sana. Baada akaleta kiti na beer zake tukaanza kupiga soga.

Ilikuwa kama zogo wadada wanabishana na kuchambana ghafla tukaingia kwenye mazungumzo mazito tukaondoka kwenye Dunia yao ya party tukawa kama wawili tu katika faraga. Tukaongea mengi sana.

Aliniambia kama tunaweza kuwa wapenzi lakini hatutaoana kwani ana date mtu mkubwa serikalini pia Hana mpango wa kuolewa na mtu mweusi anataka mzungu. Nilishangaa sana nikaona kama amajiwekea mitihani mkubwa sana. Nilini atakutana na huyo future husband wake? na ni wapi? . Hivyo Vyote hajui.
Anataka mzungu mpaka atakapokuja.
Tukamaliza party siku ile lakini bado nikawa naona kama ni dream kubwa sana kwake. Maana ni rahisi kuweka dreams ya kupata mali au nyumba lakini kukutana na mtu naona ni ngumu sana. What if wazungu wote wamkatae?

Kuna siku nilikuwa nungwi kwenye mapumziko yangu nasoma vitabu mbali mbali nilikutana na Dada mwingine tena nae aliniambia amekuja kisaka Mume mzungu.

Leo nimekutana na mwanaDada mrembo mwembamba amzuri akaniambia ametoka Mwanza Kuja Dar kusaka wazungu.

Mbona Mimi naona kama ni dreams kubwa sana kwa mtu kujiwekea kwenye Maisha?

Mtafute baada ya miaka 10 ijayo utakuta ameolewa na Tuntufye Mwasakafyuka.
 
tatizo wanatudhalilisha sie waafrica, wana olewa na mizee kitu ambacho kinashusha thamani yao duniani, kama kweli unaona bongo miyayusho kwanini usioe au kuolewa na kijana mwenzio? matokeo yake kuonesha unathamani ndogo unaoa au kuolewa na mzungu mzee. tungefurahi kuona dada zetu kuolewa na vijana sio mizee ambayo ishapoteza mvuto kwao.
 
Back
Top Bottom